Naomba kuuliza kwa wote wanaomuamini Yesu

Naomba kuuliza kwa wote wanaomuamini Yesu

kuna mkristo nilimuuliza akakiri kua hapa kuna makosa ktka huo mstari
acha ushabiki embu fikiria kweli Mungu wenu mnamuita mpumbavu?
Hiyo Aya hapo haimsemi Mungu kuwa “mpumbavu” wewe ndiye unaetaka kuelekeza isomwe/iseme hivyo na mind you hapa unachuma dhambi bila sababu za msingi.

Mkristo anayejua Imani yake anaelewa huo mstari hapo umemaanisha nini hata wewe unajua kilichomaanishwa hapo ubishi wako tu.
 
Hivi yesu alivaa kanzu au Suluari?na alitawaadha au hakutawadha,na alipiga ishara ya Msalaba au alisujudu. Alikaa kwenye mabenji wakati wa kuswali au alikaa chini kitako


Na mama yake pia Bikira Maria alivaa gauni,sketi,suluari,au Baibui? Alivaa Hijabu au aliacha kichwa wazi,alipiga ishara ya msalaba au alisujudu,aliimba kwaya wakati wa kusali au alikaa kimya
Nikueleweshe kidogo uarabuni na Israel ni jangwa lenye mchanga mwingi sehemu kubwa joto kali ,vumbi jingi

Hivyo mavazi stahiki kwa halina hewa ile ni kanzu sababu haibani hivyo.kuwezesha unafuu wa joto

Zile tinted wanavaa wanawake au nikabu ni kwa ajili ya kujistiri vumbi likitimka lisiwaingie machoni ndio maana hata wanaume wa jangwani huvaa vilemba kujiepusha vumbi kichwani na machoni
Lakini unakuta eneo ambalo hakuna vumbi mwanamke katandika tinted au Nikabu hata macho hayaonekani anasema mwanamke wa kiislamu ndio anatakiwa kuvaa hivyo!!

Vazi lingine ni kobazi sababu mchanga mwingi unaingia kwenye nyayo.Ukiingia nyumba ya mtu unaacha makombazi nje kwa kuwa nyayo zake sababu zimejaa mivumbi mtu anatakiwa kutawadha miguu kabla kuingia ndani ya nyumba yeyote au msikiti

Mavazi haya yanayoitwa ya kiislamu na kutawadha sio hasa takwa la kidini ni takwa la hali ya hewa huko uislamu uliotoka ila ukaingizwa kwenye uislamu

Lakini ukweli hata wakristo waishie maeneo ya jangwa huvaa hivyo na hutawadha kabla kuingia majumbani

Mfano hata kwenye Biblia kulikuwa na magudulia ya kutawadhia miguu kabla mtu kuingia ukumbini kwenye harusi ya Kana ili watu waingie na mivumbi na michango miguuni ukumbini

Yohane 2:1-25 BHN​

Siku ya tatu kulikuwa na harusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo, naye Yesu alikuwa amealikwa harusini pamoja na wanafunzi wake. Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, “Hawana divai!” Yesu akamjibu, “Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado.” Hapo mama yake akawaambia watumishi, “Lolote atakalowaambieni, fanyeni.” Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha. Yesu akawaambia, “Ijazeni mitungi hiyo maji.” Nao wakaijaza mpaka juu. Kisha akawaambia, “Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu.” Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai.

Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi, akamwambia, “Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!” Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini. Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache. Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda juu Yerusalemu.

Basi, akawakuta mle hekaluni watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao. Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazitawanya sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao. Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, “Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!” Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: “Upendo wangu kwa nyumba yako waniua.” Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, “Utafanya mwujiza gani kuonesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?”

Yesu akawaambia, “Vunjeni hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu.” Hapo Wayahudi wakasema, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arubaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?” Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya hekalu ambalo ni mwili wake. Basi, alipofufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakayaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno ambayo Yesu alikuwa amesema.

Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizofanya. Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote. Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
 
Hivi yesu alivaa kanzu au Suluari?na alitawaadha au hakutawadha,na alipiga ishara ya Msalaba au alisujudu. Alikaa kwenye mabenji wakati wa kuswali au alikaa chini kitako...
makanisa hayakuepo,aliabudu ndani ya sinagogi,,Jewish religion
 
Ukiachana na mambo ya kimwili (kuvaa, kula, kutembea nk), naona ungeweka ya kiroho, mfano, hivi Yesu alihubiri kulipa kisasi au kutoa msamaha? Nadhani hapo ndipo panapotofautisha uisilamu (unaohimiza kulipa kisasi) na Ukristu (unaohimiza kutoa msamaha)
kwani kauli ya jino Kwa jino asili yake wapi hasa?[emoji16]
 
Mimi ndio niliouliza swali we ukaja kuniuliza swali badala ya kujibu ila nilipokwambia mimi ndio niliyouliza swali ukasema jibu langu lipo kwenye swali lako uliyouliza, nadhani kuna sehemu unajichanganya.
Ok Ngoja nikusaidie...
Kwahiyo point ni kutangulia kusema ndio huhesabika kuwa ni yaliyosemwa ni ya ukweli?
Hilo 👆 lilikua swali lako...
Kipimo cha ukweli ni Kipi?
Katika fani ya historia tuna vigezo kadhaa vya kupima ukweli wa matukio yaliyotokea zamani kisha yakabahatika kuandikwa.
Narudi kwako kipimo chako cha ukweli wa matukio ya miaka 2000 iliyopita ni kipi?
Nikakuambia jibu lipo ndani hapo👆
Na sasa nimebold kipande husika na kukiwekea uandishi tofauti ili unielewe..

Baada ya hapo nafikiri umeona
Nafikiri husomi kwa makini...Baada ya kujibu hoja yako hujaona swali langu?
Nipe kipimo chako cha namna ya kugundua ukweli wa matukio ya zamani Kwanza kisha Nipo hapa nitathibitisha uwepo wa Yesu.

Jibu lako kwanza Ushahidi wangu utafuatia.

Angalizo usihame katika hoja hiyo pia usitoroke.
Ninakurudisha hapo juu kidogo.....Nafikiri umesoma na Sasa umeelewa.
 
kuna mkristo nilimuuliza akakiri kua hapa kuna makosa ktka huo mstari
acha ushabiki embu fikiria kweli Mungu wenu mnamuita mpumbavu?
Samahani mkuu embu fungua uzi special kwa hili....mada zinakua nyingi hapa...majibu mabishano yawe kule.
 
Hiyo Aya hapo haimsemi Mungu kuwa “mpumbavu” wewe ndiye unaetaka kuelekeza isomwe/iseme hivyo na mind you hapa unachuma dhambi bila sababu za msingi.

Mkristo anayejua Imani yake anaelewa huo mstari hapo umemaanisha nini hata wewe unajua kilichomaanishwa hapo ubishi wako tu.
ubishi wangu vipi wakati ata mtoto wa darasa la 4 atakujibu kma mm nilivokujibu mna huo mstari upo wazi kabisaaa

Kaisome bible yko inaonesha huisomi kabisaaa
 
Samahani mkuu embu fungua uzi special kwa hili....mada zinakua nyingi hapa...majibu mabishano yawe kule.
kwaiyo umeona mm tu ndo ninojaza servers? au mm tu ndo nino comment kila wakati ?

Tatizo ukweli unaumaaa
 
Nasikitika kusema “umepanc” tena sana!

Usually upande wako huwa hakuna utulivu wa mafundisho,kutia chuki na maneno ya karaha ili usiendelee kubanwa ndo trick inayotumiwa kuzima kujulikana udhaifu wa imani yako!
Hhhh pole kijana

Umdhaniae ndie kumbe sie
 
Yes alifanya yote wanayofanya wavaa makobazi wa sasa na alikuwa na kikundi chake cha kigaidi chenye wafuasi 12 wakieneza chuki na vitendo vya kigaidi mjini Yerusalemu na Kapenaumu. Na mwisho alinijitoa muhanga pale msalabani kama wanavyojitoa muhanga wavaa makobazi wa leo

Vipi umeridhika au?
Ww jamaa kwel una akili ya kimkakati
 
Kuna watu watatoa sana macho siku hiyo ambayo Mungu hatajinasibisha na dini yoyote isipokua hii Ykb 1:27.
 
Swali langu ulilielewa lakini?
Ok nafikiri tunapoteza mda hapa... Twende mbele..Kwa sababu naona ubishi usio na mwisho. Acha nikupe jibu straight Aliyetangulia ndiye msema kweli.

Sasa rudi hapa.....

Kipimo cha ukweli ni Kipi?
Katika fani ya historia tuna vigezo kadhaa vya kupima ukweli wa matukio yaliyotokea zamani kisha yakabahatika kuandikwa.
Narudi kwako kipimo chako cha ukweli wa matukio ya miaka 2000 iliyopita ni kipi?
Kisha unijibu sasa Huyo aliyekuja miaka 600AD baadae anaweza vipi kuyasemea matukio ya nyuma ingali hakuwapo.

Nahitaji hicho kipimo na kama akitokea yeyote akakitumia atapata majibu sawa.

Kwa upande wangu nitajikita kumuelezea Yesu Kristo wa Nazareti kama Historical Figure...Si unataka na evidence nitakupatia pia.
 
kwaiyo umeona mm tu ndo ninojaza servers? au mm tu ndo nino comment kila wakati ?

Tatizo ukweli unaumaaa
Nimekujibu kwa namna hiyo kwa sababu yupo pia aliyetangulia kukiomba kufanya hivyo...Hapa utakua unafanya spin off...wala hujazi servers za Jf.

Ni busara sana kujikita kwenye jambo moja.

Sio kwamba sitakujibu swali hilo ila ingekua vyema ukaliweka katika eneo lingine spesheli kwa mada hiyo.
 
Hili swali limenifikirisha sana nataka kujua siku atakapoludi,ataludi katika stairi ipi?amevaa suti kama wachungaji wanavyomuhubiri au amevaa kanzu kama Mashehee
Vazi halina connection na kuja kwa yesu!! Umedanganywa tu weye!! unapomtaja Yesu pia uwe specific ni yesu yupi una maanisha make wako wengi!!........huyo yesu mzungu unaemjua weye wa kwako atakuja na kanzu! ni sawa kwani shida iko wapi?? manake uko sahihi....

Yesu wangu hakuhusu weye!! muache ale Bata Mbinguni kwa Baba! ...... Mbona hatumsemi sie wa kwenu huyo lkn wa kwetu mnalazimisha kila siku eti mnataka kumjua mweee!
 
Back
Top Bottom