Najivunia ushamba na ulimbukeni huu ulinipitia mbali

Najivunia ushamba na ulimbukeni huu ulinipitia mbali

Ni muunganiko wa mambo ambayo umeyapitia kwenye ukuaji wako ambayo yanaweza kuwa ya unyanyasaji na ndio yamefanya ubongo wako unashindwa kufurahia maisha halisi
Sasa mi sijapitia unyanyasaji mkuu.
Nani ameninyanyasa sasa
 
Mwasibu umefanya wanachofanya hao ila kwa platform tofauti.

Watu wana flex kitofauti tofauti… Mmeshawahi kujiuliza matajiri na matajiri wenzao wakikutana kwenye social gatherings zao wanaongea nini? wanatambiana nini?

Si ushamba… Kuna levels kwa kila kitu… na walengwa kwa kila kitu.

It’s me, someone ambaye sipost personal staffs kwa status zaidi ya moments/location nayo ni incognito.. Ni lazima utauliza hapo ni wapi….! Napost memes/jokes pia…
 
Na ata mtu ambaye hana furaha na maisha yake kiasi cha kushindwa kuyafurahia uyo lazima anaelekea kua kichaa kwasababu ya msongo wa mawazo na ukitaka kujua kuwa anaenda kua kichaa ndio kama hivyo yeye anajidai hataki ku Post lakini anaumia kuona wengine wana post sasa kama hapendi kupost kuna haja gani ya yeye kuongelea mada izo si akae kimya ili iwe serious kabisa yuko nje ya mitandao

Chimbuko la furaha au huzuni ni moyoni mwa mtu mwenyewe, hivyo furaha ya mafanikio bado mtu anaweza akabaki nayo mwenyewe maana hata asipoionesha kwa watu itaendelea kuwa ni furaha tu, huitaji justification ya watu kuyafanya mafanio yako yawe mafanikio.

Nakuuliza swali, kwa nini watu hupendelea kupost mafanikio tu zaidi ya mambo ya huzuni?
 
Mm ata kuweka status tu ni shida

Kwa mwaka inaweza kua mara mbili au tatu
 
Sasa bwana muhasibu kwani Jf sio mtandao wa kijamiii? Mbona hapa sasa ushatupostia hayo mafanikio yako!!

Waacheni watu wafanye yale yanayowafurahisha ilimradi hawavunji sheria. Sio ushamba mtu kufanya jambo ambalo wewe hufanyi.
 
Chimbuko la furaha au huzuni ni moyoni mwa mtu mwenyewe, hivyo furaha ya mafanikio bado mtu anaweza akabaki nayo mwenyewe maana hata asipoionesha kwa watu itaendelea kuwa ni furaha tu, huitaji justification ya watu kuyafanya mafanio yako yawe mafanikio.

Nakuuliza swali, kwa nini watu hupendelea kupost mafanikio tu zaidi ya mambo ya huzuni?
Kama unaona unahitaji kukaa nayo moyoni then kinacho kuleta JF kuwalaumu wanao onyesha furaha zao na kuwaita washamba ni nini unaonaje kama ukikaa kimya na uache wengine wafurahie maisha yao kwa amani na wewe ukae na siri zako kwa amani
 
Baadhi ya mambo ambayo yakizidi sana huwa nayaona ushamba na ulimbukeni. Haya mambo mimi yamenipita mbali kabisa.

1. Kujipost WhatsApp status
Hata kama nitafanya jambo gani, hata kama nimepata nini cha mafanikio huwezi kukikuta status. Mwaka jana nimegraduate taaluma mbili tofauti lakini huwezi kukuta status. Acha status hata graduation sikuhudhuria(Japo sio ushamba)
Sijui nimenunua gari kali najisikia aibu sana kujipost. Hata picha tu ya gari sina, na zile zilizotumiwa na Mjapani nilishazifuta.

Kuna mdogo wangu alikuwa anapenda kupiga picha na gari anajipost. Nikamkataza.

Yule baby alikuwa anapenda kujiselfie na mimi halafu anajipost. Nikamkata kistaarabu tu baby don't do that. Hata kesho nikifanya harusi nadhani hakutakuwa na status.

Naona wenzangu wanapost matokeo ya watoto wao yaliyotoka jana. Mimi A tupu za wakwangu siwezi kuzipost, naona ulimbukeni. Ahadi ya zawadi niliyompa akipata A zote nitampatia, nitamtia moyo aongeze bidii na kumpeleka vacation ya kisima.

2. Kutumia elimu na kazi yangu kujiona bora
Nina mavyeti mengi tu lakini sio bora kuliko wengine. Sio bora kuliko mlinzi na mfagizi pale ofisini. Wakati wengine wakipita bila hata kumsalimia mlinzi na kusaini daftari getini. Mimi lazima nimjulie hali nijitambulishe. Hata akisema basi nenda tu, namwambia hapana nitasaini hapa na kule kwa Mkurugenzi nitasaini. Maana ndio utaratibu.

Tukiwa shamba mimi sio bora kuliko kibarua. Kwa hiyo msosi wa shamba utakula wote.
Nimeipenda hii boss
 
Mkuu wewe kama mimi tuu
Kuna wanangu niliomaliza nao Telecom pale Cive walikua watu wa ku show off status ila mii wala

Nulipo piga electrical south africa wala hakuna ndugu aliyekua anajua an ni mtu wa kimya kimya..

Juzi nimeenda dubai lakini cha ajabu sijapiga picha hata kidogo. Mpaka mdogo angu anashangaa huyu blaza vipi ila naona normol tuu..

Maisha ya mtandaoni kujianika mi ndo siwezi kabisa aiseee
Hii ni nature niliyonayo toka advance nilipo piga A ya phy na chem wala sikua mtu wa show off zaidi zaidi waliokuwa and anapost matokeo yangu ni wale ndgu wa karibu tuu..
Hahah🤣🤣🤣
 
Mie ndio maana kila siku nasema,,. Waache watu wafanye vile wanataka kufanya as long as hawamkeri mtu

Matajiri wenyewe kina Zuck" wanapost kila siku.

Asa wewe ndio umefanya nini?, maana umeandika maisha yako yote hapa tofauti na hao uliowasema ni platforms tu😄🤣
 
Mwasibu umefanya wanachofanya hao ila kwa platform tofauti.

Watu wana flex kitofauti tofauti… Mmeshawahi kujiuliza matajiri na matajiri wenzao wakikutana kwenye social gatherings zao wanaongea nini? wanatambiana nini?

Si ushamba… Kuna levels kwa kila kitu… na walengwa kwa kila kitu.

It’s me, someone ambaye sipost personal staffs kwa status zaidi ya moments/location nayo ni incognito.. Ni lazima utauliza hapo ni wapi….! Napost memes/jokes pia…
Hapana mkuu. Ili kujenga hoja yangu ilikuwa muhimu kufanya hivyo
 
Endeleeni kukaa nayo,.

Tena mie ninavyopenda show off. Chochote tu napost iwe meme, iwe sijui nimetoka out. Nikiwa ofisini tu najipost mda mwingine,.

Na ninaishi vizuri tu, kama kuna ninayemkera animute
Unakera ujui tuu....
 
Back
Top Bottom