Naomba tuongee UHALISIA kuhusu biashara ya Real Estate kutumia mfano HAI

Naomba tuongee UHALISIA kuhusu biashara ya Real Estate kutumia mfano HAI

Hii biashara ni nzuri mkuu, usije kuthubutu kuuza hiyo nyumba, utajuta, kikubwa tuendelee kuvumilia tu pengine bank zitatambua biashara hii na kutoa mikopo...
Next time, nenda kanunue kiwanja eneo karibu na chuo alafu jenga chumba choo...wanafunz sio wasumbufu...
Usiuze nyumba
Sijui kwa nn Bank hazijaona hii fursa.
 
Sijui tuwaambie mara ngapi kwamba hii ni biashara kichaa. Unless uwe unaitumia kama security au hizo hela umeziiba ila kama ndio biashara ya kukufanya ufanikiwe my friend hapo umefeli tiyari.

Uliwahi ona mtu kajenga nyumba ikazalisha hela ya kujenga nyumba nyingine ndani ya miaka kumi? Sasa tafuta biashara kama spare parts, electronics, vyakula, retail stores uone nyingine ndani ya miaka mitano inazaa biashara nyingine kama hiyo. Wewe hapo unataka umiliki nyumba nyingi kwa kutumia nyumba hiyohiyo nakuhakikishia utasubiri mpaka miguu iingie tumboni.

Yani bora umiliki bodaboda nyingi nitakuelewa kuliko kumiliki nyumba. Bodaboda inataka kitu kimoja tu, ROHO NGUMU basi. Nyumba ina forces ambazo ni gharama kuzipa control na return yake ndogo.

Yani hata ufanye nini, hutokaa uwe tajiri wa kwanza wa real estate hapa Bongo. Tunao matajiri wa mabasi, madini, mazao, kilimo, usafirishaji, n.k. Tajiri specifically wa biashara za nyumba ni nani hata mmoja tu? Kwanini asiwepo, ni kwa sababu biashara hiyo hailipi wala sio kuwa watu hawaoni fursa
 
Kama eneo ni zuri na nyumba ni ya kisasa,kama ulivyosema ni vyumba viwili ulitakiwa upate 450,000/- kwa mwezi...

Kama kiwanja unacho tayari hiyo 450,000/- unaweza kuanza ujenzi kidogo kidogo tena isiwe nyumba kubwa iwe tu chumba na choo chake na jiko dogo ndio nyumba zinazopata wapangaji kwa haraka...

Hakikisha hiyo kodi sio ya matumizi yako ya kilasiku haitoweza kukuzalishia nyumba nyingine..

kama huna kiwanja napo ni changamoto ,maana itabidi u save ununue kiwanja uanze kujenga ni mlolongo...
 
Sijui tuwaambie mara ngapi kwamba hii ni biashara kichaa. Unless uwe unaitumia kama security au hizo hela umeziiba ila kama ndio biashara ya kukufanya ufanikiwe my friend hapo umefeli tiyari.

Uliwahi ona mtu kajenga nyumba ikazalisha hela ya kujenga nyumba nyingine ndani ya miaka kumi? Sasa tafuta biashara kama spare parts, electronics, vyakula, retail stores uone nyingine ndani ya miaka mitano inazaa biashara nyingine kama hiyo. Wewe hapo unataka umiliki nyumba nyingi kwa kutumia nyumba hiyohiyo nakuhakikishia utasubiri mpaka miguu iingie tumboni.

Yani bora umiliki bodaboda nyingi nitakuelewa kuliko kumiliki nyumba. Bodaboda inataka kitu kimoja tu, ROHO NGUMU basi. Nyumba ina forces ambazo ni gharama kuzipa control na return yake ndogo.

Yani hata ufanye nini, hutokaa uwe tajiri wa kwanza wa real estate hapa Bongo. Tunao matajiri wa mabasi, madini, mazao, kilimo, usafirishaji, n.k. Tajiri specifically wa biashara za nyumba ni nani hata mmoja tu? Kwanini asiwepo, ni kwa sababu biashara hiyo hailipi wala sio kuwa watu hawaoni fursa

Mbona kama umeongea kwa hasira sana mkuu shida nini? Kama boda boda inahitaji roho ngumu kwanini isiwe nyumba? Je biashara haikosi kua na changamoto na changamoto hizo uzitafutie ufumbuzi...Halafu pia tuulizane biashara unafanya ili uwe tajiri tu? Na kama kweli hailipi, kwanini kuna kampuni kubwa za real estate afrika zinazofanya vizuri, je wao waliamka asubuhi wakajenga magorofa na apartments? Tunaona project kubwa kubwa za nyumba sehem mbalimbali kama ni mfuatiliaji, je wao kwanini wanafanya kitu ambacho hakilipi?
 
Umetumia 70M ili ikupatie 450,000 kwa miezi mitatu? Kama umestaafu, umeiba hizo hela, umerithi hapo sishangai. Au kama una biashara nyinginezo hapo umefanya diversification kupunguza risk ya kufirisika napo ni sawa. Tofauti na hapo basi ulifanya the worst investment in your life

Unadhani good investment of the life ilipaswa kua nini bosi kwa milioni 70...

Ingekua mimi mtu amekuja kwangu anaomba ushauri on present situation kwamba nina hiki, nitafanyaje niongeze kingine kwa kutumia nilichonacho, au kubadilisha kuongeza kingine, ningelimshauri kulingana na alichonacho, na sio kuanza kumlalamikia kwamba alichofanya hakikua sawa.
 
ebu fikilia mfano umejenga nyumba yako hadi unamaliza ujenzi umetumia million 24, alafu baadae unakuja kupangisha mpangaji kwa kodi ya mwezi mfano Tsh 400,000/= kwa mwezi, hapo itakubidi usubiri miaka 6 ili uweze kwanza kurudisha million 24 zako kabla haujaanza kula faida, hapo kumbuka ni miaka 6 ili uweze kurudisha pesa yako kwanza kabla haujala faida [emoji1784]………..
Na asset inaongezeka thamani.
 
Wazo zuri...Mimi kwenye hizo ngazi ulizoweka naangukia kwenye hilo kundi la wadogo.
USHAURI:
*Kwa kuanza lazima uwe na shughuli nyingine sambamba hadi hapo utakapoimarika..Fedha inayopatikana hapa kiuchumi inaitwa passive income..inapatikana kidogo kidogo.
  • Hujasema uko wapi lakini nakushauri ujenge kwa kuzingatia mtindo wa maisha ya sasa..watu hawakai na familia kubwa kwa muda mrefu..watoto wanasoma shule za bweni hivyo vyumba viwili na ukumbi tosha sana.
  • Angalia Mji uliopo kwa mfano Dodoma wafanyakazi wengi wako bado na familia zao Dar na maeneo mengine .hivyo rudia ujenzi niliokueleza hapo juu..vyumba viwili toshaa kwa maana ukubwa wa familia ni mdogo.
  • Watu hawataki shida ya kuchangia vitu .hivyo ingia gharama za kila mpangaji kujitegemea kwenye huduma za maji,umeme nk
*Kuwa mbunifu kwenye ujenzi wa majengo yako na eneo ulilokuwa nalo..acha kujenga vyumba vikuubwa ambavyo vitakuchua eneo kubwa.
* Kuwa na mpango mzuri wa ujenzi .mfano eneo lako linatosha kujenga majengo manne..Anza kwanza na moja likamilishe hadi liishe na lianze kutoa huduma halafu fedha kidogo utakazokuwa unapata endelezea ujenzi wa sehemu inayofuatia .hapa wapo ambao wanaanzisha ujenzi wa majengo yote kwenye eneo na kuishia njiani kwa Fedha kwisha.
*Hakikisha eneo linakuwa na faragha na usalama kwa kujenga uzio ..
Kwa Leo hayo yanatosha kwa kuanzia.
Land Lord.
 
Mnajua wabongo wakati mwingine tunashangaza kweli. Sasa wewe unauliza unawezaje kuifanya nyumba moja ya kupangisha ikufanye uwe na nyumba nyingi!!!! Huna tofauti na bodaboda anayeuliza nitafanyaje ili nimilkiki magari mengi ya abiria! Hili nalo ni la kuuliza? Jibu ni kuwa tafuta fedha uongeze nyumba. Na fedha zinatafutwa kwa kufanya kazi kwa bidii huku ukiwa na nidhamu ya matumizi na mipango thabiti. Ukitegemea hiyo nyumba moja kuingiza fedha za kukufikisha kwenye ndoto yako hutafanikiwa.

Kwani yafaa jamii forum kuuliza maswali yapi yanayotakiwa kuulizwa?

Anyway japo umeruka ruka, kama msomi unatakiwa kujibu kulingana na ulichoulizwa na sio kukejeli kwamba nimeuliza swali lisilopaswa kuulizwa, mtu anakuja kwako anakuuliza nina duka la mpesa tigo pesa , napata kamisheni ya laki 2 na 50 kwa mwezi, anaomba ushauri atainukaje kwenda juu zaidi kuongeza mradi au miradi mingine, unamwambia "tafuta fedha kwa kufanya kazi kwa bidii ukiwa na nidhamu ya matumizi na mipango thabiti" uhalisia hapa upo wapi? Mbona ni kama maneno ya wale motivation speakers?
 
Mkuu umelaza hela Sana!!! Kwahyo hela na faida unayotarajia yaani hata haviendani!!
Boss hii 70m nikipata Mimi nitatuta coster mbili!!
Kila siku nalaza hamsini kwa kila moja
2@50,000/= 100,000/=
Kwamwezi zifanye kazi siku 26
100,000 x 26 =2,600,000 kwa mwezi
2,600,000 x 12 = 31,200,000/= kwa mwaka
31,200,000 x 3 =93,600,000/= kwa miaka mitatu
Hapa unakuwa umerudisha mtaji unaanza kula faida!!!
Mkuu ukipata zingine tumia na hii njia!!
hii pia ni kichaa kuandika ni rahisi lakini kwenye uhalisia ni tofauti labda uwe dereva mwenyewe ukiwapa madereva wakuletee hesabu utajuta

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Na asset inaongezeka thamani.
Inflation inaongezeka kwahiyo hiyo future value ya asset sio halisi sana. Bado nyumba inafanyiwa ukarabati kila baada ya miaka kadhaa ili iende na wakati na kuvutia wateja, bado ukarabati kutokana na kupasua mabomba, vyoo kuziba, kuvuja (assumptions tu ila ni vizuri utarajie worst case scenarios). Na kuna muda mpangaji atatoka kisha ukose wa kuishi immediately
 
Huwezi thibitisha hasira kwenye andiko langu kwahiyo niwewe umesoma kwa makasiriko. Taja hayo makampuni ya real estate hapa Tanzania tugundue kitu.

Changamoto zipo kila biashara ila kwenye biashara kuna vigezo vingi vya kuchagua aina ya uwekezaji. Ndio maana nimempa baadhi ya scenario ila nikamshangaa kama ametumia 70M kuzalisha 450,000 kwa miezi mitatu? Ndio mnafanya biashara hivyo?

Ukikosa kuzingatia profitability ya business idea yako basi wewe sio mjasiriamali, mfanyabiashara au muwekezaji. Unless mtu ajenge ili aitwe "baba mwenye nyumba"

Bado hujanijibu swali langu, kwamba kama ni biashara isiyokua na faida yoyote , project kubwa na makampun ya real estate yapo na yanafanya kazi kwa saababu gani? Sina haja ya kutaja kampuni mana ziko nyingi, na usianglie tanzania tu , panua akili pia angalia afrika huko ..

Shida moja ya sisi watanzania tunapenda kua wajuaji sana na pia wengi wetu tuna selfish attitude, nikiwa na milioni 20, nikitaka kufanya biashara ya kuuza viatu, utani crush na kutaka nifanye biashara unayotaka wewe, nisipofanya unayotaka wewe unatoa conclusion kwamba biashara uliyochagua kufanya haina faida yoyote, kwanini kama msomi unayejielewa, mtu huyo unamuambia sasa sababu biashara umeifanya au kuianza na inakuletea kias hiki kwa muda huu, sasa unatakiwa ufanye moja mbili tatu nne tano, either uongeze biashara kama hio au kubadilisha, lakin sisi baadhi ya watanzania utasikia aaah wewe unafanya biashara kichaa, wewe umepotea, wewe this, wewe that, !!
 
Wazo zuri...Mimi kwenye hizo ngazi ulizoweka naangukia kwenye hilo kundi la wadogo.
USHAURI:
*Kwa kuanza lazima uwe na shughuli nyingine sambamba hadi hapo utakapoimarika..Fedha inayopatikana hapa kiuchumi inaitwa passive income..inapatikana kidogo kidogo.
  • Hujasema uko wapi lakini nakushauri ujenge kwa kuzingatia mtindo wa maisha ya sasa..watu hawakai na familia kubwa kwa muda mrefu..watoto wanasoma shule za bweni hivyo vyumba viwili na ukumbi tosha sana.
  • Angalia Mji uliopo kwa mfano Dodoma wafanyakazi wengi wako bado na familia zao Dar na maeneo mengine .hivyo rudia ujenzi niliokueleza hapo juu..vyumba viwili toshaa kwa maana ukubwa wa familia ni mdogo.
  • Watu hawataki shida ya kuchangia vitu .hivyo ingia gharama za kila mpangaji kujitegemea kwenye huduma za maji,umeme nk
*Kuwa mbunifu kwenye ujenzi wa majengo yako na eneo ulilokuwa nalo..acha kujenga vyumba vikuubwa ambavyo vitakuchua eneo kubwa.
* Kuwa na mpango mzuri wa ujenzi .mfano eneo lako linatosha kujenga majengo manne..Anza kwanza na moja likamilishe hadi liishe na lianze kutoa huduma halafu fedha kidogo utakazokuwa unapata endelezea ujenzi wa sehemu inayofuatia .hapa wapo ambao wanaanzisha ujenzi wa majengo yote kwenye eneo na kuishia njiani kwa Fedha kwisha.
*Hakikisha eneo linakuwa na faragha na usalama kwa kujenga uzio ..
Kwa Leo hayo yanatosha kwa kuanzia.
Land Lord.

Asante mkuu, atleast wewe umeweza kunielezea kulingana na kilichopo mezani. Haswa point ya kwanza inayosema kuwepo na shuhuli nyingine hadi hapo kuimarika kutakapokuwepo..
 
Mimi simshauri kwa alichonacho. Sio vibaya kukosea na uzuri ukimkosoa yeye mwenyewe ashaona uhalisia. Kuliko nitumie milioni 70 kujenga nyumba ya kunilipa 450,000 kwa miezi mitatu si bora nijenge sehemu niwe na restaurant. Hapo nikiweka 40M narudi na zaidi ya 1M kwa mwezi hapo wajingawajinga wote kina TRA nishamalizana nao.

Hata ninunue ng'ombe ninenepeshe kisha kuuza kwa wachinjaji. Au kumiliki bucha kadhaa maeneo tofauti. Hiyo 70M si inafungulia bucha za kawaida 7 ukikodisha frame tofauti.

Kuna options nyingi sana za kufanya kuliko mazishi ya 70M ili kupata 450,000 @ 3 months. Nimemuuliza kastaafu, kwamba hakuwahi fanya biashara asije akapotea? Kama ni hivyo sawa
Kwani ndugu ukiwa unafanya kazi au kustaafu huwezi fanya biashara na ukawa na malengo ya kuongeza miradi mingine zaidi , nadhan ni tanzania tu wastaafu wanaonekana ni.kama.watu ambao hawajui biashara au kuna mentality kwamba wanafanya biashara ili waishi tu na kupata hela ya kula tu, na sio ndoto za kujenga empire kubwa kibiashara
 
Mkuu umelaza hela Sana!!! Kwahyo hela na faida unayotarajia yaani hata haviendani!!
Boss hii 70m nikipata Mimi nitatuta coster mbili!!
Kila siku nalaza hamsini kwa kila moja
2@50,000/= 100,000/=
Kwamwezi zifanye kazi siku 26
100,000 x 26 =2,600,000 kwa mwezi
2,600,000 x 12 = 31,200,000/= kwa mwaka
31,200,000 x 3 =93,600,000/= kwa miaka mitatu
Hapa unakuwa umerudisha mtaji unaanza kula faida!!!
Mkuu ukipata zingine tumia na hii njia!!

Nakushukuru mkuu kwa mchanganuo wako, fikiria hela hio ingeisha yote kwa kufanya ufuska, au kuifanyia starehe pombe na wanawake, yote ikaisha,,nadhan ningekua nimeshaoga matusi mengi hadi sasa, lakin sio kwamba cash haipo, ipo lakiin sasa iko katika mfumo wa nyumba.
 
Back
Top Bottom