Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Mimi ni Mkristu dhehebu la RC na nililelewa kwenye familia yenye kufuata mafundisho ya RC na nimebatizwa,kupata komunyo ya kwanza hadi kipaimara na kufunga ndoa ya kikatoliki.

Lililonileta ni kuwa nimekuwa sipendezwi na imani yoyote haswa hizi za dini naona kama uongo na ni mifumo ya watu fulani hapa namanisha Ukristu na madhehebu yake yote naona kama udwanzi na uislam ndo kabisa siulewagi kabisa kwa kifupi siamini kama Mungu yupo(nina ground zangu) na kama yupo hatambui hii mifumo iliyowekwa na makundi ya binadamu(dini) na hana uwezo huo anaosifiwa na dini zote zilizoanzishwa.

Nimegundua kwenye kuifuata dini tunapoteza muda tu na hela mfano mimi huu mwaka wa 5 anaenda kanisani ni wife tu ila hajawahi leta chochote kutoka KANISANI zaidi ya sisi kupeleka vitu kibao include hela zetu(sadaka,zaka na michango mingine) na mavuno zaidi zaidi kuna matawi ya muwese la enzi za kuanza kwa mfungo wa kwa resma na bado hayo matawi alienda nayo yeye likabalikiwa akalileta home pamoja na maji ya baraka.

Changamoto niliyonayo ni kuwa wife kajiunga kwenye jumuia alafu huwa anawapa namba yangu viongozi wa jumuia na nimezinguana nae sana kwa hilo swala kiasi kwamba wananisumbua kwa kuniletea ma bahasha mengi ambayo hata nikitoa siamini kama lolote naongezewa zaidi zaidi naona kama napungukiwa kwa sababu natoa kitu live alafu narudishiwa ahadi ya kubarikiwa ambapo siwezi pima hizo baraka kama zinahusiana na kusali au kutoa kwangu.

OMBI LANGU
Nisaidien mbinu za kukwepa ushiriki wa hizi habari za kusali jumuia au kanisani maana nahisi wameona kuna magari matatu yard kwangu ndio maana wananisakama na ndio maana nikiweka hela ndogo kwenye bahasha wanapanic kuwa "huyu sio wa kuchangia elf 20". Kuna siku walifanya uchaguzi wakanichagua kuwa Mhasibu/Mweka hazina wa parokia na huku kwenye jumuia wakanichagua kuwa katibu wa jumuia nilishangazwa na uchaguzi wao wa kushinda bila kushiriki ikabidi nikatae kwa kisingizio cha muda wangu hautoshi kutokana na nature ya kazi yangu na wakataka kulazimisha sana ila walishindwa.

In short najiuliza nawezaje kuwatoka kistaarabu na wakatambua kuwa mimi sihitaji kuwa mshiriki wa hizi imani maana imani yangu mimi nikufight na maisha na kuinjoy matokeo kwa kuwekeza nguvu na akili chache nilizonazo.Naomba ushauri ili kuepuka kuwakwaza majirani na watu tunaoheshimiana nao wasije ona nimejaa kiburi kumbe mimi nimeona kuwa nawekeza effort za kufungua mlango uliochorwa ukutani.

Jamii kushiriki nayo kwenye mambo mengine nahitaji ila sio haya mambo ya kusali pamoja nipo tayari kama kuna umoja wa kuchangiana au kuwa na kikundi cha kusaidiana kwenye raha na shida ila sio hivi vikundi vya dini vikekaa kinyonyaji sana yaani wanatupa hewa(maombi) sisi tunawapa vitu tangible n valuable.
Maisha yetu yamejaa utoaji,utafanya kwa hiari au lazima ,usijidikie vibaya kutoa
 
Kabisa kwan kuzikwa ni nn kwamba mtu akisema mungu baba mrehemu ndio umeenda peponi au
Ndio uendelee na upagani wako kwa uhuru, na uwaachie wanaoamini vingine waendelee kuabudu kwa uhuru pia. Inashangaza mtu ni mpagani halafu anataka na wengine wawe kama yeye!
 
😂 katibu unakataa ukatibu wakati kuna watu wanajisifu hata kusoma neno pale mbele na wamewekeana zamu!, ila haka ka dunia katamu sana mi nimekapenda na nilichokipendea ni kitu kimoja waumini sio wachoyo!..😂
Nakumbuka ndoa yangu iliishia hapa ni miaka mitano (5 ) sasa.....
 
Miaka 50,60,70.. hata 100 mbona sio mbali 😀 siku ukifa mbona utapata majibu yote huko roho yako itakapoenda.
 
Bado narudi pale pale. Unatumia nguvu nyingi, hadi matusi, kulazimisha watu waamini ambacho wewe unaamini. Kwani tukitofautiana na kila mmoja akabaki na anachoamini, tatizo liko wapi?
Sawa baki na hivyoo sasa wacha sisi wapagani tuenjoy life
 
FB_IMG_1716437123815.jpg
 
Jifanye unasali dhehebu lingine. Wajue haujakimbia ukristo ila unasali dhehebu la baba yako. Mfano mimi mambo ya jumuiya yalinikera nikaamua kusali SDA sababu hawana hizo jumuiya.

Nikaja kugundua ukiondoa kusali jumamosi SDA taratibu zao tamu sana kwa mtu asiye na mambo mengi
SDA mimi naona wanachosha kwenye yale mambo ya makambi na sunday school.. masharti ya kula kunywa si magumu sana
 
Kabla ya yote aliye na ID ya pengo amu-Quote hata kama nae anatumia I'd fake tumu quote aje hapa ajibu

Kwanini Wana watisha waumini eti usipotoa zaka mara sadaka na michango huzikwi ukipatwa na matatizo husaidiwi?

Kuna askofu alisusa kabisa kutoa kipaimara kisa tu watu wametoka michango kidogo wahusika walilia sana walikuwa wamejiandaa asee walilia mno lkn hakujari kama utani akaondoka!

Hili dhehebu Kwa Sasa lipo kibiashara live.

Kuna mwezi nilipiga hesabu ikaja
157,600/=

Sijui zawadi ya mototo yesu 10,000
Mshumaa wa xmaa5000
Mchango wa kununua msalaba mkubwa wa parokia then na wakigango35,000/=

Michango ya jumuiya,ujenzi pamoja na kumtegemeza katekista yote hapa iligota laki na uchafu

Hapa sadaka haipo Wala zaka!

Halafu katekista Unakuta kalewa vibaya
 
Jifanye unasali dhehebu lingine. Wajue haujakimbia ukristo ila unasali dhehebu la baba yako. Mfano mimi mambo ya jumuiya yalinikera nikaamua kusali SDA sababu hawana hizo jumuiya.

Nikaja kugundua ukiondoa kusali jumamosi SDA taratibu zao tamu sana kwa mtu asiye na mambo mengi
Ulinogewa na viporo? Maana SDA huwa hawapiki j.mosi. Au nyimbo zao zisizo na ala?
 
SDA mimi naona wanachosha kwenye yale mambo ya makambi na sunday school.. masharti ya kula kunywa si magumu sana

Kwanza SDA hawana sunday schools. Wao wanasali jumamosi

Pili Makambi sio lazima ile ni mikutano ya kidini tu wiki nzima. Hata wale SDA damu damu huwa hawaendi kila siku. Wanakuwa kazini siku zingine.

Pia Kula na kunywa sio sheria kusema unasimamiwa. Wanafundisha tu kuacha kula vyakula vyenye madhara kiafya. Maana kwao health lifestyle ni part ya mafundisho ya imani yao.
 
Ulinogewa na viporo? Maana SDA huwa hawapiki j.mosi. Au nyimbo zao zisizo na ala?

Wabongo wape kichwa cha habari. Stori watatengeneza wenyewe.

Binafsi nilisikia mengi sana kuhusu wasabato. Ila siku niliyoenda kusali kwao. Nikajua kwamba niliyoyasikia nje mengi sio ya kweli. Ni chumvi tu za watu.

Mfano wewe mtu mzima kabisa akili yako inaamini SDA huwa hawapiki jumamosi wala kuosha vyombo ?
 
Mimi ni Mkristu dhehebu la RC na nililelewa kwenye familia yenye kufuata mafundisho ya RC na nimebatizwa,kupata komunyo ya kwanza hadi kipaimara na kufunga ndoa ya kikatoliki.

Lililonileta ni kuwa nimekuwa sipendezwi na imani yoyote haswa hizi za dini naona kama uongo na ni mifumo ya watu fulani hapa namanisha Ukristu na madhehebu yake yote naona kama udwanzi na uislam ndo kabisa siulewagi kabisa kwa kifupi siamini kama Mungu yupo(nina ground zangu) na kama yupo hatambui hii mifumo iliyowekwa na makundi ya binadamu(dini) na hana uwezo huo anaosifiwa na dini zote zilizoanzishwa.

Nimegundua kwenye kuifuata dini tunapoteza muda tu na hela mfano mimi huu mwaka wa 5 anaenda kanisani ni wife tu ila hajawahi leta chochote kutoka KANISANI zaidi ya sisi kupeleka vitu kibao include hela zetu(sadaka,zaka na michango mingine) na mavuno zaidi zaidi kuna matawi ya muwese la enzi za kuanza kwa mfungo wa kwa resma na bado hayo matawi alienda nayo yeye likabalikiwa akalileta home pamoja na maji ya baraka.

Changamoto niliyonayo ni kuwa wife kajiunga kwenye jumuia alafu huwa anawapa namba yangu viongozi wa jumuia na nimezinguana nae sana kwa hilo swala kiasi kwamba wananisumbua kwa kuniletea ma bahasha mengi ambayo hata nikitoa siamini kama lolote naongezewa zaidi zaidi naona kama napungukiwa kwa sababu natoa kitu live alafu narudishiwa ahadi ya kubarikiwa ambapo siwezi pima hizo baraka kama zinahusiana na kusali au kutoa kwangu.

OMBI LANGU
Nisaidien mbinu za kukwepa ushiriki wa hizi habari za kusali jumuia au kanisani maana nahisi wameona kuna magari matatu yard kwangu ndio maana wananisakama na ndio maana nikiweka hela ndogo kwenye bahasha wanapanic kuwa "huyu sio wa kuchangia elf 20". Kuna siku walifanya uchaguzi wakanichagua kuwa Mhasibu/Mweka hazina wa parokia na huku kwenye jumuia wakanichagua kuwa katibu wa jumuia nilishangazwa na uchaguzi wao wa kushinda bila kushiriki ikabidi nikatae kwa kisingizio cha muda wangu hautoshi kutokana na nature ya kazi yangu na wakataka kulazimisha sana ila walishindwa.

In short najiuliza nawezaje kuwatoka kistaarabu na wakatambua kuwa mimi sihitaji kuwa mshiriki wa hizi imani maana imani yangu mimi nikufight na maisha na kuinjoy matokeo kwa kuwekeza nguvu na akili chache nilizonazo.Naomba ushauri ili kuepuka kuwakwaza majirani na watu tunaoheshimiana nao wasije ona nimejaa kiburi kumbe mimi nimeona kuwa nawekeza effort za kufungua mlango uliochorwa ukutani.

Jamii kushiriki nayo kwenye mambo mengine nahitaji ila sio haya mambo ya kusali pamoja nipo tayari kama kuna umoja wa kuchangiana au kuwa na kikundi cha kusaidiana kwenye raha na shida ila sio hivi vikundi vya dini vikekaa kinyonyaji sana yaani wanatupa hewa(maombi) sisi tunawapa vitu tangible n valuable.
Rafiki yangu hayati Shirima(RIP) wa Tandale alikuwa na duka kubwa kiasi hakuwa anashiriki jumui ndogo mtaani ila alituma michango yote,siku alipofariki hakuna kiongozi yoyote wa RC aliyekuja kwenye mazishi yake hadi walokole fulani walikuja kuokoa jahazi.
Bora usitoe mchango wowote jiunge na kanisa la Masanja Mkandamizaji au la Lovely Irene Uwoya.
 
Back
Top Bottom