Naibu Waziri mteule wa Madini, Francis Kumba Ndulane ashindwa kusoma kiapo kwa ufasaha, uteuzi wake watenguliwa

Kwenye hotuba yake Rais JPM amewatumbua naibu waziri wa madini kwa kushindwa kuapa, na mkurungenzi wa Geita kwa kununua gari la zaidi ya 400 milioni.
Imeisha hiyo...
Huyu naibu hana jina?
 
Atakuwa aidha ni kihiyo au ana ugonjwa wa macho. Yote hayo yanamfanya kuwa si mtu sahihi wa kuchunga madini yetu yasiendelee kuporwa na wajanja.
 
Nadhan tuanzishe syllabus ya self confidence n stress management kuanzia vidudu, nlifikiri angesema ivo badala yake kasema tuwafundishe zaidi historia
 
Huyu jamaa bungeni aliapaje? Ningepata clip yake ningeelewa zaidi......pamoja na uoga ila jamaa inawezekana pia mambo ya kitamaduni yamehusika
 
Mkuu bado tu unaongelea uchaguzi, achilia maisha ya endelee utapata ugonjwa wa kideri kwa mawazo

Kama bado tunamuongelea Nyerere, ndio itakuwa huo uchaguzi wa juzi?
 
😂😂😂 Mimi sishangai sababu ndani ya chichiemu kuna yule muweka nia yule mdada alishindwa kujielezea
 
Naibu waziri kashindwa kusoma kiapo..alikuwa km mtu asiyejua kusoma au labda hakuwa anaona maandishi. Inasikitisha
Dah aisee uchawi upo, unaona maandishi yamepandana mpaka unashikwa kigugumizi. Walimwengu washafanya yao.
Serikalini katika nyadhifa za juu usipokuwa mtu wa kimila hutoboi!
 
So sad huyu mtu alipaswa kupewa nafasi nyingine ya kuapa tena alipaniki sana.
 
Tunaposema CCM huwa inaokota watu wenye mitindio ya ubongo wa kisiasa na kuipa vyeo haya ndio matokeo yake.
Kuna mbunge wa Cdm alishindwa kutaja tarakimu bungeni

Msikosoe tu muwe na kumbukumbu
 
Laana za waliouwawa, kuteswa kubambikiwa kesi na kufungwa ili yy ashinde! Hiyo ndo karma ya mayalla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…