Nabii Josephat Mwingira anena Mazito kwenye Salamu za Heri ya Krismasi

Nabii Josephat Mwingira anena Mazito kwenye Salamu za Heri ya Krismasi

Salamu za Heri zinaendelea kumiminika. Hapa chini ni kutoka kwa nabii Mwingira:

View attachment 2058365

Salamu za kama hizi zinapoendelea kutufikia ni vyema kujitafakari. Ni wazi kuwa kama Taifa hatuko vizuri.

Walikuwapo kina Desmond Tutu, leo hatuko nao. Walifanya sehemu yao, wamekwenda. Angalia katika kuwaomboleza hakuna dongo hata moja.

"Tunayo ya kujifunza."

Kila mtu kwa nafasi yake anayo sehemu yake ya kufanya, atakayo kumbukwa nayo.

Ni wazi kuwa chuki tunazoziona kwetu ni matokeo ya kumea kwa mbegu zake tunazozipanda wenyewe.

Haki huinua taifa.

Barikiwa mtumishi wa bwana, nabii Mwingira.
Kuna ngedere watakuja hapa kumtetea mwendazake eti ameacha legasi mfyuuu?!
 
Askofu kaamua kutapika nyongo.
(Naona legacy inazama).

Screenshot_20211226-164603.png
 
Hawa ndio aina ya wachungaji tunaowataka, sio unakuta mchungaji kazi yake kuhimiza michango, kupiga majungu kama anavyofanya Gwajima na kusifia serikali. kkkt na Rc mjitafakari. Kazi yenu sio kumsifia rais na serikali

Askofu Shoo ni KKKT. Askofu Niwemugizi ni RC. Sheikh Ponda ni Mwislam.

IMG_20211226_084753_973.jpg


Hakuna dini ina bariki ushetani.

Mengine haya ni mapungufu binafsi.
 
Kuna ngedere watakuja hapa kumtetea mwendazake eti ameacha legasi mfyuuu?!

La msingi ni kuwa hata wao wanajua hawana hoja. Kuna mmoja nimemwona ana avatar ya kiroboto. Binafsi nimeona nimsome kwanza kumfahamu yu mtupu kiasi gani 😁😁.
 
Kwani mkuu serikali:

1. haikukwiba kura?
2. haijabambikiza watu kesi?
3. haijapoteza watu?
4. haijadhulumu watu yakiwamo maisha yao?
5. haikuhusika na magenge ya wasiojulikana?
6. Nk. Msururu ni mrefu.

Haya sisi yanatuhusu moja kwa moja.

Kwenye hayo tuko na nabii.

Kwa povu lote hili, kwani kitengo chako hasa kwenye hii kadhia ni kipi au hapo? Au ni #3 mkuu?
Sina povu lolote lazima nayeye aambiwe kabla ya kuinyooshea serikali je nayeye angalau ni msafi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom