Naomba kujua Faida yoyote ya Jeshi lolote la Afrika Kuficha Taarifa za Kuuwawa kwa 'Ambush' kwa Wanajeshi wake

kuimarisha molare jeshini na kutoa heshima kwa ndugu wafiwa.
 
Tawala nyingi za ki-Afrika ni za Kinafiki, Ghilba, uongo na ku-fake kila kitu.Kwa kifupi ni tawala zisizostaarabika, tawala za kinafiki na za kidikteta zaidi, haziko real. Wakati tawala nyingi zilizopo nchi nyingi nje ya Afrika, hususani Ulaya na Amerika, ni tawala zilizostaarabika, ziko real, za kidemokrasia ya uwazi na ukweli na siyo wanafiki.
 
Nimeipenda hio ya Puerto Rico alumni umenisahau mimi ni mmoja wa wachache waliosoma nchini Puerto Rico, usisahau
 
Kumbuka vita inajumlisha Propaganda ukitangaza mafanikio ya adui maana yake anakumudu . Pia kumbuka Ugaidi na Media ni marafiki yaani kama wanajeshi wamepigwa na haijadikika kwenye media Gaidi anaona mipango ni migumu na aliyewatuma anashindwa kutoa pesa ya kutosha. Kumbuka Ugaidi wa mozsmbiq tumepandiwa na hao unawasifia kusudi gas na wese tushindwa kufaidika nalo.

Amka toka usingizini maana mpaka sasa kinzal ya urusi inasema imepiga mitambo ya ulinzi ya USA kule Ukrine na USA inakataa na Ukrine ukipiga picha waliposhambuliwa unakwenda jela ndiyo maana hatuna hata picha moja mpaka sasa ya majeruhi wa vita wakiwa wametapakaa damu. Hivyo taarifa za kivita na majeruhi zinaendelea kuwa siri Duniani kote kwa kudhibiti propaganda na kuwavunja moyo wapiganaji wa mstari wa mbele na wale walio tayari kwenda kwenye mapambano. Ukiambiwa Jeshini ni siri elewa.
 
Unataka hao UN waondoe vipengere vya kuwalinda wahuni waliowaunda wao wenyewe?[emoji16].

Yaan kiufupi hao wahuni(magaidi) tunaopigana nao kila siku na hawaishi sababu kuu ni kuwa wako undercontrol ya hao hao ambao ndio wanaucontrol huo umoja wa Kishenzi wa UN na hao AU, kiufupi magaidi na ugaidi hautokuja kuisha maana unafadhiriwa na watu tunaowaamini ambao ndio hao hao wametutungia kanuni na sheria za kupambana na changamoto walizoziunda wao.

Ukiona sehemu siri imevuja ujue ishu ni hii hii, ugaidi hauna nguvu kama Kusingekuwa na NGUVU kubwa nyuma yake inayoufadhiri.

AU, UN, WHO, UNHCR, Red Cross na mashirika ama Miungano mingine ya kinchi ni mambo ya kipuuzi tu ambayo yamewekwa kuchelewesha michakato ya kuyafikia maendeleo ya usalama duniani.

Jambo la msingi kila nchi ilinde mipaka yake kwa umakini bila kumtegemea mjomba wa nchi wanachama.

Dunia hii ina upuuzi sana.
 
Inashangaza sana, congo drc, msumbiji, somalia na sasa sudan tena moto unawaka, kenya isipokuwa makini na ushenzi huo raila anaiwasha moto wenyewe kwa wenye AU, UN na hao akina red cross watakimbilia huko kwa kile kitu kinaitwa peace keeping mission. UN bure kabisa tangu miaka ya 60 haijafanikiwa kumaliza mapigano drc congo pamoja na mission zake nyingi huko
 
Sio hilo tu. Hata machafu ya rsisi na kiongizi huwekwa wazi akiwa hai au amekufa.
Clinton mambo yake machafu yaliwekwa wazi ingekuwa Afrika yangefichwa.
Mambo ya kuficha ficha ni dalili za kuwa unaishi bara la giza.
 
Mkuu
Umeweka hoja nzito sana. Serikali zetu zinatufanya sisi raia kama watoto au mapoyoyo fulani hivi.

Kwa mfano, kule mpakani kwetu na Msumbiji kuna balaa linaendelea na tunaumizwa sana. Ukienda Mtwara kuna amri ya kutotembea usiku baadhi ya maeneo jambo ambalo linapaswa kuidhinishwa na Bunge lakini hakuna taratibu zinazofuatwa kikatiba.

Transparency inapokosekana kwenye issues kama hizi ndo hupelekea hata viongozi wakiumwa hadi kufariki inafanywa siri ilihali kodi zetu ndo zinatumika hapo
 
Ni ujinga kuogopa kusema ukweli dadadeki acha wapigwe hao ngedere wa nchi za Africa
Na wamepigwa kweli kweli katika Ambush wakiwa 400 na Idadi ya Waliotuaga katika Jeshi hilo la Barani Afrika wanafikia 40 huku Majeruhi wakiwa ni Wengi katika Hospitali zao za Kijeshi na ile Kubwa iliyoko wanakoelekea Wawekezaji wa DP World Barani Afrika.
 
Naendelea kusisitiza Jeshi la Bara la Afrika likiwa na Wanajeshi wake 400 waliokuwa Wamejiachia ( Kubweteka ) Kambini Kwao wamekutana na Ambush ya maana kutoka kwa Wanamgambo wa Al Shabaab nchini Msumbiji na Askari 40 Kufa ( Kuuwawa ) huku Wengi wao wakiwa ni Majeruhi kwa Kuvunjika Mikono, Miguu, Viuno, Ulimi, Ugoko, Kolomero na Masikio yao.

Wengine waliagwa katika Hospitali Kubwa ya Jeshi la Barani Afrika Alhamisi iliyopita kwa Maziko na Wengine pia Wanazikwa leo ( Jumapili ) huko huko Barani Afrika.

Na kwa mujibu wa Taarifa nilizonazo kutoka huko huko Jeshi la Barani Afrika Wanajeshi Wawili waliokuwa Mahututi baada ya Kuumia vibaya kutokana na Ambush hiyo nao Wamekufa hivyo Idadi Kuongezeka.

Familia za Wanajeshi hao wa Barani Afrika wameombwa kuwa Kimya na Kupewa ONYO kutosema lolote juu ya Tukio hili ila Fedha zote za Waume zao watapewa Wao na wawe Wasiri mno.

ANGALIZO

Jeshi linalozungumziwa hapa ni la Afrika na siyo la nchi yoyote ile ya Barani Afrika sasa Wewe jifanye Kisokolokwinyo ( Kiherehere ) kuwa umenielewa sana GENTAMIYCINE niliyefuzu vyema Kozi za Masuala Mtambuka huko nchini Cuba na Puerto Rico.
 
Na hizo nchi za Africa kuna moja ya kishamba sana inaficha upumbavu wakiwa mission kazi yao ngono tu
 
Tofauti na majeshi mengine, wao hata wakiuwa magaidi huwa hawatangazi, hivyo hawana sababu ya kutangaza pale ikitokea wamepoteza wapiganaji wao.

Magaidi wanapenda publicity, dawa yao ni misheni ya kimyakimya. Joto likizidi utasikia vilio vya ndugu kuwa vijana wao wanapotea kusikojulikana. Nadhani mnakumbuka kilichowapata wale magaidi wa ule mkoa wa pwani barani Afrika.
 
Na hizo nchi za Africa kuna moja ya kishamba sana inaficha upumbavu wakiwa mission kazi yao ngono tu
Na hiyo hiyo nchi Mkuu kuna batch yake moja imerudi kutoka kwa akina Fally Ipupa na Ferre Gora na Wanajeshi wake kama 15 na Wakike wakiwa ni Watatu ( 3 ) tayari Wameshaambukizwa Dally Kimoko Virus na sasa na Wao Wanavieneza tu huko Makambini Kwao Barani Afrika.

Kazi ipo.....!!
 
HIV
 
Mungu awapumzishe mashujaa wetu
 
Vita ya ugaidi ni ngumu kuliko unavyofikiri.
Hao jamaa hushambulia na kurudi kujichanganya raia ...utawatambua je?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…