Naombeni msaada wa haraka, NMB wamenikalia kooni

Naombeni msaada wa haraka, NMB wamenikalia kooni

Wandugu poleni na majukumu, mwaka huu mwezi wa 2 nilienda kuwapelekea deni la loarn board walinunue na kwa kuwa nilikua na mkopo nao hao NMB wakanipigia mahesabu ya jumla kuwa pamoja na kununua hilo deni na kutoa deni lao watanipa jumla ya Tsh 5,660,000 nikasema poa tu kwakuwa nilikua na uhitaji sana, kufupisha stori ni kuwa jumla ya mkopo wote walinipa 17,400,000, sasa walipoingiza mimi nikakuta jumla ya 9,456,000 kwenye akaunti yangu.

Kwa haraka nilijua kuwa hiki ndicho kiasi changu nikatoa baadhi ya pesa na kuendelea kumalizia kibanda changu na kumaliza pesa yote. Sasa baada ya siku 10 afisa mikopo wa NMB akanipigia kuwa nirudishe mpunga wote yaani ile 9,456,000 maana lile deni la Loan Board halijalipwa bado!

Nikamuuliza kwanini hajalipa akasema mimi niliwahi kutoa pesa kabla hawajakata! Nikawapigia makao makuu, (audio clip ninazo) wakadai kuna makosa pande zote kwanza wao walitakiwa washikilie hiyo pesa kwanza mpaka miamala yote ifanyike, lakini pia walitakiwa ndani ya saa 72 kuwasiliana na mteja maana kumuachia mtu pesa zaidi ya wiki moja na kipindi hiki tunakijua ni mtihani, lakini pia wakasema nilifanya kosa la kutoa pesa ambayo ilizidi (kitu ambacho nilikubali) sasa jambo la ajabu wameniwekea credit -4,234,000 kwenye mshahara wangu na hivyo mshahara wangu wamezuia kwa ajili ya deni hilo.

Nimefanya njia zote ikiwemo kwenda tawini na kuongea nao, kuandika maelezo n.k lakini mpaka sasa wamegoma na option wananipa ni kurudisha pesa.

Nisaidieni wakubwa maana nimewaomba walau wakate kidogo kidogo pia wanagoma na sasa wanashikilia mshahara wote mpaka deni liishe ni zaidi ya miezi 8 na wote tunajua maisha ya mfanyakazi bila salary. Nisaidieni nifanyeje.

NB: Sipendi kuulizwa kwanini niliamua kutumia pesa zote.
Washitaki ofisini kwako, hawatakiwi kukata mshahara wako wote, kisheria lazima 1/3 ibaki, hao NMB wasubilie au waongeze muda wa mkopo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wandugu poleni na majukumu, mwaka huu mwezi wa 2 nilienda kuwapelekea deni la loarn board walinunue na kwa kuwa nilikua na mkopo nao hao NMB wakanipigia mahesabu ya jumla kuwa pamoja na kununua hilo deni na kutoa deni lao watanipa jumla ya Tsh 5,660,000 nikasema poa tu kwakuwa nilikua na uhitaji sana, kufupisha stori ni kuwa jumla ya mkopo wote walinipa 17,400,000, sasa walipoingiza mimi nikakuta jumla ya 9,456,000 kwenye akaunti yangu.

Kwa haraka nilijua kuwa hiki ndicho kiasi changu nikatoa baadhi ya pesa na kuendelea kumalizia kibanda changu na kumaliza pesa yote. Sasa baada ya siku 10 afisa mikopo wa NMB akanipigia kuwa nirudishe mpunga wote yaani ile 9,456,000 maana lile deni la Loan Board halijalipwa bado!

Nikamuuliza kwanini hajalipa akasema mimi niliwahi kutoa pesa kabla hawajakata! Nikawapigia makao makuu, (audio clip ninazo) wakadai kuna makosa pande zote kwanza wao walitakiwa washikilie hiyo pesa kwanza mpaka miamala yote ifanyike, lakini pia walitakiwa ndani ya saa 72 kuwasiliana na mteja maana kumuachia mtu pesa zaidi ya wiki moja na kipindi hiki tunakijua ni mtihani, lakini pia wakasema nilifanya kosa la kutoa pesa ambayo ilizidi (kitu ambacho nilikubali) sasa jambo la ajabu wameniwekea credit -4,234,000 kwenye mshahara wangu na hivyo mshahara wangu wamezuia kwa ajili ya deni hilo.

Nimefanya njia zote ikiwemo kwenda tawini na kuongea nao, kuandika maelezo n.k lakini mpaka sasa wamegoma na option wananipa ni kurudisha pesa.

Nisaidieni wakubwa maana nimewaomba walau wakate kidogo kidogo pia wanagoma na sasa wanashikilia mshahara wote mpaka deni liishe ni zaidi ya miezi 8 na wote tunajua maisha ya mfanyakazi bila salary. Nisaidieni nifanyeje.

NB: Sipendi kuulizwa kwanini niliamua kutumia pesa zote.

Nenda ongea nao sana sana, na waambie kama Hawa kati kidogo kidogo una Acha kazi unatafuta ingine maana huwezi survive, watanyoka tu!
 
Washitaki ofisini kwako, hawatakiwi kukata mshahara wako wote, kisheria lazima 1/3 ibaki, hao NMB wasubilie au waongeze muda wa mkopo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huyo alichofanya ni uwizi.. Alishaambiwa halali yake ni 5m yeye kakuta 9m kachukua yote bila hata kuuliza..

Mkopo atakatwa kama kawaida lakini pia ile ya uwizi anatakiwa kuilipa. Hapa ushauri wowote unaotolewa bank hawatausikiliza, jamaa akomae kulipa tu hiyo 4m na si vinginevyo..

Njia nzuri ni yeye kama ana biashara achukue hati yake then akopee bank kwa hiyo biashara yake au hata kama yeye hana biashara basi atafute mtu mwenye biashara amkopee na yeye akubali kuweka hiyo hati yake kama dhamana..

Tofauti na hili tusidanganyane jamani, eti mtu anamwambia akaongee na meneja, zile fedha si za meneja ni za taasisi. Maneno hayatafanya asamehewe au mkataba ubadilishwe, bali alipe tu as long as anakubali kwamba aliitumia..
 
Hivi hizi akili za kujenga kwa kukurupuka huwa mnazitoa wapi?!

Unakwenda kujenga huko nje ya mji ambapo hata ukikosa nauli kuja mjini ni shughuli....

Kwann usisave then upate kiasi cha kuanzia kujenga baada ya muda....
 
Nilishasema, sipati pesa nikaiwekeza kwenye nyumba ili hali haina mrejesho wa uchumi. Ungekuwa na akili ya biashara ungeitumbukiza huko ukaja kujenga kwa madaha.
 
😆😆😆 Ilo jumba bovu lime mwangukia loan officer aliye issue claims yako ...we mwachie liporomokeee kabisaaa yaan we waambie pesa umewekeza shambani
Kuna mdau aliuza deni la CRDB kwa bank X. Kosa walilofanya bank X walimpa mdau milioni 6 cash akalipe deni CRDB. Hakurudi tena na CRDB hakulipa. Walipoenda kuingiza makato kwa mwajiri wakakuta bado deni la CRDB bado lipo. Walimbembeleza arudishe ila wapi
 
Hii habari mleta mada umeiandika sijui huku unakimbizwa na maofisa mikopo wa NMB wanataka kukunyang'anya na simu kabisa ili wapunguze deni.


Hebu ainisha bila kificho mambo yafuatayo bila kutuchanganyia madawa...

1. Deni la bodi ya mikopo (HELSB) ni kiasi gani?!
2. Ulikuwa unadaiwa na NMB kabla ya kupelekea deni la helsb ama ulimaanishaje?!
3. Hiyo amount ya milioni 5,600,000 inahusiana na nini na hii 17,400,000 ni nini?!
4. Kwa mujibu wa NMB na utaratibu wao wa kukopesha na makato, inakuwaje wanakulamba mshahara wote?!
5. Mshahara wako ni kiasi gani ili tuweze kukusaidia kucalculate makato sahihi?!

Hebu tunyooshee habari maana umeandika kwa kuruka ruka sana...
 
Nawaza hivi lakini Je kama mkopo wa NMB alishatumia hati ya nyumba kama dhaman??
Halafu nasikia SASA hivi japo sina uhakika Sana Wana mtandao mmoja na ukishajulikikana wewe si mwaminifu hutakopesheka Kwa Benki yote nchini.
 
Hukuwa na kosa lolote kwani sheria inasema kama umekuta pesa kwenye akaunti ukaamini ni ya kwako hutakiwi kudaiwa. Wewe uliamini hiyo pesa ni yakwako kwa sababu ulichukua mkopo.
Mkuu wewe si mwaminifu,sheria za kibenki zinasema ukikuta pesa imepungua au kuongozeka kwa account yako toa taarifa,nikuulize tu ungekuta mfano hakuna hata shilingi 50 elfu kwa account yako bila taarifa ungekaa kimya au ungeenda benki kuulizia?

Tena naona adhabu waliyokupa ni ndogo ulipaswa uwe sero.

Siku nyingine jifunze kuwa muaminifu na haya yote hayatakukukuta mkuu.
 
Mkuu huyo alichofanya ni uwizi.. Alishaambiwa halali yake ni 5m yeye kakuta 9m kachukua yote bila hata kuuliza..

Mkopo atakatwa kama kawaida lakini pia ile ya uwizi anatakiwa kuilipa. Hapa ushauri wowote unaotolewa bank hawatausikiliza, jamaa akomae kulipa tu hiyo 4m na si vinginevyo..

Njia nzuri ni yeye kama ana biashara achukue hati yake then akopee bank kwa hiyo biashara yake au hata kama yeye hana biashara basi atafute mtu mwenye biashara amkopee na yeye akubali kuweka hiyo hati yake kama dhamana..

Tofauti na hili tusidanganyane jamani, eti mtu anamwambia akaongee na meneja, zile fedha si za meneja ni za taasisi. Maneno hayatafanya asamehewe au mkataba ubadilishwe, bali alipe tu as long as anakubali kwamba aliitumia..
Wàtu hawajui kuwa mkopo maana yake ni "kipato chako cha baadaye umeamua kukitumia leo" . When you decide to use all your future income today then make sure you have strategies to survive in the future. Jamaa alitumia pato lake la leo tangu juzi, tena alitumia kujengea nyumba, ale hiyo nyumba sasa kama inalika.
 
Katika nchi za watu wanaojitambua, nchi ambazo watu wanaenda shule ili kila mtu apate ujanja kichwani ili asitokee mmoja au taasisi ya kumwonea mwingine, benki haiwezi kumlazimisha mwajiri wako eti mshahara wako upitishiwe kwao benki.

Ingekuwa ni kiasi cha wewe kwenda kumwambia dada wa human resources, ee bana eehh, kuanzia leo mshahara wangu nautaka mkononi! Cheki au cash money. Shenz type.

Halafu hao benki mngeendelea kudaiana pembeni mtaani huko.
 
Nilishasema, sipati pesa nikaiwekeza kwenye nyumba ili hali haina mrejesho wa uchumi. Ungekuwa na akili ya biashara ungeitumbukiza huko ukaja kujenga kwa madaha.
Mkuu kwa hiyo unapata hela unaenda kupangisha nyumba unalipa kodi!?? Well and good
 
Katika nchi za watu wanaojitambua, nchi ambazo watu wanaenda shule ili kila mtu apate ujanja kichwani ili asitokee mmoja au taasisi ya kumwonea mwingine, benki haiwezi kumlazimisha mwajiri wako eti mshahara wako upitishiwe kwao benki.

Ingekuwa ni kiasi cha wewe kwenda kumwambia dada wa human resources, ee bana eehh, kuanzia leo mshahara wangu nautaka mkononi! Cheki au cash money. Shenz type.

Halafu hao benki mngeendelea kudaiana pembeni mtaani huko.
Hakuna cha nchi inayojitambua mkuu.. mdhamini wa mkopo wako ni mwajiri, Sasa mkibadilisha akaunti ya mshahara kwa njama basi marejesho yasipoonekana anafuatwa mwajiri. Bado haujasolve tatizo hapo
 
Hakuna cha nchi inayojitambua mkuu.. mdhamini wa mkopo wako ni mwajiri, Sasa mkibadilisha akaunti ya mshahara kwa njama basi marejesho yasipoonekana anafuatwa mwajiri. Bado haujasolve tatizo hapo
Mwajiri anapokudhamini, ukifukuzwa kazi inakuaje?

Au tuseme bongo hamna suala la kufukuzana kazi, okay, ukifa inakuaje? Mwajiri analipa deni?
 
Back
Top Bottom