Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Mimi ni Mkristu dhehebu la RC na nililelewa kwenye familia yenye kufuata mafundisho ya RC na nimebatizwa,kupata komunyo ya kwanza hadi kipaimara na kufunga ndoa ya kikatoliki.

Lililonileta ni kuwa nimekuwa sipendezwi na imani yoyote haswa hizi za dini naona kama uongo na ni mifumo ya watu fulani hapa namanisha Ukristu na madhehebu yake yote naona kama udwanzi na uislam ndo kabisa siulewagi kabisa kwa kifupi siamini kama Mungu yupo(nina ground zangu) na kama yupo hatambui hii mifumo iliyowekwa na makundi ya binadamu(dini) na hana uwezo huo anaosifiwa na dini zote zilizoanzishwa.

Nimegundua kwenye kuifuata dini tunapoteza muda tu na hela mfano mimi huu mwaka wa 5 anaenda kanisani ni wife tu ila hajawahi leta chochote kutoka KANISANI zaidi ya sisi kupeleka vitu kibao include hela zetu(sadaka,zaka na michango mingine) na mavuno zaidi zaidi kuna matawi ya muwese la enzi za kuanza kwa mfungo wa kwa resma na bado hayo matawi alienda nayo yeye likabalikiwa akalileta home pamoja na maji ya baraka.

Changamoto niliyonayo ni kuwa wife kajiunga kwenye jumuia alafu huwa anawapa namba yangu viongozi wa jumuia na nimezinguana nae sana kwa hilo swala kiasi kwamba wananisumbua kwa kuniletea ma bahasha mengi ambayo hata nikitoa siamini kama lolote naongezewa zaidi zaidi naona kama napungukiwa kwa sababu natoa kitu live alafu narudishiwa ahadi ya kubarikiwa ambapo siwezi pima hizo baraka kama zinahusiana na kusali au kutoa kwangu.

OMBI LANGU
Nisaidien mbinu za kukwepa ushiriki wa hizi habari za kusali jumuia au kanisani maana nahisi wameona kuna magari matatu yard kwangu ndio maana wananisakama na ndio maana nikiweka hela ndogo kwenye bahasha wanapanic kuwa "huyu sio wa kuchangia elf 20". Kuna siku walifanya uchaguzi wakanichagua kuwa Mhasibu/Mweka hazina wa parokia na huku kwenye jumuia wakanichagua kuwa katibu wa jumuia nilishangazwa na uchaguzi wao wa kushinda bila kushiriki ikabidi nikatae kwa kisingizio cha muda wangu hautoshi kutokana na nature ya kazi yangu na wakataka kulazimisha sana ila walishindwa.

In short najiuliza nawezaje kuwatoka kistaarabu na wakatambua kuwa mimi sihitaji kuwa mshiriki wa hizi imani maana imani yangu mimi nikufight na maisha na kuinjoy matokeo kwa kuwekeza nguvu na akili chache nilizonazo.Naomba ushauri ili kuepuka kuwakwaza majirani na watu tunaoheshimiana nao wasije ona nimejaa kiburi kumbe mimi nimeona kuwa nawekeza effort za kufungua mlango uliochorwa ukutani.

Jamii kushiri nayo kwenye mambo mengine nahitaji ila sio haya mambo ya kusali pamoja nipo tayari kama kuna umoja wa kuchangiana au kuwa na kikundi cha kusaidiana kwenye raha na shida ila sio hivi vikundi vya dini vikekaa kinyonyaji sana yaani wanatupa hewa(maombi) sisi tunawapa vitu tangible n valuable.
Kama wanakuja kwako fuga midogi tu

Ova
 
Si wataniona najidai
Aisee umenishangaza kweli kweli. Eneo nililozawali mimi wakazi wake karibu wote ni wakatoliki. Kuna wazee wengi tu hawaendi kanisani na wala hawajishughulishi na mambo ya jumuia. Na kila mtu alishawajua. Hawakanyagi kanisani ng'o, hawatoi mchango wowote na wala hawashiriki kwenye lolote. Kwa kifupi wanaitwa wapagani. Sasa wewe kinakushinda nini? Dunia hii ukiogopa kufanya jambo eti binadamu wengine watafikiria vile... unaweza kujikuta unakwama kwenye mambo mengi.
 
Mnalazamisha na ndio maana asipoenda jumuiya hata kama anahudhuria Ibada kanisani mnaanza kumpa vitisho mara ooh ukifa padiri Haji kwenye maziko Yako, mara ooh kanisa linakutenga, basi kama vipi bomoeni makanisa ili tubaki na jumuiya tu.
Hivi serikali hawaoni haja ya kuweka sheria ya kuchoma moto miili. Maana kuna watu dini unatishiwa hautazikwa as if huo mwili una umuhimu tena duniani.Kwanini pasiwepo na kuchoma miili moto ili tusave muda na nafasi?
 
Jana wametangaza upanuzi wa kanisa unahitaji bajeti ya 700M ambayo naona ni nyingi. Parokia yetu ni changa haijatabarukiwa (kuwekwa wakfu), ila nikipiga hesabu naona tangu parokia inaanzishwa nikiwa A level huwa watu wanachangishwa tu. Mapato ya kanisa kwa mwaka ni around 100M, naona dalili ya kukamuliwa hela inakuja ingawa siishi tena uko.

Nakumbuka tulianza vijana wengi ila sasa tumepungua, naamini na watu wazima wamepungua.
Huwa ni changamoto kujenga kanisa au kulifanyia maboresho watu wenye roho nyepesi hukimbia.

Vitu sipendi ni kupotezewa muda mara vijana jogging, misa na askofu, matembezi ya nini sijui, beach mass.

Kanisa nilitaka nilitupe ila nikajiuliza nikitaka kuoa mke anayesali na asiyesali naoa nani, anayesali. Watoto wangu watakuwa wanasali au atheists, bora wasali. Nikabaki
 
Hata Ushoga ulianza na hoja kama hizi hizi, mwishowe unaanza kuenea kwa Kasi. Hili nalo ni eneo lingine la wanaompinga Mungu linavyoanza.

Hamia Freemason, wanamuabudu Shetani na pesa za kula Bata wanapata.
Usiwe na akili finyu kiasi hiki, jibu hoja kwa hoja. Mtu kauliza swali ww unaanza kuleta mambo ya ushoga yanahusiana nn hapa?
 
Aisee umenishangaza kweli kweli. Eneo nililozawali mimi wakazi wake karibu wote ni wakatoliki. Kuna wazee wengi tu hawaendi kanisani na wala hawajishughulishi na mambo ya jumuia. Na kila mtu alishawajua. Hawakanyagi kanisani ng'o, hawatoi mchango wowote na wala hawashiriki kwenye lolote. Kwa kifupi wanaitwa wapagani. Sasa wewe kinakushinda nini? Dunia hii ukiogopa kufanya jambo eti binadamu wengine watafikiria vile... unaweza kujikuta unakwama kwenye mambo mengi.
Hujanielewa wife ndiye ananirudisha nyuma kwa sababu anawaomba msaada kuwa mimi nimeingiliwa na shetani so wanakuwa na matumaini na mimi
 
Mimi ni Mkristu dhehebu la RC na nililelewa kwenye familia yenye kufuata mafundisho ya RC na nimebatizwa,kupata komunyo ya kwanza hadi kipaimara na kufunga ndoa ya kikatoliki.

Lililonileta ni kuwa nimekuwa sipendezwi na imani yoyote haswa hizi za dini naona kama uongo na ni mifumo ya watu fulani hapa namanisha Ukristu na madhehebu yake yote naona kama udwanzi na uislam ndo kabisa siulewagi kabisa kwa kifupi siamini kama Mungu yupo(nina ground zangu) na kama yupo hatambui hii mifumo iliyowekwa na makundi ya binadamu(dini) na hana uwezo huo anaosifiwa na dini zote zilizoanzishwa.

Nimegundua kwenye kuifuata dini tunapoteza muda tu na hela mfano mimi huu mwaka wa 5 anaenda kanisani ni wife tu ila hajawahi leta chochote kutoka KANISANI zaidi ya sisi kupeleka vitu kibao include hela zetu(sadaka,zaka na michango mingine) na mavuno zaidi zaidi kuna matawi ya muwese la enzi za kuanza kwa mfungo wa kwa resma na bado hayo matawi alienda nayo yeye likabalikiwa akalileta home pamoja na maji ya baraka.

Changamoto niliyonayo ni kuwa wife kajiunga kwenye jumuia alafu huwa anawapa namba yangu viongozi wa jumuia na nimezinguana nae sana kwa hilo swala kiasi kwamba wananisumbua kwa kuniletea ma bahasha mengi ambayo hata nikitoa siamini kama lolote naongezewa zaidi zaidi naona kama napungukiwa kwa sababu natoa kitu live alafu narudishiwa ahadi ya kubarikiwa ambapo siwezi pima hizo baraka kama zinahusiana na kusali au kutoa kwangu.

OMBI LANGU
Nisaidien mbinu za kukwepa ushiriki wa hizi habari za kusali jumuia au kanisani maana nahisi wameona kuna magari matatu yard kwangu ndio maana wananisakama na ndio maana nikiweka hela ndogo kwenye bahasha wanapanic kuwa "huyu sio wa kuchangia elf 20". Kuna siku walifanya uchaguzi wakanichagua kuwa Mhasibu/Mweka hazina wa parokia na huku kwenye jumuia wakanichagua kuwa katibu wa jumuia nilishangazwa na uchaguzi wao wa kushinda bila kushiriki ikabidi nikatae kwa kisingizio cha muda wangu hautoshi kutokana na nature ya kazi yangu na wakataka kulazimisha sana ila walishindwa.

In short najiuliza nawezaje kuwatoka kistaarabu na wakatambua kuwa mimi sihitaji kuwa mshiriki wa hizi imani maana imani yangu mimi nikufight na maisha na kuinjoy matokeo kwa kuwekeza nguvu na akili chache nilizonazo.Naomba ushauri ili kuepuka kuwakwaza majirani na watu tunaoheshimiana nao wasije ona nimejaa kiburi kumbe mimi nimeona kuwa nawekeza effort za kufungua mlango uliochorwa ukutani.

Jamii kushiri nayo kwenye mambo mengine nahitaji ila sio haya mambo ya kusali pamoja nipo tayari kama kuna umoja wa kuchangiana au kuwa na kikundi cha kusaidiana kwenye raha na shida ila sio hivi vikundi vya dini vikekaa kinyonyaji sana yaani wanatupa hewa(maombi) sisi tunawapa vitu tangible n valuable.
Sasa hapo unaanza kufunguka! Believe me or not I don't care! Hizi dini zoote kwa majina yake nyuma yake hiko roho inayokamata fahamu na kuamini unamtumikia Mungu lakini kiundani unatumikia taasisi za kinyonyaji za kibepari na kibwenyenye zilizojenga mtandao na kufungamana na nguvu za giza! Kama wewe ni wa hiyo dini kama ulivyosema na hiyo dini ndo iliyokufungisha ndoa umefungamana na madhabahu ya hiyo dini na hiyo roho ukitaka kuihasi lazima uhadhibiwe na mwisho watasema "unaona? Mungu kaanza kumpiga"! Broh! Kuna njia moja tu ya kukimbia dini nayo kuokoka! Just you and your faith in Jesus Christ! You don't even need to go to divinity churches! Unaweza kuvuta nguvu za Mungu ukiomba na kusikiliza mafundisho sahihi na kusimama kivyako na ukatoboa bila kutishwa na kupigwa na maroho ya mashetani yaliyomo kwenye dini! Maroho ya dini yana nguvu kuliko wachawi!
 
Back
Top Bottom