Naomba kujua Faida yoyote ya Jeshi lolote la Afrika Kuficha Taarifa za Kuuwawa kwa 'Ambush' kwa Wanajeshi wake

Naomba kujua Faida yoyote ya Jeshi lolote la Afrika Kuficha Taarifa za Kuuwawa kwa 'Ambush' kwa Wanajeshi wake

Unataka hao UN waondoe vipengere vya kuwalinda wahuni waliowaunda wao wenyewe?[emoji16].

Yaan kiufupi hao wahuni(magaidi) tunaopigana nao kila siku na hawaishi sababu kuu ni kuwa wako undercontrol ya hao hao ambao ndio wanaucontrol huo umoja wa Kishenzi wa UN na hao AU, kiufupi magaidi na ugaidi hautokuja kuisha maana unafadhiriwa na watu tunaowaamini ambao ndio hao hao wametutungia kanuni na sheria za kupambana na changamoto walizoziunda wao.

Ukiona sehemu siri imevuja ujue ishu ni hii hii, ugaidi hauna nguvu kama Kusingekuwa na NGUVU kubwa nyuma yake inayoufadhiri.

AU, UN, WHO, UNHCR, Red Cross na mashirika ama Miungano mingine ya kinchi ni mambo ya kipuuzi tu ambayo yamewekwa kuchelewesha michakato ya kuyafikia maendeleo ya usalama duniani.

Jambo la msingi kila nchi ilinde mipaka yake kwa umakini bila kumtegemea mjomba wa nchi wanachama.

Dunia hii ina upuuzi sana.
Suala la kule Cabo Delgado Msumbiji siyo Ugaidi kama watu wengi wanavyodhani, wale wapigani wa kule ni waasi wa kisiasa wa Chama cha Upinzani cha RENAMO. Mgogoro ule ni wa enzi na enzi tangu kuondolewa kwa mkoloni wao Mreno, sababu ya vita ikiwa ni dhulma za kisiasa na kijamii. Serikali ya FRELIMO inalijua vyema kabisa suala hili.
 
S
Sasa kama jeshi la uswahilini limeshambuliwa kwa ambush kwa nini wasiongeze vikosi kwenda kulipiza kisasi kwa kuiteka nchi nzima ya msumbiji kama wao wameshindwa kuwafagia wahuni hao nchini mwao?

Msumbiji inatia aibu kwa kweli, nchi kubwa inasumbuliwa na kikundi kidogo cha kihuni mpaka kusaidiwa na majeshi kidogo ya umoja wa kikanda kama AU na UN, mara SADC

Sasa kama jeshi la uswahilini limeshambuliwa kwa ambush kwa nini wasiongeze vikosi kwenda kulipiza kisasi kwa kuiteka nchi nzima ya msumbiji kama wao wameshindwa kuwafagia wahuni hao nchini mwao?

Msumbiji inatia aibu kwa kweli, nchi kubwa inasumbuliwa na kikundi kidogo cha kihuni mpaka kusaidiwa na majeshi kidogo ya umoja wa kikanda kama AU na UN, mara SADC
Drc-m23, Somalia - Alshabaab, Nigeria-Boko Haram, Ethiopia - Tigrey nk omba yasikukute endelea kusikia tu kwa majirani usiilaumu sana Msumbiji.
 
Suala la kule Cabo Delgado Msumbiji siyo Ugaidi kama watu wengi wanavyodhani, wale wapigani wa kule ni waasi wa kisiasa wa Chama cha Upinzani cha RENAMO. Mgogoro ule ni wa enzi na enzi tangu kuondolewa kwa mkoloni wao Mreno, sababu ya vita ikiwa ni dhulma za kisiasa na kijamii. Serikali ya FRELIMO inalijua vyema kabisa suala hili.
Renamo ni tofauti kabisa na wale magaidi wa Cabo del gado, acha kuchanganya mambo.
 
Majeshi ya Bara la Ulaya, America, Mashariki ya Kati na Mashariki ya mbali huwa hayana Upuuzi wa Kuficha au Kuwaficha Wananchi wa Nchi zao Taarifa za Kuuwawa kwa Wanajeshi wake katika Ambush wakiwa Vitani au katika Misheni za AU au UN.

Ila kwa Bara la la Afrika Majeshi yao hupenda sana kuficha au kufanya Siri kama Wanajeshi wao mfano 400 wakishambuliwa katika Ambush na Wanajeshi 40 Kufa.

Na kinachoshangaza zaidi haya Majeshi ya Bara la Afrika yataficha Taarifa hizo za Vifo vya Wanajeshi wao na hata Kuwatisha Ndugu wasiseme ila wanasahau kuwa Asili ya Waafrika ni Umbea hivyo kuna Ndugu zao tu hawana Uvumilivu na midomo yao itawawasha na Kuwaambia Waafrika Wenzao.

GENTAMIYCINE nichukue nafasi hii kuwapa Pole zangu nyingi Wanajeshi 400 wa Bara la Afrika walioshambuliwa na Ambush Kali huko nchini Msumbiji na Waasi wa Al Shaabab na Wanajeshi kati ya 40 hivi Kufa na Wengine Kujeruhiwa vibaya na sasa Wanatibiwa katika Hospitali za Kijeshi za Majeshi ya huko huko nchi za Barani Afrika.

Geniuses adriz na Bila bila mpo Ndugu zangu? Nawakubali mno kwakuwa huwa ni wepesi mno Kunielewa kwani tulisoma Wote Kozi zetu zile Ngumu na Makini nchini Cuba na Puerto Rico.

Waafrika bhana.....! Unaficha Msiba?
 

Attachments

  • Screenshot_20231219_113054_com.facebook.katana.jpg
    Screenshot_20231219_113054_com.facebook.katana.jpg
    163.3 KB · Views: 1
Renamo ni tofauti kabisa na wale magaidi wa Cabo del gado, acha kuchanganya mambo.
Hujui kwa kina kuhusu mgogoro ule. Uislamu pale umetumika tu kama 'Scapegoat' ya kuweza kuungwa mkono na mataifa mengine na ili wapiganaji hao waweze kupata msaada wa silaha kutoka huko kwa Washirika wao, na wamefanikiwa malengo yao kwa kutumia strategy hio.
 
Ule ni ugaidi mkuu, usijaribu kupindisha maneno.

Hujui kwa kina kuhusu mgogoro ule. Uislamu pale umetumika tu kama 'Scapegoat' ya kuweza kuungwa mkono na mataifa mengine na ili wapiganaji hao waweze kupata msaada wa silaha kutoka huko kwa Washirika wao, na wamefanikiwa malengo yao kwa kutumia strategy hio.
 
Mtu dhaifu kiakili ni vigumu kukubali kwamba ana madhaifu hata yakitokea huyaficha ili kulinda brand dhaifu.
 
Ule ni ugaidi mkuu, usijaribu kupindisha maneno.

Kwani neno "ugaidi" maana yake nini? Je, nini tofauti kati ya ugaidi na "uanaharakati" wa kisiasa au wa haki za binadamu?
Kumbuka:Hata Nelson Mandela alifungwa jela miaka takribani 30 kwa sababu ambayo Utawala wa Makaburu waliiita kuwa in "vitendo vya kigaidi."
Aidha, hata ukichunguza au ukitafiti kwa kina sana kuhusu mgogoro wa Boko Haram kule Nigeria, pia utakuja kugundua kwamba sababu ya kuibuka au kuwepo kwa kundi hilo ni "uasi wa kisiasa," wala siyo ugaidi kama tunavyoaminishwa na watawala wa Nigeria. Na vuguvugu like lilianza tangu miaka ya 1960s wakati wa vita ya kujitenga ya "Biafra," na suala la Uislamu pale limetumika ili kupata uungwaji mkono kutoka kwa nchi za nje na ili wapiganaji waweze kupata msaada wa silaha. Hata maeneo yenye tatizo la Boko Haram ni yale yale maeneo yaliyokumbwa na vita vya kujitenga vya Biafra.
 
Back
Top Bottom