Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Any way acha iwe mwenye bidhaa zake ndiyo mwenye maamuzi ya mwisho.

Lakini Je, vipi kuhusu sisi kumjua yeye.
Tunamjua yeye kupitia vitabu vyake vya dini (mfano Biblia na Qur'an).

Swali ni Je, kwanini sasa vitabu vya dini vituambie stori tofauti kwenye kitu kile kile kimoja ?

It means kuna kitabu kitakuwa kimepotosha ?
Biblia ina vitabu sitini na sita vilivyoandikwa na waandishi arobaini, kwa muda usiopungua miaka elfu moja mia sita. (1600) kutoka kiebrania na aramaic agano la kale na kigiriki agano jipya. Katika nyakati hizo kulikuwa na ukuaji wa lugha, mabadiliko ya tafsri, rejista nk. Ukumbuke sasa hivi kuna biblia ya wakatoliki, wasabato, mashahidi wa yehova nk. Yote ni sehemu ya mkanganyo wa tafsiri za kibiblia.
 
Hi
Kwa Nini usiku.. record video unitumie.. skia fuatilia Sayansi. Kuna kitu kinaitwa hallucinating..Ni kuhisi, kunusa, kusikia na kuona vitu ambavyo havipo. Ndo unaskia sijui mtu kaona jini, Mara katokewa na Mariam, zote Ni akili tu inakuchezea Ila sio kila kitu unachokisense Ni Cha ukweli. Ndo maana vitu vya hivyo haviwezi kutokea kwenye camera na Kama Kuna video jua Ni edited.
Huko hakuna video mkuu.
Kumbe kila kundi lina Mungu wao tofauti na mwingine.

Any way achana na wahindu au budhah, hao wana miungu (wako wengi) siyo MUNGU.

Mimi nataka kujifunza GOD OF THE MOST HIGH (SUPER GOD).
Kwanini umewabagua wahindu na wabudha????
 
Chakula kikiwa kibaya analaumiwa mpishi au chakula.
Mchoro ukiwa mbaya analaumiwa mchoraji au mchoro.
Ndo hivyo bro
Uzuri wa chakula au ukamilifu based on or influenced by personal feelings, tastes, or opinions. Ni subjective... ww huli pilipili na chakula chote kimewekwa pilipili unasema mpisha kakosea kupika wakati kwake huo ndio ukamilifu?
 
Hayo mambo yana mkanganyiko mkubwa sana.


Ila in short the God displayed in religious books (bible & quran) sio Mungu mwenyewe au nguvu iliyoumba ulimwengu mzima.

Maana vitabu vinasema mungu anajua hatima ya kila mtu hata kabla hajaumbwa kama ni wa kwenda mbinguni au jehanamu na bado anakuumba na kukuleta duniani hivyo hivyo.

Ni hivi, hakuna jema wala baya machoni pa mungu wa kweli sinche they are from within na anatupenda sana tu.
 
Any way acha iwe mwenye bidhaa zake ndiyo mwenye maamuzi ya mwisho.

Lakini Je, vipi kuhusu sisi kumjua yeye.
Tunamjua yeye kupitia vitabu vyake vya dini (mfano Biblia na Qur'an).

Swali ni Je, kwanini sasa vitabu vya dini vituambie stori tofauti kwenye kitu kile kile kimoja ?

It means kuna kitabu kitakuwa kimepotosha ?
Hivyo vitabu mnavyosoma wajanja wenu akina Paulo wamevichakachua Kwa makusudi Ili kukupotezeni msifuate dini ya Mungu ila mfuate dini yao

Hi yapa the same story Mungu alimuhadithia nabii Musa baadae akaja kumuhadithia mtume Muhammad kuhusu wale malaika walioenda Kwa nabii Ibrahim kumbashiria mtoto Isihaka

Mwanzo 18:2
Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,
Mwanzo 18:3
akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako.
Mwanzo 18:4
Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu.
Mwanzo 18:5
Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema.
Mwanzo 18:6
Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate.
Mwanzo 18:7
Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng'ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa.
Mwanzo 18:8
Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala.
Mwanzo 18:9
Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani.
Mwanzo 18:10
Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake.



Quran 51:24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.


Bibilia inasema wale wageni Ibrahim alipowaandalia chakula walikula

Quran inasema walipoandaliwa chakula hawajakula na hapo ndipo Ibrahim alipojua kuwa wale ni malaika

Ukweli ni kwamba Malaika hawali chakula so hiyo story katika bibilia imechakachuliwa
 
Umeandika mambo mengi lakini mistake kubwa umeifanya hapo juu nilipo quote,.....
Ipo hivi unapozungumzia Mungu Muumbaji unazungumzia Mungu mmoja Tu, aliyeumba Ulimwengu mzima na kila kitu.
So, kiukweli kabisa kwa Jamii na tamaduni zote za Dunia hii basi Mungu wao ni Mmoja ila baadhi ya watu wameacha kumuabudu Mungu aliyewaumba wakaabudu viumbe.

Mfano, Mtu anayeabudu Ng'ombe ukimuuliza Ng'ombe kaumba nini? Bila shaka atajibu hakuna Maana hata huyo Ng'ombe ni kiumbe wa Mungu aliyeumba Ulimwengu na viumbe wote.

Hivyo basi, fahamu kwamba Mungu ni Mmoja tu kwa Africa, Asia, Ulaya, America, Australia, Antarctica hivyo concept yako kwamba kila watu Wana mungu wao haina maana.... Bali tunaposema Mungu inabidi tumaanishe Mola wa watu wote regardless races zao.
Nani anaabudu ng'ombe...nitajie hii dini.
 
Uzuri wa chakula au ukamilifu based on or influenced by personal feelings, tastes, or opinions. Ni subjective... ww huli pilipili na chakula chote kimewekwa pilipili unasema mpisha kakosea kupika wakati kwake huo ndio ukamilifu?
Hivi umeelewa nachomaanisha. Chakula kikiwa kibaya au kina makosa analaumiwa mpishi au chakula.
 
Umeandika mambo mengi lakini mistake kubwa umeifanya hapo juu nilipo quote,.....
Ipo hivi unapozungumzia Mungu Muumbaji unazungumzia Mungu mmoja Tu, aliyeumba Ulimwengu mzima na kila kitu.
So, kiukweli kabisa kwa Jamii na tamaduni zote za Dunia hii basi Mungu wao ni Mmoja ila baadhi ya watu wameacha kumuabudu Mungu aliyewaumba wakaabudu viumbe.

Mfano, Mtu anayeabudu Ng'ombe ukimuuliza Ng'ombe kaumba nini? Bila shaka atajibu hakuna Maana hata huyo Ng'ombe ni kiumbe wa Mungu aliyeumba Ulimwengu na viumbe wote.

Hivyo basi, fahamu kwamba Mungu ni Mmoja tu kwa Africa, Asia, Ulaya, America, Australia, Antarctica hivyo concept yako kwamba kila watu Wana mungu wao haina maana.... Bali tunaposema Mungu inabidi tumaanishe Mola wa watu wote regardless races zao.
Na ujumbe wa huyo Mungu mmoja huujui, hujui yupoje. Hujui anataka Nini, hujui atafanyaje, so usimpe sifa na sheria ambazo watu wa kale walimbunia.
 
Mkuu, kumjua Mungu wala sio changamoto hasa kama Mungu mwenyewe ni Yule Muumba wa kila kitu maana kila kitu kipo wazi.

Kuhusu vitabu vya dini kutofautiana, kwa kuwa unaonekana ni Open Minded jaribu kusoma pia sources nyingine nje ya Biblia Ili uelewe zaidi ukweli wa mambo mfano unaweza kupitia Qur'an na vitabu vingine.

Najibu maswali yako sasa :-
1. Makao ya majini ni hapa duniani na si mbinguni,... Bali Ibilisi(jini) ambaye ndiyo Shetani Hadith yake ni kwamba kulitokea uasi mkubwa uliofanywa na Jamii ya majini kwenye Dunia hii,. hivyo Mwenyezi Mungu akaagiza Malaika wake waje kutoa adhabu kwa Majini hao waliokithirisha maasi duniani, kwenye kazi hiyo ya kutoa adhabu kwa Majini ndiyo wakakuta mtoto wa kijini(Ibilisi) wakaamua wasimdhuru bali walimchukua na kwenda nae mbinguni, hivyo jini huyo(Ibilisi) akaishi pamoja na Malaika tokea hapo.
So, Shetani kuishi pamoja na Malaika ilikua ni special case.

2. Kuhusu hili swali, Shetani alishakataa kuomba msamaha na ashaandikiwa miongoni mwa viumbe wa motoni.., (kuhusu kwamba akiomba Msamaha sasahvi atasamehewa au Laa, Hilo anajua Mungu mwenyewe)
Mkuu naona uko vizuri, hasa upande wa dini yako (uislam).

Na kweli unavyosema, mimi huwa nasoma maandiko mengi na mengine hata siyo biblia wala Qur'an lakini ni yahusuyo tu imani.

Sasa nikuulize tena kitu kimoja, nitatumia mbinu gani kupima kuwa hiki kitabu ni cha kweli na hiki siyo (mfano kati ya Qur'an na biblia) na ukizingatia vyote vinamzingatia Mungu muumbaji ?

Na je, unaweza kunambia kati ya Biblia na Qur'an ni kipi kilianza kuwepo ?
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Nijaribu kukujibu. Kabla sijafanya hivyo nitoe angalizo kwamba maswali juu ya Mungu hayana empirical answers, isipokuwa logical answers. Ukilazimisha logical iwe empirical na kinyume chake basi ni vyema ukaacha kuamini uwapo wa Mungu na nguvu zake.

Swali lako juu ya shetani na nguvu zake: Uwapo wa shetani ndio unaodhihirisha uwapo wa Mungu, bila usiku mchana haupo, bila kulia kushoto hakutakuwapo. Bila adhabu zawadi haina maana. Kadhalika Mungu aliumba hao malaika, na moja akasaliti Mungu akamfanya awe adhabu ya milele itakayotofautisha walio wake na wasio wake. Ni kwa nguvu zake Mungu alimfanya Lucifer awe shetani, yaani nguvu kinzani. Na mara nyingi Mungu ameonyesha ushindi dhidi ya shetani. Ungeuliza pia kwanini Mungu anayesamehe kila Jambo hakumsamehe shetani, jibu ni hilo hapo juu: lazima kuwe na usiku ili tuujue mchana. Lazima kuwe na wovu tuujuwe wema. The two are separable but interdependent.

Swali kwamba Mungu alimpa Adam msaidizi dhahifu hadi akashawishiwa na nyoka kula tunda katazwa.

Ndugu, kwani aliyekuambia kwamba Adamu hakuwa dhahifu Nani? Unadhani Adamu alisamehewa dhambi kwasababu alipewa tu lile tunda? Wote walikuwa dhahifu na Mungu alijuwa hilo ndio maana akawaonya wasile tunda walilokatazwa. Yaani binadamu wote ni dhaifu tangu kuumbwa, kumbuka Mungu hakuumba binadamu kama malaika. Hata Yesu aliyeshuka kwa baba akavaa ubinadamu naye alikuwa dhahifu na akakili udhahifu wake mbele ya mitume wake.
 
Biblia ina vitabu sitini na sita vilivyoandikwa na waandishi arobaini, kwa muda usiopungua miaka elfu moja mia sita. (1600) kutoka kiebrania na aramaic agano la kale na kigiriki agano jipya. Katika nyakati hizo kulikuwa na ukuaji wa lugha, mabadiliko ya tafsri, rejista nk. Ukumbuke sasa hivi kuna biblia ya wakatoliki, wasabato, mashahidi wa yehova nk. Yote ni sehemu ya mkanganyo wa tafsiri za kibiblia.

Nafikiri kuna baadhi ya biblia za lugha zingine zina vitabu zaidi ya 66, kuna biblia zina vitabu hadi zaidi ya sabini na kitu na zingine zaidi ya themanini na kitu, vp kuhusu hilo ?

Na je, kama biblia original iliandikwa katika lugha za kiebrania,kigiriki na aramaic, ina maana kufasiri kuja kwenye lugha zingine za dunia ndiyo kunaweza kuwa kulipotosha maana halisi labda ?
 
Nijaribu kukujibu. Kabla sijafanya hivyo nitoe angalizo kwamba maswali juu ya Mungu hayana empirical answers, isipokuwa logical answers. Ukilazimisha logical iwe empirical na kinyume chake basi ni vyema ukaacha kuamini uwapo wa Mungu na nguvu zake.

Swali lako juu ya shetani na nguvu zake: Uwapo wa shetani ndio unaodhihirisha uwapo wa Mungu, bila usiku mchana haupo, bila kulia kushoto hakutakuwapo. Bila adhabu zawadi haina maana. Kadhalika Mungu aliumba hao malaika, na moja akasaliti Mungu akamfanya awe adhabu ya milele itakayotofautisha walio wake na wasio wake. Ni kwa nguvu zake Mungu alimfanya Lucifer awe shetani, yaani nguvu kinzani. Na mara nyingi Mungu ameonyesha ushindi dhidi ya shetani. Ungeuliza pia kwanini Mungu anayesamehe kila Jambo hakumsamehe shetani, jibu ni hilo hapo juu: lazima kuwe na usiku ili tuujue mchana. Lazima kuwe na wovu tuujuwe wema. The two are separable but interdependent.

Swali kwamba Mungu alimpa Adam msaidizi dhahifu hadi akashawishiwa na nyoka kula tunda katazwa.

Ndugu, kwani aliyekuambia kwamba Adamu hakuwa dhahifu Nani? Unadhani Adamu alisamehewa dhambi kwasababu alipewa tu lile tunda? Wote walikuwa dhahifu na Mungu alijuwa hilo ndio maana akawaonya wasile tunda walilokatazwa. Yaani binadamu wote ni dhaifu tangu kuumbwa, kumbuka Mungu hakuumba binadamu kama malaika. Hata Yesu aliyeshuka kwa baba akavaa ubinadamu naye alikuwa dhahifu na akakili udhahifu wake mbele ya mitume wake.
Mbona sijakuelewa, sio kweli kwamba kila kitu kizuri lazma kiwe na kibaya. Mfano wizi una adhabu lakini hamna zawadi ya kuishi bila kuiba. Hizi adhabu na zawadi zimeletwa na dini ili kufosi watu kuamini vitu visivyoaminika.
 
Hivi umeelewa nachomaanisha. Chakula kikiwa kibaya au kina makosa analaumiwa mpishi au chakula.
Hujaelewa nini? Maana ili useme kina makosa lazima uwe na reference for comparison hapa hatuna reference ya Mungu kumuumba binadamu timilifu au sio timilifu ili utuambie Mungu kakosea tupe reference ya utimilifu!
 
Hi

Huko hakuna video mkuu.

Kwanini umewabagua wahindu na wabudha????
Wale wanaabudu miungu na masanamu siyo Mungu.

Ni miungu yao iko mingi, mfano hindu mpaka ng'ombe anaabudiwa, una kuna Mungu mke sijui na wana majina tofauti tofauti sana hao miungu wao.

Sasa mimi wale binafsi nawaona hawako upande wa SUPER GOD muumbaji amabe ni mmoja tu.
 
Hayo mambo yana mkanganyiko mkubwa sana.


Ila in short the God displayed in religious books (bible & quran) sio Mungu mwenyewe au nguvu iliyoumba ulimwengu mzima.

Maana vitabu vinasema mungu anajua hatima ya kila mtu hata kabla hajaumbwa kama ni wa kwenda mbinguni au jehanamu na bado anakuumba na kukuleta duniani hivyo hivyo.

Ni hivi, hakuna jema wala baya machoni pa mungu wa kweli sinche they are from within na anatupenda sana tu.
Hapo kujua hatima ya kila mtu kabla hajamuumba ndipo kunakoniumizaga kichwa pia 🤔🤔🤔
 
Mbona sijakuelewa, sio kweli kwamba kila kitu kizuri lazma kiwe na kibaya. Mfano wizi una adhabu lakini hamna zawadi ya kuishi bila kuiba. Hizi adhabu na zawadi zimeletwa na dini ili kufosi watu kuamini vitu visivyoaminika.
Hakuna zawadi ya kuishi bila kuiba? Amri ya usiibe ina maana gani kama usipoiba hakuna adhabu. By the way sijasema kila kitu lazima kiwe na zawadi na adhabu. Jibu kufuatana na kinachoongelewa, tafadhali. Tusianze mada juu ya mada.
 
Wale wanaabudu miungu na masanamu siyo Mungu.

Ni miungu yao iko mingi, mfano hindu mpaka ng'ombe anaabudiwa, una kuna Mungu mke sijui na wana majina tofauti tofauti sana hao miungu wao.

Sasa mimi wale binafsi nawaona hawako upande wa SUPER GOD muumbaji amabe ni mmoja tu.
Wewe umejuaje SUPER GOD ni mmoja????? USHAWAHI KUMUONA AU UMEKARIRISHWA????Na una tofauti gani kiimani na hao wabudha na wahindu??????? KIPI KINSCHOKUFANYA UJIHESABIE HAKI NA KUWAHUKUMU WAO????
 
Hivyo vitabu mnavyosoma wajanja wenu akina Paulo wamevichakachua Kwa makusudi Ili kukupotezeni msifuate dini ya Mungu ila mfuate dini yao

Hi yapa the same story Mungu alimuhadithia nabii Musa baadae akaja kumuhadithia mtume Muhammad kuhusu wale malaika walioenda Kwa nabii Ibrahim kumbashiria mtoto Isihaka

Mwanzo 18:2
Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,
Mwanzo 18:3
akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako.
Mwanzo 18:4
Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu.
Mwanzo 18:5
Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema.
Mwanzo 18:6
Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate.
Mwanzo 18:7
Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng'ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa.
Mwanzo 18:8
Akatwaa siagi na maziwa, na ndama aliyoiandaa, akawaandikia mbele yao, akasimama karibu nao chini ya mti, nao wakala.
Mwanzo 18:9
Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani.
Mwanzo 18:10
Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake.



Quran 51:24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?

25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.

26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.

27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?

28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.

29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!

30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.


Bibilia inasema wale wageni Ibrahim alipowaandalia chakula walikula

Quran inasema walipoandaliwa chakula hawajakula na hapo ndipo Ibrahim alipojua kuwa wale ni malaika

Ukweli ni kwamba Malaika hawali chakula so hiyo story katika bibilia imechakachuliwa
Duuh...mkanganyiko ni mwingi aisee.

Lakini kabla sijakubali kuwa Biblia imechakachuliwa naomba nikuulize kitu.

Nnavyojua mimi kupitia haya haya maandishi ya kidini ni kwamba:Roho (mfano malaika au chochote cha kiroho) kinaweza kufanya chochote cha kimwili ikiwa tu na chenyewe kimejibadilisha na kuwa kwenye form ya mwili muda huo, sasa kama wale malaika waliomwendea Ibrahimu walishajibadilisha na kwenda pale kimwili, unadhani walikuwa wanaweza kushindwa kula kweli kwenye hiyo hali ya kimwili waliyo kuwa nayo kwa muda huo ?
 
Back
Top Bottom