Naanza kuamini Bundi kulia usiku Mahali palipo na mgonjwa ni ishara mbaya

Nimekwambia tuonyeshe analiaje sio unajichenga show us how he sing tuonyeshe analialiaje akija kufuatilia mzoga analiaje?
Kwa hiyo uonyeshwe bundi analiaje hii point imeonyesha una mambo mengi ya kujifunza alafu bado kwenye maisha yako hujapitia mengi inaweza ukawa mkubwa wa umri ila hujapitia mengi
Nyie ndo wale mnataka watu wabweke kama mbwa
 
Napata shida kuelewa hoja yako, kwamba umeelewa kwamba nilichoeleza kinamaanisha kuwa watu huuliwa na bundi? Hebu fafanua kidogo ulichoelewa katika bandiko langu.

Ova
Huyo ni mtoto kifikra anaweza akawa mkubwa kiumri ila kifikra ni mtoto sana
 
Fact,Bundi akilia na kama una mgonjwa asilimia za huyo mgonjwa kupona ni ndogo Sana


Kuna elimu yake ingawa hakuna uhusiano na ushirikina kama wengi tujuavyo
 
Ingekua kweli,hapa kiembe bundi kijitonyama,tungezika mtaa mzima.
Maana wana kiota chao hapa na milio kwenda mbele.
 
Kwanza kabisa kiumbe chochote kinapokua katika na hali ya kukaribia kufa seli ndizo hunza kufa so bundi anaouwezo wa kutambua seli za kiumbe ambacho kinaenda kufa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo uonyeshwe bundi analiaje hii point imeonyesha una mambo mengi ya kujifunza alafu bado kwenye maisha yako hujapitia mengi inaweza ukawa mkubwa wa umri ila hujapitia mengi
Nyie ndo wale mnataka watu wabweke kama mbwa
Bweka km Bundi tukusikie Bundi analiaje unaweza ukawa hata hujui Bundi analiaje
 
Wanasema bundi Ana uwezo wa kupata harufu ya kitu kilichokufa kabla ya siku 30
 
Watu wengine wabishi tu, ndege, bundi hata wanasanyansi husema, anauwezo wa kunusa, halufu ya binadamu, aliyehai karibu kufa, ndo uwezo wao, kila jamii, ya kiumbe hai duniani, inauwezo wake binafsi, bundi ndio uwezo wake huo, na kinyonga anauwezo wa kubadilika, rangi lakini bundi, hana huo uwezo, huo ni mfano kidogo, ila kunamifano, mingi tu.
 

Pia, bundi ana uwezo wa kuona kwa takribani mara ya saba ya binadamu. Hii inampa uwezo wa kuona mbali kwa usahihi, lakini inampunguzia uwezo wa kuona karibu.

Ova
 

Mchawi Binadamu, Bundi anatumwa tu.
 
Hatar sana
 
Mbona hatuwaonagi ostabei,,mbezi,,,Masaki huko??au wenzetu hawaumwagi au maskini tunarogana Sana Kwa kuwa ujinga,,Umaskini na maradhi vimetuathiri,,,vinatuathiri na vitaendelea kutuathiri,,,Fikra za kimaskini ni za hovyo Sana!!
 
Bundi ana uwezo wa kunusa mzoga kwa mileage ndefu hivo anaweza kunusa hata zile seli za mtu zilizoanza kufa. Inasemekana mgonjwa akiwa anakaribia kufa huwa seli zake za damu (nyeupe na nyekundu) huwa ndo zinaanza kufa mdogomdogo kabla ya kifo kamili so bundi unusa ile harufu ya mizoga seli za mgonjwa anaekaribia kufa ndipo huwa anasogelea kwa ukaribu zaidi eneo hilo akijipa imani ataokota mzoga na kujisevia msosi bila kujua kwamba anaekaribia kufa pale ni binadamu ambae hata akifa hatoweza kuondoka na mzoga huo, na ndio maana mnapoizika tu ile maiti harufu pia utoweka na bundi atatoka eneo hilo kwakuwa atakuwa anusi tena ile harufu ya mzoga akiyoipata kabla.
 
Katika ndege niliokuwa nawaogopa, na sasa siwaogopi basi ni bundi.

Sehemu ninayoishi ni makazi mapya kuna bundi huwa analia mara kwa mara. Haiwezi kupita wiki mbili hajalia, na wakati mwingine anaweza kufululiza hata siku tatu analia kila siku usiku. Siku zingine analia juu ya bati la nyumba kabisa.

Lakini mwaka wa pili sasa naishi hapa, na hakuna chochote kilichotokea. Hizo ni imani za uongo uongo tu bundi ni ndege kama wengine tu.
 
Niliwahi kusikia mahali kuwa bundi amebarikiwa kuhisi harufu ya mzoga hata kabla kiumbe hakijapoteza uhai wake ndio maana ni kawaida bundi kulia sehemu ambayo kuna mgonjwa
Sasa kwa nn alie usiku tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…