Namna wachezaji mpira wa nje wanavyomiliki Ardhi Tanzania

Sehemu kubwa ya Dunia,inawezekana kasoro tu.Ardhi ya za Zanzibar & Rwanda.


Ubaguzi na chuki kwa wenzio sio nzuri.
Hata mda huu nenda Congo utapata ardhi TU mbona.
 
Wewe si unaogopa kuuwa tembo kuchukuwa meno ukauze, waache matajili waendelee kuwa matajili.

Hakuna utajili wa halali labda waliorithi kama kina Manji na Mo Dewji na bado lazima umanipulate mfumo ili kuutunza utajiri na kuupanuwa utajili.
 
Mashamba yanaunzwa bei ya kutupa lakini vijana wengi hawana plan za kuyanunua.

Mnachoweza ni kujadili plan za Simba na Yanga.

Ila wageni wakinunua ardhi mnaanza kuhoji!
 
Nenda Arusha uone, ndio maana Botswana walishituka hii mambo
 
Kama umiliki ni wa mtoto unamuonea wivu au ni nini? Yani hamtaki hata uwekezaji kidogo? Ardhi ni nini? Unataka huyo mtoto aende wapi kama kazaliwa hapa?
Wanataka wapigwe mkuyenge kama aliopigwa Mirembe na RC mtuhumiwa.Wazee wa Sanda banahhh
 
Wanataka wapigwe mkuyenge kama aliopigwa Mirembe na RC mtuhumiwa.Wazee wa Sanda banahhh
Ukute hata kula mchana hujala na bado unashabikia ujinga.

Taifa lililojaa wanjinga. Hii mali haina mwenyewe hii.

Wacha muibiwe.
 
Bora hao wachezaji kuliko wachina na waturuki wanaozaa na kuwatelekeza watoto wao bila kitu.
 
We jamaa kumbe una ufahamu mdogo kiasi hiki??
 
Kila nchi Ina utaratibu wake, je utaratibu wetu ndio huo? Sheria zetu zinaruhusu?
 
Kama umiliki ni wa mtoto unamuonea wivu au ni nini? Yani hamtaki hata uwekezaji kidogo? Ardhi ni nini? Unataka huyo mtoto aende wapi kama kazaliwa hapa?
Unamuonea tu aliyeweka hii mada, sio yeye bali sheria zetu
Mtoto kuzaliwa hapa sio sababu, anaweza luzaliwa hapa Ila akaamua kuwa raia walipotoka wazazi wake. Lazima tujue kwanza mtoto ni raia wa wapi
 
Uchoyo Ni nn? Sheria zetu zinasemaje? Ni mleta mada ndio aloyetunga hizo sheria?
Uchoyo ni kuwa na imani inayopitiliza kwamba kila mgeni anataka kutuibia, matokeo yake tunazeeka na kuaga dunia bila ya kuendeleza kile tunachojaaliwa na Mungu.

Huo 'usisi' na 'umimi' unapokuwa umetujaa ndani yetu kwa kisingizio cha kulinda rasilimali unatunyima pia fursa nyingi zinazotupita kanda.
 
Sehemu kubwa ya Dunia,inawezekana kasoro tu.Ardhi ya za Zanzibar & Rwanda.


Ubaguzi na chuki kwa wenzio sio nzuri.
Hata mda huu nenda Congo utapata ardhi TU mbona.
Kichekesho ni kwamba ukiwa njiani unatoka Dar kwenda huko mikoani ukiangalia kushoto na kulia kuna ardhi nyingi tu haijaguswa mpaka leo tangu tupate uhuru 1961.

Sisi wenyewe hatuna ubunifu kwani elimu zetu hazitupi udadisi wa kimaisha na hilo ni kosa la kisera limekuwa likirudiwa miaka na miaka.

Mawazo ya hiki ni chetu au cha kwangu yanatupotezea fursa nyingi na sio makosa ya wageni wanaokuja kutaka kuwa wabia wetu katika kufanya miradi mbalimbali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…