Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Mkuu

Nije nikuchukue usiku nikuonyeshe roho zipo wapi???
Unatishia kuniua au. In short concept ya Roho imetungwa na watu kipindi kile ambao hawakuelewa Sayansi ya ubongo. Wanasayansi wamegundua Hilo kwa kufuatilia watu wenye matatizo ya ubongo, mapacha walioungana na kadhalika. Wakagundua akili ikifa na kila fikra na uamuzi huishia hapo.
 
Unatishia kuniua au. In short concept ya Roho imetungwa na watu kipindi kile ambao hawakuelewa Sayansi ya ubongo. Wanasayansi wamegundua Hilo kwa kufuatilia watu wenye matatizo ya ubongo, mapacha walioungana na kadhalika. Wakagundua akili ikifa na kila fikra na uamuzi huishia hapo.
Sio kukuua mkuu,bali nakupeleka makazi ya hizo roho mkuu.
 
TUKUFUNZE KUHUSU MUNGU YUPI SASA??????MUNGU WA KIARABU AU MUNGU WA KIYAHUDI AU MUNGU WA KIHINDU AU MUNGU WA KICHINA AU MUNGU WA KIBANTU??????
Ndo maana nasema tuachane na hizi dini tuamini tu kila kitu kilikuwepo na Kama kiliumbwa hatumjui na hatujui sheria zake na haingilii maisha yetu. Na hizi dini Ni Binadamu katika kujaribu kuelewa vitu wasivyovielewa.
 
Tufanye Binadamu tumweke pembeni maana yeye ana mwili.

Vipi kuhusu Lucifer na wenzake walioasi, maana wao ni roho pia (hawana mwili).
Binadamu siwezi kumweka pembeni ndio nachat nae hapa anatumia akili kusoma na kuelewa anachosoma na kuandika, anatumia utashi kufanya maamuzi, ana roho ambayo imebeba uhai wake na ndio huyo ananiuliza kuhusu lucifer anahitaji kupanua maarifa yake kuhusu ufahamu.
 
Sio kukuua mkuu,bali nakupeleka makazi ya hizo roho mkuu.
Kwa Nini usiku.. record video unitumie.. skia fuatilia Sayansi. Kuna kitu kinaitwa hallucinating..Ni kuhisi, kunusa, kusikia na kuona vitu ambavyo havipo. Ndo unaskia sijui mtu kaona jini, Mara katokewa na Mariam, zote Ni akili tu inakuchezea Ila sio kila kitu unachokisense Ni Cha ukweli. Ndo maana vitu vya hivyo haviwezi kutokea kwenye camera na Kama Kuna video jua Ni edited.
 
Hi
Kwa Nini usiku.. record video unitumie.. skia fuatilia Sayansi. Kuna kitu kinaitwa hallucinating..Ni kuhisi, kunusa, kusikia na kuona vitu ambavyo havipo. Ndo unaskia sijui mtu kaona jini, Mara katokewa na Mariam, zote Ni akili tu inakuchezea Ila sio kila kitu unachokisense Ni Cha ukweli. Ndo maana vitu vya hivyo haviwezi kutokea kwenye camera na Kama Kuna video jua Ni edited.
Huko hakuna video mkuu.Kama unaogopa ucku bas twende kesho asubuhi mkuu.
 
Kuhusu Dunia au other heavenly bodies in the universe kuzunguka bila kugongana, umejuaje kama hazijawahi kugongana hapo kabla??

Inawezekana hizo bodies ziligongana sana hapo mwanzo, Hadi ikafika kipindi Bodies zote Zika obey kanuni Fulani ambayo ilikuwa strong.

Pia hadithi za biblia kuhusu uumbaji, zinaibua maswali kuhusu Mahali alipokuwa amekaa Mungu akifanya huo uumbaji.

Ukisema Mungu alikuwa (mf. Mbinguni) wakati anafanya uumbaji. it means, Mbingu ilikuwepo kabla ya Mungu au mbingu ndiyo ilimtoa Mungu. Ukisema hakua sehemu yeyote, unamaanisha Mungu hayupo
Duuh...

Swali la Mungu alikuwa aliishi wapi kabla ya kuiumba MBINGU ambayo ni makao yake ni swali la msingi sana, na inabidi wataalamu wa haya mambo mje mjibu huku (ila kwa reference siyo kwenye fikra zenu).

Lakini mimi nikujibu hilo la heavenly bodies kugongana, probably inawezekana zamani viliwahi kugongana na hata wanasayansi wanasema hivo.

Na hata wana sayansi wa leo (modern scientists) wanatuambia kuwa miaka bilioni kadhaa ijayo hii galaxy yetu (milky way) itakuja kugongana na galaxy ya jiran (Adromeda galaxy) na bado ya mgongano huo itazaliwa galaxy mpya kwa jina lingine,lakini hakuna proof maana haijatokea bado.

Lakini pia, can you imagine kwenye galaxy yetu pekee (milky way) kuna kana kadiriwa kuwa na nyota kati ya bilion 300 mpaka bilion 500, pamoja na sayari zisizopungua bilion 100.

Sasa, hii galaxy yetu ni mojawapo ya galaxy ndogo sana, alafu fukiria idadi ya nyota zilizopo kwenye hiyo galaxy, fananisha na galaxy zingine kubwa zaidi ya yetu zitakuwa na nyota ngapi na sayari ngapi.

Alafu kumbuka galaxy zenyewe zipo nyingi sana, na kila galaxy ina ina mabilioni ya nyota na sayari.

Alafu imagine the whole observabale universe inakadiriwa kuwa na nyota siyo chini ya trilion 12.

Alafu wanasayansi wanakadiria kuwa "The number of stars in the universe is much bigger than all the grains of sand in the beaches on planet earth"

Na hivyo vyote viko kwenye motion, waweza nambia kama hivi vitu havina anayevidhibiti huoni kuwa vingekuwa vinagongana kila sekunde ?

Au hujaskia matukio ya Austronomy, wakisema kuwa "kuna jiwe kubwa la angani linakuja uelekeo wa dunia kuja kuiogonga la likiigonga dunia ndiyo maisha kwa heri" .

Lakini mara unashangaa wanatoa repoti tena kuwa hilo jiwe lililokuwa linakuja uelekeo wa dunia sasahivi limeshabadili mwelekeo siyo hatari tena kwa dunia.

We unadhani huo mwelekeo linabadilisha tu lenyewe bila mdhibiti ?

Kuna designer wa huu ulimwengu broo hata kama hatumwoni kwa macho.
 
Hahaha kwa Nini Hilo taifa lisiwe Roman empire, au uingereza kipindi Cha ukoloni ambao walichukua robo tatu ya dunia. Na kingine hivyo vitu unaviita ushafu Ni kwako na mwanzilishi sio marekani ye mwenyewe kavikuta vipo katika historia ya binadamu. Soma historia za empire mbalimbali utaelewa.
Anaeiendeleza Kwa Serikali za Dunia Kwa tishio za sanctions ni Marekani,
Roman empire haijawahi force kuamini Imani zao na waliheshimu desturi za watu.
 
Duuh...

Swali la Mungu alikuwa aliishi wapi kabla ya kuiumba MBINGU ambayo ni makao yake ni swali la msingi sana, na inabidi wataalamu wa haya mambo mje mjibu huku (ila kwa reference siyo kwenye fikra zenu).

Lakini mimi nikujibu hilo la heavenly bodies kugongana, probably inawezekana zamani viliwahi kugongana na hata wanasayansi wanasema hivo.

Na hata wana sayansi wa leo (modern scientists) wanatuambia kuwa miaka bilioni kadhaa ijayo hii galaxy yetu (milky way) itakuja kugongana na galaxy ya jiran (Adromeda galaxy) na bado ya mgongano huo itazaliwa galaxy mpya kwa jina lingine,lakini hakuna proof maana haijatokea bado.

Lakini pia, can you imagine kwenye galaxy yetu pekee (milky way) kuna kana kadiriwa kuwa na nyota kati ya bilion 300 mpaka bilion 500, pamoja na sayari zisizopungua bilion 100.

Sasa, hii galaxy yetu ni mojawapo ya galaxy ndogo sana, alafu fukiria idadi ya nyota zilizopo kwenye hiyo galaxy, fananisha na galaxy zingine kubwa zaidi ya yetu zitakuwa na nyota ngapi na sayari ngapi.

Alafu kumbuka galaxy zenyewe zipo nyingi sana, na kila galaxy ina ina mabilioni ya nyota na sayari.

Alafu imagine the whole observabale universe inakadiriwa kuwa na nyota siyo chini ya trilion 12.

Alafu wanasayansi wanakadiria kuwa "The number of stars in the universe is much bigger than all the grains of sand in the beaches on planet earth"

Na hivyo vyote viko kwenye motion, waweza nambia kama hivi vitu havina anayevidhibiti huoni kuwa vingekuwa vinagongana kila sekunde ?

Au hujaskia matukio ya Austronomy, wakisema kuwa "kuna jiwe kubwa la angani linakuja uelekeo wa dunia kuja kuiogonga la likiigonga dunia ndiyo maisha kwa heri" .

Lakini mara unashangaa wanatoa repoti tena kuwa hilo jiwe lililokuwa linakuja uelekeo wa dunia sasahivi limeshabadili mwelekeo siyo hatari tena kwa dunia.

We unadhani huo mwelekeo linabadilisha tu lenyewe bila mdhibiti ?

Kuna designer wa huu ulimwengu broo hata kama hatumwoni kwa macho.
Upo sahihi sana, Kiranga unaamini kuwa Kuna designer wa Kila kitu, tukiachana na mambo ya dini?
Anyway Kuna muda ukiwaza sana lazima utakuja kwenye conclusion ya kuwa Yupo aliyedesign huu ulimwengu na kuweka sheria za kimahesabu katika ulimwengu huu na zinajiendesha zenyewe bila makosa yaani ziko programmed
 
Upo sahihi sana, Kiranga unaamini kuwa Kuna designer wa Kila kitu, tukiachana na mambo ya dini?
Anyway Kuna muda ukiwaza sana lazima utakuja kwenye conclusion ya kuwa Yupo aliyedesign huu ulimwengu na kuweka sheria za kimahesabu katika ulimwengu huu na zinajiendesha zenyewe bila makosa yaani ziko programmed
Kwa nini unafikia conclusion hiyo?
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Kwenye swala la uumbaji wa binadamu Mungu hakuumba binadamu aliyekamilika. Kumbuka Adam na Hawa walikuwa na mapungufu ya kutokuwa na uelewa juu ya mema na mabaya. Had hapo naweza sema walikuwa hawajakamilika
 
Kwenye swala la uumbaji wa binadamu Mungu hakuumba binadamu aliyekamilika. Kumbuka Adam na Hawa walikuwa na mapungufu ya kutokuwa na uelewa juu ya mema na mabaya. Had hapo naweza sema walikuwa hawajakamilika
Kama adam na hawa walikuwa na Mapungufu, hapo wa kulaumiwa ni nani kati ya Muumbaji na Waumbwaji 🫢
 
Upo sahihi sana, Kiranga unaamini kuwa Kuna designer wa Kila kitu, tukiachana na mambo ya dini?
Anyway Kuna muda ukiwaza sana lazima utakuja kwenye conclusion ya kuwa Yupo aliyedesign huu ulimwengu na kuweka sheria za kimahesabu katika ulimwengu huu na zinajiendesha zenyewe bila makosa yaani ziko programmed
Exactly ukiwaza sana, huu ulimwengu uko programmed kama unavyosema 🫠
 
Anaeiendeleza Kwa Serikali za Dunia Kwa tishio za sanctions ni Marekani,
Roman empire haijawahi force kuamini Imani zao na waliheshimu desturi za watu.
Roman Empire nafikiri pia ameelezewa kwenye kitabu cha Danieli.

Kama.mnyama wa kutisha mwenye miguu ya chuma sijui, kwa mujibu wa wafasiri lakini 🫢
 
TUKUFUNZE KUHUSU MUNGU YUPI SASA??????MUNGU WA KIARABU AU MUNGU WA KIYAHUDI AU MUNGU WA KIHINDU AU MUNGU WA KICHINA AU MUNGU WA KIBANTU??????
Kumbe kila kundi lina Mungu wao tofauti na mwingine.

Any way achana na wahindu au budhah, hao wana miungu (wako wengi) siyo MUNGU.

Mimi nataka kujifunza GOD OF THE MOST HIGH (SUPER GOD).
 
Roman Empire nafikiri pia ameelezewa kwenye kitabu cha Danieli.

Kama.mnyama wa kutisha mwenye miguu ya chuma sijui, kwa mujibu wa wafasiri lakini 🫢
Yes Roman empire ilielezwa kwenye kitabu Cha Danieli.
Ila Marekani na Anguko lake Kwa tafsiri yangu binafsi, naona Ufunuo 17&18....
Marekani itaanguka na kuwa nchi ya kawaida although sijajua lini .
 
Kumbe kila kundi lina Mungu wao tofauti na mwingine.

Any way achana na wahindu au budhah, hao wana miungu (wako wengi) siyo MUNGU.

Mimi nataka kujifunza GOD OF THE MOST HIGH (SUPER GOD).
Yes Kila dini Ina Mungu wake
Waislamu wana Mungu wao.
Wakristo na Wayahudi Wana Mungu wao .
Wahindi Wana Mungu wao.
Wabahai Wana Mungu wao
Wa-Bantu Wana Miungu Yao, mfano Wahaya waliabudu Mungu asiyeonekana anaitwa Mukama ila mizimu kwao ni Malaika wema wanaosaidia matatizo madogomadogo yale makubwa wanampelekea Mukama asiyeonekana Wala kuchorwa.
Wasumeria walikuwa wanaabudu Enki na Enlil ambao inasemekana kuwa ni ma-aliens waliokuwa na uwezo wa ajabu.
Ila Designer yupo mmoja tu, shida tuliyonayo ni , Huyu ni nani? Kusudi la kutengeneza universe ilikuwa ni nini? Na pia je anajihusisha nayo au kaamua kuachana nayo?
Imagine tu system tu za mwili wako ukivotengeneza, imagine kuwa Simba, chui na wengine licha ya kwamba ni Mammalia ila hawana akili kama zako.
 
Back
Top Bottom