Namtafuta Mama Yangu popote alipo

Ungetoa ABC kidogo why unadhani sio Mama yako Mzazi! Then tungeweza kukusaidia kama uko sahihi au lah, hili lingekusaidia uweze kuendelea na mchakato wa kumtafuta Mama yako au kusitisha hilo zoezi.....
 
Mkuu situmii hivyo vitu kabisa na sijawahi kugusa sijui vinatumiwaje ila Mama yangu anatumia ndio maana nasema huyu sio Mama yangu
Sasa wewe yanakuhusu nini maisha yake? Kuna Siku ulilala njaa? Uliwahi kukosa Ada au kushindwa kufuliwa nguo? If not, muache na maisha yake. Kuna Watu wamesomeshwa na pesa ya gongo....
 
Kwahyo ipo siku mtoto wa Gigy money nae atakuja umu kusema yule sio mamaake
Hili sio swali la kuniuliza mkuu, sijui umetumia vigezo gani kuniuliza hili swali
 
Wahi haraka hospital ya vichaa mirembe
 
Yaani unategemea mwanamke awe mtunza siri? Siri anazoweza kutunza mwanamke ni mbili, kuchepuka na kuua yeye mwenyewe hizo zingine ni breaking news.

Kuna mama mmoja alipoingia madarakani kwa mara ya kwanza ndio tulisikia kwa uwazi kuwa mawaziri wanaruhusiwa kula ila wale kidogo wenyewe wakawa wanakomba mboga wanalamba na chungu🤣🤣🤣

Huyo ndio mama yako mkuu usimlazimishe awe mwanaume
 
Ingekua ni baba kungekua na uwalakini, ila kwakuwa ni mama naomba nikwambie acha ujinga

Angekuokota angekwisha kukwambia
 
Kapime DNA.
 
Akusikie popote alipo na ID fake yako?
 
Mkuu kuwa serious kidogo!!, Unamtafuta mama yako wakati huo hutoi taarifa kamili juu yako na utata wa kumthibitisha huyo kama sio mama yako.
Siku hizi kuna hivi vipombe vya chupa vinasumbua sana vijana!!.
 
ULIMWENGU NDIO MAMA. Ukiufahamu na ukiutambua hilo utapata utulivu wa nafsi yako na utakuwa NURU.
UPENDO ndio silaha na ngao imara kwako itumie vyema itakusaidia sana.
 
Watu tushaambiwa najuta kuwazaa ila imani haikushuka hata tone we kuhisi tu unaanza kutafuta mama mwingine. Kaza mzee kaza acha kulendemka.
 
Mkuu kuwa serious kidogo!!, Unamtafuta mama yako wakati huo hutoi taarifa kamili juu yako na utata wa kumthibitisha huyo kama sio mama yako.
Siku hizi kuna hivi vipombe vya chupa vinasumbua sana vijana!!.
Situmii hivyo vitu mkuu mwili wangu hauna aina yoyote ya alcohol zaidi ya maji sinywi kilevi chochote hata chai na kahawa kwangu mwiko situmii situmii
 
Ridhika na uyo uliekua nae unaweza Kuta mama Yako mzazi mgaigai,, Anadaiwa kausha damu,vikoba,upatu. Atakuletea mikosi utajuta kumjua Mambo Yako yote yataenda ovyo.
 
Au karopoka kua alikuokota?
Anaongea kinyume chake ila unajua kutokanana anachokiongea anamaanisha kabisa wewe sio mwanangu na Mimi sio Mama yako sometimes anakwambia nenda kamtafute Mama yako alipo, kuna treatment ya Mama kwenda kwa mtoto na kuna kipindi niliwahi kumhoji Mzee kwani Mimi Mama yangu yupo wapi? Hakuwahi kunipa jibu linaloeleweka sababu nilishagundua huyu sio Mama yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…