Yaani hapo ndio balaa, kuipata. Nikikutana na polis mmoja hivi akaniuliza umeomba nafasi maana alijua mm ni muhitimu wa chuo kwa namna tulivyokutana pale. Nikamwambia yeah nimeziona akanishauri Kaombe maana saivi ajira ni ngumu ila ungekuwa na mtu ingekuwa rahisi zaidi lkn usiache kujaribu kwasababu huwezi jua. Yeye sasa[emoji3] Akaniambia mm nilitafuta kazi weeeh sikupataga sasa zikatangazwa za jeshi nilikuwa na mtu nikapigiwa simu nikaenda tena huku nalindwa[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] nikasema duuh!!! Nikaingia kozi mpk sasa nipo kazini na ni kijana tu. Nikaona watu tunauwezo wa kurahisishiana sana tofauti na hapo ni DUA TU NS KUDRA ZA MWENYEZI MUNGU zikitimia na ikiwa imeandikwa basi lazima tutapata tu, Tusikate tamaa tuendeleeni kujaribu kwa nafasi zetu...