Najiskia kuwa mnyonge, na moyo wangu umebondeka sana. Eehh Mungu nitie nguvu

Najiskia kuwa mnyonge, na moyo wangu umebondeka sana. Eehh Mungu nitie nguvu

Mzee si ufungue nini kinachokusibu huenda hapa kuna mtu alishapitia the same exactly na jaribu na akapata njia so funguka mtoto wa kiume
Itoshe kusema tu, asante kwa maoni yako mkuu. Ipo siku yaja nawe utajiskia kama nilivyo jiskia mimi na hata familia yetu ilikua ikinitazama mimi ili nitende jambo lakini haikuwezekana.
Unapo barikiwa kupata mahitaji ya kukidhi familia, pia ukajitunzia akiba kwaajili ya kusaidia familia.... kisha siku moja ukapata maumivu pamoja na familia, wakati huo maumivu hayo yakahitaji maombi ama faraja..... then ninaamini utakuja kuelewa ninacho maanisha.
 
Mzee wangu Ushimen Mungu akujalie upite katika hiki kipindi ambacho unapitia nimezoea kukuona mcheshi na utani mwingi sana.

ila leo unaonekana mnyonge sana ni dhahiri shahiri kweli mambo yamekuzidia...

M/Mungu akufanyie wepesi uweze kupita hapo..
Kwani kwenye vitabu vyenu Rejea Quran na Biblia ameahidi hivyo...
Katika 1 wakorintho 10:13
View attachment 2791923

Na katika Quran Suratul baqara aya 286 (Quran 2:286)

View attachment 2791927
Nhamala ooneee ni hakika kama aliahidi mwenyewe atatenda Hivyo bhasi amini atatenda kikubwa ni subira..

Kwa maana wanasema hakika Mungu yuko pamoja na wenye kusibiri
Asante kwa maombi na faraja mkuu, Mungu akutunze na akubariki wewe na familia yako pamoja na uzao wako...🙏
 
Pole sana mdogo wangu, nini shida?
Mungu akufanyie wepesi katika mambo yako.
 
Huwa na soma post zako classmate Ushimen kimya kimya nakuona ni mmoja wa member wako very strong emotionally sijawahii kuona ukijokes kutafuta attention kiasi hiki hata mara moja...Naamini unapitiaa katika moja ya mitihani ambayo ukuitegemea katika maisha yako na unajihisi hauna majibu,

Tunaishi katika Dunia moja lakini Mungu anatupa mitihani tofauti tofauti kwa wakati tofauti na mitihani hiyo haiwezi kuwa imeishaa mpaka siku tutakayokuwa tumemaliza muda wetu wa kuwepo hapa Duniani.Ishi mkuu,tafakarii na rudi kwake YEYE atupaye mitihani hakika majibu yake utayapata na utapita kwenye mitihani hiyo...Sio rahisi,lakini ni Rahisi mno kwa wale wanaoamini and you are among of them.
Umenipa neno kubwa sana katikati ya maoni yako, sina hakika kama umeliweka kwa bahati mbaya ama lahh.... lakini kwakifupi umenikumbusha jambo la muhimu sana na umenijenga hata nimejiskia kuimarika.
 
Pole sana brother...
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho....
Kikubwa ni kuuombea huo mwisho uwe mzuri....
 
Kujua tatizo la mtu ili kumuingiza kwenye maombi ni bora zaidi huenda anataka kuombewa matatizo anayopitia kumbe amebaka katoto ka mtu kesi inaanza kufukuta anataka tumuombee je hiyo ni sawa? huo ni mfano tu simaanishi ndg ushimeni amebaka but ingependeza akashare mapito hayo japo kwa kuhide vipande
Yesu...🙊
 
Pole sana
Nini shida??
Mmepatwa na nini??

You're in my prayers.
Mungu awavushe[emoji120][emoji120][emoji120].


Bwana awainulie Nuru za uso wake na awape Amani[emoji120]
Maombi yako yamekua msingi imara zaidi kwenye hili jaribu letu, na hakika Mungu atatutetea kwakua yeye ni muaminifu sana.
 
Mungu aliweka Summer, Autumn, Spring na Winter.
Na kila kipindi hapo kina raha na machungu yake.
Kuna kipindi tulipitia wakati mgumu saana kama familia, ulipoisha niligundua ya kwamba kilikuwa ni kipindi bora sana ktk maisha yetu kama familia.
Fikiri tungeishi summer au winter throughout all the year, maisha yangepoteza msisimko wake.
Hivyo hivyo na katika maisha yetu ili yawe na ile thamani lazima magonjwa yawepo ili ujue thamani ya afya, njaa ili ujue thamani ya shibe, kukataliwa ili uijue thamani ya kukubalika nk
Screenshot_20231025-231459~2.png
 
Mnaosema Mungu anapitisha watu kwenye majaribu sidhani kama mnashauri vyema..

Labda mnafanya Counselling ya psychotherapy.

Mungu akupitishe kwenye majaribu ili uteseke?

Mungu akupe majaribu, kwamba yeye hajui Nia yako hadi akupime kwa majaribu?

Majaribu yote na shida zote hutokana na dosari za kibinadamu
 
Mungu aliweka Summer, Autumn, Spring na Winter.
Na kila kipindi hapo kina raha na machungu yake.
Kuna kipindi yulipitia wakati mgumu saana kama familia, ulipoisha niligundua ya kwamba kilikuwa ni kipindi bora sana ktk maisha yetu kama familia.
Fikiri tungeishi summer au winter throughout all the year, maisha yangepoteza msisimko wake.
Hivyo hivyo na katika maisha yetu ili yawe na ile thamani lazima magonjwa yawepo ili ujue thamani ya afya, njaa ili ujue thamani ya shine, kukataliwa ili uijue thamani ya kukubalika nk
Upo sahihi mkuu, and all of those are the meaningful of life.
Lakini pamoja na hayo yoote, maumivu bado hayaepukiki mkuu
 
'Nami nikasema nilikua kijana na Sasa ni Mzee, sijawahi kuona mwenye haki ameachwa wala watoto wake kutangatanga barabarani'

Pole sana Komredi Mungu ni mwaminifu ni suala la muda atawavusha salama.
Muhimu msisahau kushukuru kwa kila jambo.
Asante chief
 
Pole, usiache kumtegemea Mungu

soma Zaburi 9:10, ishi hapo....
Muombe Mungu tu na mizimu ya kwenu ila usimuomba kwa kupitia Uislam na Ukristu.....hutofanikiwa kamwe. Fikiria wewe ni mbongo unamuomba Mungu kwa kupitia Wataleban na Wayahudi, wapi na wapi.....inakuja kichwani kwako kweli hii?
 
Back
Top Bottom