Najuta kumtia umasikini Mama yangu

Najuta kumtia umasikini Mama yangu

Mimi ni kijana Ambae nimezaliwa mwanzoni mwa mwaka 1990. Hapa hapa kwenye jiji la MAKONDA. Japo Baba na Mama yangu Kila mmoja ni mwenyeji wa mkoa wake.

Mama yangu alibahatika kusoma Hadi darasa la 7. Alifanikiwa kusoma typing enzi hizo ilikuwa hot sana kozi hiyo kama ilivyo computer siku hizi. Alisomeshwa hiyo kozi ili atafutiwe kazi ukizingatia kuwa mjomba wake alikuwa na cheo kikubwa TU wizara ya AFYA {R.I.P BABU}

Bahati haikuwa yake kwani katika harakati hizo za kutafutiwa kazi ikagundulika kuwa yeye Mama ni mjamzito. Hapo ndipo maisha yake yalipoanza kuwa ya kawaida nadhani mimba hiyo ilimtoa kabisa kwenye reli😭😭😭

Wenzie aliosoma nao enzi hizo Wana maisha mazuri na majina makubwa mfano Mtendaji mkuu wa NMB. Mh Ruth Zaipuna amesoma na mama yangu darasa Moja.

Nisingekuwa mimi kuja Duniani pengine mama yangu hivi sasa angekuwa mbali sana kimaisha.

Ujio wangu hapa Dunia umefanya mama amekuwa na maisha ya kawaida sana. Amehangaika sana na kwa kiasi Fulani Bado ananihangaikia😭😭😭

Nina huzuni sana licha ya kuwa nimesoma lakini elimu yangu haijanisaidia. Ni kama ubongo wangu umefungwa minyororo nashindwa Cha kufanya😭😭😭

View attachment 2808722

Na umri wangu huu nikiumwa ikahitaji milioni 1 TU haki vile nitakufa huku najiona. Umri wa mama yangu unaenda Kwa Kasi itafikia kipindi ataitaji msaada wangu.

Na Mimi Bado najitafuta japo namuomba sana Mungu anisaidie nijipate haraka. Na Nina muomba sana Mungu asimchukue mama yangu kabla sijajipata. Na ni Bora anichukue Mimi kwanza japo natamani sana siku Mungu atakayonichukua anichukue nikiwa nimemuacha Mama yangu pazuri 😭😭😭

Mwenzenu najuta sana kumpa mama yangu UMASIKINI​
Kwaio wewe ndo ulimpa mama yako umasikini ??
Kama ulikua na uwezo wa kumpa umasikini bas na uwezo wa kumpa utajiri pia unao.
 
Hata mimi ninaunga mkono kwamba bora angeitoa tu mimba yako kwasababu ya upumbavu ulio nao. Kama umezaliwa 90 mwanzoni ina maana wewe ni mtu unatakiwa uwe na familia kabisa. Unavyosema hadi sasa hivi mama yako anakupambania INASHANGAZA SANA. Kilichonikera zaidi ni uliposema umesoma. Mama yako pamoja na majanga yake alitimiza wajibu wake kwa 100% wewe ndo unamletea ushenzi. Neno langu la busara kwako ni kuwa uache upumbavu na pambana ujitegemee badala ya kumtegemea mama yako. Hivi vijana mliozaliwa Dar mna shida gani?
 
Sidhani kama ajutii japo aniambii ila dah. Inatia hudhuni imagine marafiki zangu niliosoma nao 75% wanaajira zinazoeleweka.

Inafikia kipindi mama nikimpigia simu ananiambia mtafute rafiki yako Fulani pengine anaweza kukuunganishia kazi.

Huku huyo rafiki yangu nikiwa Sina mawasiliano nae yoyote SI unajua tena Kila hatua mtu anayo piga anakuwa na marafiki wapya.

Nina miaka 30+ lakini Bado 75% ya maisha yangu IPO mikononi Kwa mama.​
Hudhuni = huzuni. Kwa uandishi huu utapata wapi kazi? Kama 75% ya maisha yako unamtegemea mama si bora tu uolewe?
 
Hata mimi ninaunga mkono kwamba bora angeitoa tu mimba yako kwasababu ya upumbavu ulio nao. Kama umezaliwa 90 mwanzoni ina maana wewe ni mtu unatakiwa uwe na familia kabisa. Unavyosema hadi sasa hivi mama yako anakupambania INASHANGAZA SANA. Kilichonikera zaidi ni uliposema umesoma. Mama yako pamoja na majanga yake alitimiza wajibu wake kwa 100% wewe ndo unamletea ushenzi. Neno langu la busara kwako ni kuwa uache upumbavu na pambana ujitegemee badala ya kumtegemea mama yako. Hivi vijana mliozaliwa mna shida gani?[/]

😅😅

We nae😀
 
Mimi naona tofauti, emotionally hauko matured, na hii inaweza kuwa sababu ya kuzaliwa na kulelewa na emotional immature parents. Tafuta namna ya kukomaza hisia zako kwanza ndipo utaweza kusamehe, kujisamehe na kukubali kilichotokea na kuamua kuanza mapambano upya.

Je wajua kuwa mtoto yatima, au yule aliyekulia mtaani anaweza kuwa amekomaa kihisia kuliko mtoto mwenye wazazi wote wawili au mzazi mmoja? Hii ni kwasababu wazazi wengi kuna muda tunashindwa kuficha hisia zetu kwa watoto hasa zile hisia hasi (Huzuni, hasira, maumivu, addictions zilizopitiliza etc). Watoto naturally wanafeel wanachofeel wazazi wao bila wazazi kujua na hii huleta athari kwa mtoto kama hizi.

Key take aways: Vijana kabla hatujaamua kuleta watoto duniani tujipime kama tuko tayari kihisia, ili tuweze kulea na kuwakuza in a functional environment. Watoto wengi wana struggle na mambo ambayo hata hawajui yamewafikaje, mbaya zaidi hayashikiki, yangekuwa yanashikika wangeweza kuyavua wakakimbia.
 
Mimi naona tofauti, emotionally hauko matured, na hii inaweza kuwa sababu ya kuzaliwa na kulelewa na emotional immature parents. Tafuta namna ya kukomaza hisia zako kwanza ndipo utaweza kusamehe, kujisamehe na kukubali kilichotokea na kuamua kuanza mapambano upya.

Je wajua kuwa mtoto yatima, au yule aliyekulia mtaani anaweza kuwa amekomaa kihisia kuliko mtoto mwenye wazazi wote wawili au mzazi mmoja? Hii ni kwasababu wazazi wengi kuna muda tunashindwa kuficha hisia zetu kwa watoto hasa zile hisia hasi (Huzuni, hasira, maumivu, addictions zilizopitiliza etc). Watoto naturally wanafeel wanachofeel wazazi wao bila wazazi kujua na hii huleta athari kwa mtoto kama hizi.

Key take aways: Vijana kabla hatujaamua kuleta watoto duniani tujipime kama tuko tayari kihisia, ili tuweze kulea na kuwakuza in a functional environment. Watoto wengi wana struggle na mambo ambayo hata hawajui yamewafikaje, mbaya zaidi hayashikiki, yangekuwa yanashikika wangeweza kuyavua wakakimbia.
Huyu ndg yetu inaonekana amelelewa na mama peke yake, bahati mbaya zaidi akalelewa kimama (huenda akawa ni mtoto wa pekee) kwahyo amekuja kushtuka akiwa amechelewa kidogo😀

Princes, Kijana wa kiume hutakiwi kulaumu kitu kama hicho, yaani unatamani mama angetoa mimba😳😳

Umasikini haujaanzia kwako wala kwa mama yako, kuna watu ni maskini ukiwaona hitojitambua kama masikini tena ila wao wameridhika na hawana wa kumlaumu..

Pamoja na hayo si kila aleyesoma alipata kazi mwaka 90 sio mbali kihivo.. kwani wangapi ni wasomi wazuri lakini hawana kazi? Huwaoni??

Huenda mama yako hata bila kubeba mimba asingepata kazi na maisha yangeenda tu na hivyo ndivyo ilikuwa, kwani pamoja na kutoajiriwa; aliwezaje kukulea na mpaka sasa umesema unamtegemea kwa kiasi kikubwa na bado wewe unamzidi elimu, anawezaje?
 
Mimi ni kijana Ambae nimezaliwa mwanzoni mwa mwaka 1990. Hapa hapa kwenye jiji la MAKONDA. Japo Baba na Mama yangu Kila mmoja ni mwenyeji wa mkoa wake.

Mama yangu alibahatika kusoma Hadi darasa la 7. Alifanikiwa kusoma typing enzi hizo ilikuwa hot sana kozi hiyo kama ilivyo computer siku hizi. Alisomeshwa hiyo kozi ili atafutiwe kazi ukizingatia kuwa mjomba wake alikuwa na cheo kikubwa TU wizara ya AFYA {R.I.P BABU}

Bahati haikuwa yake kwani katika harakati hizo za kutafutiwa kazi ikagundulika kuwa yeye Mama ni mjamzito. Hapo ndipo maisha yake yalipoanza kuwa ya kawaida nadhani mimba hiyo ilimtoa kabisa kwenye reli😭😭😭

Wenzie aliosoma nao enzi hizo Wana maisha mazuri na majina makubwa mfano Mtendaji mkuu wa NMB. Mh Ruth Zaipuna amesoma na mama yangu darasa Moja.

Nisingekuwa mimi kuja Duniani pengine mama yangu hivi sasa angekuwa mbali sana kimaisha.

Ujio wangu hapa Dunia umefanya mama amekuwa na maisha ya kawaida sana. Amehangaika sana na kwa kiasi Fulani Bado ananihangaikia😭😭😭

Nina huzuni sana licha ya kuwa nimesoma lakini elimu yangu haijanisaidia. Ni kama ubongo wangu umefungwa minyororo nashindwa Cha kufanya😭😭😭

View attachment 2808722

Na umri wangu huu nikiumwa ikahitaji milioni 1 TU haki vile nitakufa huku najiona. Umri wa mama yangu unaenda Kwa Kasi itafikia kipindi ataitaji msaada wangu.

Na Mimi Bado najitafuta japo namuomba sana Mungu anisaidie nijipate haraka. Na Nina muomba sana Mungu asimchukue mama yangu kabla sijajipata. Na ni Bora anichukue Mimi kwanza japo natamani sana siku Mungu atakayonichukua anichukue nikiwa nimemuacha Mama yangu pazuri 😭😭😭

Mwenzenu najuta sana kumpa mama yangu UMASIKINI​
Kwa hiyo humjuwi baba'ko?
 
Kila jambo lina sababu yake,huwezi kujua hiyo kazi kama angeipata ni nini kinge enda kumtokea,huenda Mungu alimnusuru ili asiende kufanya hiyo kazi kwa nia njema kabisa,

Endelea kupambana na usimtupe Mama yako,kwa muda huu ambao hujajipata,kaa na Mama karibu yake na umuongeleshe mambo yatakayo mfurahisha,usipende kusikitika mbele yake au kulaumu ugumu wa maisha mbele yako,mpe hope kua hivi karibuni mambo yatakua mazuri na atasahau machungu yaliyopita,

Vipi mshua wako yeye bado yupo?
Yupo na Bado wanaishi pamoja...anafanya kazi serikalini yupo na cheo Cha sita kutoka chini🤣🤣🤣 japo amebakiza nusu mwaka astaafu...!
 
Sijaelewa umemtia umasikini vipi mama yako?

Kimsingi kauli hiyo ingetoka kwa baba yako ama mama yako mwenyewe ingemake sense...wao ndio wamefanya mchakato wa wewe kupatikana

Enwei,endelea kupambana,kujuta haikusaidii kitu
Asante kipenzi. Nakupenda
 
Back
Top Bottom