Naomba msaada mume wangu amekamatwa na polisi nyumbani saa nane usiku kwa tuhuma za kununua simu ya wizi. Vituo vyote wanadai hayupo na tusimtafute

Naomba msaada mume wangu amekamatwa na polisi nyumbani saa nane usiku kwa tuhuma za kununua simu ya wizi. Vituo vyote wanadai hayupo na tusimtafute

its either ana link ya ujambazi au ugaidi. Ni kweli wasihangaike kumtafuta..

Hii iwe somo tuache kununua simu za mikononi kwa watu ambao hatuwafahamu..
Sheria hazipo hivyo mkuu hata kama ana kosa kila kosa lina adhabu yake na utaratibu wake na si utashi wa polisi , apelekwe mahakamani tutajua mbivu na mbichi ukiruhusu polisi kujiamulia utakuwa umeruhusu watu kuhukumiana mtaani maana polisi nao ni binaadamu kama sisi wana wivu na hulka nyingine za kibinaadamu, unaonaje siku polisi akakukutaa na demu anayemoenda beach akaamua kukumaliza kwa kusema alikuwa jambazi sugu tumemalizana nae
 
Sheria hazipo hivyo mkuu hata kama ana kosa kila kosa lina adhabu yake na utaratibu wake na si utashi wa polisi , apelekwe mahakamani tutajua mbivu na mbichi ukiruhusu polisi kujiamulia utakuwa umeruhusu watu kuhukumiana mtaani maana polisi nao ni binaadamu kama sisi wana wivu na hulka nyingine za kibinaadamu, unaonaje siku polisi akakukutaa na demu anayemoenda beach akaamua kukumaliza kwa kusema alikuwa jambazi sugu tumemalizana nae
Hahahahaha..

Sawa subiri waende polisi
 
Hayo maelezo. Kuna vitu binti anaficha.

Polisi sio wajinga hawakurupuki.

Mpaka polisi wakufate nyumbani usiku wa manane maana yake wameshakujua tabia zako. Mnunuzi wa kawaida angepigiwa simu tu afike kituoni. Ndio angekamatwa..ila wa kufatwa usiku wa manane ujue ni mtu wa matukio.

Kununua simu ya wizi sio sababu kuu

Mimi nilivyoona mkazi wa mburahati na mambo ya simu ya wizi. Akili yangu inaniambia mumewe ni mwizi mtu wa matukio. Kuna maeneo dar es salaam yamejaa watu wa matukio ndio wanaishi. Mojawapo ni kigogo mburahati, tandika kwa kindande, yombo taa nyekundu, chanika. Hayo maeneo yamejaa vibaka na majambazi

Nahisi Huyo mumewe ni mwizi na polisi huwa hawawacheleweshi wezi.
Huwa wanawawahisha wapi????
Inavyoonekana wewe ni miongoni mwa Askari Polisi wadhalimu waliopo hapa nchini ambao kamwe hawakubaliki mahali popote pale, siyo duniani wala siyo mbinguni kotekote hawakubaliki.
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tz, Uhaini ndio kosa kubwa zaidi kuliko yote hapa nchini, lakini Katiba ya Nchi na Sheria nyinginezo hazisemi kwamba Polisi wanapomkamata mtu yoyote yule anayetuhumiwa kwa kosa la Uhaini basi wanatakiwa kumuua on the spot bila kufunguliwa Mashitaka Mahakamani. Polisi hawana mamlaka hayo kisheria.
 
Hayo maelezo. Kuna vitu binti anaficha.

Polisi sio wajinga hawakurupuki.

Mpaka polisi wakufate nyumbani usiku wa manane maana yake wameshakujua tabia zako. Mnunuzi wa kawaida angepigiwa simu tu afike kituoni. Ndio angekamatwa..ila wa kufatwa usiku wa manane ujue ni mtu wa matukio.

Kununua simu ya wizi sio sababu kuu

Mimi nilivyoona mkazi wa mburahati na mambo ya simu ya wizi. Akili yangu inaniambia mumewe ni mwizi mtu wa matukio. Kuna maeneo dar es salaam yamejaa watu wa matukio ndio wanaishi. Mojawapo ni kigogo mburahati, tandika kwa kindande, yombo taa nyekundu, chanika. Hayo maeneo yamejaa vibaka na majambazi

Nahisi Huyo mumewe ni mwizi na polisi huwa hawawacheleweshi wezi.
Na hapo ukute kashapiga watu nondo na kucharanga wenzie viwembe!
 
Niliibiwaga vitu vyote na simu 3 asee 2017,Daah haya mambo magumu ila omba yasikukute,haki itendeke
Wanakudunga na visu au bisibisi! Hawa watu tunaongea tu ila hawafai... inawezekana alivyokamatwa huko ameunganishwa kwenye kesi nyingi hivyo chain inatafutwa. Wawe wavumilivu tu....
 
Kaka naomba unisaidie kunielezea matatizo yangu kwenye ule mtandao wenu wa jamii forums ulionisaodia kipindi kile, wakati huu nahitaji msaada sana

Haya ni maneno ya binti ambaye anaitwa Rahma Shaabani Kiwangala,mwenye mtoto mdogo wa takriban mwaka mmoja mkazi wa Manzese mburahati ,mtaa wa kwa jongo Kata ya makurumla ambaye saa nane usiku akiwa na mume wake nyumbani walifuatwa na mjumbe wa mtaa anayeitwa Zuhura Ngwenje namba zake ni 0715328582 (yupo tayari kutoa ushirikiano) akiwa ameambatana na maaskari wawili WA kituo kikubwa cha polisi CHANIKA MWISHO ambao majina Yao ni Mussa Ally na Bonifas Gablier ambao walimkamata mume WA binti huyu anayeitwa OMAR MWELEA HUSSEIN kwa kosa la kununua simu ya wizi.

Polisi hao wawili walimchukua mpaka kituo kikuu cha polisi CHANIKA MWISHO, asubuhi ndugu wa mtuhumiwa walikuja kumuangalia ndugu Yao na kufuatilia kesi yake wakaambiwa kesi IPO kwenye upelelezi na hawakupewa ruhusa ya kumuona ndugu yao, kuanzia siku hiyo kila wakija kufuatilia wakawa wanazungushwa bila kuruhusiwa kumuona ndugu Yao,na wakati mwingine wakawa wanakuja na mjumbe wao aliyefanikisha kukamatwa kwake lakini jibu la mwisho wakajibiwa kwamba HAKUNA KESI KAMA HIYO KITUONI HAPO NA WASIENDE TENA KUFUATILIA HAPO.

Binafsi nimempgia mjumbe na amekiri kutokea kwa tukio hilo na amesikitika sana kwa sheria kupindishwa na ndugu hao kutopata haki ya kusikilizwa,kujua wapi alipo ndugu Yao na amesema ameenda kwa mkuu kulifikisha swala hilo na amewakuta maaskari hao wapo kituoni hapo na akawatambua kuwa ndio walewale walikuja kumkamata Bwana Omary lakini bado hakupewa ushirikiano wowote.

Tukio hili limetokea usiku WA tarehe 18 mwez WA pili jumamosi kuamkia jumapili saa nane usiku.mpaka Leo umetimia mwezi mmoja bila ndugu kujua lolote na wameambiwa Hakuna kesi Kama hiyo WASIENDE kufuatilia kituoni HAPO.

Tunaomba serikali ya Jamhuri ya Tanzania iwasaidie ndugu hawa kujua ukweli unaofichwa ni upi katika hili, ili iwasaidie familia hii kujua alipo ndugu Yao?

Mke wake na ndugu kwa ujumla wanasema wanahitaj tu kujua hata Kama polisi hawa wamemuuwa ndugu Yao basi waonyeshwe mwili wakazike ama wajue tu kuwa ameuwawa wazike nguo zake.

Inauma sana kwa kweli imagine ni ndugu yako ndio amefanyiwa hivyo,ndugu zangu tumsaidie huyu Bwana asiyejulikaana alipopelekwa,familia yake na mke wake kwa ujumla angalau wafaham alipopelekwa na polisi hawa

Tukumbuke Tanzania ni ya kwetu sote na sote tuna haki sawa.

Mama wasaidie wanao, kwani waliopewa mamlaka ya kusaidia ndio wamepata maguvu ya kukandamiza wenzao
Maumivu yanapozidi na tunakosa msaada...tukubaliane tu...tuanzishe genge la kimafia....litatusaidia kupunguza maumivu...Sema aameen.. 👍
 
Hayo maelezo. Kuna vitu binti anaficha.

Polisi sio wajinga hawakurupuki.

Mpaka polisi wakufate nyumbani usiku wa manane maana yake wameshakujua tabia zako. Mnunuzi wa kawaida angepigiwa simu tu afike kituoni. Ndio angekamatwa..ila wa kufatwa usiku wa manane ujue ni mtu wa matukio.

Kununua simu ya wizi sio sababu kuu

Mimi nilivyoona mkazi wa mburahati na mambo ya simu ya wizi. Akili yangu inaniambia mumewe ni mwizi mtu wa matukio. Kuna maeneo dar es salaam yamejaa watu wa matukio ndio wanaishi. Mojawapo ni kigogo mburahati, tandika kwa kindande, yombo taa nyekundu, chanika. Hayo maeneo yamejaa vibaka na majambazi

Nahisi Huyo mumewe ni mwizi na polisi huwa hawawacheleweshi wezi.
Ni dhambi kumzania mtu bure. Unajifanya ww ni Mungu unajua kila kitu?
 
Anapatkana vipi huyu Kama anaweza kuwasaidia basi tuwape mawasiliano yake awasaidie màana hata hawajui mama na mtoto WA mwaka mmoja asubuhi watakula nini

Inauma sana mkuu
bashite ni wakuvizia kwenye mikutano yake ccm wanamficha si wanamjua anaweza akamtumbua hata waziri yule akiachwa azulule mitaani, aende ofisi za ccm kama wanaweza mpa ratiba zake za mikutano si mwenezi yule, hata pata msaada kokote amtafute bashite kijukuu cha jiwe jpm bashite atamtafutia mtu wake akiwa hai au ametolewa kafara
 
Kununua simu ya wizi mtu afuatwe saa 8 usiku pamoja na mjumbe?
Hapana.
Kuna jambo jingine.
Kama huyo mwanamke hataki kufunguka hawezi kusaidiwa hapa.
Ile michongo ya polisi wahuni wanaouza simu kisha baadaye wanakuja kwa sura nyingine kukukamata na kukutisha kuwa simu iliibwa pamoja na vitu vya milioni 5. Mara mwenye simu kafa kwa kisu wakati unampora.
Hamna hamna milioni 4, 5 inakutoka wanakuachia kiaina kesi haina hata jalada mahali popote duniani.
Wanafanya dhambi kubwa sana. Kesho wanaiuza mtandaoni keshokutwa anashikwa mwingine.
Na kesi za simu unashikwa kwa kuoigiwa simu, wanampigia mtu wako wa karibu kisha huyo mtu wanamwambia akupigie mbele yao ili wakukamate.
Hii ya usiku wa maneno pamoja na wajumbe ni ya Ujambazi au ugaidi.
 
Hayo maelezo. Kuna vitu binti anaficha.

Polisi sio wajinga hawakurupuki.

Mpaka polisi wakufate nyumbani usiku wa manane maana yake wameshakujua tabia zako. Mnunuzi wa kawaida angepigiwa simu tu afike kituoni. Ndio angekamatwa..ila wa kufatwa usiku wa manane ujue ni mtu wa matukio.

Kununua simu ya wizi sio sababu kuu

Mimi nilivyoona mkazi wa mburahati na mambo ya simu ya wizi. Akili yangu inaniambia mumewe ni mwizi mtu wa matukio. Kuna maeneo dar es salaam yamejaa watu wa matukio ndio wanaishi. Mojawapo ni kigogo mburahati, tandika kwa kindande, yombo taa nyekundu, chanika. Hayo maeneo yamejaa vibaka na majambazi

Nahisi Huyo mumewe ni mwizi na polisi huwa hawawacheleweshi wezi.
Hata angekuwa jambazi sawa ila je hawana haki ya kumuona au kumuekea dhamana? Sheria ikoje

Mwezi mzima mtu hayupo
 
hIZI SIMU ZINASHIDA SANAA
WENGINE UNAKUTA WAMEUAAA

OLE WAKUKUTE NASIMU YA MAREHEMU

CHUNGUZAA KAMA ALIEIBIWA YUKO HAI

KAMA NDIO PONA YAKE KAMA KAFAA NDUGU NAPITATU
Majbazi wengine wakifanya tukio huwa wanapora simu ya waliowapora au kuua halafu hizo simu hutupa barabarani wakijua kuna mtu ataokota ataitumia na polisi ndie watamdaka kama jambazi na muuaji

Simu nunua dukani usinunue ya mkononi wala ya kuokota
 
Huyo mjumbe anachoskitika ni kitu gani kama sio mnafiki

Inamaana yeye hajui sheria kwamba polisi hatakiwa kumkamata mtuhumiwa saa nane za usiku?

Alitakiwa asitoe ushieikiano sababu haitakiw kwa mujibu wa sheria polis kumkamata mtu nyumban kwake saa nane usiku
Ukamataji kwa police unafanyika saa yoyote ile,kutegemeana na kosa la mtuhumiwa! Kwa hiyo kazi inabaki kwa mpimaji kosa mwenyewe!!
 
Back
Top Bottom