Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Nakusudia kuishtaki Serikali (TCRA) kuzima Simcard za wateja wa mitandao

Wewe nawe hakuna ulichokiandika hapa ila ni kuthibitisha "maajabu" ya watanzania kama mtoa mada anavyopata tabu kutuelewa.

Unaposema kitambulisho cha mpiga kura hakikuhusisha uhakiki wa uraia maana yake ni sawa na kusem "anayestahili kupiga kura si lazima awe raia bali ni mtu yeyote anayejiandikisha". Je, katiba ndo inaelekeza hivyo? Je, kushindwa kufanya ukakiki wa uraia wa mpiga kura sio uzembe?

Je kutoa hati za kusafiria (passport) bila uhakiki wa raia sio maajabu? Au unataka kutuambia hakuna mtu asiye raia wa Tanzania mwenyekuweza kumiliki kitambulisho cha NIDA?

Aliyetoa mada hii ana akili kubwa kuliko zako.
Passport, leseni, kitambulisho cha kura kwa sasa ni vitambulisho vinavyozarauliwa na utawala huu, ni vioja kwani hakuna Taifa Duniani kote linaweza kuvidharau hivyo vitambulisho kama Tanzania, ni Aibu kusajili line kwa kutumia kitambulisho kimoja pekee kisicho na Tin number zaidi ya kumbukumbu za kawaida tu.
 
Jitafakari ulicho andika!!
Kitambulisho cha NIDA ni mradi ulioanza kabla ya Magufuli kuwa raisi wa JMTZ.
Wala yeye sie alie agiza au kuidhinisha mradi huo.
Passport na leseni na kitambulisho cha kura siyo vitambulisho? Kwa nini havitumiki kusajili Line? NIDA kuanza zamani kipindi cha kikwete ina uhusiano gani na kudharau vitambulisho vingine?
 
Passport na leseni na kitambulisho cha kura siyo vitambulisho? Kwa nini havitumiki kusajili Line? NIDA kuanza zamani kipindi cha kikwete ina uhusiano gani na kudharau vitambulisho vingine?
Ungesoma comment yake na yangu ungeelewa what is the connection, And if you don't see the connection then I can not help you.
 
Vipi passport ya kusafikiria ambayo inatolewa na uhamiaji leo ukienda kusajilia laini au kununulia laini mpya wanakataa ..


Nipe majibj..

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui kama unajua utaratibu wa kupata passport mpya?!
Huwezi kupata bila kitambulisho cha taifa.

Passport ya zamani ilikuwa inatolewa bila kukidhi vigezo vya cheti cha kuzaliwa maaana walikuwa wanapokea hadi affidavit ambayo nimeeleza udhaifu wake.

Jambo jingine hizo passport za zamani kulikuwa na mapungufu ya ukusanyaji taarifa za anuani za makazi.
Hakukuwa na kigezo cha kuweka nambari au kitalu cha nyumba unayo ishi.

Hiki kitambulisho cha NIDA kimekuja kuunganisha na utambuzi wa anuani za makazi ktk mfumo wa Postal code, ndio zile namba nne za mwisho za kwenye kitambulisho cha NIDA.

Nadhani kwa haya machache utakuwa umeelewa na kujifunza kitu.
CC: Pascal Mayalla , My Son drink water TUJITEGEMEE
 
Umepotosha kuwa mtu hakutakiwa kuwasilisha cheti cha kuzaliwa. Hata sasa hivi si kila Mtanzania ana cheti cha kuzaliwa.
Nimepotosha nini wakati passport za zamani hata usipokuwa na cheti cha kuzaliwa uliruhusiwa kutumia affidavit.
Kama uliwahi kumiliki passport ya zamani na uliifuatilia mwenyewe bila kutoa chochote na kuletewa nyumbani kama ambavyo leseni za udereva hizi mpya na za zaman, ilikuwa unaweza toa pesa elfu kumi kadhaa zaidi ya malipo halali unaletewa bar au nyumbani hata bila kwenda driving school.

Labda nikuulize uliwahi kumiliki hiyo pass ya zamani?
Ulisoma au kuuliza mashariti ya kuipatampale kwenye viambatanisho?

Je ni kosa la serikali kwa baadhi ya watu kutofuatilia kumiliki cheti cha kuzaliwa wakati kila wilaya vinatolewa hukohuko hata kama umezaliwa porini?
 
Nchi ya majuha hii jamaa yupo sahihi kabisa, punguzeni uccm jadilini mada

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wewe hapa ndio umejadili nini?
Je mimi nimejadili nini?
Yupo sahihi kwa jambo gani kati ya aliyosema au aliyo lalamikia?

Weka hoja yako basi utuoneshe wewe sio juha kwa kudhania mtu yeyote anaye pinga kuilaumu serikali vitu kwa hoja potofu ni CCM?
Usipoweka hoja zako kutetea hoja za mleta mada wewe ndio utaonekana ni juha na sio unao watuhumu.
 
Nimepotosha nini wakati passport za zamani hata usipokuwa na cheti cha kuzaliwa uliruhusiwa kutumia affidavit.
Kam uliwahi kumiliki passportya zamani na uliifuatlia mwenyewe bila kutoa chochote na kuletewa nyumbani kama ambavyo leseni za udereva hizi mpya na zamani ulivyo kuwa unatoa pesa elfu kumi kadhaa zaidi ya malipo halali unaletewa bar au nyumbani hata bila kwenda driving school.

Labda nikuulize uliwahi kumiliki hiyo pass ya zamani?
Ulisoma au kuuliza mashariti ya kuipatampale kwenye viambatanisho?

Je ni kosa la serikali kwa baadhi ya watu kutofuatilia kumiliki cheti cha kuzaliwa wakati kila wilaya vinatolewa hukohuko hata kama umezaliwa porini?

Vyeti vya kuzaliwa vilianza kutolewa lini kwani?
 
Vyeti vya kuzaliwa vilianza kutolewa lini kwani?
Kaulize RITA,
Kwa kukusaidia tu vilianza kutolewa miaka mingi sana zaidi ya miaka 45 iliyopita.
Sasa sijui hao ambao hawana miaka yote hii serikali iwasaidiaje?
Inaonekana hao hata ukiwaacha bila kuwalazimisha kama sasa wanaweza kumaliza miaka 45 mingine bado hawajafuatilia vyeti vyao vya kuzaliwa.
 
Sijui kama unajua utaratibu wa kupata passport mpya?!
Huwezi kupata bila kitambulisho cha taifa.

Passport ya zamani ilikuwa inatolewa bila kukidhi vigezo vya cheti cha kuzaliwa maaana walikuwa wanapokea hadi affidavit ambayo nimeeleza udhaifu wake.

Jambo jingine hizo passport za zamani kulikuwa na mapungufu ya ukusanyaji taarifa za anuani za makazi.
Hakukuwa na kigezo cha kuweka nambari au kitalu cha nyumba unayo ishi.

Hiki kitambulisho cha NIDA kimekuja kuunganisha na utambuzi wa anuani za makazi ktk mfumo wa Postal code, ndio zile namba nne za mwisho za kwenye kitambulisho cha NIDA.

Nadhani kwa haya machache utakuwa umeelewa na kujifunza kitu.
CC: Pascal Mayalla , My Son drink water TUJITEGEMEE
Hivi una akili kweli wewe ??? Mbona Kuna watu mnaandika ujinga mpaka mtu anatamani atapike ... Hivi hii nchi imerogwa kweli !!!


Tangu nchi hii imepata Uhuru Leo ndio nasikia idara ya uhamiaji ilikuwa inatoa passport bila anuani ... We Ni kichaa sio bure ukute Ni baba mtu mzima na una watoto ila kichwani ni tabulasa ...

Hivi unaelewa maana na nguvu ya affidavid ??? Inakuaje leo mnaona affidavit eti Ni ujinga ...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaulize RITA,
Kwa kukusaidia tu vilianza kutolewa miaka mingi sana zaidi ya miaka 45 iliyopita.
Sasa sijui hao ambao hawana miaka yote hii serikali iwasaidiaje?
Inaonekana hao hata ukiwaacha bila kuwalazimisha kama sasa wanaweza kumaliza miaka 45 mingine bado hawajafuatilia vyeti vyao vya kuzaliwa.

Nikaulize RITA wakati umejinasibu ujuaji wa hizo habari? Nakupa formula rahisi. Kila mtu (Mtanzania) ambae hana makovu ya chanjo za ndui, ukoma na kifaduro hawezi kuwa na cheti cha kuzaliwa. Serikali zilizopita ambako zilikuwa na watu wengi wenye akili timamu na competent (awamu ya tatu na kurudi nyuma) walilijua hilo. Ndio maana kukawa na umuhimu wa kutumia affidavit. Na wenye umri huo bado wapo.
 
Mkuu pamoja na ukweli uliosema, makazi iwe mjini au kijijini sio taarifa ya kudumu.
Ni kweli sio makazi ya kudumu na ndio maana kwa kulitambua jambo hilo serikali imeweka ukomo wa tarehe ya matumizi ya kitambulisho cha NIDA ili unapokwenda kuomba tena kipya uweze kubadili baadhi ya taarifa zilizo badilika kama makazi.

in fact kam ulikuwa unafuatilia mijadala ya wakati wa kutoa elimu juu ya vitambulisho hivi kabla ya mradi kuanza walisema kusudio ni kuwa ukibadili makazi ukaripoti NIDA waweze kubadili taarifa zako za makazi.

Kwa kukusaidia tu, zile namba au tarakimu nne za mwisho za namba ya kitambulisho chako cha NIDA ni physical address ya mtaa au kijiji unachoishi. Hivi vitambulisho vimekuja kuimarisha na kampeni ya anuani za makzi sio aduani za postal zile logical address( post office box au P.O.Box).
Lengo tutumie mfumo wa anuani kama wenzetu ulaya na Amerika unaletewa barua au mzigo wako hadi mlangoni kwako.

Watu wengi kwa kutojuwa haya mambo mazuri yaliyo ktk mipango ya baadae huja kulalamika ovyo.
 
Hivi una akili kweli wewe ??? Mbona Kuna watu mnaandika ujinga mpaka mtu anatamani atapike ... Hivi hii nchi imerogwa kweli !!!


Tangu nchi hii imepata Uhuru Leo ndio nasikia idara ya uhamiaji ilikuwa inatoa passport bila anuani ... We Ni kichaa sio bure ukute Ni baba mtu mzima na una watoto ila kichwani ni tabulasa ...

Hivi unaelewa maana na nguvu ya affidavid ??? Inakuaje leo mnaona affidavit eti Ni ujinga ...

Sent using Jamii Forums mobile app
Umemaliza kunitukana?
kama bado niongezee na matusi mengine tena mazito ya nguoni au nitukanie hadi wazazi ili ufurahi na hoja yako iweze kueleweka vizuri zaidi kuliko hoja yangu.

Ukimaliza kunitukana matusi yote mazito niambie tuanze ujadili hoja kama watu wazima wenye elimu angalau ya msingi.
 
Nikaulize RITA wakati umejinasibu ujuaji wa hizo habari? Nakupa formula rahisi. Kila mtu (Mtanzania) ambae hana makovu ya chanjo za ndui, ukoma na kifaduro hawezi kuwa na cheti cha kuzaliwa. Serikali zilizopita ambako zilikuwa na watu wengi wenye akili timamu na competent (awamu ya tatu na kurudi nyuma) walilijua hilo. Ndio maana kukawa na umuhimu wa kutumia affidavit. Na wenye umri huo bado wapo.
Hakiki taarifa zako usiamini habari za vijiweni.
Miaka 45 iliyopita ni mwaka 1975 tu hapo ambapo kuna watu wamezaliwa kabla ya hapo wana vyeti vya kuziliwa.

Unavyo onesha hauna taarifa sahihi unabishana kama kijiwe cha kahawa haujuwi kama hata mzee wamiaka 70 au zaidi anaweza kwenda wilayani kwake au pale RITA hata kesho na kuomba cheti cha kuzaliwa atahojiwa na kuombwa nyaraka flani kisha anapewa cheti chake muda mfupi tu, kama akiombea RITA anapata ndani ya siku 4 hadi 14.

Na utaratibu huo upo miaka mingi tu toka enzi zaawamu zingine.

Sitakujibu tena sababu naona wewe hujui na unahisi unajua unaanza kubishana nahisi hutaki kujua unanipotezea muda tu.
Samahani lakini kama kauli zangu nimekukosea na kukukwaza.
Kam upo Tanzania sas nakutakia usiku mwema mkuu wangu.
 
Wewe nawe msahaulifu mkubwa zaidi.
Umesahau wakati wa vitambulisho vya mpiga kura au leseni ya udereva hakukuwa na uhakiki/usahili wa idara ya uhamiaji kujiridhisha uraia wa muombaji.
Umesahau ktk vitambulisho vya kura hakukuwa na uwasilishaji cheti cha kuzaliwa.

Umesahau passport za zamani ilikuwa sio lazima upeleke cheti cha kuzaliwa, kuna waliopeleka affidavit tu ambazo ni rahisi kughushi(forge), unaenda na mtu yeyote mahakamani au kwa mwanasheria unasema alikuwepo nilipozaliwa kisha unalipia stamp duty haifiki mwekundu wa msimbazi mmoja au balimi 5.

Umesahau wakati wa vitambulisho vya wapiga kura haikuwa lazima kutambuliwa nambari ya nyumba au kitalu kwa wakazi wa mijini ambako wageni ni wengi.

#Ujuaji mwingi mbele giza.
#Waacheni wenye wajibu na taaluma zao wafanye kazi zao kitaalamu, sio kila kitu siasa.
NIDA ya wapi huko wanataka kadi za kuzaliwa pamoja na hakiki za idara ya uhamiaji?
Mimi nina rafiki zangu vyeti vya kuzaliwa hawajui hata vinafananaje na wamepata hayo makolokolo ya Nida.
.
Lengo la serikali ni kusumbua watu na hidden agenda yao imeshafahamika mimi kama nilitumia kitambulisho cha kura kufanya usajil wa laini zangu na bado naibia watu mitandaoni mmeshindwa kunidhibiti kwa kitambulisho cha NIDA mtawezaje?
.
Vyeti vya kuzaliwa havina taarifa za kuaminika hata kidogo, nitakupa mfano hai mimi katika cheti changu cha kuzaliwa kinasoma taarifa za uongo kwa maslahi yangu binafsi tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa sio uhalisia wangu, uhamiaji uliowasema ambao kimsingi hawako ni rahisi kuwaongopea ninavyotaka.
La mwisho mashine zenu ni za kipuuzi hazifanyi hata detection ya taarifa za mtu kwenye kitambulisho cha kura na NIDA nimetumia majina mawili ya mwisho yasiyofanana na cha kura na wala sijagundulika
 
NIDA ya wapi huko wanataka kadi za kuzaliwa pamoja na hakiki za idara ya uhamiaji?
Mimi nina rafiki zangu vyeti vya kuzaliwa hawajui hata vinafananaje na wamepata hayo makolokolo ya Nida.
.
Lengo la serikali ni kusumbua watu na hidden agenda yao imeshafahamika mimi kama nilitumia kitambulisho cha kura kufanya usajil wa laini zangu na bado naibia watu mitandaoni mmeshindwa kunidhibiti kwa kitambulisho cha NIDA mtawezaje?
.
Vyeti vya kuzaliwa havina taarifa za kuaminika hata kidogo, nitakupa mfano hai mimi katika cheti changu cha kuzaliwa kinasoma taarifa za uongo kwa maslahi yangu binafsi tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa sio uhalisia wangu, uhamiaji uliowasema ambao kimsingi hawako ni rahisi kuwaongopea ninavyotaka.
La mwisho mashine zenu ni za kipuuzi hazifanyi hata detection ya taarifa za mtu kwenye kitambulisho cha kura na NIDA nimetumia majina mawili ya mwisho yasiyofanana na cha kura na wala sijagundulika
Hongera.
Endelea kuwaibia.
Waelekeze ulivyo fanya hawa wanao lalamika wakapate vitambulisho vyao.
Case closed.
 
Hivi idara ya uhamiaji wana hakiki au wana gonga muhuri tu. Hivi wana nyenzo gani wanatumia kutambua huyu ni mtanzania au siyo?

Kuhusu affidavity hata sasa zinatumika. By the way ni nyumba ngapi zina namba? 90% ya wakazi wa dar wanahama hama kila siku, hivi mtu anapo hama taarifa zake za makazi huko NIDA pia zinabadilika?

Mtoa mada yuko sahihi, serikali haijajipanga na inatumia resources vibaya. Information must be captured and stored once...
Mkuu yale mahojiano kuna kitu wanaweza kumtilia shaka mtu mgeni, ni kazi yao wamesomea.
Uraia haupimwi na kipimo kama cha hospital bali mahojiano, lafudhi, maelezo yako na muonekano wako.
Ni kazi yao wewe unaweza kuona wnacheza tu kwa vile hauna mafunzo yao.

Kuhusu kubadilika makazi ndio maana vitambulisho vina tarehe ya ukomo ( expiry date) ili ukienda kuomba upya ubadili na hizo taarifa zilizopitwa na wakati.
 
Jamani tuwe wawazi kwenye kusajili line kwa kitambulisho cha taifa wamekurupuka sana wao walitakiwa wawawezeshe NIDA wawe kwenye kila makao makuu ya tarafa au kata ili iwe rahisi kwa kila mtu kufika ,kuna maeneo Tanzania hii mtu anatumia zaidi ya elfu 30 kufika wilayani
Wameona watumie neno kudajili laini ndo mtajitokeza wengi.... Hapo mwanzo watu walipuuza sana,

Iyo ndo nafasi pekee mtaenda tu utake usitake.

MashineNene[emoji533][emoji1646]
 
Hii nchi kuna mambo mengi hufanyika bila kufikiria mbele. Leo tunakimbizwakimbizwa kwa ajili ya kitambulisho cha NIDA. Lakini kwa mujibu wa sheria ya utambulisho wa uraia, kadi/namba ya NIDA ndio kithibitisho pekee halali cha uraia wa mtanzania; yaani aliyesajiliwa NIDA ndo anatambulika kisheria kuwa ni raia wa Tanzania.

Wakati NIDA hutumia alama za vidole (fingerprint) katika kusajili raia, juzi tu hapa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imetanganza kufanya maandalizi ya kuanzisha kanzidata ya taifa ya vinasaba (National Centre for Human DNA Database). Kanzidada hii itatumika katika utambuzi wa watu/raia na kwamaana hiyo kanzidata hii itaunganishwa na za mamlaka zingine hasa zile za NIDA kuboresha utambuzi wa raia.

Biometria ya alama za vidole (fingerprint) inayotumiwa na NIDA ina mapungufu ukilinganisha na ile ya vinasaba (DNA fingerprint). Mathalani, fingerprint haiwezi kuonesha uhusiano (unasaba) wa ndugu wa karibu (closely related individuals). Zaidi, fingerprint haiwezi kutumia sampuli ya mwili ulioharibika kubaini utambulisho wa mwenye huo mwili au ndugu yake wa karibu.

Ingawa fingerprint ni biometria ya haraka, isiyo na gharama kubwa na haihitaji mtaalamu katika ukusanyaji wake, haikupaswa kutumiwa na NIDA kutokana na udhaifu wake kama ulivyooneshwa hapo juu na badala yake mamalaka hiyo ingetumia DNA profiles za watu zitazoandaliwa na GCLA. Hii ni kwasababu moja ya masharti ya NIDA ni muombaji usajili kutoa uthibitisho wa "makaratasi" kuonesha uraia au asil ya wazazi wake kwasbabu makaratasj hayo yanaweza kuwa na taarifa za uwongo hata kama zinatolewa na mamlaka halali kama vile RITA au Mahakama/Wakili.

Wasiwasi uliopo ni kwamba hapo baadae kutakuwa na usumbufu kwa raia kwasabu kanzidata ya DNA profile zitakazozoandaliwa na GCLA zitakinzana na taarifa za uhusiano (nasaba) za mzazi na mwanawe zinazokusanywa leo na NIDA kwa kutumia ushahidi wa "makaratasi". Je, ikitokea DNA profile ya raia X hairandani na ya mzazi wake (raia Y) aliyemtaja kwenye taarifa za NIDAQ
Sijui kama unajua utaratibu wa kupata passport mpya?!
Huwezi kupata bila kitambulisho cha taifa.

Passport ya zamani ilikuwa inatolewa bila kukidhi vigezo vya cheti cha kuzaliwa maaana walikuwa wanapokea hadi affidavit ambayo nimeeleza udhaifu wake.

Jambo jingine hizo passport za zamani kulikuwa na mapungufu ya ukusanyaji taarifa za anuani za makazi.
Hakukuwa na kigezo cha kuweka nambari au kitalu cha nyumba unayo ishi.

Hiki kitambulisho cha NIDA kimekuja kuunganisha na utambuzi wa anuani za makazi ktk mfumo wa Postal code, ndio zile namba nne za mwisho za kwenye kitambulisho cha NIDA.

Nadhani kwa haya machache utakuwa umeelewa na kujifunza kitu.
CC: Pascal Mayalla , My Son drink water TUJITEGEMEE
Utaandika sana kutetea lakini nakuhakikishia kuwa hakuna taarifa mpya katika usajili wa NIDA ambayo haikuhusika kwenye passport au leseni ya udereva. Naona unajaribu kusisitiza "nguvu" ya cheti cha kuzaliwa katika kuthibitisha uraia, lakini kumbuka kwenye cheti hicho kuna maandishi madogo yanasmomeka "cheti cha kuzaliwa sio uthibitisho wa uraia".

Kwa taarifa yako affidavity hutumika pia na NIDA kama mbadala wa cheti cha kuzaliwa kwa mtu asiye nacho. Lakini unaposema postal code si lolote bali ni anwani ya makazi ambayo kwenye kwenye fomu za maombi ya passport pia huhitajika.
 
Back
Top Bottom