Naomba kujulishwa taratibu za kubadili uraia kutoka kuwa mtanzania bara na kuwa mzanzibari

Hapana, uraia ndio kitu kikubwa kuliko ukaazi, naendelea kusisitiza, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT, kwa maoni yangu, kuiita nchi yako kuwa ni nchi ya kusadikika ni upungufu wa uzalendo.
P
Pia wana Rais wa Zanzibar anayechaguliwa kikatiba na pia wana Spika wa Bunge lao na Jaji mkuu wa Zanzibar.
 
Mkuu umetisha hahaha.. 😂😂😂
Naona umetoa ya uvunguni mwa moyo...😂
 
, Zanzibar sio nchi
Mnachanganya sana watu, sijui kwa faida ya nani?

Kuna mahali popote ndani ya sheria za JMT inayosema "Zanzibar siyo nchi"?
Lakini maandishi yapo chungu nzima tokea huko ndani ya "nchi ya Zanzibar" yanayo itambulisha kuwa ni nchi, na sheria zinazo ainisha mipaka ya nchi hiyo; na wakazi wa nchi hiyo wanaotambuliwa kuwa "WaZanzibari"; akiwemo na rais wa JMT!

Imebaki tu siku moja kumpata shujaa, mZanzibar shujaa ajitokeze mbele na kukana huo uTanzania unaolazimishwa watu wa nchi hiyo wawe nao.
Shujaa huyo atamke wazi hadharani kwamba yeye hautambui uTanzania, anaolazimishwa awe nao bila ya ridhaa yake.
 
Hapana, uraia ndio kitu kikubwa kuliko ukaazi, naendelea kusisitiza, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT, kwa maoni yangu, kuiita nchi yako kuwa ni nchi ya kusadikika ni upungufu wa uzalendo.
P
Mkuu 'Paskali' usifikiri hueleweki kwa hivyo vikaratasi vya uTanzania; kama vilivyo vile vya Katiba yenyewe.

We exist in ambiguity, and as long as maslahi hayaguswi, hayo mengine potezea tu. Hakuna mjinga atakayehoji chochote.
 
Tanzania ni nchi moja ya JMT, yenye uraia mmoja tuu, Zanzibar sio nchi, bali ni sehemu ya JMT, yenye utawala wake wa ndani na utambulisho wake wa ndani uitwao ukaazi, sio uraia, ni utambulisho tuu!.
P
Kaka Pascal utahojiwa tena... This time Zanzibar ni nchi au siyo nchi
 
Mnachanganya sana watu, sijui kwa faida ya nani?

Kuna mahali popote ndani ya sheria za JMT inayosema "Zanzibar siyo nchi"?
Tanzania ni nchi moja tuu ya JMT, yenye sehemu mbili, Tanzania Bara na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani. Hivyo ndivyo isemavyo katiba ya JMT.

Katiba ya Zanzibar inayoitambulisha Zanzibar kama nchi, haitambuliki na katiba ya JMT, hivyo haituhusu, wala haiihusu JMT!.

Kwa vile Zanzibar iko huru kwenye mambo yake ya ndani, rukhsa kujiita vyovyote, as long as mwisho Chumbe, tusiwaingilie.
Hili jambo tumelizungumza sana humu, mimi hadi nimeliandikia makala Je, umefika wakati kutimiza Uzalendo wa kweli wa kwenda kwenye Serikali moja? P
 
Nenda Zanzibar, onana na uhamiaji wa huko watakupa utaratibu.
 
Lazima kuna vigezo vyao, Mbona Mzee Mwinyi na Mzee Jumbe wote ni Watanganyika na wakapata mpaka Urais wa Zanzibar.

Ni kufata taratibu zao tu na vigezo vipo tayari, nahisi licha ya watu hao wawili maarufu, kuna wengi wengine wasio maarufu wana uraia wa huko.
 
Itakuwa ngumu kuliko kuomba uraia wa Israeli.
Nani alikwambia uraia wa israel mgumu kuupata? Wanahaha kutafuta watu huko.

Nani anataka rusha roho za Hams, Hebolla na sasa Wayemeni.

Wale Watanzania wa Bashe walirudi au wameselelea hukohuko?
 
Nani alikwambia uraia wa israel mgumu kuupata? Wanahaha kutafuta watu huko.

Wale Watanzania wa Bashe walirudi au wameselelea hukohuko?
Uwe unalala au ma wewe mme ameenda shirikishi?

Makosa ya kiufundi achana nayo
 
Muungano wetu ni complicated kidogo! Lakin kichaa pekee narudia kichaa pekee ndo atadhubutu kuvunja muungano.Hakuna namna mtu mwenye akili timamu atakubal kupoteza sehem ya nchi yake!Russia na ukubwa wake inanyang'anya maeneo ya ukraine ikidai ni yake nakadhalika. Halaf mwendawazim mmoja anataka kutengane ili tuanze kushare vitu tulivyokuwa tunapata bure na kwa ukubwa kama bahari na airspace.
 
Kwani raia wa huko ni nani hasa. Waarabu?

Jumbe na Mwinyi walikuwa huko kabla ya Tanzania kuwepo, kwa hiyo wao hili haliwahusu. Lakini akina Karume na wao walikuwa huko, Wazanzibari kamili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…