Naomba Ushauri: Nisimame na Baba Mzazi au wa kambo?

Naomba Ushauri: Nisimame na Baba Mzazi au wa kambo?

Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni

Pole na misukosuko.

Navyoiona.

Baba yako mzazi anakuja kuvuna tu, japo alijitokeza mara moja moja ila tambua kwamba msingi wa mtoto ni muhimu sana na huo msingi unajengwa udogoni. Baba wa kambo alikuchukua kama mwanaye anasimama kwenye nafasi ambayo baba yako mzazi alishindwa.

Mpe heshima yake huyo Mzee hata kama ni mshirikina. Angekuwa na nia mbaya na wewe, angekuulia mbali ukiwa mdogo. Ushirikina ni mambo yetu ya kiafrika na ni mambo yake binafsi maadamu hajakushirikisha, tambua anakuheshimu.

Baba yako mzazi pia pamoja na kutokusimamia majukumu yake, alionesha kukutambua na mapenzi yake kwako, lakini hakulipia gharama za wewe kufika hapo. Fikiria asingetokea baba wa kambo kumuoa mama yako na akakubali kukulea wewe ungekuwa na maisha gani? Hapo ndo utaelewa kwamba baba mzazi alifufail.

Ningekuwa wewe, kwa sasa ningemshauri mama arejee mezani waongee, wapange namna ya kuwaruhusu nyie kuendelea na maisha yenu. Baba wa kambo mfanye msimamizi katika mchakato wa kuoa, huyo ndo amekupa maisha.

Baba yako pia umshirikishe akubali na kumheshimu huyo baba wakambo na maamuzi yako ya kumpa jukumu la kukusimamia kwenye ndoa. Yeye utamshirikisha na kushirikiana naye kama baba.

Yote haya unafanya kulinda heshima yako, ya mama yako, baba zako wawil. Lakini zaidi ya yote, unajenga future yako.


I hope nimeongea angalau point moja.
 
Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni
Simama na wote kwa sababu:-
Baba mlezi - kulipa fadhila maana alikutunza
Baba mzazi - ana baraka zako
 
Hongera kwa kuwa na baba wawili. Ni kama Rich dad na Poor Dad. Nenda nao wote kwani hujaonyesha ugumu uko wapi.

Wewe songa na maisha wakati ukiwajulia hali.
Kuhusu ndoa, mwambie huyo dingi kuwa wewe huwezi kumlazimisha mama kurudi...na unahitaji kuoa. Hivyo endelea na mipango ya ndoa.
 
Hiyo miaka 13 mama ambayo hakuwepo nani alikulea? Na ww sio mtoto wake?

Laana nyingine tunazitafuta wenyewe na tunazipata kirahisi sana....! Au umeungana ma mama Yako?

Stick na Baba wa Kambo...huyo Baba mzazi kama kawaida avute noti kistyle...mpulizie mara kwa mara kukwepa laana yake!

Ila maisha mpe baba wa Kambo...
 
Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni
Kaka nakushauri usimame na wote kila mmoja kwa nafasi yake,haki yake na ushiriki wake katika malezi yako. Zingatia kusimamia haki hata kama hisia zako zinakinzana nayo.
 
Baba mzazi na baba mlezi wote ni wazazi wako. Baba mzazi una bloodline nae alitamani kuishi nawe utotoni sema mama yako changamoto, thus hakukutupa alikukumbuka kwa zawadi. Baba mlezi ni mtu muhimu Sana aliyetengeneza future yako.
Mama ni mama haijalishi mapungufu yake. Huo ni ugomvi wao wazazi hayakuhusu.
USHAURI MKUU
1.Simama neutral usiegemee upande wowote waheshimu wazazi wako watatu.
2.Watambue wote ni Baba zako ya huku ni ya huku na ya kule ni ya kule yabakie siri yako, hata mama YAKO usimwambie, maana upo ugomvi wa asili Kati ya mwanamke na mwanaume usioisha hasa kwa waliohitilafiana, wanawake ni watu wanaoishi na bifu, mioyo yao ni migumu kusamehe.
3.Toa matumizi potepote sio lazima uwape wote kwa pamoja. SAsa ndio kipindi Mlezi wako anahitaji Sana fadhila zako
4.Sioni kama pana haja ya kuwaficha watoto wako kutowatambulisha kwa baba zao, sema wanatokea ukoo mmoja.
 
Wote hao wanayo nafasi katika maisha yako, Baba wa kambo ndiye anaonekana kuchukua nafasi kubwa ya malezi yako hivyo huna budi nawe kulipa fadhila juu ya hilo yaani usimtupe kwani masikitiko yake dhidi yako Mungu anaweza kupokea na ukashikwa na shida nk, basi usimtupe, kumbuka alivyokulea isitoshe hata ubini wako ni jina lake ulipokuwa ukisoma shule.

Baba mzazi naye anayo nafasi pekee kwani huyo ndiye damu yako imeanzia hapo, bila ya yeye usingeweza kuja duniani na wala usingepata nafasi ya kwenda kuishi huko kwa baba wa kambo, kwa.jinsi ulivyoeleza baba mzazi naye alikuwa akija kukutembelea na kukuletea zawadi alipopata nafasi hiyo ilikuwa.ni ishara ya upendo kwako na tayari unao watoto na huyo Baba mzazi anawajua na kuwatambua watoto wako isitoshe ndugu wa upande wa Baba mzazi wanakutambua kama.mmoja ya wanafamilia wao basi huwezi kuwakiuka kwani hao ndio damu yako.

Hitimisho ni kwamba; Baba wa kambo anayo nafasi yake kwako kutokana na jinsi alivyokulea halikadhalika Baba mzazi ndiye aliyekuleta duniani na ndiye damu yako na damu ni nzito kuliko maji, basi kila mmoja mpe haki yake inayostahili kulingana na uwezo wako kwani kuhudumia watu wawili kwa wakati mmoja inabidi mtu ujipange lakini utafanyaje na hali ndio imekuwa hivyo, basi Omba Mungu akusaidie.

Hayo ni maoni yangu kulingana na hadithi yako, labda kuwepo na jambo kubwa lililojificha ambalo linakuogopesha na hukulisema, mfano Ushirikina wa baba wa kambo, kwani wewe unahofia nini juu ya huo ushirikina wake??, je unaogopa anaweza kukutoa wewe kafara au?, ushirikina wake upoje?, kumbuka pia kwa huyo baba wa kambo kuna wadogo zako wa damu mnaochangia mama hivyo tayari kumeshakuwepo na udugu kati ya wewe na huyo baba wa kambo kupitia hao wadogo zako.
Ushauri mzuri. wajali wote tu. Kama baba yako mzazi pia ameoenesha upendo kwenye maisha yako ww huna budi kumpenda na kumjali pia. Mda mwengine huwezi jua yeye alishindwana nn na mama ako wakaachana. Vitu vyengine huwezi mwambia mtoto. Utaleta uchonganishi usio na maana kwa mzazi mwenza. Ushauri wangu nenda nao sawa tu utabarikiwa. Usimtenge mtu au kuhukumu kisa hajakulea.
 
Sijaona sehemu "Baba wa kambo" alikunyanyasa.

Ni mshirikina unaogopa atadhuru wanao, mbona hakukudhuru wewe?

Ukiondoa kula vizuri mjini mara moja kwa mwaka " baba mzazi" kuna jambo lolote aliwahi kukusaidia?
Umesomeshwa na nani?

Amekulisha nani?

Nani kasimamia malezi yako?

Unadhani ni baba mzazi kisa tu umeambiwa au kuskia? Una uhakika ni kweli?

Lakini unajua kuwa "Baba wa kambo" alikuwepo pale "providing" wakati unakua.

Ugomvi wake na mama ako haukuhusu Dingi yako ni huyo aliyekulea.

Na uache kumtusi kumuita mshirikina.
Thread closed.
 
Anatumia majina ya baba mlezi kwenye vyeti vipi hili kuna namna ya kuweza kubadili au aachane nalo
 
Eti baba mlezi ni Mshirikina, tena maneno hayo unayapata kutoka upande wa ndugu wa baba.

Huo ni upuuzi. Kama anafanya ushirikina kwenye biashara yake, basi afanye. Si kwa nia ya kulinda mambo yake? Kakudhuru? Jibu ni Hapana. Mama yako aliondoka miaka 13 imepita sasa, angekuwa na nia ungekuwa msukule wake muda huu.

Hao ndugu wa baba ni washenzi sana. Wanataka kukuvuta uegemee upande wako zaidi. Achana nao.

Bila kusita sita, enenda na baba yako mlezi. Huyo ndiye mzee wako. Kakulea na kukukuza mpaka umekuwa jitu. Gharama zake unazijua!? Kama ni hivyo vichips vya mara moja moja kutoka kwa sperm donor, hata mtu yeyote angeweza kukutendea hayo. Muheshimu tu kama mbegu iliyokutengeneza.

Nakushauri, kuwa makini sana na watu wanaopenda kuwaongelea wengine kwa mabaya tu.
 
Simama na wote pale wanapokuhitaji, sijaona sehemu ukisema kuna aliekubagua kipindi unakua…so ni vyema kutokuwabagua pia. Fanya kwa kila mmoja kadri uwezo wako utakapoishia
 
Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni

Simama na atakayesimama na wewe.
Hayo mengine waachie Waume wa Baba yako.

Atakayekukorofisha piga Chini, akijirudi mnaendelea mlipoishia
 
Eti baba mlezi ni Mshirikina, tena maneno hayo unayapata kutoka upande wa ndugu wa baba.

Huo ni upuuzi. Kama anafanya ushirikina kwenye biashara yake, basi afanye. Si kwa nia ya kulinda mambo yake? Kakudhuru? Jibu ni Hapana. Mama yako aliondoka miaka 13 imepita sasa, angekuwa na nia ungekuwa msukule wake muda huu.

Hao ndugu wa baba ni washenzi sana. Wanataka kukuvuta uegemee upande wako zaidi. Achana nao.

Bila kusita sita, enenda na baba yako mlezi. Huyo ndiye mzee wako. Kakulea na kukukuza mpaka umekuwa jitu. Gharama zake unazijua!? Kama ni hivyo vichips vya mara moja moja kutoka kwa sperm donor, hata mtu yeyote angeweza kukutendea hayo. Muheshimu tu kama mbegu iliyokutengeneza.

Nakushauri, kuwa makini sana na watu wanaopenda kuwaongelea wengine kwa mabaya tu.

Mshirikina ni mshirikina, mshirikina hajawahi kuwa MTU Mzuri.
Hata awe NI mama yako.

Ukishagundua mtu ni mshirikina kaa naye Kwa machale. Ikiwezekana muepuke
 
Back
Top Bottom