Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

Naomba kufundishwa mbinu za kuepuka watu wa Jumuiya na Parokia

SDA mimi naona wanachosha kwenye yale mambo ya makambi na sunday school.. masharti ya kula kunywa si magumu sana
Hivi SDA ni kanisa la kihistoria kama lutheran na Roman Catholic au ni kanisa la ki-pentekoste yaani la kilokole?
 
Njia rahisi ni kuwakwepa kwepa kijanja hivyo hivyo. Ikitokea event yoyote unatengeneza excuse usijumuike nao ingawa usiache kwenda katika ibada. Mwishoe watachoka na kukupotezea. Kwetu sisi introverts ni kazi rahisi mno hiyo.
Yaan ni rahisi saana hata hupigizani kelele na mtu unachoamua ndo hicho hicho!!!
 
Njia rahisi ni kuwakwepa kwepa kijanja hivyo hivyo. Ikitokea event yoyote unatengeneza excuse usijumuike nao ingawa usiache kwenda katika ibada. Mwishoe watachoka na kukupotezea. Kwetu sisi introverts ni kazi rahisi mno hiyo.
Sidhani kama njia sahihi, siku ya siku utatengenezewa zengwe utaitwa mbele ya madhabahu kuwa unachaguliwa kuwa Fulani na hutaweza kuchomoa. Unadhani hao viongozi wa parokia na jumuiya huwa hawawasiliani na viongozi wakuu wa kabisa kuwa kuna mtu potential mahala. Utanasa Tu
 
Uliisha waonjesha asali. Ukitaka wasikutafute, usitoe chochote. Hata ukienda kanisani usitoe, wakileta bahasha usitoe, wakiandika barua usijibu, wakikualika jumuiya usiende, wakikualika harambee usiende na usichangie,wakija kwako usiwepo.
Watakuacha.
 
Uliisha waonjesha asali. Ukitaka wasikutafute, usitoe chochote. Hata ukienda kanisani usitoe, wakileta bahasha usitoe, wakiandika barua usijibu, wakikualika jumuiya usiende, wakikualika harambee usiende na usichangie,wakija kwako usiwepo.
Watakuacha.

Hakuna kanisa katoliki linalobembeleza imani ya mtu hivi ati kisa ana hela mtaani halipo. Huyu jamaa anawapiga fix. Bilionea Mrema alitengwa na kanisa sababu hakuwa mshiriki leo huyu kisa magari matatu ati parokia imng'ang'anie? Aseme ishu ni mke wake hana control naye, kwani akimkanya mke wake asimletee watu wa kanisa kwake na hataki mambo hizo si atatatua tatizo feki ambalo halipo.

 
Haya always huandikwa na wasio Wakatoliki,lakini tunaoelewa huwa tunawapuuza.

Hakuna kitu kama hicho ndani ya Kanisa na hatishwi mtu kila mtu na utashi wake wa kuamua anachoona kinamfaa
Jizuie kujilazimisha kupindisha uhalisia wa ile kweli kwa maana ni hakika kuwa yapo matamko yasemayo " usipotimiza ya Jumuiya na ikitokea ukapata tatizo au tukio (mf. ndoa, ubatizo, kifo etc) linalohitaji Msaada wa parokia; hutasaidiwa",.

Hali hiyo inafanana na ya Miaka ya 1,500 na ndio sababu ya kuundwa Kwa uprotestant, hivyo hata Sasa hii post in m'protestant wa yaliyomo Jumuiya.
 
Mimi ni Mkristu dhehebu la RC na nililelewa kwenye familia yenye kufuata mafundisho ya RC na nimebatizwa,kupata komunyo ya kwanza hadi kipaimara na kufunga ndoa ya kikatoliki.

Lililonileta ni kuwa nimekuwa sipendezwi na imani yoyote haswa hizi za dini naona kama uongo na ni mifumo ya watu fulani hapa namanisha Ukristu na madhehebu yake yote naona kama udwanzi na uislam ndo kabisa siulewagi kabisa kwa kifupi siamini kama Mungu yupo(nina ground zangu) na kama yupo hatambui hii mifumo iliyowekwa na makundi ya binadamu(dini) na hana uwezo huo anaosifiwa na dini zote zilizoanzishwa.

Nimegundua kwenye kuifuata dini tunapoteza muda tu na hela mfano mimi huu mwaka wa 5 anaenda kanisani ni wife tu ila hajawahi leta chochote kutoka KANISANI zaidi ya sisi kupeleka vitu kibao include hela zetu(sadaka,zaka na michango mingine) na mavuno zaidi zaidi kuna matawi ya muwese la enzi za kuanza kwa mfungo wa kwa resma na bado hayo matawi alienda nayo yeye likabalikiwa akalileta home pamoja na maji ya baraka.

Changamoto niliyonayo ni kuwa wife kajiunga kwenye jumuia alafu huwa anawapa namba yangu viongozi wa jumuia na nimezinguana nae sana kwa hilo swala kiasi kwamba wananisumbua kwa kuniletea ma bahasha mengi ambayo hata nikitoa siamini kama lolote naongezewa zaidi zaidi naona kama napungukiwa kwa sababu natoa kitu live alafu narudishiwa ahadi ya kubarikiwa ambapo siwezi pima hizo baraka kama zinahusiana na kusali au kutoa kwangu.

OMBI LANGU
Nisaidien mbinu za kukwepa ushiriki wa hizi habari za kusali jumuia au kanisani maana nahisi wameona kuna magari matatu yard kwangu ndio maana wananisakama na ndio maana nikiweka hela ndogo kwenye bahasha wanapanic kuwa "huyu sio wa kuchangia elf 20". Kuna siku walifanya uchaguzi wakanichagua kuwa Mhasibu/Mweka hazina wa parokia na huku kwenye jumuia wakanichagua kuwa katibu wa jumuia nilishangazwa na uchaguzi wao wa kushinda bila kushiriki ikabidi nikatae kwa kisingizio cha muda wangu hautoshi kutokana na nature ya kazi yangu na wakataka kulazimisha sana ila walishindwa.

In short najiuliza nawezaje kuwatoka kistaarabu na wakatambua kuwa mimi sihitaji kuwa mshiriki wa hizi imani maana imani yangu mimi nikufight na maisha na kuinjoy matokeo kwa kuwekeza nguvu na akili chache nilizonazo.Naomba ushauri ili kuepuka kuwakwaza majirani na watu tunaoheshimiana nao wasije ona nimejaa kiburi kumbe mimi nimeona kuwa nawekeza effort za kufungua mlango uliochorwa ukutani.

Jamii kushiriki nayo kwenye mambo mengine nahitaji ila sio haya mambo ya kusali pamoja nipo tayari kama kuna umoja wa kuchangiana au kuwa na kikundi cha kusaidiana kwenye raha na shida ila sio hivi vikundi vya dini vikekaa kinyonyaji sana yaani wanatupa hewa(maombi) sisi tunawapa vitu tangible n valuable.
Kwanza unajichanganya mwenyewe kwenye maelezo yako. Unakaataje Mungu hayupo bila uwepo wake? Huwezi kukataa uwepo WA kitu bila kitu kenyewe Ku exist first. St Anselm, alisema wapumbavu husema hakuna Mungu, wakati mawazoni mwao the concept God is already there.


Tuje kwenye jumuiya na ukatoliki, hakuna kanisa katoliki bila jumuiya. Jumuiya ndogondogo ndio msingi WA kanisa lenyewe rejea kitabu cha matendo ya mitume kwenye agano jipya, wakiristu WA mwanzo mitume WA Yesu na wafuasi Wao waliishi maisha ya jumuiya. Waliweka vitu pamoja na kugawana kadiri ya mahitaji. Kwasasa ndani ya kanisa katoliki jumuiya zinatusaidia kujuana, kusali pamoja na kusaidiana.

Umesema umebatizwa, umepokea komunyo na kipaimara na ndoa ndani ya kanisa katoliki lakini hujaelewa Imani ya kanisa katoliki. Kanisa katoliki linafundisha juu ya Imani na halilazimishi wala kutafuta waumini wabakie ni hiyari yako kama unaona kanisa katoliki si mahali pako nakushauri uondoke huna sababu ya kukwepa jumuiya.
 
Jizuie kujilazimisha kupindisha uhalisia wa ile kweli kwa maana ni hakika kuwa yapo " usipotimiza ya Jumuiya na ikitokea ukapata tatizo au tukio (mf. ndoa, ubatizo, kifo etc) linalohitaji Msaada wa parokia; hutasaidiwa",.matamko yasemayo

Hali hiyo inafanana na ya Miaka ya 1,500 na ndio sababu ya kuundwa Kwa uprotestant, hivyo hata Sasa hii post in m'protestant wa yaliyomo Jumuiya.
Sawa kwa muktadha wa niliye-quote hapo juu yeye ameshayakataa hayo Kanisa linamlazimisha vipi kuyakubali wakati yeye ameshaikataa imani?

Hayo kwenye bold yanamuhusu muumini mwenye imani Catholic akishakuwa siyo Mkatoliki huna namna utamlazimisha mtu aamini.
 
Back
Top Bottom