Naendelea kule mbao na bati,
Sasa pesa 5M haitoshi kupiga bati lakini sina mpango tena wa kuongezea kiasi kilichobaki kama hicho kwa siku za karibuni maana sasa madeni yapo mpaka shingoni, naogopa hata familia sasa itanishinda, hasa karo za shule, lakini sasa kuna uwezekano wa mke mkubwa kuona mambo hapa hayapo sawa labda huyu mwanaume ana kitu sio cha kawaida.
Maana kazidi anaenda tena anarudi usiku mwingi kama kawaida, maana yake hizo over time anazoniambiaga anafanya zipo, na safari za mikoani huko bado anenda sasa tatizo ni is, mbona kama pesa inapungua hapa ndani. Wakati mwingine hata watoto wanarudishwa shule sababu ya karo au wanasubiria sana kwenda shulle zikifungulia.
Lakini wakati mwingine nikiwa naw anaona sina raha kabisa, ilifikia kipindi inabidi anipe pesa na kunifukuza nyumbani nikajumuike na wenzangu baa ili nimtolee upuuzi wangu wa kujiinamia namia hapo ndani.
Hapo ndipo bi mdogo aliponishauri, hiyo pesa ikiendelea kukaa, tutaitumia kwa hiyo ni bora tupige bingo kwenye kuku,
Tukakubalianani wazo zuri ingawa tulikuwa tunajua risk yake, tukanunu kwa mala ta kwanza vifaranga 1500, tukaweka bandani, sasa tunamwomba Mungu vikue salama, kwa mahesabu tuliyopiga tukikuwa na uhakika wa kupiga kama 10 M bila ubishi na hapo bati sasa lingepigwa kama kumsukuma mlevi.
Wiki ya kwanza ikapita vizuri, wiki ya pili ikapita vizuri,ila mifuko ya chakula ndio kasheshe ingawa tulijitahidi sana kuwaangalai kama watoto wetu, wakati mwingine nikilala pale, inabidi nikeshe kwenye kama na mimi ni kuku sasa, maana vumbi langu kila kitu, ili kusikilizia mafua yote na kuwatoa wenye mafua, Wiki ya tatu kabla hata haijafika mwisho, Kila siku tulikuwa tunatoa kuku 30 mpaka 70 waliokufa, siku za mwishoni kwa hiyo wiki ya tatu, tulikuwa tunatoa mpaka 150 kwa siku waliokufa, kiufupi wali survive kama kuku 120 tu tulioweza kuwaza,
Na 5 MILLION IKAISHIA HAPO
SASA? WHATS NEXT
ngoja ninyooshe Miguu kwanza