Uchaguzi 2020 Nani mkweli kati ya hawa watu? Spika, NEC au CHADEMA?

Uchaguzi 2020 Nani mkweli kati ya hawa watu? Spika, NEC au CHADEMA?

Jambo ambalo naamini mimi ni CDM wamepeka majina maana Kama cdm wangekuwa hajapeleka majina na tunavyowaaminia makamanda (Halima & wenzie) wasingekubal kwenda bungeni LAKINI yanaweza kuwa hayajapelekwa na Mnyika
Kwa hiyo wakapeleka jina la ayeko mahabusu kwamba mamlaka ni ya Cdm sio au umejiondoa ufahamu?
 
Ukweli utaupata kwa nani wakati vyombo vyote vilivyotakiwa kuutoa huo ukweli vipo mfukoni mwa Serikali, na hiyo Serikali ndiyo chanzo cha huu uchafu wote?

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ndio upuuzi nisio utaka. Kama kweli barua ilikuwa forged,mahakama ipewe taarifa,amru ya uchunguzi ifanyike. Mahakama ikipindisha tutajua.
 
Huu mjadala ni wa kitoto sana.

Wakati uchaguzi unaanza tulishuhudia wanachama wa CHADEMA wakilalamika kwa wakurugenzi wa uchaguzi kunyimwa fomu kwa kile kinachodaiwa kuwa wameshachukua fomu ya ubunge kwenye majimbo X. Hivyo wakurugenzi wa uchaguzi hawatoi fomu hiyo tena kwa wagombea wa CHADEMA.

Waliochukua fomu walidaiwa kuwa walifika kwenye ofisi za wakurugenzi wa uchaguzi wakiwa na barua za CHADEMA zilizogongwa mhuri wa katibu wao wa jimbo/mkoa.

Hili sakata liliwakumba wagombea kadhaa wa udiwani kupitia CHADEMA, siwakumbuki kwa majina nafikiri baadhi ya majimbo ni Ubungo na Kibamba.

Je kesi hizi ziliishaje? Wale wagombea feki walichukuliwa hatua gani ? Barua zenye mihuri ya CHADEMA walipewa na nani?

Mwishoni wagombea halali walipewa fomu kwa amri kutoka juu nafikiri. Ni NEC waliona mapungufu hayo nchi nzima au nani alitoa suluhisho sikumbuki.

Kilikuwa ni kituko kwa wakurugenzi kuwanyima fomu wagombea kwa kisingizio cha kuwa tayari mwanachama wao ameshachukua fomu tena kwa barua halali ya uteuzi kutoka kwenye chama chao wenyewe.

Sasa turudi kwenye hili. NEC wamepokea barua halali kutoka kwa Mnyika. Mnyika anasemaje? Kama anakataa, je alazimishwe kuwa aliandika? Kama barua ilikuwa feki kwa nini NEC isikubali yaishe na wakisikilize chama cha CHADEMA ili haki itendeke. Barua halali ya majina halali ipelekwe NEC. Kama CHADEMA hawataki kupeleka majina, je walazimishwe?

Kama wasipopeleka majina, Je sheria au Katiba inasemaje kuhusu hilo.

Imefikia kipindi kila chombo kifanye jukumu lake na kiache ubabaishaji. Nchi hii ina wasomi na ni aibu kuonekana kituko kwa mambo yanavyofanyika bila weledi.

Kuwa mzalendo ni pamoja na kusema ukweli sio kutetea ubabaishaji hata kama ni kwa manufaa yako.

Asalaam
 
Hapo hakuna hata mmoja aliye mkweli wote vyura wanapiga kelele vichwa nje kiwiliwili majini, wakisikia mchakacho wanazama majini
 
Huu mjadala ni wa kitoto sana.

Wakati uchaguzi unaanza tulishuhudia wanachama wa CHADEMA wakilalamika kwa wakurugenzi wa uchaguzi kunyimwa fomu kwa kile kinachodaiwa kuwa wameshachukua fomu ya ubunge kwenye majimbo X. Hivyo wakurugenzi wa uchaguzi hawatoi fomu hiyo tena kwa wagombea wa CHADEMA.

Waliochukua fomu walidaiwa kuwa walifika kwenye ofisi za wakurugenzi wa uchaguzi wakiwa na barua za CHADEMA zilizogongwa mhuri wa katibu wao wa jimbo/mkoa.

Hili sakata liliwakumba wagombea kadhaa wa udiwani kupitia CHADEMA, siwakumbuki kwa majina nafikiri baadhi ya majimbo ni Ubungo na Kibamba.

Je kesi hizi ziliishaje? Wale wagombea feki walichukuliwa hatua gani ? Barua zenye mihuri ya CHADEMA walipewa na nani?

Mwishoni wagombea halali walipewa fomu kwa amri kutoka juu nafikiri. Ni NEC waliona mapungufu hayo nchi nzima au nani alitoa suluhisho sikumbuki.

Kilikuwa ni kituko kwa wakurugenzi kuwanyima fomu wagombea kwa kisingizio cha kuwa tayari mwanachama wao ameshachukua fomu tena kwa barua halali ya uteuzi kutoka kwenye chama chao wenyewe.

Sasa turudi kwenye hili. NEC wamepokea barua halali kutoka kwa Mnyika. Mnyika anasemaje? Kama anakataa, je alazimishwe kuwa aliandika? Kama barua ilikuwa feki kwa nini NEC isikubali yaishe na wakisikilize chama cha CHADEMA ili haki itendeke. Barua halali ya majina halali ipelekwe NEC. Kama CHADEMA hawataki kupeleka majina, je walazimishwe?

Kama wasipopeleka majina, Je sheria au Katiba inasemaje kuhusu hilo.

Imefikia kipindi kila chombo kifanye jukumu lake na kiache ubabaishaji. Nchi hii ina wasomi na ni aibu kuonekana kituko kwa mambo yanavyofanyika bila weledi.

Kuwa mzalendo ni pamoja na kusema ukweli sio kutetea ubabaishaji hata kama ni kwa manufaa yako.

Asalaam
Pumba gani hizi unaweka hapa? Hapa substance ni barua kutoka Chadema kwenda ni original? Ndio inayompa kiburi Ndugai,we unaleta porojo za uchaguzi. Zinatusaidia nini kwa sasa?
 
Sioni sababu ya kwenda mahakamani. CHADEMA impelekee tu Spika barua kuwa CC imewavua uanachama hao wabunge wao.

Kama katiba inaruhusu mbunge kutokuwa na chama chochote kilichomdhamini, hilo ni la hawa walioufanya huu uchafu. Huu uchafu umeshirikisha Serikali nzima pamoja na mihimili ambayo imewekwa mfukoni mwa serikali.

CHADEMA isikpoteze muda na wala isithubutu kwenda mahakamani. Siku zote adui yako haweza kukuelekeza njia ya kupita salama. Huko mahakamani, kwa kuwa nao ni mhimili uliowekwa mfukoni mwa mtawala, watakuwa wamewaandaa watu wao. Mkienda tu huko, hawatataka mliongelee suala hilo kwa maelezo kuwa suala lipo mahakamani. Na pia mahakama hii iliyopo mfukoni mwa Serikali itatumika kumsafisha spika, NEC ha wote walioshiriki kwenye uchafu huu.

CHADEMA wakishapeleka barua kumtaarifu spika, wamemaliza. Akina Mdee wakiendelea kuwa wabunge, ni sawa tu. Watakuwa wabunge maalum wa Kongwa na Chattle.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni hivi, CHADEMA inataka wale Wabunge waendelee kuwepo bungeni, ndiyo maana wanaenda mahakani badala ya kumwandikia spika kwamba wameshawatema.

CHADEMA wanajaribu kuhadaa watu ili wasishukiwe kwamba wamebadili gia on air.

Kifuatacho mahakama itabariki kwamba Wabunge wale ni halali, na hapo mjadala utafungwa rasmi ili mihimili isipigane.
 
Chadema wanasema hawakupeleka majina NEC,nani alipeleka?

NEC wanasema Mnyika kama katibu mkuu aliwapelekea majina tena yaliyopewa baraka na kamati kuu ya Chadema. Hii ni kweli au sio kweli?

Spika anadai hawezi kuvua ubunge wabunge ambao kwa mujibu wa katiba ya JMT sasa hivi hawana chama maana walishatimuliwa Chadema. Kisa tu NEC ya Wilson Mahera ilimpa majina. Ok kama NEC ilimpa majina bado wanasifa za kuwa wabunge kama ibara ya 67(b) na 71(e) inavyoweka wazi?

Au ndio kusema undavaundava tu hata kwenye mambo ya kuzingagia Katiba na sheria?

Chadema wanaweza kuupa ukweli umma wa watanzania ili tujue nani alipeleka majina? Nahisi kuna jinai inanukia, kama haipo kuna mtu mkubwa Cdm mpenda dili anahusika,Tanzania nzima inamfahamu.
Ngoma inapelekwa mahakamani mbivu na mbichi zitajulikana.
 
Hivi hiyo ruzuku itakayo tokana na wabunge 19 itaenda wapi? Kina Mdee niajilini mie niwe nawapokelea nitawatunzia vizuri
 
Pumba gani hizi unaweka hapa? Hapa substance ni barua kutoka Chadema kwenda ni original? Ndio inayompa kiburi Ndugai,we unaleta porojo za uchaguzi. Zinatusaidia nini kwa sasa?
Soma uelewe sio unakurupuka tu.

Barua hiyo unajua nani aliiandika na nani kasaini? Kama ni Mnyika basi ni halali kama sio yeye basi sio halali. Kuhusu CC ya CHADEMA itamwajibisha kama kweli barua ni halali maana aliandika bila baraka kutoka CC.

Ila kama Mnyika hausiki basi NEC inaleta ubabaishaji. Kuhusu Ndungai yeye anasubiri tu taarifa kutoka NEC.

Wenye kutueleza ukweli ni Mnyika kwanza, akikana basi NEC watueleze ukweli.

Nimefanya reference ya uchaguzi kuonesha CHADEMA walivyochezewa rafu sasa pumba ipo wapi?
 
Maswali mengine ni kam kujaribu kuwasafishA hawA wendawazimu wazalendo uchwara. Spika na Nec hao wote ni mawakalA wa yule muovu shetani na ndiye anayewAtuma kufanya wayafanyayo.
 
Nakunukuu:"NEC wanasema Mnyika kama katibu mkuu aliwapelekea majina tena yaliyopewa baraka na kamati kuu ya Chadema"

Sasa mkuu kama NEC wanadai ya kwamba wamepokea majina kutoka chadema yenye baraka za kamati kuu,kwani kikao cha kamati kuu kinaweza kufanyika kwa kificho?Kuna kikao cha kamati kuu cha chadema ambacho kimewahi kukaa?Si lazima taarifa zingevuja ya kwamba kuna kikao cha kamati kuu kilikaa?
Wachache wenye muda wa kutafakari kwa kina.NEC ,N DUGAI na DPP lao moja.Lengo "kutakatisha" fedha za mabeberu. Hoja kama hizo hazipatiwi majibu stahiki. Ni kukanusha kwa povu la kabudi bila uthibitisho. Inasikitisha sana.
 
Back
Top Bottom