Naomba mfano wa Taifa lililoshusha gharama ya maisha kwa kutumia Katiba?


Katiba mpya: vigogo wezi wasiowajibika kwa wizi wao hawatakuwapo:



Katiba mpya: vigogo dhulumati wasiowajibika kwa dhuluma zao hawatakuwapo:



Katiba mpya: mzigo wa vigogo walamba asali wasiolipa kodi hautakuwapo:



Yako mengi muda mchache.

Habari ndiyo hiyo.
 
Brother brother brother nimekuita mara 3, jibu swali langu sio unaniletea ngonjera hakuna mtu anaeishi below poverty line anaeweza kulipa million 30 ili mumewe atolewe jela, hakuna

Ushanielewa sijui
 
Brother brother brother nimekuita mara 3, jibu swali langu sio unaniletea ngonjera hakuna mtu anaeishi below poverty line anaeweza kulipa million 30 ili mumewe atolewe jela, hakuna

Ushanielewa sijui

Pole sana. Ila peleka mrejesho Kwa maana tumedhamiria kweli kweli. Tunachokitaka tunakijua, kwanini tunakitaka tunajua na namna gani tutakipata tunajua.

Bottom line:

"Mtaleta hesabu za wote na wapi mliwapeleka wakiwamo kina Ben, Azory, Lijenje na nani mliwasokomeza kwenye viroba."

Wewe tumemalizana.
 
Sasa katiba ikisema lazima watoto wanahudumiwa na serekali hapo si tayari garama ya maisha imeshuka?
Ikisema Wazee walipwe posho nayo vipi? Maisha si yatakuwa nafuu?
Haya ikisema walio na uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka 18+ na hawana ajira serekali inawajibika vipi hapo maisha si yatashuka?

Mimi naamini katiba ikiwa nzuri na inafuatwa maisha yatashuka
 
Wewe eleza new constitution itasaidiaje mtu anaeishi below poverty line, huna maelezo kaa kimya ujitunzie heshima yako sio unabwatuka bwatuka tu
 
Achilia mbali nguvu ya wananchi kuhoji jambo
Kuna mihimili inakosa nguvu ya kuhoji mihimili mingine mfano kilichomkuta ndugai kinaonyesha jinsi gani muhimili aliyokuwepo nidhaifu
Katiba mpya haitoleta chakula mezani ila itafungua njia ya kukifata chakula na kukileta mezani
 
Hakuna mtu anayeingia JF na hasa kuanzisha na/au kushiriki mijadala ya Jukwaa la Siasa asiyeelewa maana na umuhimu wa katiba kiasi cha kuuliza swali la chini kabisa (on basics) kama la hii mada.

Ni dhahiri kuwa sala la katiba mpya makini ni β€œchukizo” kuu kwa makundi ya kimafia ndani ya CCM. Hivyo, wamesambaza chawa na wanapropaganda kila Kona kupotosha, kuvuruga hata kujaribu kuanzisha mijadala ya ki-β€œintellectual” ili kuwachepushia wadau wanaoonekana kuwa makini katika mizunguko ya midahalo isiyo na mantiki wala mwisho!

Well guys, continue enjoying the endless joyride!😁
 
Acheni upotoshaji, katiba mpya haija contain ubora wa maisha kwa wananchi tu bali inajenga mustakabali mpya wa Taifa na muongozo thabiti kwa maendeleo ya nchi. Acheni ujinga wa kusema katiba mpya haikuletei chakula nyumban shubaamit!
Je na italeta wafanyakazi wapya???
 
Wee mburula watu hawadai katiba kwa ajili ya kushusha gharama za maisha!

Katiba ni kwa ajili ya utawala bora, haki za binadamu na Uhuru!

Umepewa ubongo kwa ajili ya kufikiri na siyo kuwa chawa!
 
Umemjibu vizuri sana, asipokuelewa basi atakuwa kilaza na punguani
 
PUMBAVU! Katiba inaweka viongozi/taasisi imara/makini yenye uwajibikaji ambyo itapelekea kuondoa mambo ya ovyo kama hayo
 
Kazi ya katiba ni mkataba kati ya mtawala na mtawaliwa.
Kazi nyingine kuu ni kutoa mwongozo wa upatikanaji wa haki na pili ni muongozo kwa viongozi namna ya kusimamia na kulinda rasilimali za nchi.

Hizo mnazoongekea ni longolongo.
 
Kama unawaza sawasawa hili swali huwezi kuuliza, either unazingua au we ni mtoto
 
Katiba... Tupiganie kuipata kwanza. Baadhi yetu tutayajua manufaa yake hapo ikishapatikana.
 
Wee mburula watu hawadai katiba kwa ajili ya kushusha gharama za maisha!

Katiba ni kwa ajili ya utawala bora, haki za binadamu na Uhuru!

Umepewa ubongo kwa ajili ya kufikiri na siyo kuwa chawa!
 
Nimekuelewa vizuri... Asante
 
Umeanzisha mjadala kisha umeufunga kwa kutoa uamuzi wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…