Naomba ushauri: Kijana wangu amepata kazi Shirika la Good Neighbors na Halmashauri, aende wapi?

Naomba ushauri: Kijana wangu amepata kazi Shirika la Good Neighbors na Halmashauri, aende wapi?

Huko Good Neighbors amepata mkataba wa kudumu?
Kama sivyo aende Serikalini sababu mishahara sawa, serikalini job security kubwa, ajira ya kudumu.
Pia kwa baadaye kuna urahisi wa kupata ruhusa ya kwenda kujiendeleza kielimu huku akilipwa mshahara.
 
Ni kitinda mimba wangu. Amepata kazi Serikalini kwenye Halmashauri moja Mkoani Shinyanga na pia kwenye Shirika linaitwa Good Neighbors Tanzania. Mishahara ni kama inalingana,aende wapi?naomba ushauri wapendwa

Mwambie atazame long run benefits Faida za muda mrefu.

Akiwa Serikalini -Atakuwa amepata kazi ya kudumu Ila Serikalini huwa hakuna changamoto za kukua kifikra, kitaaluma wala kiakili Ila faida inabaki hiyo moja kuwa ni ajira ya kudumu ambayo anaweza kuifanya hadi mwisho.

Kuhusu kwenye hilo shirika- faida yake kuna ukuaji wa kitaaluma, exposure, kukua kiakili na kupata uzoefu ambao utamfanya awe marketable na kuwa na potential.

Hasara - anaweza kuwa redundancy, mkataba kuisha, ajira sio ya kudumu n.k

Ushauri.

Utamtazama kijana wako ikiwa sio hard worker - hana roho ya upambanaji hustler, basi muache aende Serikalini.

Ila ikiwa anajiamini na ni MTU mpambanaji mwenye spirit ya Kutaka mafanikio basi muache aende kwenye mashirika atakutana na watu wenye exposure kubwa watamjenga na baada ya mda atakuwa valuable.

Nadhani huu ushauri nimeelezea utapata A,B,C all the best.
 
Kama Halmashauri ni Mkataba wa muda mrefu aende Halmashauri kwasababu Good Neighbours wa kawaida sana...ingekua Mashirika makubwa angeacha hiyo ya Halmashauri...Halafu huyo Jamaa yako anasali kwa Mungu yupi anaempa kazi mbili mbili wakati watu wameoga na mafuta ya manabii hawapati hata Kibarua ??
 
Mkuu ungeelezea kidogo hao good neighbors wanafanya project gani na ni ya muda gani ingekua vizuri zaidi.
Lakini kwa maoni yangu, carrier growth ya kitinda wako ni muhimu sana kuliko the so called job security. Nadhani ni vizuri kijana wako after 3-5 years to come aje afanye evaluation kua nmetoka hapa saiv nipo hapa kwenye carrier yake.
 
Mkuu ungeelezea kidogo hao good neighbors wanafanya project gani na ni ya muda gani ingekua vizuri zaidi.
Lakini kwa maoni yangu, carrier growth ya kitinda wako ni muhimu sana kuliko the so called job security. Nadhani ni vizuri kijana wako after 3-5 years to come aje afanye evaluation kua nmetoka hapa saiv nipo hapa kwenye carrier yake.
Maisha ya kibongo hayana career growth Wala nn.. ukipata kichaka serikalin kahichimbie huko. Mm mwaka jana nilikuwa shirika flani, kazi zao zina work load kubwa sana yani unajitoa mpaka wikend kufanya kazi na mishahra ya kawaida sana.

Mwambie aende halmashaur, atarelax, hela za Bure na secured salary hapo itampa uhuru wa kufanya mishe nyingine hata kwa kuzifatilia kwa makin zaidi.
 
Halmashauri ni kazi ya kudumu ila huko kwenye mashirika ni mkataba, hivyo aache huo mshahara mnono wa muda akale mshahara mwembamba wa kudumu.
Mimi nashauri akachukue mnono wa muda mkataba ukiisha afanye mambo mengine
 
Back
Top Bottom