Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Hii ni rahisi sana mkuu anza na viongozi wako wa jumuia kuwaeleza huamini katika dini yoyote nao watamfikishia paroko wako na wala hutosumbuliwa tena ila shida ipo kwa mwenzi wako yeye anaendelea kuamini katika ukristo hivyo watakuja kwake tu.
 
Mimi nikimkata jicho mwenyekiti wa jumuiya lazima aharishe hawezi kuniomba hata shilingi kumi.

Wanawachezea wajinga, kwangu hawathubutu.

Kuna siku walijidai wanakuja kusali jumuiya niliwatimua kama panyabuku walisambaratika hovyo. Hawajawahi kurudi.

Jumuiya ya kazi gani? inanisaidia nini?

Cc: Lamomy Extrovert cocastic Maghayo
 
Mna shida sana mnoishi kwa kuangalia jamii itachukuliaje 😭
 
Hata Ushoga ulianza na hoja kama hizi hizi, mwishowe unaanza kuenea kwa Kasi. Hili nalo ni eneo lingine la wanaompinga Mungu linavyoanza.

Hamia Freemason, wanamuabudu Shetani na pesa za kula Bata wanapata.
Shida shetani nae ni kiumbe wa Mungu
 
Havifanani hivyo vitu
 
Hama dhehebu
 
Kuogopa watu watakuonaje ni janga la kitaifa. Mimi toka nijue wabongo wengi ni wanafiki, huwa sijali mtu ananionaje na maamuzi yangu. Naishi maisha yangu bila kufuata mkumbo.
 
Yes mkuu na jiran alikuwa rc akachana na jumuiya alipokufa waliwauliza viongozi wa jumuiya akajibiwa alijitoa padre akagoma tukaenda kutaftaa mlokole akameza 50000 yake akasalisha tukazika
Nashangaa watu eti wanakataa kuzika mfu, kazi kweli. Hivi ile ya samehe mara sabini inatumikaga wapi? Usihukukumu n.k. ila wakuzika wapo kibao tu, wengine wanaona neema kuzika .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…