Nakumat yainunua Shoprite Tanzania

Nakumat yainunua Shoprite Tanzania

Naogopa kuchangia uzi huu lakini wacha nichangie tu haina jinsi, kama kweli Nakumat ni kutoka Kenya na kama kweli miongoni mwa sababu zilizochangia Shoprite kuondoka ni kwa sababu ya kuuza bidhaa kutoka South Africa. Sasa kwa Nakumat mtachemsha zaidi na zaidi maana mtakula kila kitu kutoka Kenya na mbaya zaidi hata wafagizi watatoka Kenya maana Kenya ni karibu watakuja hata kwa Dar express.Huniamini acha lakini nawajua sana Wakenya ni wabinafsi saana nakuambia

kaka mbona muoga sana kwani wakenya hawaruhusiwi kuajiriwa tanzania?? support local products ni moja ya vigezo vya nakumatt kupewa tenda so kwa hilo hata kama watapendelea bidhaa za kwako p[pia na za kwetu lazima waziuze
 
tatizo sisi pia hatuthamini vya kwetu kuna ndugu yangu alikuwepo finland amerudi mwezi uliopita ananiamia huko wafini wanajali sana vitu vya kwao sometimes huwa bidhaa zao huwa ni bei maradufu kuliko bidhaa zinnazotoka nje lakini wapo tayari wanunue bidhaa zao na sio za nje hawataki kumfaidisha wakuja burebure so hili la kuchgua bidhaa lingeanzia kwetu sio mtu eti unaenda shoprite kununua sijui nyanya na mboga wakati masokoni unaweza kupata hizo na tena zikiwa fresh.tusingekuwa tunanunua hizo mboga zao na nyanaya toka s.a sidhani kama wangeendelea kuzileta
Precisely the point unachosema, uzalendo unaimizwa kwa namna zingine nchi nyingi tu za europe uwa wana campign zao za support local farmers, produce na hata serikali zinatoa incentives sana kwa wakulima hili waweze endelea kulima na kufuga, lakini sera za kulazimishana kutumia products fulani bila ya kuzingatia gharama za mfanyabiashara ni ujuha hata wao wanajua ndio maana kuna sector zingine zina dorora ama kufa kabisa as in textile industry. Halafu hata huo uzalendo wa kununua bidhaa za kwenu kwa upendeleo ata kama bei ni za juu una depend na mfuko wa wananchi na how far kipato kinatimiza mahitaji mengine muhimu ya familia vinginevyo ni changamoto, huko Scandinavia wanaongoza kwa kuwa na kipato bora na maisha bora na idadi ndogo ya walalahoi ndio maana linawezekana.

Ngoja nitoe mfano mmoja korosho inayo limwa mtwara hadi kufika dar kipakti cha korosho ambayo imechomwa kienyeji kupitia mchanga, kuni/mkaa na karai na kufungwa kwenye kapakti kwa kuchomewa na kibatari kinauzwa na machinga sh.2500. Machinga alipi kodi ya ushuru, rent, umeme na gharama zingine za mwenye duka. Kipakti cha size hiyo hiyo UK kinauzwa 99p karibu paundi 1. Korosho ya dukani UK imetoka shambani huko ilipotoka mpaka port au kiwandani, imepitia industrial processes, mkulima uko kawekewa tax na yeye kaweka faida, mfanyabiasha uko kawekewa tax na yeye kaweka faida, ikapanda meli ikawekewa gharama, kufika UK tena ika wekewa tax na mwenye duka bado anaona kuna faida ya kuuza sawa na korosho ya Mtwara.

The point nayotaka toa kwanza inabidi waangalie environment inayomfanya mtu alete machungwa kutoka south africa in the first place. Tanzania gharama za chakula ni nafuu sana ukienda vijijini lakini ukianza gharama za usafirishaji, idadi ya walaji bei inabidi ziwe kubwa hili kuona faida au hata ku-break even maana wengi wetu ni wakulima. Vile vile technologia ambazo zinaweza fanya wingi wa industrial processes bado ndio maana gharama za kutoka shambani mpaka kwenye kopo zinakuwa juu na kufanya bidhaa ziwe juu kwa mlaji. Sasa supermarket ni tertiary sector wao wataangalia cheapest secondary environment hiko wapi na wanaokoa kiasi gani, lakini mtu awezi leta machungwa kutoka south afrika if it was cheap for him to buy locally independently, ujui on his bulk shipping anaokoa kiasi gani in short lazima tujue hesabu zao kabla ya kuwalaumu.

Mwisho swala la kununua shoprites lazima kwanza tuangalie wao kama biashara walikuwa wanamlenga nani na asilimia gani yetu. Mteja wa shoprite ni mtanzania yupi na mwenye kipato kipi, na kwanini aende hapo is it quality,convenience, trend shoppers, upmarket etc hili uweze hata sema ataleta impact gani kwa mkulima usije ukawa unamletea uhuni na fujo hili akachukue machungwa na mboga kwenye mashamba ya vigogo kadhaa tu, maana kwa shoprite hata kama watanunua machungwa na mboga za tanzania hawatakuwa na impact yeyote kwenye kilimo in general sana sana wataifaidika a handfull of farmers only.

Tuna environment ngumu sana kufanya biashara lakini the opportunity is vast in Tanzania tatizo ni capital, CDM vipi hawana hela za miradi nijiunge huko habari za siasa za mbele hazina mpango.
 
kaka mbona muoga sana kwani wakenya hawaruhusiwi kuajiriwa tanzania?? support local products ni moja ya vigezo vya nakumatt kupewa tenda so kwa hilo hata kama watapendelea bidhaa za kwako p[pia na za kwetu lazima waziuze

ndugu yangu Mndengereko mimi nawajua waKenya sana,hakuna cha local product wala nini bora tungeng'ang'ana na hao watoka mbali
 
Hapa hakuna vya local products wala nini,kwani bidhaa ngapi zinatoka Kenya zinauzwa hapa kwa bei rahisi kuliko zinazozalishwa hapa.Wakenya wamejipanga sana kwa hili.
Biashara hii ni huria na kuna sheria za biashara zakimataifa,na kwamba huwezi kumbana mtu kwa kiwango kikubwa kwamba lazima achukue bidhaa zako.We unashindwaje kufungua maduka yako na kuuza za kwako mpaka umlazimishe yeye auze zako wakati ubora wa kimatatifa nao pia tatizo.

Subiri hiyo NAKUMAtt Westgate mpya ifanye yake.
Hapa kama kweli wao wanataka watanzania wapige hatua kwa bidhaa zao basi wawavutia wawekezaji wa ndani wafungue Maduka makubwa kama hayo.Kwa nijuavyo mie kwa Historia ya nchi alietaka kujaribu ni marehem IMALASEKO tu.
 
Precisely the point unachosema, uzalendo unaimizwa kwa namna zingine nchi nyingi tu za europe uwa wana campign zao za support local farmers, produce na hata serikali zinatoa incentives sana kwa wakulima hili waweze endelea kulima na kufuga, lakini sera za kulazimishana kutumia products fulani bila ya kuzingatia gharama za mfanyabiashara ni ujuha hata wao wanajua ndio maana kuna sector zingine zina dorora ama kufa kabisa as in textile industry. Halafu hata huo uzalendo wa kununua bidhaa za kwenu kwa upendeleo ata kama bei ni za juu una depend na mfuko wa wananchi na how far kipato kinatimiza mahitaji mengine muhimu ya familia vinginevyo ni changamoto, huko Scandinavia wanaongoza kwa kuwa na kipato bora na maisha bora na idadi ndogo ya walalahoi ndio maana linawezekana.

Ngoja nitoe mfano mmoja korosho inayo limwa mtwara hadi kufika dar kipakti cha korosho ambayo imechomwa kienyeji kupitia mchanga, kuni/mkaa na karai na kufungwa kwenye kapakti kwa kuchomewa na kibatari kinauzwa na machinga sh.2500. Machinga alipi kodi ya ushuru, rent, umeme na gharama zingine za mwenye duka. Kipakti cha size hiyo hiyo UK kinauzwa 99p karibu paundi 1. Korosho ya dukani UK imetoka shambani huko ilipotoka mpaka port au kiwandani, imepitia industrial processes, mkulima uko kawekewa tax na yeye kaweka faida, mfanyabiasha uko kawekewa tax na yeye kaweka faida, ikapanda meli ikawekewa gharama, kufika UK tena ika wekewa tax na mwenye duka bado anaona kuna faida ya kuuza sawa na korosho ya Mtwara.

The point nayotaka toa kwanza inabidi waangalie environment inayomfanya mtu alete machungwa kutoka south africa in the first place. Tanzania gharama za chakula ni nafuu sana ukienda vijijini lakini ukianza gharama za usafirishaji, idadi ya walaji bei inabidi ziwe kubwa hili kuona faida au hata ku-break even maana wengi wetu ni wakulima. Vile vile technologia ambazo zinaweza fanya wingi wa industrial processes bado ndio maana gharama za kutoka shambani mpaka kwenye kopo zinakuwa juu na kufanya bidhaa ziwe juu kwa mlaji. Sasa supermarket ni tertiary sector wao wataangalia cheapest secondary environment hiko wapi na wanaokoa kiasi gani, lakini mtu awezi leta machungwa kutoka south afrika if it was cheap for him to buy locally independently, ujui on his bulk shipping anaokoa kiasi gani in short lazima tujue hesabu zao kabla ya kuwalaumu.

Mwisho swala la kununua shoprites lazima kwanza tuangalie wao kama biashara walikuwa wanamlenga nani na asilimia gani yetu. Mteja wa shoprite ni mtanzania yupi na mwenye kipato kipi, na kwanini aende hapo is it quality,convenience, trend shoppers, upmarket etc hili uweze hata sema ataleta impact gani kwa mkulima usije ukawa unamletea uhuni na fujo hili akachukue machungwa na mboga kwenye mashamba ya vigogo kadhaa tu, maana kwa shoprite hata kama watanunua machungwa na mboga za tanzania hawatakuwa na impact yeyote kwenye kilimo in general sana sana wataifaidika a handfull of farmers only.

Tuna environment ngumu sana kufanya biashara lakini the opportunity is vast in Tanzania tatizo ni capital, CDM vipi hawana hela za miradi nijiunge huko habari za siasa za mbele hazina mpango.
nimekupata vyema mkuu.
 
Hawa Nakumat Bei zao si mchezo, yaani ukiringanisha na shoprite basi utaona kama vile shoprite walikuwa wanauza kwa hasara, Hawa wahindi wao wanalenda watu wa daraja la juu, Bidhaa zao huwa ni ghari mno, Pale moshi naona siku hizi wanaingia wazungu tu, wachaga wanaishia kwa Mangi na kwa Kimario, Tehe tehe
 
Hapa hakuna vya local products wala nini,kwani bidhaa ngapi zinatoka Kenya zinauzwa hapa kwa bei rahisi kuliko zinazozalishwa hapa.Wakenya wamejipanga sana kwa hili.
Biashara hii ni huria na kuna sheria za biashara zakimataifa,na kwamba huwezi kumbana mtu kwa kiwango kikubwa kwamba lazima achukue bidhaa zako.We unashindwaje kufungua maduka yako na kuuza za kwako mpaka umlazimishe yeye auze zako wakati ubora wa kimatatifa nao pia tatizo.

Subiri hiyo NAKUMAtt Westgate mpya ifanye yake.
Hapa kama kweli wao wanataka watanzania wapige hatua kwa bidhaa zao basi wawavutia wawekezaji wa ndani wafungue Maduka makubwa kama hayo.Kwa nijuavyo mie kwa Historia ya nchi alietaka kujaribu ni marehem IMALASEKO tu.

Mkuu ni kweli Pale Moshi wapo tiyari na Bidhaa karibia zote ni za Kenya, na wanauza bei za kufa mtu huwezi walinganisha na Shoprite kwa bei
 
Asije mtu akaingia kwenye hayo maduka ni maadui wa Alshahabab.
 
Hao Nakumatt tatizo lao ni wale wakenya waliopo humo hutongoza sana wafanyakazi maana nimewahi kusoma humu jaffari taarifa yao hadi nikachoka akili.
 
Nakumat wakoo vizuri tumeona bidhaa na bei zao shindani sana, bei za kawaida mno. Ngoja wafike kipande hii tuone. Tunategemea tofauti kubwa kulinganisha na shoprite
 
tutashukuru kama watathamini products za nyumbani. TSN supermarket wanajitahidi kwa hili.
 
Nakumat nawakubali kwani vitu vyao ni vya high quality ukilinganisha na vya kichina vinavyouzwa na Shoprite. ukiingia pale Moshi mjini kwenye duka lao kuna vitu vizuri na vya quality pamoja na bei reasonable sana
 
Natafuta kazi ya suppermarket lakini sijui ni ipi ambayo ni nzuri kwa maslahi kati ya hizo tatu. Msaada wenu please!
 
Natafuta kazi ya suppermarket lakini sijui ni ipi ambayo ni nzuri kwa maslahi kati ya hizo tatu.

Msaada wenu please!
 
Natafuta kazi ya suppermarket
lakini sijui ni ipi ambayo ni nzuri
kwa maslahi kati ya hizo tatu.
Msaada wenu please!


Kwani kutafuta kazi ndio kupata? Nenda katafute kwanza ukikubaliwa kote ndio uje kuuliza ili uchague.
 
Back
Top Bottom