Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Lea familia zako
Familia ipi mkuu, unamanisha zote au moja,
Kama ni moja ipi? Kama ni zote Mimi nalea ila mwisho najua mtanipa ushauri mzuri tu
 
Aisee Kaka mkubwa polee!, bado nasubiri umalize mkasa wako.
 
Mzee malizana na bi mkubwa Kiri kosa, leta watoto wako hao wawili kwa bi mkubwa, bi mdogo piga chini, beba kila kilicho chako!!
 
Naendelea kule mbao na bati,

Sasa pesa 5M haitoshi kupiga bati lakini sina mpango tena wa kuongezea kiasi kilichobaki kama hicho kwa siku za karibuni maana sasa madeni yapo mpaka shingoni, naogopa hata familia sasa itanishinda, hasa karo za shule, lakini sasa kuna uwezekano wa mke mkubwa kuona mambo hapa hayapo sawa labda huyu mwanaume ana kitu sio cha kawaida.

Maana kazidi anaenda tena anarudi usiku mwingi kama kawaida, maana yake hizo over time anazoniambiaga anafanya zipo, na safari za mikoani huko bado anenda sasa tatizo ni is, mbona kama pesa inapungua hapa ndani. Wakati mwingine hata watoto wanarudishwa shule sababu ya karo au wanasubiria sana kwenda shulle zikifungulia.

Lakini wakati mwingine nikiwa naw anaona sina raha kabisa, ilifikia kipindi inabidi anipe pesa na kunifukuza nyumbani nikajumuike na wenzangu baa ili nimtolee upuuzi wangu wa kujiinamia namia hapo ndani.

Hapo ndipo bi mdogo aliponishauri, hiyo pesa ikiendelea kukaa, tutaitumia kwa hiyo ni bora tupige bingo kwenye kuku,
Tukakubalianani wazo zuri ingawa tulikuwa tunajua risk yake, tukanunu kwa mala ta kwanza vifaranga 1500, tukaweka bandani, sasa tunamwomba Mungu vikue salama, kwa mahesabu tuliyopiga tukikuwa na uhakika wa kupiga kama 10 M bila ubishi na hapo bati sasa lingepigwa kama kumsukuma mlevi.


Wiki ya kwanza ikapita vizuri, wiki ya pili ikapita vizuri,ila mifuko ya chakula ndio kasheshe ingawa tulijitahidi sana kuwaangalai kama watoto wetu, wakati mwingine nikilala pale, inabidi nikeshe kwenye kama na mimi ni kuku sasa, maana vumbi langu kila kitu, ili kusikilizia mafua yote na kuwatoa wenye mafua, Wiki ya tatu kabla hata haijafika mwisho, Kila siku tulikuwa tunatoa kuku 30 mpaka 70 waliokufa, siku za mwishoni kwa hiyo wiki ya tatu, tulikuwa tunatoa mpaka 150 kwa siku waliokufa, kiufupi wali survive kama kuku 120 tu tulioweza kuwaza,

Na 5 MILLION IKAISHIA HAPO

SASA? WHATS NEXT

ngoja ninyooshe Miguu kwanza
 
Mzee malizana na bi mkubwa Kiri kosa, leta watoto wako hao wawili kwa bi mkubwa, bi mdogo piga chini, beba kila kilicho chako!!
Ni rahisi hivyo kupiga chini na kubeba kulicho chako?
Ingekuwa hivyo watu wasinguana kwenye ndoa au kugawana vyumba,
Maana ulipolalia wewe wenzio ndio wanaamkia,

Any way hadithi bado ndefu

Mtanipa ushauri mzuri tu, am sure
 
Mkuu stori ni tamu ila ina vituo vingi sana. Hebu jaribu kumwaga ya kutosha.
 
Ila watoto bwana,
Hivyo hii kauli umeiona ni sahihi kabisa kuitoa kwa mtu alosema ana miaka 50 seriously..?
Bora Dada nashukuru,
Vijana wengine badala ya kuona hili ni somo kwao, wanafikili hayatawakuta, lakini sio mbaya omba sana Mungu yasikukute, ila kwa sababu ni kijana wa kiume sijui,
Labda asitamani wanawake,
Maana wanawake ni wapi pia wana akili wakati mwingine kukuzidi unafikilia
 
Sasa mil 5 ndio imepotea kinachofuatiani nini, Kuna mtu anaweza kunijibu hapo kabla sijaendelea
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Baba hivi unavyotusimulia ndio unapata unafuu fulani toa nyongo zote usiogope kuchambwa hakujui mtu humu
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…