Nahisi kama napoteza mahusiano na mzazi

Nahisi kama napoteza mahusiano na mzazi

Achana na matatizo endelevu.
Leta majibu ya maswali yafuatayo kwanza;

1. Wewe ni jinsia gani?
2. Una umri wa miaka mingapi?
3. Una wazazi wote wawili au mmoja?
4. Km una mzazi mmoja,7bu iliyo watenganisha ni kifo ama migogoro?
5. Kama ni mgogoro,je ulikuwa na umri gani kipindi hicho?
6. Je,ulikuwa upande upi kati ya wawili hao?
7. Mvutano wako na mzazi wako una uhusiano na kutengana na mwenza wake?
8. Je,mama kamkaribisha mrithi wa baba yako na wewe hukubariani na uamzi wake?
9. Unadhani mienendo na matendo yako yanakubalika ndani ya jamii yako?

Nitaendelea baada ya kupata mrejesho wako.
1. me
2. 19
3. mmoja
4. kifo
7. hapana
8. hapana
9. hapana,
 
Wazazi nao wanazinguaga basi tu ndio vile washakua wakubwa kwetu so tunajitahidi kuishi humo kwenye nidhamu

Kama sababu za ugomvi wenu ni kupishana mitazamo mfano mama anataka uende kanisani wewe hutaki,hataki utembee usiku basi jitahidi kumsikiliza anayotaka yeye...muhimu hayana madhara kwako
Kwa mtu anaeishi kwao mara nyingi shida inakuaga ni mtoto.

Ile kujiona kakua, au kuona mzazi hafanyi fair.
 
1. Mheshimu mzazi lakini kamwe usiwe mtumwa wake. Mheshimu Kwa mazuri na Mema lakini Kwa mabaya mwambie yeye kuwa mzazi haimpi uhalali wa kukupandia juu Kwa vitu visivyoeleweka.

2. Endelea kutekeleza wajibu wako kama Mtoto. Msalimie lakini Isiwe kila Siku kama anakauli za kukera. Salimia wiki Kwa wiki. Kama hamna bond.

3. Mwambie yeye ndio anakujua vizuri. Aliposema yeye ni mama yako ulimsikiliza na kumheshimu. Halikadhalika akisema yeye sio Mama yako pia utamsikiliza na kumheshimu. Mwambie hujawahi kulazimisha kuwa yeye ni mzazi wako. Ila unasikia na kuambiwa.

4. Ukiongea naye akujue wewe ni MTU wa Haki. Utamjibu na kumtendea Kwa haki. Na sio upendeleo.
 
Mzazi ukiwa mpole na mtu wa kujishusha mnapatana sana sana.

Inaumiza sana kujibishana na mzazi, mdogo wako tu akikujibu fyatu unamlapua. Sasa mama kukupiga hawezi ushakua kijeba anaishia kuishi kwa makasiriko tu.

Ujana wa kutorudi home tushaupitia ila waambie ukweli ni kipi kinakuweka huko.
 
1. Mheshimu mzazi lakini kamwe usiwe mtumwa wake. Mheshimu Kwa mazuri na Mema lakini Kwa mabaya mwambie yeye kuwa mzazi haimpi uhalali wa kukupandia juu Kwa vitu visivyoeleweka.

2. Endelea kutekeleza wajibu wako kama Mtoto. Msalimie lakini Isiwe kila Siku kama anakauli za kukera. Salimia wiki Kwa wiki. Kama hamna bond.

3. Mwambie yeye ndio anakujua vizuri. Aliposema yeye ni mama yako ulimsikiliza na kumheshimu. Halikadhalika akisema yeye sio Mama yako pia utamsikiliza na kumheshimu. Mwambie hujawahi kulazimisha kuwa yeye ni mzazi wako. Ila unasikia na kuambiwa.

4. Ukiongea naye akujue wewe ni MTU wa Haki. Utamjibu na kumtendea Kwa haki. Na sio upendeleo.
Huu ushauri wako unampotosha bwana mdogo.
Kwanza kabla ya hayo yote inabidi amjue mzazi wake ni mtu wa namna gani, ana elimu gani ukimwambia hayo mambo ya haki na upendeleo atakuelewa??

Wazazi wetu wengi hawakwenda shule, wanaishi kimila zaidi eti usimsalimie aloo unajitaftia majanga tu na kuongeza makwazo.

Kijana kama ni msomi atumie emotional intelligence kumaliza tatizo. Haihitaji mambo ya haki na upendeleo. Kinachofanya tatizo liwe kubwa ni hisia.

Mama anahisi hivi, mtoto anahisi vile. Sasa mtoto ajue hisia za mama yake na acheze nazo, simple kabisa.
 
hata mimi nimeona hii ndo nzuri mkuu
Kama huwa humpigii sim basi jaribu kua unampigia hata mara 3 kwa wiki.

Mpigie jumapili mwambie umeenda kanisani kama ndo kitu hupenda kusikia. Kama anahisi unakula bata mueleze magumu unayopitia huko. Mwambie umemmisi muahidi siku utakayoenda nk.

Kama mnakwazana mara kwa mara nenda ukae siku 2 au 3 za furaha then geuka zako chuo.

Ni mama yako na ni mwanamke pia, wanatumia sana hisia kwenye maamuzi yao, inabidi ufanye akuamini wewe zaidi ya mtu mwingine anaetoa taarifa kuhusu wewe. Yeye huko anaskia wanachuo mnaolewa na mishangazi, anaskia mnakula bata, anaskia muda mwingi hamuendi chuo, mnapewa hela nyingi na serikali nk ila wewe humwambii kitu so anapigia mstari anayoambiwa na hivyo hizo tabia zako ndo kabisaaa anasema huyu kapata pesa kawa jeuri kumbe sivyo, hisia tu.
 
Huu ushauri wako unampotosha bwana mdogo.
Kwanza kabla ya hayo yote inabidi amjue mzazi wake ni mtu wa namna gani, ana elimu gani ukimwambia hayo mambo ya haki na upendeleo atakuelewa??

Wazazi wetu wengi hawakwenda shule, wanaishi kimila zaidi eti usimsalimie aloo unajitaftia majanga tu na kuongeza makwazo.

Kijana kama ni msomi atumie emotional intelligence kumaliza tatizo. Haihitaji mambo ya haki na upendeleo. Kinachofanya tatizo liwe kubwa ni hisia.

Mama anahisi hivi, mtoto anahisi vile. Sasa mtoto ajue hisia za mama yake na acheze nazo, simple kabisa.

Haki ya mzazi aliyesoma na asiyesoma hazifanani.
Atende Haki.
 
Kama huwa humpigii sim basi jaribu kua unampigia hata mara 3 kwa wiki.

Mpigie jumapili mwambie umeenda kanisani kama ndo kitu hupenda kusikia. Kama anahisi unakula bata mueleze magumu unayopitia huko. Mwambie umemmisi muahidi siku utakayoenda nk.

Kama mnakwazana mara kwa mara nenda ukae siku 2 au 3 za furaha then geuka zako chuo.

Ni mama yako na ni mwanamke pia, wanatumia sana hisia kwenye maamuzi yao, inabidi ufanye akuamini wewe zaidi ya mtu mwingine anaetoa taarifa kuhusu wewe. Yeye huko anaskia wanachuo mnaolewa na mishangazi, anaskia mnakula bata, anaskia muda mwingi hamuendi chuo, mnapewa hela nyingi na serikali nk ila wewe humwambii kitu so anapigia mstari anayoambiwa na hivyo hizo tabia zako ndo kabisaaa anasema huyu kapata pesa kawa jeuri kumbe sivyo, hisia tu.
Huyu mwamba amebonga ukweli mtupu
 
Mtoa mada kina mengi umetuficha Kati yako na mzazi wako,sidhani Kama mzazi anaweza kumchukia mwanaye bila sababu ya kueleweka.

Kama kweli ulimkosea mzazi wako nakuomba uurudishe moyo wako nyuma,jishushe Kisha nenda umuombe msamaha kea upole Sana.Ukishafanya hivyo bila Shaka mzazi wako atarudisha imani Yake kwako.

Mzazi Ni Mungu wako wa pili baada ya Mungu mwenyezi.
 
Nimekua nikipata changamoto kwenye mahusiano na mzazi, kuna kuwa hamna maelewano kati yetu, tunagombana sana, hatuwezi kukaa sehemu moja tukazungumza usitokee ugomvi kati yetu. Kinachonishangaza zaidi, nikijaribu kuangalia sababu sielewi, hii hali imekua ikiendelea kwa muda mrefu sasa na inanipa mawazo kwa kweli.

Sasa hii hali imenipelekea kukwepa kwenda nyumbani kwa miaka karibia mitatu sasa, nipo chuo, na nikiwa likizo najiweka mbali na mzazi. Mfano mwaka jana ilitokea mzozo kwelikweli, nilikua nimefunga chuo nikagoma kufikia kwa mama alipokua kikazi, kwasababu hakuweza kuwa nyumbani kwa muda huo, tuligombana sana mpaka ikafikia hatua ya yeye kunikaripia 'usipokuja kuniona wewe sio mwanangu' basi ikabidi niende kishingo upande ila sikua na amani.

Tumeendelea kuishi hivi hivi kwa kulumbana mpaka hivi sasa, bado ugomvi unatokea mara kwa mara, hivi sasa tumefunga chuo nimebaki huku huku chuo kufanyia field, imekua mzozo kweli kweli mara aniambie simpendi ndo maana sitaki kwenda kumuona, leo tumezozana anadhani naishi na binti huku nimempa mimba, anataka aje kuona nnapoishi.

Najua mtaona kama kuna maovu yangu naficha, ndio maana nagombana na mzazi, nakubali kuna makosa nimefanya nikagombana na mzazi lakini tuliyamaliza, ila hii hali ni tofauti, nikiwa karibu na mzazi nahisi vibaya, sijui kwanini, natamani tu nijiweke mbali nae. Hii hali inanitesa sana, na nikifikiria huyu ndo mzazi pekee niliyebaki nae, naumia zaidi, natamani kuithibiti hii hali, ila inajirudia.

Najua humu kuna watu wazima mmeshapita ujana na changamoto zake, hebu nishaurini kwa mtazamo wenu nifanyeje ili kurudisha mahusiano na mzazi.
Kama ni wakiume Acha kiburi alafu angalia na marafiki wa kike ulionao kama unagombana na bi mkubwa,..

Kama ni wakike hiyo ni kawaida ila ukimaliza jitahidi uolewe na mwanaume anaye eleweka hapo mama anapoa..



Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Nimekua nikipata changamoto kwenye mahusiano na mzazi, kuna kuwa hamna maelewano kati yetu, tunagombana sana, hatuwezi kukaa sehemu moja tukazungumza usitokee ugomvi kati yetu. Kinachonishangaza zaidi, nikijaribu kuangalia sababu sielewi, hii hali imekua ikiendelea kwa muda mrefu sasa na inanipa mawazo kwa kweli.

Sasa hii hali imenipelekea kukwepa kwenda nyumbani kwa miaka karibia mitatu sasa, nipo chuo, na nikiwa likizo najiweka mbali na mzazi. Mfano mwaka jana ilitokea mzozo kwelikweli, nilikua nimefunga chuo nikagoma kufikia kwa mama alipokua kikazi, kwasababu hakuweza kuwa nyumbani kwa muda huo, tuligombana sana mpaka ikafikia hatua ya yeye kunikaripia 'usipokuja kuniona wewe sio mwanangu' basi ikabidi niende kishingo upande ila sikua na amani.

Tumeendelea kuishi hivi hivi kwa kulumbana mpaka hivi sasa, bado ugomvi unatokea mara kwa mara, hivi sasa tumefunga chuo nimebaki huku huku chuo kufanyia field, imekua mzozo kweli kweli mara aniambie simpendi ndo maana sitaki kwenda kumuona, leo tumezozana anadhani naishi na binti huku nimempa mimba, anataka aje kuona nnapoishi.

Najua mtaona kama kuna maovu yangu naficha, ndio maana nagombana na mzazi, nakubali kuna makosa nimefanya nikagombana na mzazi lakini tuliyamaliza, ila hii hali ni tofauti, nikiwa karibu na mzazi nahisi vibaya, sijui kwanini, natamani tu nijiweke mbali nae. Hii hali inanitesa sana, na nikifikiria huyu ndo mzazi pekee niliyebaki nae, naumia zaidi, natamani kuithibiti hii hali, ila inajirudia.

Najua humu kuna watu wazima mmeshapita ujana na changamoto zake, hebu nishaurini kwa mtazamo wenu nifanyeje ili kurudisha mahusiano na mzazi.
Tunagombana sana[emoji848] aisee hii hajakaa sawa hata kidogo.

Acha kabisa tabia ya kugombana na mama wewe ni mtoto hata kama unaona kuna sababu ya kukukera.
Moyo wa mzazi unaumia na kusononeka ndani kwa ndani unapokosa kumheshimu.
Kuna maneno ya uchungu ambayo mzazi huyatamka wazi wazi au kwa siri ambayo matokeo yake utayaone baada ya kuchelewa

Zuia kinywa chako.

MTOTO KWA MAMA HAKUI.
 
Back
Top Bottom