Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

Nafikiri ni jambo la kujifunza kwa sisi wengine endapo mtu akikuambia jambo zito kama hilo unatakiwa kumsikiliza kwa umakini ikiwezekana kuwa nae Karibu na Mara kwa Mara onyesha kwa kiwango unamjali.
 
Poleni wanaJF,
Pole mtoa mada,
Pole kwangu

kwakweli inasikitisha.
 
Nafikiri ni jambo la kujifunza kwa sisi wengine endapo mtu akikuambia jambo zito kama hilo unatakiwa kumsikiliza kwa umakini ikiwezekana kuwa nae Karibu na Mara kwa Mara onyesha kwa kiwango unamjali.
hakika mkuu
 
Kama sikosei,mara nyingi mtu akitaka kujinyonga hata kama atakwambia utaona kama anatania lakini kumbe anataka kufanya kweli. Kwa hiyo usingeweza kusaidia cho chote,labda ungemwona live anajinyonga na wewe hukuchukua hatua yo yote hapo ndipo ungesikia hukumu moyoni.
Mimi naona uwe na amani tu!
 
Kama sikosei,mara nyingi mtu akitaka kujinyonga hata kama atakwambia utaona kama anatania lakini kumbe anataka kufanya kweli. Kwa hiyo usingeweza kusaidia cho chote,labda ungemwona live anajinyonga na wewe hukuchukua hatua yo yote hapo ndipo ungesikia hukumu moyoni.
Mimi naona uwe na amani tu!
Mkuu asante kwa ukarimu wako wakunipa faraja!
 
Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
siku ya Idd nilimpigia simu rafiki yangu nikitaka kujua kwanini hakunialika/kunikaribisha kwenye IDD wala hakunitumia ujumbe hata zile za kufowadiana tu ( Yeye alikua mwislam) na tulikua na mazoea haya ya kukaribishana au hata kujuliana hali tu kila mara, basi nikapiga, haikupokelewa, nikazidi kupatwa mashaka maana haikua kawaida yake, nikajua akiona missed call yangu atanipigia, ila hadi asubuhi ya siku iliyofuata hakupiga, nikazidi kukosa amani. Nakumbuka ilikua mida ya saa tatu asubuhi nilikua nimetoka home nikapiga tena simu ila nikaanza kukosa tu amani bila sababu ya msingi, mara simu ikapokelewa na sauti ya kike, sikustuka maana ni kawaida simu yake siku nyingine kupokelwa na mke wake. Nilivyosikia sauti ya kike nikaanza kumtania "Shemeji imekuaje mmekula iddi peke yenu bila kunikaribisha?:" nikaona kama vile yule mtu hanifahamu, ikabidi nitulie nimuulize, wewe si ni mama fulani? Akajibu akasema "Mimi ni Shemeji yake, jana nilikua kwako Baba fulani ni mgonjwa, hivyo wakati naondoka nikasahau nikabeba simu yao nikaacha yangu, wapigie kwenye namba ya airtel"

Nikaipiga namba ya mshkaji akapokea mke wake akaniambia jamaa yako ni mgonjwa, nikamwambia mpe simu niongee nae, akasema hawezi hata kuongea, aagh kidogo sikuamini maana tangu nimefahamiana na jamaa zaidi ya 15 years ago sijawahi kusikia anaumwa kiasi hiki, shida nini akaniambia. nikawashauri wampeleke hospital........ila hawakuweza.

Jioni ya siku ile nikapiga simu tena, nikaambiwa jmaaa bado hali yake sio nzuri, nikaongea na ndugu zake na bado nikasisitiza wampeleke hospital, Kaka yake akanijibu kuwa ni vyema niende kwanza nikamuone then mambo ya hospital yatafuata, Siku ya Mechi ya Kazier Chiefs na Simba SA bikajisemea moyoni wacha hii mechi ikiisha niende kwake hata kama ni usiku nikamchukue nimpeleke hospital.

Mechi iliish akwa Simba kufungwa, nikasema wacha tu nikalale muda huu nitaenda asubuhi nikamchukue nimpeleke hospital maana ndugu zake walikua wanasema amerogwa hivyo sikutaka sana kuingilia mambo ya ndugu japo mkewe alinielewa.

Asubuhi saa kumi na moja moja kuna namba ngeni ilinipigia mara mbili ila sikusikia simu, saa 12 asubuhi nikaamka nisikilize DW nikaona missed calls, nikawa najiiliza huyu anayepiga simu mida hii nani? Kupiga ile namba nikapokelewa na KILIO cha Mwanamke, dah nilikufa ganzi aiseeee....

Pengine ningeacha kwenda mpirani jana yake ningeweza kumuokoa Jamaa......Hii scenerio bado mbichi kabisa, nimeshiriki kila kitu kwenye msiba wake but naona nina hatia kubwa sana. Pumzika kwa amani Kaka.
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.


Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
Pole kedekede kwa yaliyokukuta.

Taarifa ziko za aina tatu:

1. Kwa ajili ya kuzingatia (For Noting):
Hii ni kwamba mtu anakuarifu kitu, ili ujue tu, kipo hicho kitu. Huna nafasi ya kufanya chochote kile kuhusu hicho kitu kukizuia au kukifanya kiendelee.

2. Kwa ajili ya Kupendekeza (For Endorsement):
Hii ni pale mtu anapokuarifu kitu, ili ukichekeche na kuwa na nafasi ya kukipendekeza kiende kwa yeye ambaye anao uwezo wa kukizuia au kukifanya kiendelee. Kwenye hili unakuwa kwanza umezingatia (you have noted), halafu ukikubali kupendekeza jambo linaendelea mbele ya safari. Usipopendekeza, unaweza kumrudishia mwenyewe kwamba sipendekezi mpaka ufanye yafuatayo utakayotaka wewe ili upendekeze. Au unaweza kuendeleza mchakato kwa kutoa maoni yako kwamba hupendekezi, lakini taarifa isonge mbele. Mtoa maamuzi atajua kwamba hukupendekeza, lakini umeruhusu mchakato uendelee. Yeye ataweza kutoa uamuzi kurudisha suala kwako lirekebishwe mpaka ukubali kupendekeza, au ataendelea na mchakato huku akizingatia kwamba hukupendekeza.

3. Kwa ajili ya Kuridhia (For Approval):
Hii ni pale unapoletewa taarifa kwamba kitu fulani hakiwezi kufanyika, mpaka wewe utoe uamuzi kwamba kifanyike au kisifanyike.


Kwa hiyo, ile taarifa uliyopewa inaangukia fungu lipi?
 
siku ya Idd nilimpigia simu rafiki yangu nikitaka kujua kwanini hakunialika/kunikaribisha kwenye IDD wala hakunitumia ujumbe hata zile za kufowadiana tu ( Yeye alikua mwislam) na tulikua na mazoea haya ya kukaribishana au hata kujuliana hali tu kila mara, basi nikapiga, haikupokelewa, nikazidi kupatwa mashaka maana haikua kawaida yake, nikajua akiona missed call yangu atanipigia, ila hadi asubuhi ya siku iliyofuata hakupiga, nikazidi kukosa amani. Nakumbuka ilikua mida ya saa tatu asubuhi nilikua nimetoka home nikapiga tena simu ila nikaanza kukosa tu amani bila sababu ya msingi, mara simu ikapokelewa na sauti ya kike, sikustuka maana ni kawaida simu yake siku nyingine kupokelwa na mke wake. Nilivyosikia sauti ya kike nikaanza kumtania "Shemeji imekuaje mmekula iddi peke yenu bila kunikaribisha?:" nikaona kama vile yule mtu hanifahamu, ikabidi nitulie nimuulize, wewe si ni mama fulani? Akajibu akasema "Mimi ni Shemeji yake, jana nilikua kwako Baba fulani ni mgonjwa, hivyo wakati naondoka nikasahau nikabeba simu yao nikaacha yangu, wapigie kwenye namba ya airtel"

Nikaipiga namba ya mshkaji akapokea mke wake akaniambia jamaa yako ni mgonjwa, nikamwambia mpe simu niongee nae, akasema hawezi hata kuongea, aagh kidogo sikuamini maana tangu nimefahamiana na jamaa zaidi ya 15 years ago sijawahi kusikia anaumwa kiasi hiki, shida nini akaniambia. nikawashauri wampeleke hospital........ila hawakuweza.

Jioni ya siku ile nikapiga simu tena, nikaambiwa jmaaa bado hali yake sio nzuri, nikaongea na ndugu zake na bado nikasisitiza wampeleke hospital, Kaka yake akanijibu kuwa ni vyema niende kwanza nikamuone then mambo ya hospital yatafuata, Siku ya Mechi ya Kazier Chiefs na Simba SA bikajisemea moyoni wacha hii mechi ikiisha niende kwake hata kama ni usiku nikamchukue nimpeleke hospital.

Mechi iliish akwa Simba kufungwa, nikasema wacha tu nikalale muda huu nitaenda asubuhi nikamchukue nimpeleke hospital maana ndugu zake walikua wanasema amerogwa hivyo sikutaka sana kuingilia mambo ya ndugu japo mkewe alinielewa.

Asubuhi saa kumi na moja moja kuna namba ngeni ilinipigia mara mbili ila sikusikia simu, saa 12 asubuhi nikaamka nisikilize DW nikaona missed calls, nikawa najiiliza huyu anayepiga simu mida hii nani? Kupiga ile namba nikapokelewa na KILIO cha Mwanamke, dah nilikufa ganzi aiseeee....

Pengine ningeacha kwenda mpirani jana yake ningeweza kumuokoa Jamaa......Hii scenerio bado mbichi kabisa, nimeshiriki kila kitu kwenye msiba wake but naona nina hatia kubwa sana. Pumzika kwa amani Kaka.
Mkuu tupo jahazi moja inauma sana.Pole sana mkuu.
 
Back
Top Bottom