Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

Ana fungus kwenye uke!Atumie clomatrizol 1% ointment + vaginal tablett !kuhusu kula udongo ni craving anayotakiwa aache coz udongo si kitu kinachohitajika kwenye mwili wa mwanaadamu hasa kwenye utumbo mpana/appendix thats a foreign substance!

Asante sana docta kwa msaada wako.
 
ninasumbuliwa na tatizo la maeneo mbalimbali ya mwili wangu nahisi kama joto kali linalonipa maumivu kwa ndani, nikiwa katika mazingira ya baridi hali hii hubadilika na kuhisi baridi kali kati ya maeneo yafuatayo hasa miguuni, mapajani, kiunona na mgongoni pia, hali hii husababishwa na nini? na tiba yake inakuwaje? natanguliza shukrani.
Una umri gani na wewe ni jinsia gani?
 
Kuna mtu nimemjibu kuhusu oligomenorrhea ambayo ipo classified kama amenorrhea isipokuwa amenorrhea inaweza kuanzia miaka 16 na hedhi inaweza ipotee zaidi ya miezi.Na jinsi inavyosababishwa nimeandika pia.Nikagusia polycystic ovarian syndrome(kupata viuvimbe/cysts vingi kwenye mayai) ambayo husababishwa na kuongezeka/disturbance ya homoni ya kiume(androgens) ambayo husaabishwa pia imbalance ya homoni nyingine kama estrogen. Hii hupelekea msawajiko ktk mfumo wa hedhi,kuota kwa ndevu au vinyoleo kwa wanawake,matatizo kwenye mfumo wa uzazi na hata kisukari(Diabetes Type II).Hali hio hujitokeza kipindi cha balehe mpaka miaka 19 na watu wenye tatizo hili mara nyingi wanasumbuliwa na uzito vilevile.
Tiba ni tofauti:

  • Kama unataka ujauzito ni clomifen.

  • Kupunguza male characteristics vidonge vya uzazi wa mpango vinaweza kutumika mf ethinylestradiol(vinasaidia kuweka sawa mfumo wa hedhi,NB:inachukua miezi 8 mpaka uone mabadiliko) au spironolactone(aldactone) na dexamethasone ili kupunguza production ya homoni za kiume.
  • Kama una kisukari dawa za kisukari zinahusika mf metformin/Glucophage.Hizi itasaidia kucontrol kisukari na kupunguza uzalishaji wa homoni za kiume,kuuweka mfumo wa hedhi sawa,na hatimae kuongeza possibilties za kupata ujauzito.

owkey asanteh!
 
Kuna mtu nimemjibu kuhusu oligomenorrhea ambayo ipo classified kama amenorrhea isipokuwa amenorrhea inaweza kuanzia miaka 16 na hedhi inaweza ipotee zaidi ya miezi.Na jinsi inavyosababishwa nimeandika pia.Nikagusia polycystic ovarian syndrome(kupata viuvimbe/cysts vingi kwenye mayai) ambayo husababishwa na kuongezeka/disturbance ya homoni ya kiume(androgens) ambayo husaabishwa pia imbalance ya homoni nyingine kama estrogen. Hii hupelekea msawajiko ktk mfumo wa hedhi,kuota kwa ndevu au vinyoleo kwa wanawake,matatizo kwenye mfumo wa uzazi na hata kisukari(Diabetes Type II).Hali hio hujitokeza kipindi cha balehe mpaka miaka 19 na watu wenye tatizo hili mara nyingi wanasumbuliwa na uzito vilevile.
Tiba ni tofauti:

  • Kama unataka ujauzito ni clomifen.

  • Kupunguza male characteristics vidonge vya uzazi wa mpango vinaweza kutumika mf ethinylestradiol(vinasaidia kuweka sawa mfumo wa hedhi,NB:inachukua miezi 8 mpaka uone mabadiliko) au spironolactone(aldactone) na dexamethasone ili kupunguza production ya homoni za kiume.
  • Kama una kisukari dawa za kisukari zinahusika mf metformin/Glucophage.Hizi itasaidia kucontrol kisukari na kupunguza uzalishaji wa homoni za kiume,kuuweka mfumo wa hedhi sawa,na hatimae kuongeza possibilties za kupata ujauzito.

owkey asanteh.
 
Hormone unbalance inasababishwa na kutawala kwa homoni ya kike estrogen au kuongezeka kwa homoni ya estrogen na mapungufu ya progesterone mwilini.Estrogen inatengenezwa kwenye mayai na ina husika na kujamiiana.Ina husika pia na hedhi na inahakikisha mwili unakuwa katika hali ipasayo kwenye kipindi ambacho mwanamke anaweza kubeba ujauzito yaani akiwa fertile!Estrogen inahakikisha mayai yanapevuka ipasavyo kwenye follicle phase na progesterone inaharibu yai ambalo limepevuka na halikurutubishwa.Jinsi umri unavyokwenda ndivyo mayai(ovaries yanapunguza)uzalishaji wa estrogen na progesterone na kupeleka hormonal in balance.Tiba ni hormone replacement therapy
gorgeousmimi Ubarikiwe sana kwa msaada unaotupatia humu, naomba kujua zaidi juu ya hiyo tiba ya hormone replacement therapy iko vipi. Asante sana.
 
Last edited by a moderator:
gorgeousmimi Ubarikiwe sana kwa msaada unaotupatia humu, naomba kujua zaidi juu ya hiyo tiba ya hormone replacement therapy iko vipi. Asante sana.
Ahsante everlenk,
Hormone replacement theraphy inatumika kwa watu waliofikia menopause.

Haishauriwi kutumika kwa watu waliofertile kwa sababu inaoongeza risk ya kupatikana kwa cancer ya kizazi,breast cancer, tromboembolism na hata osteoporosis. Na hapa hormones zinazohusika ni estrogen na progesterone.

Androgen therapy ni njia nyingine ya hormone therapy inatumika kwa watu wenye hypogonadism au wenye matatizo ya nguvu za kiume kutokana na magonjwa n.k
 
Last edited by a moderator:
nina mabaka usoni yaliyotokana na chunusi.nin tiba yake?
 
Dokta,mke wangu anakula sana udongo na mchele mbichi,je kuna tiba yoyote ya kumsaidia ili aache?pia wakati wa tendo la ndoa anatoka uchafu kama maziwa mgando au mchele uliolowekwa sana,ni nini tatizo?na tiba ni ipi?Tips:huwa anaosha sehemu zake za siri juux2 tu na maji...hatumii sabuni wala haingizi kidole,ndivyo alivyofundishwa kwao.

Mkuu salito,Hali ya mkeo kula udongo na mchele mbichi kipindi cha ujauzito ni carving inayotokana na ujauzito.Ni aghalabu kushauri tiba kwa wajazito kama wanaafya njema na wanatatizo kama la mkeo.Mjamzito anapaswa apate tiba pale tu inapoidi kwa sababu afya yake ni muhimu na ugonjwa wake unaweza kuwa na madhara kwa mtoto.Ningependa kama ungefunguka zaidi je mkeo ana washwa ukeni?amekuwa mwekundu kwenye eneo la uke?
salito na gorgeousmimi ngoja nitoe msaada hapa;

Ulaji wa udongo au barafu mara nyingi huusishwa na upungufu wa madini chuma mwilini...

Mara nyingi tabia hii huoneshwa sana na wamama wajawazito kwa kuwa kipindi cha ujauzito mwanamke huwa na uhitaji sana wa madini chuma...

Kwa kawaida madaktari hutoa prescription maalumu ya tembe za madini chuma na huwa ni kidonge kimoja kwa siku...

Onyo usinywe vidonge vya madini chuma pasipo ushauri wa daktari kwanza...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu asante kwa thread hii ukiyoianzisha..hakika ni msaada wa bure na wa kitaalamu..huwa Nina tatizo la tonsils tangu mdogo ...huwa tatizo linakuja na kutoweka.je nitumie dawa gani ili tatizo hili liishe?hapa SAA 8 hii uck nimebanwa haswa nimeamka nikameza panadol tu ila ucngz umegoma tangu SAA 6 na asbh natakiwa kibaruani.nitashukuru mku.

Mungu akubariki sana
 
aisee huu uzi umenikosha sana...

Naomba tu unisaidie nini madhara ya kutumia dawa kama FUROSEMIDE kwa muda mrefu.
 
Dr. Naomba ushauri kwenye bandiko hili!

Dr. Mke wangu hakuona siku zake na alipofanya 'pregnancy test' ilikuwa positive. Akashauriwa kutumia 'Misoprostal' vidonge vinne ambapo viwili alimeza na viwili alivitumbukiza ukeni. Usiku akaingia hedhi lakini damu ilitoka kwa kiwango kidogo sana. Baada ya siku 6 hivi akapima tena bado jibu likawa positive. Akatumia tena jana. Akaona tena hedhi damu ilikuwa nyingi kiasi lakini ilitoka kwa muda mfupi. Leo amefanya tena kipimo na jibu ni positive. Matukio yote haya yamefanyika ndani ya majuma mawili haya. Baada ya kuwasiliana na tabibu, pamoja na mambo mengine alimshauri kutumia tena lakini atumie wakati wa kulala.

Sasa, swali langu je ni ipi njia sahihi ya kutumia hizo dawa? Na, je, ni sawa akiirudia?

Natanguliza shukrani.

#Kaka
 
Habar yko dkt...? nina tatizo la kupata ganzi baadhi ya sehemu kwenye mwili wng,hususan kwenye sehemu za mikono,miguu na shingo!! naomba unijuze nn hasa chanzo cha tatzo hli?
 
Hello chasuzy!
  • Diabetes type 1 inasababishwa na mwili kutokuwa na production ya insulin,hali hii mtu anazaliwa nayo na inaweza kuwa genetic pia.Wagonjwa wa diabetes type 1 wanahitaji sindano za human insulin.Diabetes type 1 haina tiba unatakiwa uchome sindano ya insulin maisha yako yote.
  • Diabetes type 2 wanakuwa na production ya insulin lakini si ya kutosha.Kitu kingine ni insulin resistance( jinsi unavyokula vyakula vya sukari/unhealthy ndivyo mwili unajaribu kuproduce insulin ili kuvunjavunja hio sukari na baada ya muda kwasababu ya overproduction uzalishaji wa insulin inapungua),mapungufu ya insulin receptors,matatizo ya insulin binding au insulin receptor haipati signal za kutosha.Diabetes type 2 unaweza kupona ukibadili lifestyle kwa kula vyakula healthy,kufanya mazoezi,na kujitibu ipasavyo.Usipofata tiba kwa uyakinifu unaweza kupata complications kwenye viungo vingine kwasababu sukari inaathiri nerves na mishipa ya damu mfano ya macho, pia mafigo.Kitu kingine ni pia wenye diabetes type 2 wanaweza kuworsen na kwenda kwenye diabetes type 1 kwasababu uzalishaji wa insulin unapungua na hatimae kupotea kabisa.
  • Nimegusia complication za diabetes kuwa zinaweza kuathiri nerves na mishipa ya dam na inahusiana na mishipa ya uume, ya miguu na kusababisha (diabetic foot)-unakosa sense kwenye miguu kwa sababu nerves ziko damaged au kuathiri mishipa miyembamba ya dam ya macho na kupeleka kutokuona vizuri hatimae upofu.
  • Insulin ni hormone inayotengenezwa kwenye pancreas.Kwa lugha nyepesi naweza kusema ni ufungo kwasababu insulin inasafirisha sukari kutoka kwenye damu na kwenda kwenye cells za mwili.Na pia inavunjavunja glucose to glucagon.
View attachment 236428

Nashukuru sana kwa majibu ya ufasaha,nimekuelewa.Sasa naomba kujua tiba ya awali kwa mtu anayeanza kulipata hilo tatizo,yaani mfano leo sukari inakuwa juu kesho inakuwa chini,yaani ina-fluactate
 
Mkuu asante kwa thread hii ukiyoianzisha..hakika ni msaada wa bure na wa kitaalamu..huwa Nina tatizo la tonsils tangu mdogo ...huwa tatizo linakuja na kutoweka.je nitumie dawa gani ili tatizo hili liishe?hapa SAA 8 hii uck nimebanwa haswa nimeamka nikameza panadol tu ila ucngz umegoma tangu SAA 6 na asbh natakiwa kibaruani.nitashukuru mku.Mungu akubariki sana
Njia pekee ni kufanya operation ya kuondoa hizo tonsils….
 
aisee huu uzi umenikosha sana... Naomba tu unisaidie nini madhara ya kutumia dawa kama FUROSEMIDE kwa muda mrefu.
Madhara ya furosemid ni kusababisha electrolyte unbalance kwasababu inaongeza release ya sodium, potassium, chloride, calsium na magnesium.

Low levels za potassium ions zinaweza kusababisha matatizo kwenye rhythm ya moyo.Ni muhimu kupima serum levels ya potassium na kupatiwa potassium supplement ukitumia furosemid.
 
Mguu wa kulia una ganzi zaidi ya mwaka sasa..
1. Nini madhara ya ganzi kwa muda mrefu?
2. Tiba ni nini?
 
Nashukuru sana kwa majibu ya ufasaha,nimekuelewa.Sasa naomba kujua tiba ya awali kwa mtu anayeanza kulipata hilo tatizo,yaani mfano leo sukari inakuwa juu kesho inakuwa chini,yaani ina-fluactate
Tiba ya Diabetes type 2 ni vidoge.First choice ni Metformin/Glucophage:

Hii inashusha bloodglucose kwa kupunguza uzalishaji wa glucose kwenye ini na hatimae kupunguza release of glucose kwenye dam.Vilevile inasaidia glucose iende zaidi kwenye mifupa na zina effect tofauti kwenye triglycerides.

Kama upo overweight ni kawaida pia kupewa metformin.Sulphonylureas ni dawa nyingine inasaidia release ya insulin kutoka kwenye pancreas mfano wa dawa hizi ni glibenclamide, glimepiride.

Glitazones(thiazolidnediones) inasaidia bodycells ziwe sensitiv na insulin na zinasaidia realse ya insulin kama sulphonylureas.

Zipo pia dawa nyingine kama DPP-4-inhibitors(Gliptins)n.k
 
Back
Top Bottom