Hayo ni moja ya mapungufu tunayotakiwa kuyaboresha leo.Yeriko usalama wa Taifa ambao mpaka watu wa nje ndo wanakuja tuambia kuwa Zenji ni hub ya dawa za kulevya,usalama huu huu umeshindwa jua aliyemuua padri mpaka twakopa watu toka nje,mkuu wa wilaya anateuliwa kumbe ana kesi,mifano mingine watatoa wenzangu
Hapana mkuu tuna usalama wa taifa,
Ah jamaa wameingiza siasa mno kwenye utendaji! ndio maana wengine tunadhani ni usalama wa CCM!
Nina jamaa yangu huko ....huwa ananishangaza sana nikimwambia mie na familia yangu na majirani ni fuul CHADEMA..huwa anatoa majibu yanayo nishangaza mno, kwanza anakasirika...then anajiapiza! kuwa haitawezana CDM waje waongoze nchi!! kuna siku alinitilea hata pisto kunitisha! nilimdharau sana yeye pamoja na wenzie wote!!
Pole sana mkuu, ungefuata sheria kwakumfikisha polisi na sheria ingechukua mkondo wake.
Hakuna aliyejuu ya sheria
Yericko tiss ilikuwa zamani sio sasa hivi ajira zake zinakwenda kwa vimemo, mtoto wa flani, nepotism nk. Nahisi sasa hata kagame ameshapenyeza watu wake pale sbb tuko vulnerable sana. zamani kuajiriwa pale mtu alikuwa vetted toka kijijini kwake alikozaliwa, shule aliyosoma na kila sehemu aliyopitia nk.
nakumbuka rafiki yangu mmoja aliajiriwa na tiss enzi hizo. kwanza yeye hakujua sbb kazi hii ilikuwa haiombwi na mhusika. watu walichujwa. jamaa kanambia kuwa alitumiwa ujumbe aende stand ya msamvu morogoro enzi hizo na kuwa ataikuta landrover ya kijivu saa sita mchana na akiikuta apande. baada ya hapo hakuonekana mwaka mzima na alivyorudi hakusema alikuwa wapi. lkn alitokea kuwa mmoja wa maofsa mahiri kitengoni.
hali ni tofauti na sasa. vuka tu pale ng'ambo ya makao makuu ya tiss kwenye bar ya SIMBA KAPAKATWA utawakuta wanakunywa pombe huku wakiongea mambo nyeti ya usalama wa nchi wakiwa njwiii. hakuna maadili wala secrecy ya masuala ya nchi. katiba mpya nadhani inaweza kuja na solution ya tatizo hili.
Mimi pamoja na kuendelea kuamini umuhimu wa chombo hiki nyeti kwenye nchi yetu bado napata tabu sana pale watendaji wake wanapo husishwa na utekaji na utesaji wa raia wanao onekana kuwa niwa pigania haki au usawa katika jamii.
Huwa nakuwa na maswali mengi bila majibu.
Mfano. Kupigwa na kutekwa kwa Dr Ully mwanahalisi lilianika namba za simu na majina ya watendaji wa chombo hiki ambao tumeambiwa wanahudumu ikulu.
Mmoja wa maafisa wa chombo hiki kwa mujibu wa Tanzania daima (sikumbuki toleo gani) alinyetisha kuwa Dr Slaa alishinda kiti cha uraisi kwa asilimia 61 na mpaka leo habari hii haijawahi kukanushwa.
Hapa ndio huwa najiuliza.
1. TISS inafanya kazi ya nani na kwa niaba ya nani?
2. TISS iko piha kwa ajili ya serikali inayo subiri nje ya dola au kazi yake ni kulinda serikali na chama dola kisianguke?
3. Kwa nini sasa hivi kuna malalamiko mengi juu ya TISS kukibeba chama tawala badala ya kuangalia maslahi mapana ya nchi bila kuegemea upande wowote?
Mkuu Yericko Nyerere kama unaweza kudadavua haya hebu vunja kikombe.
Nimeele hapo meno yanayotakiwaMeno yapi tena teh teh teh? Wakati kwa wenzetu kumekuwa na debate kwamba CIA imekuwa paramilitary organization kwa hiyo mambo ya kama drone strikes yawe coordinated na Pentagon na wao wabaki tu kama idara ya kutafuta taarifa na kutoa ushauri kama inavyotakiwa kuwa. Sasa meno yepi tena nyie mnataka wapewe?????????????
Mkuu hapo namba 2 kwenye red una uhakika na ulichokiandika? ngoja nichukuwe miwani yangu kabisa nasubiri ufafanuzi wako na kama kuna hiyo sheria kweli basi siwezi kujisumbuwa kupiga kura za Urais wakati kuna sheria hapo ya Kuilinda serikali iliyopo madarakani CCM isianguke.Japokuwa sina ujuzi sana wa hayo lakini mimi naona hivi:
1) TISS ipo kwaajili ya taifa kwaujumla
2) Ndio inailinda serikali iliyopo madarakani isianguke, hii ni kwamjibu wa sheria iliyoiunda taasisi hiyo.
3) Malalamiko ya watu wengi juu ya taasisi hii ni kwakuwa watawala wanapwaya kwenye nafasi zao na kuipa kazi ya ziada taasisi hii hivyo ufanisi wake kutiliwa shaka,lakini vivyohivyo watanzania wengi hawajui kazi halisi ya taasisi hii, wengi wanahisi ni ile ya umbeya tu (kuchukua taarifa)
Ndio ukweli wa mambo mkuu,Mkuu hapo namba 2 kwenye red una uhakika na ulichokiandika? ngoja nichukuwe miwani yangu kabisa nasubiri ufafanuzi wako na kama kuna hiyo sheria kweli basi siwezi kujisumbuwa kupiga kura za Urais wakati kuna sheria hapo ya Kuilinda serikali iliyopo madarakani CCM isianguke.
Mengi yatasemwa kuhusu Taasisi hiyo nyeti, lakini nadhani wengi hatujui inavyofanyakazi zake unajua jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, nakumbuka kuna kipndi fulani jamaa mmoja aliposti Kitabu chake hapa JF akielezea namna ambavyo idara ya usalama wa taifa ilivyofanyakazi zake na akatahadharisha kuwa watu tusiojua namna ambavyo taasisi hiyo inafanyakazi tunaweza kufikiri kuwa imelala jambo ambalo si kweli. Binafsi nilipenda sana ile post, sijui yule jamaa yuko wapi ingefaa atuekee tena kile kitabu hapa ili tuwe angalau tunapata uwelewa badala ya kupaki tunalalama tu.
ah jamaa wameingiza siasa mno kwenye utendaji! Ndio maana wengine tunadhani ni usalama wa ccm!
Nina jamaa yangu huko ....huwa ananishangaza sana nikimwambia mie na familia yangu na majirani ni fuul chadema..huwa anatoa majibu yanayo nishangaza mno, kwanza anakasirika...then anajiapiza! Kuwa haitawezana cdm waje waongoze nchi!! Kuna siku alinitilea hata pisto kunitisha! Nilimdharau sana yeye pamoja na wenzie wote!!
usiwadharau,wewe unaijua cdm juu juu wao wanajua dhamira yake.ukishaijua utajidharau mwenyewe