Naibu Waziri wa Afya amuondolea madaraka Mkuu wa Idara Paul Koroso, aliyemjibu “Sijali lolote hata nikifukuzwa kazi”

Naibu Waziri wa Afya amuondolea madaraka Mkuu wa Idara Paul Koroso, aliyemjibu “Sijali lolote hata nikifukuzwa kazi”

Wewe Naibu waziri Mollel unataka wananchi wasiongee na wakuogope wakati unatumia nafasi uliyopewa vibaya na ovyo!. Mamlaka ya kumsweka ndani injia na kuamuru aondolewe kwenye nafasi yake uliyatoa wapi?. Unafahamu kuwa wewe ni mamluki na unaharibu image ya chama Cha mapinduzi?. Haujui kuwa wewe ni msaliti na ndiyo sababu uliwasaliti wananchi waliokuchagua pale ulipojiuzulu ubunge wa chama chako (CHADEMA) kilichokupa nafasi ukashinda Kisha ukakisaliti kwa kujiuzulu without any genuine reasons na ukabebwa sijui kwa mbeleko gani ukajiita mwanaCCM?. Watumishi wa umma kwa muda mrefu wamekuwa ni wahanga wa kudhalilishwa na wanasiasa na ni vema tabia hii mbovu na ya ovyo ikakemewa na kutokomezwa kabisa. Ni vema ukatumie nafasi uliyo nayo vizuri na utambue kuwa cheo ni dhamana.
Approach aliyotumia waziri haipo sawa. Ila kuhusu watumishi kudhalilishwa nayo haipo sawa japo nao ni mabingwa wa kudhalilisha wananchi wenye shida
Pili ukweli usiopingika ni kuwa kwenye miradi hiyo Kuna wizi wa kutisha, waziri au kiongozi yoyote asipokua macho basi hakutakua na thamani ya pesa inayoonekana.

N.b
Wafanyakazi wengi iwe wa serikali au binafsi tuna uwizi Sana(Mimi nikiwemo)
 
Tangu lini Naibu Waziri amekuwa na mamlaka ya kumtia mtu ndani? Au hata kumshusha cheo mtumishi wa umma? Tangu lini kumjibu vibaya kiongozi yeyote imekuwa kosa la jinai?

Hivi nani atamfungulia mashtaka huyo Injinia? Na hao ma dc na wengine wametajwa wapi katika mkataba? Kushirikishwa kwao ni privilege sio right. Wao kama wanataka iwe right, waiingize kwenye mkataba wa ujenzi kuwa msimamizi wa mradi atawajibika kwa DC na kamati zake.

Alipokosea injinia ni kwenye suala la Force Account. Yeye angeishia kusema tu kuwa Suma kazi imewashinda na atafutwe mkandarasi mwingine. Force account itumike kwenye ujenzi wa matundu ya vyoo na kuziba mashimo ya barabarani lakini sio kwenye miradi complex kama hospitali. Kwa kusema hivyo, nimeingia shaka na uwezo wake na huyo mwenzake wa mkoani.

Ila kwenye hili, amfungulie mashtaka Naibu Waziri kwa matumizi mabaya ya nafasi yake na kumuonea. Labda ndio yeye na wenzake watajifunza kuwa wao ni viongozi sio wanyapara.

Amandla....
Naibu Waziri hajamfukuza kazi kwasababu hana mamlaka hayo. Ila amemfuta "cheo". Cheo huwezi kukidai mahakamani au sehemu yoyote. Ni dhamana tu. Leo unapewa, kesho unanyang'anywa anapewa mtu mwingine.
 
Sina taaluma husika ila nampongeza Sana huyo engineer Kama yupo humu,nime judge kutokana na experience ya kuishi kwenye hi Nchi,wanasiasa Wana upuuzi Sanae
Engineer Hana dharau,amemaanisha anashikilia msimamo wake wa kitaalam na yupo tayari kuwajibika

NB
Kuna dalili ya kwamba engineer alitishwa kufukuzwa kazi asipokubaliana na hako ka (kipenyo)
 
Inawezekana ndugu Koroso amekosea kusema hivyo ila hawa viongozi wetu pia huwa hawana busara kabisa.....wanapenda kusema vibaya wenzao bila adabu as if wao ni malaika
 
Naibu Waziri hajamfukuza kazi kwasababu hana mamlaka hayo. Ila amemfuta "cheo". Cheo huwezi kukidai mahakamani au sehemu yoyote. Ni dhamana tu. Leo unapewa, kesho unanyang'anywa anapewa mtu mwingine.
Hana hata mamlaka ya kumfuta cheo. Kama ana hayo mamlaka basi anaweza kumpandisha cheo mtumishi yeyote wa umma. Mwenye mamlaka hayo ni Katibu Mkuu wake ambae ndie Mtendaji Mkuu wa Wizara. Na uamuzi wake unaweza kukatiwa rufaa katika Tume ya Utumishi. Watu hua hawakati rufaa kwa sababu mabadiliko hayo ya wadhfa yalikuwa hayaathiri mishahara yao. Lakini sasa kwa hii sheria ya Mwigulu, watu watakata tu rufaa.

Mawaziri sio watendaji katika wizara. Wao jukumu lao ni kusimamia sera za wizara.

Amandla...
 
Nadhani kanuni za utumishi wa umma/maadili kwa viongozi hajui
 
Chuo Kikuu cha Dar es salaam kiliheshimika kutokana na umahiri wa faculty yake ya Uhandisi na kimsingi miaka ile ya 1980 wahandisi ndio walikuwa Chuo

Eng Korosso heshima kwako!
 
Chuo Kikuu cha Dar es salaam kiliheshimika kutokana na umahiri wa faculty yake ya Uhandisi na kimsingi miaka ile ya 1980 wahandisi ndio walikuwa Chuo

Eng Korosso heshima kwako!
Mahiri kivipi hao wa Miaka hiyo kwani waligundua nini cha mainjinia labda?
 
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel ameagiza kuondolewa madarakani kwa Mkuu wa Idara ya Ujenzi wa wizara hiyo, Paul Koroso kutokana na mgogoro ulioibuka katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe unaotekelezwa kwa gharama ya zaidi ya Sh2.9 bilioni.

Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.

Dk Mollel ametoa maagizo hayo Julai 5 akiwa mjini Nansio Ukerewe alipofika kutatua mgogoro uliobuka kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi hospitali ya Rufaa ya mkoa katika kisiwa hicho ndani ya Ziwa Victoria.

"Kutokana na changamoto zilizojitokeza kwenye mradi huu, Koroso utakoma kuwa mkuu wa Idara ya Ujenzi Wizara ya Afya. Katibu mkuu atamteua mkuu mpya wa idara ambaye atakuja kusimamia mradi wa Ukerewe," alitangaza Dk Mollel.

Pamoja na viongozi na wataalamu wa Wizara, mkoa na wilaya, kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi wa CCM, halmashauri na mkandarasi Suma JKT.

Miongozi mwa malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa Wilaya ya Ukerewe dhidi ya Koroso ni kutowashirikisha viongozi wa wilaya na halmashauri katika utekelezaji wa mradi huo.

"Ofisi ya DC, halmashauri na CCM Wilaya ya Ukerewe hawakushikishwa katika utekelezaji wa mradi huu," Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Kanali Denis Mwila alimweleza Dk Mollel.

Muda mfupi kabla ya amri ya kuswekwa mahabusu, Koroso alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ingeokoa kati ya Sh180 milioni hadi Sh260 milioni iwapo ungetekeleza mradi huo kwa mtindo wa Force account (kutumia nguvu za wananchi) badala ya ukandarasi.

Kiwango kilichotajwa na Koroso kilitofautiana na kiwango cha Sh600 milioni kilichotajwa na mhandisi wa mkoa wa Mwanza, Chagu Nghoma.

Kutokana na tofauti hiyo, Dk Mollel akamtaka Koroso kutoa ufafanuzi, ndipo akasisitiza kuwa hesabu zake ndizo sahihi kwa mujibu wa kanuni na msingi wa kitaaluma na kwamba yuko tayari kuchukullwa hatua yoyote.

"Mheshimiwa Naibu Waziri, kiwango nilichotaja kimezingatia kanuni, vigezo na hesabu za kitaaluma; nitaendelea kusisitiza hilo hata kama ukinifukuza kazi sitajali," alisema Koroso.

Kutokana na kauli hiyo, Koroso aliyeketi jirani na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi Wilaya ya Ukerewe akajikuta anawekwa chini ya ulinzi na kupelekwa mahabusu.

Chanzo: Mwananchi
Matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya watu wanaosimamia taaluma zao badala ya siasa za umagufulism
 
Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.
cosbyhmm (1).png
 
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel ameagiza kuondolewa madarakani kwa Mkuu wa Idara ya Ujenzi wa wizara hiyo, Paul Koroso kutokana na mgogoro ulioibuka katika mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe unaotekelezwa kwa gharama ya zaidi ya Sh2.9 bilioni.

Dk Mollel pia ameagiza Koroso aswekwe mahabusu akidai amemtolea majibu na lugha ya kijeuri kuwa “hajali lolote hata akifukuzwa kazi”.

Dk Mollel ametoa maagizo hayo Julai 5 akiwa mjini Nansio Ukerewe alipofika kutatua mgogoro uliobuka kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi hospitali ya Rufaa ya mkoa katika kisiwa hicho ndani ya Ziwa Victoria.

"Kutokana na changamoto zilizojitokeza kwenye mradi huu, Koroso utakoma kuwa mkuu wa Idara ya Ujenzi Wizara ya Afya. Katibu mkuu atamteua mkuu mpya wa idara ambaye atakuja kusimamia mradi wa Ukerewe," alitangaza Dk Mollel.

Pamoja na viongozi na wataalamu wa Wizara, mkoa na wilaya, kikao hicho pia kilihudhuriwa na viongozi wa CCM, halmashauri na mkandarasi Suma JKT.

Miongozi mwa malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa Wilaya ya Ukerewe dhidi ya Koroso ni kutowashirikisha viongozi wa wilaya na halmashauri katika utekelezaji wa mradi huo.

"Ofisi ya DC, halmashauri na CCM Wilaya ya Ukerewe hawakushikishwa katika utekelezaji wa mradi huu," Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Kanali Denis Mwila alimweleza Dk Mollel.

Muda mfupi kabla ya amri ya kuswekwa mahabusu, Koroso alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ingeokoa kati ya Sh180 milioni hadi Sh260 milioni iwapo ungetekeleza mradi huo kwa mtindo wa Force account (kutumia nguvu za wananchi) badala ya ukandarasi.

Kiwango kilichotajwa na Koroso kilitofautiana na kiwango cha Sh600 milioni kilichotajwa na mhandisi wa mkoa wa Mwanza, Chagu Nghoma.

Kutokana na tofauti hiyo, Dk Mollel akamtaka Koroso kutoa ufafanuzi, ndipo akasisitiza kuwa hesabu zake ndizo sahihi kwa mujibu wa kanuni na msingi wa kitaaluma na kwamba yuko tayari kuchukullwa hatua yoyote.

"Mheshimiwa Naibu Waziri, kiwango nilichotaja kimezingatia kanuni, vigezo na hesabu za kitaaluma; nitaendelea kusisitiza hilo hata kama ukinifukuza kazi sitajali," alisema Koroso.

Kutokana na kauli hiyo, Koroso aliyeketi jirani na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi Wilaya ya Ukerewe akajikuta anawekwa chini ya ulinzi na kupelekwa mahabusu.

Chanzo: Mwananchi
MOLELI NI KICHAA, ALIFANYA KAZI BABATI SHIDA, SELIANI ARUSHA SHIDA, YAANI HUYU NI CHIZI CHIZI KABISA...MAGUFULI ALIMGUNDUA HUYU NI CHIZICHIZI ANA UBARIDI KICHWANI ILI ATUKANE APAMBANE NA WAPINZANI IKATIKI.....NYIE MFATILIENI MTAJUA KABISA
 
Tangu lini Naibu Waziri amekuwa na mamlaka ya kumtia mtu ndani? Au hata kumshusha cheo mtumishi wa umma? Tangu lini kumjibu vibaya kiongozi yeyote imekuwa kosa la jinai?

Hivi nani atamfungulia mashtaka huyo Injinia? Na hao ma dc na wengine wametajwa wapi katika mkataba? Kushirikishwa kwao ni privilege sio right. Wao kama wanataka iwe right, waiingize kwenye mkataba wa ujenzi kuwa msimamizi wa mradi atawajibika kwa DC na kamati zake.

Alipokosea injinia ni kwenye suala la Force Account. Yeye angeishia kusema tu kuwa Suma kazi imewashinda na atafutwe mkandarasi mwingine. Force account itumike kwenye ujenzi wa matundu ya vyoo na kuziba mashimo ya barabarani lakini sio kwenye miradi complex kama hospitali. Kwa kusema hivyo, nimeingia shaka na uwezo wake na huyo mwenzake wa mkoani.

Ila kwenye hili, amfungulie mashtaka Naibu Waziri kwa matumizi mabaya ya nafasi yake na kumuonea. Labda ndio yeye na wenzake watajifunza kuwa wao ni viongozi sio wanyapara.

Amandla....
Uko sahihi ndugu...

NW hakuwa na sababu na haki wala sababu ya kutoa uamuzi ule pale...

Kwa sababu kwa kiongozi makini naye akiwa ndiye boss wa wote wale wawili, alipaswa kujiuliza swali moja muhimu sana, kwanini hawa wahandisi wawili watofautiane wakati wote wanasimamia mradi mmoja uleule tena kwa tofauti ya figure kubwa ya fedha..?

Naye huyu Bwana Korosso sijui naye alikuwa na sababu gani tu ya ku - pre - empty maamuzi ya waziri..?

Mfano, hakuwa na sababu ya kumalizia maelezo yake kwa maneno; "........hata ukininufuza kazi..."

Hilo lilionesha dharau kwa boss wake japo boss naye ali - over react bure tu kiasi cha kutoa amri ile ambayo 100% haikuwa na umuhimu na ulazima...!
 
Back
Top Bottom