Naibu Waziri avunja bodi ya Maji Mbeya na kuagiza meneja wa RUWASA kusimamishwa kazi kwa kushindwa kutatua kero za Wananchi na kutoa ripoti za uongo

Naibu Waziri avunja bodi ya Maji Mbeya na kuagiza meneja wa RUWASA kusimamishwa kazi kwa kushindwa kutatua kero za Wananchi na kutoa ripoti za uongo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (MB) ametangaza kuivunja Bodi ya ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Mji Mdogo wa Rujewa katika Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya kwa kushindwa kuisimamia ipasavyo menejimenti ya mamlaka hiyo kutimiza majukumu yake kwa ufanisi.

Mhandisi Mahundi amechukua hatua hiyo mara baada ya kubaini ukosefu wa huduma ya uhakika ya maji kwa muda mrefu kwa wakazi wa mji wa Mbarali bila sababu za msingi.

Aidha, amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (Mbeya UWASA), Mhandisi Ndele Mengo kufanya uchunguzi ndani ya siku Nneili kubaini na kupata suluhisho la changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika wilaya hiyo.

Vilevile amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mhandisi Clement Kivegalo kumuondoa Meneja wa Wilaya ya Mbarali (RUWASA), Mhandisi Job Mwakasala pamoja na kufanya mabadiliko ya wataalamu katika wilaya hiyo.

Naibu Waziri amechukua uamuzi huo kufuatia kutoridhishwa na utendaji kazi wao baada ya kukuta changamoto nyingi katika wilaya ya Mbarali huku wakishindwa kuchukua hatua sahihi kuzitatua, ikiwemo kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusiana na utekelezaji na uendeshaji miradi ya maji.

Amesema wananchi wa Wilaya ya Mbarali wana kero nyingi kuhusiana na huduma ya maji huku wasimamizi wakishindwa kuwahudumia badala yake wakitoa taarifa zilizo tofauti ukilinganisha na uhalisia wa hali iliyopo, jambo linalokwamisha jitihada za Serikali kutatua kero za wananchi.

Awali kabla ya kuchukua uamuzi huo, Mhandisi Mahundi alitembelea miradi ya maji ya mradi wa Lunduga-Mawindi, Uhamila na Ilongo Group na kukuta hali ni tofauti na maelezo aliyopata, miradi ikiwa haitoi huduma na utekelezaji umesimama kwa muda mrefu.
 
Hongera NW ...hivi hawa watendaji wilayani wana mafungu kutekekeza wanayotakiwa kufanya na wana siasa ?? Au wanabadilishwa then business as usual
Mishahara huwa wanalipwa kwa kazi ipi?
 
Watendaji wengi kukaaa mezani kunawagharimu inatakiwa wawe wanaenda site kujionea hali halisi hasa kwenye miradi usipotembelea waweza letewa ripoti kuwa jengo linaezekwa kumbe hata msingi haujachimbwa...
Wengi hawaendi Site.

Wanatuma watu. Sasa ndio shida inakuja hapo? Utajuaje kama report ni ya ukweli
 
Wengi hawaendi. Site.
Wanatuma watu. Sasa ndio shida inakuja hapo? Utajuaje kama report ni ya ukweli
Utaenda vipi site wakati gari bovu au halina mafuta na hujapewa ela ya mafuta au ya kurekebisha gari?
 
Utaenda vipi site wakati gari bovu au halina mafuta na hujapewa ela ya mafuta au ya kurekebisha gari?
Brother unasema gari bovu? Hivyo ni visingizo vya kitoto kabisa.
Kwa taarifa yako wakuu wa vitengo.. pamoja na mkurugenzi mkuu . Magari yao guwa yanakuwa yako safi most of the time. Na service yanaenda.

I know that because once nilishafanya kazi kwenye mamlaka.
Hela ya mafuta wanayo, tena siokwamba inatoka sehemu flani..kutokana na malipo ya wateja. Hela ya mafuta inachomolewa huko.

Licha ya mabosi wengi kumiliki magari binafsi. Uzuri huwa wana ya park ndani ya ofce.


There is no excuse kwenye hili. Haswa kwenye issue ya usafiri.No excuse
 
Brother unasema gari bovu? Hivyo ni visingizo vya kitoto kabisa.
Kwa taarifa yako wakuu wa vitengo.. pamoja na mkurugenzi mkuu . Magari yao guwa yanakuwa yako safi most of the time. Na service yanaenda.

I know that because once nilishafanya kazi kwenye mamlaka.
Hela ya mafuta wanayo, tena siokwamba inatoka sehemu flani..kutokana na malipo ya wateja. Hela ya mafuta inachomolewa huko.

Licha ya mabosi wengi kumiliki magari binafsi. Uzuri huwa wana ya park ndani ya ofce.


There is no excuse kwenye hili. Haswa kwenye issue ya usafiri.No excuse

Naongelea RUWASA (hasa wilayani) na sio mamlaka ya maji. Hivyo ni vitu viwili tofauti.
 
Watendaji wengi kukaaa mezani kunawagharimu inatakiwa wawe wanaenda site kujionea hali halisi hasa kwenye miradi usipotembelea waweza letewa ripoti kuwa jengo linaezekwa kumbe hata msingi haujachimbwa.

Hongera naibu waziri
IVUNJWE HIYO BODI YA WIZARA NDIO MWAROBAINI
 
Mji wa Rujewa na baadhi ya maeneo ya Mbarali yana asili ya semi-desert climate...
 
Changamoto za Utendaji kazi ni kubwa kwa watumishi na miradi kwa ujumla.

Kuanzia na vitendea kazi na upungufu wa watumishi ikizingatiwa Serikali haijaajiri wataalamu wa sekta ya Maji kwa almost 5yrs.

Kuna miradi unaweza kuta haitoi huduma kutokana na kutokamilika kwa mradi hasa kama Mkandarasi hajalipwa Certificates zake. Hii hupelekea hata Kama mradi umekamilika kwa maana ya miundombinu, Mkandarasi anaweza kuto Supply Pump ili Ku push Malipo yake yafanyike haraka. Kwahiyo status ya mradi utaonekana umekamilika ila hautoi Huduma.
 
Back
Top Bottom