Nakuwa na maamuzi ya kusitasita kuolewa tena tangu ndoa ya kwanza inishinde 2021

Swali zuri sana hii ndio shida ya binadamu tunapenda kujiona mainnocent tunapoelezea maisha ya mahusiano mbele ya jamii na kuona wenzetu wanamakosa hasa hii ipo kwa jinsia ya kike
 
Naomba ushauri nilee wanangu hawa niliopewa na Mwenyezi Mungu au niingie tena kwenye ndoa na huyu mchumba...kiufupi Kaka wa watu hana makuu...ni mtu mwema tu na anastahili.
Nakushauri ulee tu wanao, mwanamke huolewa mara moja tu na ataishi na mumewe hadi kifo kiwatenganishe (isipokuwa kwa sababu ya uzinzi) hakuna kuachana.

Huyo mkaka unayemuona ni mpole hana makuu, mwema.... 😂😂😂 ni mwanaume kama yule aliyekuwa anakutwanga mangumi hadi ukamkimbia. Kwa kifupi hana tofauti na yule uliyamkimbia.

Kama una shauku ya kuwa na bwana, rudi tu kwa mumeo boxer, na ikiwa umechoka kutwangwa mangumi basi baki kuwa single lady ulee tu wanao.
 
Ni kweli mkuu Mungu anisaidie
 
👍🤝👏📝
 
Umesema vizuri, ndoa ya kwanza mliforce, na hii umeona penzi.
Usisite, olewa. Ukifika mtii mumeo, penda ndugu zake.
Wanaume hatufanani, tuvumilie, utii, weka mazingira safi, akiongea onyesha kuheshimu maoni/maelekezo yake hata kama unaona ni pumba, kisha kwa kutumia hekima mueleweshe kama unashauri usionyeshe kiburi!!
Hata ukiwa Kamanda wa Polisi au Kikosi cha Jeshi lolote lile, ukiwa na mumeo mpe heshima na hadhi yake.
Na Mungu akabariki ndoa yako mpya. BUT: Usiwasahau hao watoto wako, wape muda wao.
 
To yeye ,,,,najua tumekuwa na utani wa kimapenzi humu ndani kama kuitana wapenzi na makopakopa lkn kwa ajili ya kufurahi tu na mwisho siku inapita.

Kwa roho safi kabisa nashauri kubali kuolewa na huyo mwamba nahisi ana roho nzuri kama yangu, na kama anapenda watoto wako hiyo ni point kubwa mno

Wakati mwingine tunakosa mambo mazuri kwasababu ya hofu zisizo za msingi, ishinde hiyo hali kwa kuamini kila kitu kitaenda kuwa sawa

Kama unaamini he is the one basi usiuweke usiku olewa na huenda ukaja kufurahia maisha ya ndoa ambayo hukuyapata hapo kabla

Nimekupa baraka zangu zote

Mpenzi wako wa jf
Etugrul bey
 
Mwanzo atakupenda ila akishakutana na wadau watamuuliza kakubali vipi mechi ianze 2-0 na hajaonyeshwa kaburi la Ex baada ya hapo na yeye atatafuta panga kuja kukuchinja
 
Mliishi pamoja kwa muda gani, na mmeachana lini?
 
Kaa nae mda sana mpaka uone upo tayari
Mpaka umekuja kuuliza huku ni wazi bado una maswali
Ulikosea mwanzo ukikosea tena ni uzembe

Ila mwanaume anaeshindwa kutenganisha ndugu na ndoa yake ndoa inakuaga na misukosuko sana…. Speaking from experience
Mi sijapambana sana na ndugu ila kuna namna niliamua kudeal tu na mume wangu,sasa hivi tupo ok kama asilimia 70 tu
Ila wakati tunaona aisee kila ndugu alikua anatoa opinion yake ina leta stress sana kwenye ndoa
Almost 7 yrs na naona kabisa mbali na sex naona ni rafk yangu wa karibu sana siezi tena kuachana nae

Utakapo fikia hatua ya kuingia kwenye ndoa usimtegee afanye kosa au kuangalia sababu kila mara,ambacho hupendi sema mapema na weka kila kitu kwa table before any major step…
Cha mwisho mi nikiachika/tukiachana siwezi tena kuolewa na wala sitotaka coz nikiangalia nyuma kiwango cha sh**t nilichotolarate sitaweza tena ukizingatia nishakua shangazi magonjwa ya utu uzima yasijenimaliza sababu ya mtoto wa mama mkwe
 
Hii ni point hana utayari
Akishaupata wala hataitaji uzi kuleta
 
Ubarikiwe sana love
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…