Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Hii nchi kuna mambo mengi hufanyika bila kufikiria mbele. Leo tunakimbizwakimbizwa kwa ajili ya kitambulisho cha NIDA. Lakini kwa mujibu wa sheria ya utambulisho wa uraia, kadi/namba ya NIDA ndio kithibitisho pekee halali cha uraia wa mtanzania; yaani aliyesajiliwa NIDA ndo anatambulika kisheria kuwa ni raia wa Tanzania.

Wakati NIDA hutumia alama za vidole (fingerprint) katika kusajili raia, juzi tu hapa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imetanganza kufanya maandalizi ya kuanzisha kanzidata ya taifa ya vinasaba (National Centre for Human DNA Database). Kanzidada hii itatumika katika utambuzi wa watu/raia na kwamaana hiyo kanzidata hii itaunganishwa na za mamlaka zingine hasa zile za NIDA kuboresha utambuzi wa raia.

Biometria ya alama za vidole (fingerprint) inayotumiwa na NIDA ina mapungufu ukilinganisha na ile ya vinasaba (DNA fingerprint). Mathalani, fingerprint haiwezi kuonesha uhusiano (unasaba) wa ndugu wa karibu (closely related individuals). Zaidi, fingerprint haiwezi kutumia sampuli ya mwili ulioharibika kubaini utambulisho wa mwenye huo mwili au ndugu yake wa karibu.

Ingawa fingerprint ni biometria ya haraka, isiyo na gharama kubwa na haihitaji mtaalamu katika ukusanyaji wake, haikupaswa kutumiwa na NIDA kutokana na udhaifu wake kama ulivyooneshwa hapo juu na badala yake mamalaka hiyo ingetumia DNA profiles za watu zitazoandaliwa na GCLA. Hii ni kwasababu moja ya masharti ya NIDA ni muombaji usajili kutoa uthibitisho wa "makaratasi" kuonesha uraia au asil ya wazazi wake kwasbabu makaratasj hayo yanaweza kuwa na taarifa za uwongo hata kama zinatolewa na mamlaka halali kama vile RITA au Mahakama/Wakili.

Wasiwasi uliopo ni kwamba hapo baadae kutakuwa na usumbufu kwa raia kwasabu kanzidata ya DNA profile zitakazozoandaliwa na GCLA zitakinzana na taarifa za uhusiano (nasaba) za mzazi na mwanawe zinazokusanywa leo na NIDA kwa kutumia ushahidi wa "makaratasi". Je, ikitokea DNA profile ya raia X hairandani na ya mzazi wake (raia Y) aliyemtaja kwenye taarifa za NIDAQ

Utaandika sana kutetea lakini nakuhakikishia kuwa hakuna taarifa mpya katika usajili wa NIDA ambayo haikuhusika kwenye passport au leseni ya udereva. Naona unajaribu kusisitiza "nguvu" ya cheti cha kuzaliwa katika kuthibitisha uraia, lakini kumbuka kwenye cheti hicho kuna maandishi madogo yanasmomeka "cheti cha kuzaliwa sio uthibitisho wa uraia".

Kwa taarifa yako affidavity hutumika pia na NIDA kama mbadala wa cheti cha kuzaliwa kwa mtu asiye nacho. Lakini unaposema postal code si lolote bali ni anwani ya makazi ambayo kwenye kwenye fomu za maombi ya passport pia huhitajika.
This is mature argument.
Shukrani mkuu, nakuunga mkono 95% hoja yako.
 
Hii nchi kuna mambo mengi hufanyika bila kufikiria mbele. Leo tunakimbizwakimbizwa kwa ajili ya kitambulisho cha NIDA. Lakini kwa mujibu wa sheria ya utambulisho wa uraia, kadi/namba ya NIDA ndio kithibitisho pekee halali cha uraia wa mtanzania; yaani aliyesajiliwa NIDA ndo anatambulika kisheria kuwa ni raia wa Tanzania.

Wakati NIDA hutumia alama za vidole (fingerprint) katika kusajili raia, juzi tu hapa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imetanganza kufanya maandalizi ya kuanzisha kanzidata ya taifa ya vinasaba (National Centre for Human DNA Database). Kanzidada hii itatumika katika utambuzi wa watu/raia na kwamaana hiyo kanzidata hii itaunganishwa na za mamlaka zingine hasa zile za NIDA kuboresha utambuzi wa raia.

Biometria ya alama za vidole (fingerprint) inayotumiwa na NIDA ina mapungufu ukilinganisha na ile ya vinasaba (DNA fingerprint). Mathalani, fingerprint haiwezi kuonesha uhusiano (unasaba) wa ndugu wa karibu (closely related individuals). Zaidi, fingerprint haiwezi kutumia sampuli ya mwili ulioharibika kubaini utambulisho wa mwenye huo mwili au ndugu yake wa karibu.

Ingawa fingerprint ni biometria ya haraka, isiyo na gharama kubwa na haihitaji mtaalamu katika ukusanyaji wake, haikupaswa kutumiwa na NIDA kutokana na udhaifu wake kama ulivyooneshwa hapo juu na badala yake mamalaka hiyo ingetumia DNA profiles za watu zitazoandaliwa na GCLA. Hii ni kwasababu moja ya masharti ya NIDA ni muombaji usajili kutoa uthibitisho wa "makaratasi" kuonesha uraia au asil ya wazazi wake kwasbabu makaratasj hayo yanaweza kuwa na taarifa za uwongo hata kama zinatolewa na mamlaka halali kama vile RITA au Mahakama/Wakili.

Wasiwasi uliopo ni kwamba hapo baadae kutakuwa na usumbufu kwa raia kwasabu kanzidata ya DNA profile zitakazozoandaliwa na GCLA zitakinzana na taarifa za uhusiano (nasaba) za mzazi na mwanawe zinazokusanywa leo na NIDA kwa kutumia ushahidi wa "makaratasi". Je, ikitokea DNA profile ya raia X hairandani na ya mzazi wake (raia Y) aliyemtaja kwenye taarifa za NIDAQ

Utaandika sana kutetea lakini nakuhakikishia kuwa hakuna taarifa mpya katika usajili wa NIDA ambayo haikuhusika kwenye passport au leseni ya udereva. Naona unajaribu kusisitiza "nguvu" ya cheti cha kuzaliwa katika kuthibitisha uraia, lakini kumbuka kwenye cheti hicho kuna maandishi madogo yanasmomeka "cheti cha kuzaliwa sio uthibitisho wa uraia".

Kwa taarifa yako affidavity hutumika pia na NIDA kama mbadala wa cheti cha kuzaliwa kwa mtu asiye nacho. Lakini unaposema postal code si lolote bali ni anwani ya makazi ambayo kwenye kwenye fomu za maombi ya passport pia huhitajika.
Mkuu lazima kuwe na mahali pa kuanzia hiyo nia njema.
Wewe umekuja na hoja nyingine nzuri sana ya DNA, na vizuri umesema mwenyewe DNA ni gharama kubwa kuliko fingerprints.
Na hali yetu ya kiuchumi unaijua ukizingatia gharama za kupima au kuchukua cha sample za DNA kwa kila raia.

Lazima tuwe na via umbel na tujikune tunapofikia.
 
Nimepotosha nini wakati passport za zamani hata usipokuwa na cheti cha kuzaliwa uliruhusiwa kutumia affidavit.
Kama uliwahi kumiliki passport ya zamani na uliifuatilia mwenyewe bila kutoa chochote na kuletewa nyumbani kama ambavyo leseni za udereva hizi mpya na za zaman, ilikuwa unaweza toa pesa elfu kumi kadhaa zaidi ya malipo halali unaletewa bar au nyumbani hata bila kwenda driving school.

Labda nikuulize uliwahi kumiliki hiyo pass ya zamani?
Ulisoma au kuuliza mashariti ya kuipatampale kwenye viambatanisho?

Je ni kosa la serikali kwa baadhi ya watu kutofuatilia kumiliki cheti cha kuzaliwa wakati kila wilaya vinatolewa hukohuko hata kama umezaliwa porini?
Kaka huwa unasafiri kwenda vijini? Unaufahamu ukubwa wa hii nchi na umbali wa baadhi ya vijiji kutoka wilayani?
 
Kaka huwa unasafiri kwenda vijini? Unaufahamu ukubwa wa hii nchi na umbali wa baadhi ya vijiji kutoka wilayani?
Kaka miaka zaidi ya miaka 40 unashindwa kwenda wilayani mara mbili tu kufuatilia cheti cha kuzaliwa?
Kama unaweza kumiliki simu unakosa nauli ya bodaboda ya kwenda na kurudi mara mbili tu ktk miaka angalau 5 tu?

Wale masikini wasiokuwa na uwezo wa kununua hata simu siwalaumu inawezekana kukwama nauli.
 
Umeandika kwenye mada yako;
''Wenye akili wameshasoma mchezo, kuna kitu kinatafutwa hapo, kwa sababu fingerprints Tayari watu walishachukuliwa kwenye Vitambulisho vya kura na Driving Licence,sasa kuna haja gani ya kutesa watu kiasi hiki?''.

Ni kitu gani kinachotafutwa? Naomba unielimishe!

Nimekuomba unielimishe kwa sababu kwa sasa hapa Jamiiforums kumejitokeza baadhi ya wanachama ambao wanadhani hisia zao ndio ukweli lakini kibaya zaidi wanataka kuwalazimisha na watu wengine kwa hoja za nguvu waamini hisia zao!
Hata yeye hajui kinachotafutwa; labda kwa vile hakuweka tu alama ya kuuliza mwisho wa maneno aliyoandika.
Lakini hoja yake inajieleza vizuri nawe ungeelewa kuwa hata yeye hajui kinachotafutwa. Kisingekuwepo kinachotafutwa haya yanayofanyika yasingekuwepo.

Sasa kama wewe unajua, eleza, na sio kumuuliza anayetafuta jibu.

Kama huna jibu juu ya hilo, labda tueleze gharama zinazoambatana na usajiri huu. Kila sehemu iliyohitaji alama za vidole, watu wamesajiriwa kwa gharama kadhaa, na sasa gharama juu ya hizo inaendelea kurundikwa. Je huu sio ufujaji wa mali?

Au kuna hela ya uchaguzi inatafutwa hapa? Hili ni swali, kama una jibu unaweza pia ukaeleza.

Kwanza gharama zote hazijulikani tokea huko mwanzo. Hizi zitatangazwa tujue ni kiasi gani kimetumika katika zoezi la marudio yale yale yaliyokwishafanyika?
 
Sijui kama unajua utaratibu wa kupata passport mpya?!
Huwezi kupata bila kitambulisho cha taifa.

Passport ya zamani ilikuwa inatolewa bila kukidhi vigezo vya cheti cha kuzaliwa maaana walikuwa wanapokea hadi affidavit ambayo nimeeleza udhaifu wake.

Jambo jingine hizo passport za zamani kulikuwa na mapungufu ya ukusanyaji taarifa za anuani za makazi.
Hakukuwa na kigezo cha kuweka nambari au kitalu cha nyumba unayo ishi.

Hiki kitambulisho cha NIDA kimekuja kuunganisha na utambuzi wa anuani za makazi ktk mfumo wa Postal code, ndio zile namba nne za mwisho za kwenye kitambulisho cha NIDA.

Nadhani kwa haya machache utakuwa umeelewa na kujifunza kitu.
CC: Pascal Mayalla , My Son drink water TUJITEGEMEE
Naunga mkono hoja
P
 
Hivi idara ya uhamiaji wana hakiki au wana gonga muhuri tu. Hivi wana nyenzo gani wanatumia kutambua huyu ni mtanzania au siyo?

Kuhusu affidavity hata sasa zinatumika. By the way ni nyumba ngapi zina namba? 90% ya wakazi wa dar wanahama hama kila siku, hivi mtu anapo hama taarifa zake za makazi huko NIDA pia zinabadilika?

Mtoa mada yuko sahihi, serikali haijajipanga na inatumia resources vibaya. Information must be captured and stored once...
hapo taget ni wapiga kura tu
 
Kigezo ni kimmoja kimataifa ni ID ya taifa.
Tokea uhuru jambo hilo ilipuuzwa.Japo Kenya ilikuwa inatoa ID.
ID inaweka msukumo wa kuwa na cheti cha kuzaliwa.
ID inatumika kupewa Passport, ajira, mikopo,kupiga kura,driving license, dhamana,bima,hati za mali,kufunga ndoa,kufungua account bank n.k
Takwimu zake ni kiunganisho cha mtu kutambuliwa kitaifa hadi kimataifa.
Serikali itaendelea kubeba lawama kwa kupuuza ID kwa muda mrefu bila sababu ya msingi.
Japo tunaambiwa ni zoezi endelevu ni ukweli usiopingika kuwa NIDA haina nyenzo,watu,fedha za kutosha.Ilitakiwa Marshall Plan.NIDA ina umuhimu hata kuliko kuhamisha makao makuu kwenda Dodoma.
Historia itawahukumu.
CCM imetiliya mkazo ili ipate kuiba kura tu.
 
Ok' huenda kama taifa watawala wanahitaji information zetu zifahamike, tunafanya nn? Wapi? Na nani?. Tatizo ni hiyo deadline. Why? Kwann usingetafutwa mfumo endelevu urenew kwa mfumo huo wa vidole? Kwann tukimbizane na deadline? Line mpya zingeweka na mfumo wa vidole, mtu akipoteza mfumo wa vidole utumike kurenew, mtu akihitaji msaada basi aambiwe sajili kwa mfumo kwanza ndo usaidike, taratibu mpaka wote wanasajili. Sasa speed yote ya nini?
ukiwa huna ID hupigi kura hapo ndio CCM wanapopataka.
 
Mbona unadabili gia angani?
Madai yako hasa ni kuhusu vitambulisho vya NIDA? Au vitambulisho vya mpiga kura?
Maelezo yako ya awali ni kuhusu kutokuwa na umuhimu wa vitambulisho vya NIDA, ukapewa umuhimu wake umekuja na hoja nyingine kabisa ambazo kiujumla tunaweza kusema ni maboresho ya daftari la mpiga kura.

Na huku sasa ndio vijana wanaita kuhamisha magoli baada ya kubanwa na kukosa hoja kwenye malamiko yako ya awali.

Sasa turudi kwenye malalamiko yako ya uboreshaji daftari la mpiga kura, nikimaanisha hayo yote ya kudhibiti udanganyifu kwenye vitambulisho vya mpiga kura, kimsingi nakubaliana na wewe, tena ongeza na madai ya tume huru ya uchaguzi.

Kwenye siasa tubaki na siasa ila kwenye mambo ya kitaaluma kama ya kiusalama tujenge hoja au kukosoa au kushauri kama tuna uelewa mpana wa jambo husika, au kama hiyo ndiyo taaluma yetu.
Mzee bongo mambo yote ni ya siasa hakuna jambo ambalo halihusu siasa CCM ni siasa kwenda mbele wao wanalolijuwa ni kubaki madarakani kwa vyovyote tu
 
Hili suala la simcard limethibitisha tusivyo na akili za kusolve matatizo yetu...
Hivyo nakuunga mkono kama umelifikisha mahakamani
 
technically ni wakati wa kupeana mrishonyuma. Mahakamani umeenda kufungua kesi?
Kinachoendelea kwa Sasa Ni uhakiki wa taarifa kuendana law amendment iliyopitishwa na bunge tarehe 6 September 2019 ya sheria namba 306 ibara 93 ibara ndogo ya 2 inayomtaka kila mtoa huduma ya mtandao kuhakiki taarifa za mtu waliyemmilikisha SIM card,
 
Na sheria haisemi wazi Kama Ni taarifa za nida, vivyo mie bado naamini taarifa Ni zile kulingana na jedwali namba 4 la sheria mama, hivyo kufungua sim card simply hakuna taarifa za nida naona sio sahihi
 
Kinachoendelea kwa Sasa Ni uhakiki wa taarifa kuendana law amendment iliyopitishwa na bunge tarehe 6 September 2019 ya sheria namba 306 ibara 93 ibara ndogo ya 2 inayomtaka kila mtoa huduma ya mtandao kuhakiki taarifa za mtu waliyemmilikisha SIM card,
Technically alisema ana mawakili "elfu" na leo Jumatatu atafungua kesi dhidi ya serikali kwa kuwafungia laini za simu ambao hawajasajiliwa kwa namba za NIDA. Ndio namuulizia. Wewe una taarifa zozote za technically kufungua hiyo kesi?
 
Back
Top Bottom