Naomba Ushauri: Nisimame na Baba Mzazi au wa kambo?

Naomba Ushauri: Nisimame na Baba Mzazi au wa kambo?

Sijaona sehemu "Baba wa kambo" alikunyanyasa.

Ni mshirikina unaogopa atadhuru wanao, mbona hakukudhuru wewe?

Ukiondoa kula vizuri mjini mara moja kwa mwaka " baba mzazi" kuna jambo lolote aliwahi kukusaidia?
Umesomeshwa na nani?

Amekulisha nani?

Nani kasimamia malezi yako?

Unadhani ni baba mzazi kisa tu umeambiwa au kuskia? Una uhakika ni kweli?

Lakini unajua kuwa "Baba wa kambo" alikuwepo pale "providing" wakati unakua.

Ugomvi wake na mama ako haukuhusu Dingi yako ni huyo aliyekulea.

Na uache kumtusi kumuita mshirikina.
Sina haja ya kutoa tena ushauri...Huyu jamaa hapa kashamaliza kilakitu.
1.Muheshimu sana mtu ambaye huna damu naye halafu akakusimamia katika maisha yako bila manyanyaso
2.Hao ndugu wa baba mzazi wanakushirikisha mambo yao kwasababu ushakuwa mkubwa na una kipato chako. Kipindi upo mdogo ulishawahi kuwaona wakikusaidia?
Achana na mambo ya baba mzazi, yeye mpe heshima yake kama mzazi wa damu tu.
Lakini mwenye kujua uchungu wa kulea ni huyo baba wa kambo, na siku ikatokea amepiga goti kumlilia mungu juu yako aisee machozi yake hayataenda bure.
Najua damu ni nzito kuliko maji na mtu kumfahamu na kumjua mzazi wako original ni suala la kujivunia.

Ila za kuambiwa changanya na zako "Mbayuwayu"
 
Kama jaribu kujigawa kwa kidogo walichonacho uwasaidie,wote kama wanahitaji msaada wasaidie kulingana na uwezo wazo,kitendo cha baba wa kambo kujitolea kumchukua mama yako na wewe basi sio kidogo
 
Ni vyema ungeshauri kwa namna ambayo sijielewi.

Mkuu, kuna kunyanyaswa kisaikolojia. Mfano kuna kupindi alikuwa akimpiga mama waziwazi au kugombana waziwazi. Tulishawahi kulala kwa watu mara kadha wa kadha. Sikupata ule upendo wa karibu kama mtoto na hivyo kunijengea hofu na kutojiamini kwa kuwa mara nyingi alikua akigomba na kufoka kwa nguvu.
Pia mama alivyoondoka nilikua chuo mwaka wa kwanza, nakumbuka alishawahi kuniandikisha ada.
Hakuwa na upendo ule wa kutoka moyoni huenda alifanya kwa kuwa nilikua nae.

Swali nililojiuliza ni kwamba kwa kipindi hicho ni kweli alikosa mwanamke wa kumwoa asiye kuwa na mtoto??
Hii ilikua nia maana hata mdogo wangu kwa mama ulemavu wake ni wa kutupiwa yani aligeuzwa kama chuma ulete (sijui niliwekeje hili.)

Kingine ni yeye kunitaka kufanya biashara zake ambapo misingi yake ni ya kishirikina.
Nimeona mengi na sipendi kuyaandika hapa maana naweza tambulika. Kwa sasa biashara zimedorora, na hivi karibuni nilienda likizo nyumbani, niliyosimuliwa na dogo na niliyoyaona, haina budi kumuita mshirikina, Mungu anisamehenkama nakosea.

Asante

.
Nilivyo soma maelezo haya nimeumia sana tena sana.
Yaani ningekuwa nimeoa mwanamke mwenye mtoto ningefukuza huyo mtoto pamoja na mama yake na kesho wasingefika.
Samahani ila nina hasira sana na wewe yaani mtu akulee na kukusomesha umwite mshirikiana.
Vipi hao ndugu wa baba yako na baba yako walikuwa wapi kukushirikisha ukiwa upo shule?
Kuhusu kugombana na mama yako unataka kusema ugomvi ilikuwa sababu ni wewe?
Msomi alafu unaamini uchawi ambao huwezi kuthibitisha hopeless kabisa.
Je na wewe ukizaa mtoto mwenye ulemavu itakuwaje, naona wewe saivi umeanza kuenda kwa waganga ndio walio kuambia hata tatizo alilonano mdogo wako ni baba mlezi.
Wewe tuambie kuwa umemtenga maana hata watoto humwambii si hapo umemtenga tayari ila baba yako aliye kukimbia umemwambia wakati yeye hakukumbia kuwa yeye ni baba yako bali mjomba.

NGOJA NIKUULIZE SWALI

Hivi wewe unaweza kukubali hao watoto wako walelewe na baba mwingine ungali upo hai?
Ukijibu swahili hilo jaribu kufikiria kama baba yako anakupenda kweli.

NB mitoto ya kambo mingi ina akili kama za mtoa mada. Kama unailea kuwa tayari kukutana na matusi kama ya mtoa mada ili ujiandae kisaikolojia
 
Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni
Baba ni baba tu, damu yako.
Heshima kwa baba wa kambi nayo ni muhimu.
 
uwe na HEKIMA, umeshakuwa mkubwa....wote walikupenda.....heshimu UPENDO wao....wacha FIKRA za KIBAGUZI....
 
Mkuu pole sana ila unapitia kama ninayopitia mimi ila tofauti yetu ni kuwa mimi bimkubwa aliondoka miaka miwili imepita saizi anadai talaka kashafungua kesi me nimepewa kazi kumshawishi mama aachane na hilo jambo japo siwezi hukumu moja kwa moja makosa ni ya nan?
 
hii kitu ni rahisi sana anza kumuita baba mzazi ano kama mwanzo ...piah mjali sana baba wa kambo mlee kama alivokulea ww ....na mara moja kwa mwaka toka na baba mzazi mtoe out umnunulie msosi wa maana kama alivyokuwa anakufanyia ww.... ukiwa mdogo
 
Ukisikia binadamu hana shukrani ndio huku.Baba wa watu kakulea tangu mdogo wakati baba yako yupo anahangaika na familia nyingine huko.Embu muda mwingine tuwe watu wa shukrani.Baba yako ni mshirikina kwa hiyo hakukuloga miaka yote hiyo aje akuloge sasa?
 
Habari Wakuu, nakuja mbele yenu kuomba ushauri, japo nimepata shauri mbalimbali za hapa na pale kwa watu wa karibu na wa mbali niliowahi kukutana nao.

Nianze na historia yangu kwa ufupi. Nilizaliwa mwanzoni mwa miaka ya 90.
Mama alizalia nyumbani kwao wakati bado ni mwanafunzi, haikua rahisi kwa maelezo yake kwa jambo la kubeba mimba ili hali walikua jamii maskini na wapo watoto 7 kwa wakati huo japo wamezaliwa wengi zaidi ya hao.

Ilifika kipindi walimfukuza nyumbani na kuenda kukaa kwa mama mmoja mpaka alipojifungua.
Miaka hiyo ya 90 mwanzoni nikiwa bado mdogo aliolewa kwa ndoa na mwanamume mwingine ambaye sio baba mzazi.

Hakika ndoa ilikua ya kifahari maana sio kwa picha hizo nilizoona kwenye albamu ya picha enzi hizo. Sherehe ilifana sana.

Mwaka 1997 ulitokea ugomvi mkubwa kati ya mama na baba wa kambo, mama aliamua kuondoka na kurudi kijijini ila hakufikia kwa baba na mama yake ila kwa rafiki yake kipenzi wa kusoma nae.

Nakumbuka rafiki yake na mama alikua akiiuza baa maarufu hapo kwenye hiyo wilaya, ambapo alitupa chumba kimoja wapo cha wageni ili tujihifadhi hapo.

Siku moja nikiwa nacheza nje na watoto wenzangu, babu alipita na kuniona maana palikuwa na maarufu na babu alikuwa mtumishi wa serikali hivyo akitoka kupokea mshahara dirisha la halmashauri basi hupita kwenye hiyo baa na kupata kinywaji.

Aliponiona akauliza mama yuko wapi?

Watoto hua hatuna siri, basi nikajibu yupo ndani. Kisha babu akaondoka zake. Jumapili nilimuona bibi ghafla akimsihi mama waondoke nae kurudi nyumbani.

Nakumbuka siku hiyo nilitembea umbali mrefu sana hadi tukafika kwa babu na bibi. Tulikaa hapo kwa muda wa siku 7, na nilikua nasoma darasa la 1, hivyo nilikua naenda shule ya jirani ili nisikose masomo, babu aliomba kwa mkuu wa shule nisome hapo.

Jumapili ya hilo wiki baba wa kambo alikuja kutuchukua na land rover 109.

View attachment 2567033
Tukarudi mjini. Maisha yakaendelea japo nilikua mtoto sio vyote nakumbuka.

Nakumbuka siku moja tulijipata nyumbani kwa msimamizi wa ndoa ya baba wa kambo na mama. Sikumbuki kwanini. Nilikaa pale kwa muda mrefu huku nikiendelea na masomo yangu ya darasa la 2.


Tarehe 31 Desemba 1999 tulihamia kwenye nyumba aliyojenga baba wa kambo nje kidogo ya mji.

Mambo yalizidi kuwa mabaya, ugomvi ulishamiri kwa miaka mingi sana japo mama hakuwa anaondoka tena kurudi kwao, maana yake alipambana na hali yake maana hapo familia iliongezeka na kufikia idadi ya watoto wa 3 ambapo wa 2 walikua ni wa baba wa kambo

Kipindi chote cha utoto baba mzazi alikuwa anakuja kwa mwaka mara moja kuniona shule ya msingi na tulipiga picha na kwenda sehemu za mjini na kula vizuri. Nakumbuka baba mzazi nilikua namuita mjomba. Maana watoto niwaropokaji. Japo alikuwa akinunua zawadi kwa ajili yangu, mama alizificha au kugawa ili kulinda ndoa yake.

Ilifika hatua yale maisha ya ugomvi na amani kukosekana nyumbani, mama aliondoka ghafla bila kujua alipokwenda.

Ikumbukwe kwa miaka yote hiyo, hakuna mtu alitetamka kwamba nina baba mzazi ambaye yupo sehemu fulani, so kwa utoto ule nilijua baba wa kambo ndie baba mzazi. Hata majina ya shule nilitumia ya kwake.

Tusonge mbele zaidi, nilipofika advanced level, form 5 na 6 nilianza kwenda nyumbani kwa baba mzazi na mawasiliano yalipamba moto kwa kipindi hiki. Nilikua namiliki simu so ilikua rahisi kuwasiliana.

Baba mzazi alinieleza sababu kwanini hakumuoa mama, na akaoa mwanamke mwingine. Sikua huru sana wakati nipo kwa baba mzazi na ukizingatia maam wa kambo yupo maana ni mazingira mageni kwangu.. Uzuri ni kwamba nilikaa kwa baba mzazi kipindi cha likizo fupi tu.

Tuendelee mbele zaidi.
Kwa sasa ni mwajiriwa wa serikali, baba mzazi amekwisha staafu na baba wa kambo alikua mfanyabiashara lakini kwa sasa kasi na uwezo umepungua na hana msaidizi kwakua mwanae wa kwanza kwa mama ni mlemavu na wa pili bado anasoma chuo.

Kwa sasa nipo kwenye kipindi cha kuhitajika na wote, baba mzazi na wa kambo kwenye mambo mbalimbali.
Mfano nimeshindwa kufunga ndoa kisa baba wa kambo kutaka mama arudi kwanza nyumbani baada ya kuachana miaka 13 iliyopita.

Ndugu wa baba mzazi wamekua wakinitambua na kunishirikisha kwenye mambo mbalimbali ya kifamilia sasa, na kuna baadhi ya vitu baba wa kambo anavijua na vingine havijui na hii ni kutokana na ukaribu na urafiki wangu na baba yeyote nitakavyoona.

Mfano; baba wa kambo ni mshirikina kwenye biashara zake, hivyo sijawahi mueleza kuhusu watoto niliyozaa, japo baba mzazi anawajua wote.

Niwaombe ushauri wana jamvi, nisimame na yupi kwa sasa?

Pili, mimi sio mwandishi mzuri hivyo muniwie radhi.

Tatu, nipo tayari kutoa ufafanuzi mzuri endapo kuna mahali hapajaelewekaa vizuri.

Nia nikupata ushauri.
Asanteni na karibuni
Ada za shule alilipa nani?,baba mlezi au baba mzazi?
 
Mkuu

Pole

Waheshimu wote kama BINADAMU!

Lakini wekeza nguvu ZAKO KWAKO kea maisha yako ya familia!oa anzisha familia ili kipato Chako kitumike huko!

Usiwekeze kipato Chako kwao bali KIDOGO Sana pale inapobidi kama maradhi n.k!

Usichotwe akili na yeyote kati yao,FAINALI uzeeni pigania familia yako BINAFSI ifanye Kuwa TAASISI pekee!Kuwa mbinafsi na familia yako huku ukiwajali KIDOGO KIDOGO Sana!

Mshirikishe Baba wa kambo Mambo muhimu kama kuoa kwa mbaaali usimtegemee Sana!!

Mwanamme ukishakua na kazi TU panyae buku WENGI huibuka na kutaka kutafuna kila kitu Chako!ukiruhusu TU your gone my friend!!

KUA MBINAFSI JALI FAMILIA YAKO IFANYE KUWA TAASISI HATA MAMA YAKO AKIFELI MAISHA UJE UMLEE KATIKA UZEE WAKE!!

UMENISIKIA JAMAA!!!?

DONT MESSUP BY DANCING THEIR TUNES!!
Sasa hao panya buku wanaotafuta malisho kwako ndio waliokulea jamaa
 
Nimegundua mliooa single mama mnamshawishi sana Kijana amtelekeze baba yake mzazi kisa ugali wa baba wa kambo hiyo haikubaliki wahenga wanasema baba ni baba. Kijana kua makini na wapotoshaji
 
Angalia ni nani kati yao ameonyesha kukupenda na kukujali wakati wote, huyo ndiye Baba.
 
Wote hao wanayo nafasi katika maisha yako, Baba wa kambo ndiye anaonekana kuchukua nafasi kubwa ya malezi yako hivyo huna budi nawe kulipa fadhila juu ya hilo yaani usimtupe kwani masikitiko yake dhidi yako Mungu anaweza kupokea na ukashikwa na shida nk, basi usimtupe, kumbuka alivyokulea isitoshe hata ubini wako ni jina lake ulipokuwa ukisoma shule.

Baba mzazi naye anayo nafasi pekee kwani huyo ndiye damu yako imeanzia hapo, bila ya yeye usingeweza kuja duniani na wala usingepata nafasi ya kwenda kuishi huko kwa baba wa kambo, kwa.jinsi ulivyoeleza baba mzazi naye alikuwa akija kukutembelea na kukuletea zawadi alipopata nafasi hiyo ilikuwa.ni ishara ya upendo kwako na tayari unao watoto na huyo Baba mzazi anawajua na kuwatambua watoto wako isitoshe ndugu wa upande wa Baba mzazi wanakutambua kama.mmoja ya wanafamilia wao basi huwezi kuwakiuka kwani hao ndio damu yako.

Hitimisho ni kwamba; Baba wa kambo anayo nafasi yake kwako kutokana na jinsi alivyokulea halikadhalika Baba mzazi ndiye aliyekuleta duniani na ndiye damu yako na damu ni nzito kuliko maji, basi kila mmoja mpe haki yake inayostahili kulingana na uwezo wako kwani kuhudumia watu wawili kwa wakati mmoja inabidi mtu ujipange lakini utafanyaje na hali ndio imekuwa hivyo, basi Omba Mungu akusaidie.

Hayo ni maoni yangu kulingana na hadithi yako, labda kuwepo na jambo kubwa lililojificha ambalo linakuogopesha na hukulisema, mfano Ushirikina wa baba wa kambo, kwani wewe unahofia nini juu ya huo ushirikina wake??, je unaogopa anaweza kukutoa wewe kafara au?, ushirikina wake upoje?, kumbuka pia kwa huyo baba wa kambo kuna wadogo zako wa damu mnaochangia mama hivyo tayari kumeshakuwepo na udugu kati ya wewe na huyo baba wa kambo kupitia hao wadogo zako.
sahihi
 
Hii kitu iliwahi Nikuta historia hazipishani Sana,,, wote wana umuhimu sana ila aliekuzaa is the best

Kuna ishu ilinikutaga halafu nikajikuta namuhitaji sana baba mzazi kuliko wa kambo japokua nimelelewa na baba wa kambo na baba mzazi nilimuweka kando kutokana na historia alionipa mother

Oyaaa wewe nilimuhitaji dingi mzazi kinoma halafu ndio alishafariki roho inaniumaga mpka Leo nilikua nakosea kumbagua haya maumivu yake hayajawah kufutika

Wote wana umuhimu ila damu yako is the best
 
Back
Top Bottom