Sijui kwa nn Bank hazijaona hii fursa.Hii biashara ni nzuri mkuu, usije kuthubutu kuuza hiyo nyumba, utajuta, kikubwa tuendelee kuvumilia tu pengine bank zitatambua biashara hii na kutoa mikopo...
Next time, nenda kanunue kiwanja eneo karibu na chuo alafu jenga chumba choo...wanafunz sio wasumbufu...
Usiuze nyumba
Bank zingekuwa zinakopesha wafanyabiashara hii..nadhani mambo yangekuwa mazuriSijui kwa nn Bank hazijaona hii fursa.
Hii project ni nzuri, ukijenga na kuuza; kama itakuwa kupangisha, itachukua muda mrefu sana kuleta faida
Uko sahihi mkuuFaida ataipata kama hategemei hiyo hela kwa matumizi yake ya kilasiku..
Sijui tuwaambie mara ngapi kwamba hii ni biashara kichaa. Unless uwe unaitumia kama security au hizo hela umeziiba ila kama ndio biashara ya kukufanya ufanikiwe my friend hapo umefeli tiyari.
Uliwahi ona mtu kajenga nyumba ikazalisha hela ya kujenga nyumba nyingine ndani ya miaka kumi? Sasa tafuta biashara kama spare parts, electronics, vyakula, retail stores uone nyingine ndani ya miaka mitano inazaa biashara nyingine kama hiyo. Wewe hapo unataka umiliki nyumba nyingi kwa kutumia nyumba hiyohiyo nakuhakikishia utasubiri mpaka miguu iingie tumboni.
Yani bora umiliki bodaboda nyingi nitakuelewa kuliko kumiliki nyumba. Bodaboda inataka kitu kimoja tu, ROHO NGUMU basi. Nyumba ina forces ambazo ni gharama kuzipa control na return yake ndogo.
Yani hata ufanye nini, hutokaa uwe tajiri wa kwanza wa real estate hapa Bongo. Tunao matajiri wa mabasi, madini, mazao, kilimo, usafirishaji, n.k. Tajiri specifically wa biashara za nyumba ni nani hata mmoja tu? Kwanini asiwepo, ni kwa sababu biashara hiyo hailipi wala sio kuwa watu hawaoni fursa
Umetumia 70M ili ikupatie 450,000 kwa miezi mitatu? Kama umestaafu, umeiba hizo hela, umerithi hapo sishangai. Au kama una biashara nyinginezo hapo umefanya diversification kupunguza risk ya kufirisika napo ni sawa. Tofauti na hapo basi ulifanya the worst investment in your life
Na asset inaongezeka thamani.ebu fikilia mfano umejenga nyumba yako hadi unamaliza ujenzi umetumia million 24, alafu baadae unakuja kupangisha mpangaji kwa kodi ya mwezi mfano Tsh 400,000/= kwa mwezi, hapo itakubidi usubiri miaka 6 ili uweze kwanza kurudisha million 24 zako kabla haujaanza kula faida, hapo kumbuka ni miaka 6 ili uweze kurudisha pesa yako kwanza kabla haujala faida [emoji1784]………..
Mnajua wabongo wakati mwingine tunashangaza kweli. Sasa wewe unauliza unawezaje kuifanya nyumba moja ya kupangisha ikufanye uwe na nyumba nyingi!!!! Huna tofauti na bodaboda anayeuliza nitafanyaje ili nimilkiki magari mengi ya abiria! Hili nalo ni la kuuliza? Jibu ni kuwa tafuta fedha uongeze nyumba. Na fedha zinatafutwa kwa kufanya kazi kwa bidii huku ukiwa na nidhamu ya matumizi na mipango thabiti. Ukitegemea hiyo nyumba moja kuingiza fedha za kukufikisha kwenye ndoto yako hutafanikiwa.
hii pia ni kichaa kuandika ni rahisi lakini kwenye uhalisia ni tofauti labda uwe dereva mwenyewe ukiwapa madereva wakuletee hesabu utajutaMkuu umelaza hela Sana!!! Kwahyo hela na faida unayotarajia yaani hata haviendani!!
Boss hii 70m nikipata Mimi nitatuta coster mbili!!
Kila siku nalaza hamsini kwa kila moja
2@50,000/= 100,000/=
Kwamwezi zifanye kazi siku 26
100,000 x 26 =2,600,000 kwa mwezi
2,600,000 x 12 = 31,200,000/= kwa mwaka
31,200,000 x 3 =93,600,000/= kwa miaka mitatu
Hapa unakuwa umerudisha mtaji unaanza kula faida!!!
Mkuu ukipata zingine tumia na hii njia!!
Inflation inaongezeka kwahiyo hiyo future value ya asset sio halisi sana. Bado nyumba inafanyiwa ukarabati kila baada ya miaka kadhaa ili iende na wakati na kuvutia wateja, bado ukarabati kutokana na kupasua mabomba, vyoo kuziba, kuvuja (assumptions tu ila ni vizuri utarajie worst case scenarios). Na kuna muda mpangaji atatoka kisha ukose wa kuishi immediatelyNa asset inaongezeka thamani.
Huwezi thibitisha hasira kwenye andiko langu kwahiyo niwewe umesoma kwa makasiriko. Taja hayo makampuni ya real estate hapa Tanzania tugundue kitu.
Changamoto zipo kila biashara ila kwenye biashara kuna vigezo vingi vya kuchagua aina ya uwekezaji. Ndio maana nimempa baadhi ya scenario ila nikamshangaa kama ametumia 70M kuzalisha 450,000 kwa miezi mitatu? Ndio mnafanya biashara hivyo?
Ukikosa kuzingatia profitability ya business idea yako basi wewe sio mjasiriamali, mfanyabiashara au muwekezaji. Unless mtu ajenge ili aitwe "baba mwenye nyumba"
Wazo zuri...Mimi kwenye hizo ngazi ulizoweka naangukia kwenye hilo kundi la wadogo.
USHAURI:
*Kwa kuanza lazima uwe na shughuli nyingine sambamba hadi hapo utakapoimarika..Fedha inayopatikana hapa kiuchumi inaitwa passive income..inapatikana kidogo kidogo.
*Kuwa mbunifu kwenye ujenzi wa majengo yako na eneo ulilokuwa nalo..acha kujenga vyumba vikuubwa ambavyo vitakuchua eneo kubwa.
- Hujasema uko wapi lakini nakushauri ujenge kwa kuzingatia mtindo wa maisha ya sasa..watu hawakai na familia kubwa kwa muda mrefu..watoto wanasoma shule za bweni hivyo vyumba viwili na ukumbi tosha sana.
- Angalia Mji uliopo kwa mfano Dodoma wafanyakazi wengi wako bado na familia zao Dar na maeneo mengine .hivyo rudia ujenzi niliokueleza hapo juu..vyumba viwili toshaa kwa maana ukubwa wa familia ni mdogo.
- Watu hawataki shida ya kuchangia vitu .hivyo ingia gharama za kila mpangaji kujitegemea kwenye huduma za maji,umeme nk
* Kuwa na mpango mzuri wa ujenzi .mfano eneo lako linatosha kujenga majengo manne..Anza kwanza na moja likamilishe hadi liishe na lianze kutoa huduma halafu fedha kidogo utakazokuwa unapata endelezea ujenzi wa sehemu inayofuatia .hapa wapo ambao wanaanzisha ujenzi wa majengo yote kwenye eneo na kuishia njiani kwa Fedha kwisha.
*Hakikisha eneo linakuwa na faragha na usalama kwa kujenga uzio ..
Kwa Leo hayo yanatosha kwa kuanzia.
Land Lord.
Kwani ndugu ukiwa unafanya kazi au kustaafu huwezi fanya biashara na ukawa na malengo ya kuongeza miradi mingine zaidi , nadhan ni tanzania tu wastaafu wanaonekana ni.kama.watu ambao hawajui biashara au kuna mentality kwamba wanafanya biashara ili waishi tu na kupata hela ya kula tu, na sio ndoto za kujenga empire kubwa kibiasharaMimi simshauri kwa alichonacho. Sio vibaya kukosea na uzuri ukimkosoa yeye mwenyewe ashaona uhalisia. Kuliko nitumie milioni 70 kujenga nyumba ya kunilipa 450,000 kwa miezi mitatu si bora nijenge sehemu niwe na restaurant. Hapo nikiweka 40M narudi na zaidi ya 1M kwa mwezi hapo wajingawajinga wote kina TRA nishamalizana nao.
Hata ninunue ng'ombe ninenepeshe kisha kuuza kwa wachinjaji. Au kumiliki bucha kadhaa maeneo tofauti. Hiyo 70M si inafungulia bucha za kawaida 7 ukikodisha frame tofauti.
Kuna options nyingi sana za kufanya kuliko mazishi ya 70M ili kupata 450,000 @ 3 months. Nimemuuliza kastaafu, kwamba hakuwahi fanya biashara asije akapotea? Kama ni hivyo sawa
Mkuu umelaza hela Sana!!! Kwahyo hela na faida unayotarajia yaani hata haviendani!!
Boss hii 70m nikipata Mimi nitatuta coster mbili!!
Kila siku nalaza hamsini kwa kila moja
2@50,000/= 100,000/=
Kwamwezi zifanye kazi siku 26
100,000 x 26 =2,600,000 kwa mwezi
2,600,000 x 12 = 31,200,000/= kwa mwaka
31,200,000 x 3 =93,600,000/= kwa miaka mitatu
Hapa unakuwa umerudisha mtaji unaanza kula faida!!!
Mkuu ukipata zingine tumia na hii njia!!