Nafasi za Ajira za muda za Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

Nafasi za Ajira za muda za Makarani na Wasimamizi wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022

NACHUKUA NAFASI HII KUISHUKURU JAMII FORUM. SIKUWA NA KITU KICHWANI KUHUSU SENSA, LAKINI NILISHIBISHWA HAPA. MLINIPA NONDO ZA MAANA, USAILI NIKAJIBU KWA USAHIHI NA KUJIAMINI SANA. NIMSHUKURU YULE ALIYETOA JIBU LA SWALI"jukumu kuu la karani wa sensa" MUNGU AMBARIKI, MUNGU WABARIKI WANAJF NA MUNGU IBARIKI JAMII FORUM. SHIKAMOO JF.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji38][emoji38][emoji38]

Nimekuwa kichwa wakuu nimeangalia sasa hivi kwenye simu ya madau tukiwa watu watatu wa majobless wa mtaa mmoja na wote hatumo.
Temeke Majina tayari.!?
 
Nitabaki humu nikifuatilia update za mkeka wa Temeke maana kuna ndugu yangu ameomba.
 
ILALA WAMEAMUA UGOMVI


Tulianza kama utani kukimbizana kutafuta fingerprint za wadhamini, tukasubiri Kwa muda mrefu hatimaye mkeka wa kwanza ulitoka Jina langu likawemo, kama mjumbe mmoja alivyosema kwenye Uzi wa Mamba Vs predators akasema eti kwakuwa mamba anataga basi hastahili kuingiankwenye Hilo kundi, Kuna mjumbe akasema usiombe ukutane na mamba wa mto Nile, Ndio kilichonipata Jina langu likakutwa na hao Mamba, linatafunwa huku mamba chozi Lina mtoka, kiufupi nimeliwa kichwa.

Nitumie fursa hii kumshukuru Mungu Maana maandiko yametuasa kumshukuru Kwa kila jambo, lakini pia niwashukuru wote ndani ya huu Uzi Kwa kutumia vifurushi au VPN mkaleta update ya kinachoendelea huko vyumbani. Ramli zote chonganishi zilipelekea watu wakataka kutoana ngeu.

Niwape pongezi wote ambao wamevuka Salama nawaasa Wakachape kazi, uvivu hautakiwi, na posho wazitumie vizuri hatutaki kusikia Tena ooh hatuna mitaji yakujiajiri, mitaji hiyooo msihonge kawekezeni. Wengine maisha lazima yaendelee wengi walikuwa wanazipigia hesabu hizo hela, usiihesabie Hela ambayo sio yako utaishia kukata tamaa.

Naomba kuaga rasmi kutoka kwenye huu Uzi.

TUJIANDAE KUHESABIWA
Tupo pamoja na mimi wanikata ila Ilala noma sana watu karibia saba nilioomba nao wote wamekatwa hakuna hata mmoja ninayemjua halafu majina mengi yamejaa jinsi ya kike vidume tumepigwa KO
 
Tupo pamoja na mimi wanikata ila Ilala noma sana watu karibia saba nilioomba nao wote wamekatwa hakuna hata mmoja ninayemjua halafu majina mengi yamejaa jinsi ya kike vidume tumepigwa KO
Hata mimi ilala tulikuwa wa 4 tunaojuana hakuna hata mmoja alietoboa
 
nmechezea za uso aseeeee daaaaah nilikuwa nategemea huko kwa ajili ya mtaji sijui ntatoboa vip maisha aya aseeee
😂😂😆 mimi wakati wakuangalia presha ilikuwa juu maana nilishapiga hesabu kali na kuandaa mazingira ya party dah!!! baada ya kucheki nikasema uongo huu ngoja niitazame tena wapi nikasema nisearch jina langu labda wameniweka kata nyingine hapo pia nikala za kichwa sasa nipo geto nacheza gemu kujipoza machungu huku nikisikilizia michongo wangu wa mwisho .
 
Wakuu nimetoboa , Mungu amebless , daah niliomba maudhui wamenipa ukarani , Wilaya ya Magu mkoani Mwanza , za chini chini Mbunge wetu katupambania kinyama majobless.... naskia vita ilikuwa Kali Sana , zaidi ya yote Tupo pamoja Sana wanangu wa JF...
hongera sanaa mkuu upo wilaya ya magu nimezaliwa hapo mkuu lakn nimekulia sehemu moja inaitwa sogesca.
 
Wakuu nimetoboa , Mungu amebless , daah niliomba maudhui wamenipa ukarani , Wilaya ya Magu mkoani Mwanza , za chini chini Mbunge wetu katupambania kinyama majobless.... naskia vita ilikuwa Kali Sana , zaidi ya yote Tupo pamoja Sana wanangu wa JF...
nami nimetoboa mkuu,tupo pamoja sanaaa nikija magu nitakutafuta mkuu napafahamu sanaaa hapo dah ktambo sanaa mkuu,,tupo dar tunapambana na life.
 
WILAYA YA NKASI MKOA WA RUKWA INA MAMBO YA OVYO SANAAA.

kiufupi mm walinila kichwa tangu jana mkeka ulivyobandikwa halimashauri mida ya saa moja jioni. sasa mshikaji wangu yeye jina lilitoka maana alikuwa na mawasiliano mazuri na aliyemfanyia usaili. sasa kitu cha ajabu saizi asubh yale majina ya jana yamechanwa na wamebandika mengine. Sasa rafk yangu jina limetolewa tena. yani hii nchi nyieeeee. Kwanza tulifanyiwa usaili wa kihuni sanaa, no ukaguzi wa vyeti, hakuna maswali yahusuyo sensa ila maswali yaliulizwa ya elimu yako, chuo ulichosoma na kama unaweza kutumia simu janja. Nilijua siwez kutoboa na kweli sijatoboa. Mtendaji kata jirani anasema simu toka wilayani zilizidi kila mtu anaweka order ya nafasi kadhaa. Sasa sijui kwetu kwa mtendaji kata mwanamke. Haaaaa wilaya hii ndiyo maana maendeleo yake ni duni sana maana kuna madudu huko. Kama mm nayaona hayo madudu hivi mama samia haambiwi? TAKUKURU huku nadhani hawapo au hii taasisi iliwekwa ili kutishia watu tu. Hivi madudu yote haya hakuna mtu aliyekamatwa. Aiseee.
 
Back
Top Bottom