Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Kwani alitaka kupindua nchi au kuvunja amani nchini!?

Imefika muda watu tuache kufatilia issue za Mh. Makonda, tumuache afanye kazi yake vizuri na Mh Rais wetu pia alitumikie taifa.

Nape huyo atapangiwa kazi ingine ikipatikana kujua itakayomfaa na pia mambo yakipoa, kuna gemu na leo ndio mipango yao imeishia hapo.

Ilibidi nyie wananchi mbaki mnayaongelea, ha ha haaaaaaaa


Movie ya Nape baada ya kunaswa mchezo wake Junatatu, imebidi tu aimalizie kwa kuwaomba iishe hivi. Ndio maana hajatamkwa kwenye Barua kuwa yeye vipeeeee.

Hivyo Nape kapata kuondoka na bonge la plan aliyomuomba Rais au RC wa Dar apate leo, nanyi wananchi mmefurahia na kumuombea huruma na ndilo hiyo movie mmepewa.

Future ya madaraka, jina libaki kwenye midomo yenu. Na hivi wengi hamjifikirishi basi tena, wachache tu ndio watakuwa wamedaka gemu.


Nimempenda Rais kwa kumuacha asogee pembeni kwa style yake, bila kumuongelea kwa maneno mengi or kumtumbua live.


Mungu ibariki Tanzania.

Makonda oyeeeee
Dah!! Sio kwa mwandiko huu... Aisee! Taifa lina mabashite jamaniiii... Uwiiiiiiii huzuni kuuu
 
Masikini Harmo rappa akawa kama Petro wa Biblia , bastola ilipotolewa na askari yule mjinga alikimbia, nasikia amekutwa Chalinze bado anachanja mbuga.
 
Kiukweli huyo jamaa ni kiazi sijawahi kuona .... na kapelo lake kama muuza karanga,natamani niifaham sura yake ....
 
Maulidi kitenge aliwezaje kusolve ile ishu? Nimeshindwa kumwelewa kabisa.
Nothing to fear except fear itself . vijana lazima tujiamini hii ni nchi yetu tusipojisikia fahari ndani ya Tanzania tutaringia wapi?
 
nape angaamua hapo angemsukuma tu adondokee huko alafu tuone anafanya nini? anatoa bastola mchana kweupe mbele za watu hapa nchin tz? amefundishwa kweli huyo? hahaha. hivi wanafikiri hii nchi ni kampuni yao wanaweza kuifanya lolote?
Ah wapi jamaa kapanda alafu yuko fit! Nape na kitambi chake no way hahahaha
 
Hii inamkumbusha Nape kuwa unafiki haulipi.Anakwenda kuitembelea clouds badala ya Mkjane wa Mwaibabile.Sasa anatembelewa yeye
 
Niko ukurasa wa tano sijawaona Lizaboni, post Yehodaya, and Lupyee, na Laki si pesa. Natamani kuona comments zao kuhusu hili.

Vv
 
Why hajampiga tu makofi huyo mjinga na kabastola kake ? hawa jamaa washajiona miungu asee
 
huyo mkaka yuko sawa kwa mujibu wa ufikiri na akili zake na ndio akilizake zilipo fikia mwisho so msimlaumu sana, anatimiza maelekezo kutoka juu!!!!
 
Askari ni binadamu ambao unaweza ukawatuma utakavyo na wakafanya bila kuhoji hata ukiwaambia nendeni mkaue basi watatenda na yakiharibika unawakataa wanabaki wenyewe bado wataogopa kusema walitumwa heeeeee heeee narudia tena Alhamdullilah namshukuru Mungu sikutumbukia kwenye kazi hii na kwenye kizazi chetu hakuna aliekumbwa na balaa hili sijui wanalishwa nini maana baba zima ila linaweza kutumwa na Bashite na likaenda bila kuhoji [emoji23][emoji23][emoji23]
Uyo askari hapo ukimuuliza kwa nini alikua anatumia nguvu zote hizo hata mwenyewe atashangaa na anaweza kukataa kua sio yeye heee heeee
Mtaani tuliwahi kukaa na rpc wa Pwani. Baada ya form foo rpc akataka kunipeleka ccp. Daah. Kuna mtu alitokwa povu nisiende ccp. Kweli sikuenda. Namuheshimu sana mtu yule.
 
Pigilia Mstari kabisa hayo ndo majibu sahihi. Sasa tafakari kina Lema & Lissu huwa inakuwaje huko mafichoni? Je, Dr Ben Saa8 anafanywaje huko mafichoni?


Nyerere aliwahi kutahadharisha juu ya mamlaka ya Rais, pia alionya kuwa siku akapatikana Rais dikteta lazima namba isomwe.
 
Alafu bastola kaitoa kwa mkono wa kushoto alafu kulia tena[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Udhaifu kabisa. Eti ili ufunge goli lazima utumie mguu ulio zoea kuchezea?

Angekutana na anaye yajua mambo ni kumzimisha tu fasta
 
Mkuu huyo jamaa kiukweli amechafua sana makumbusho hata kama ilikuwa ni older ni njema zaidi angeangalia situation, Nape sio wa kumtoa na Bunduki, Nguvu ilitosha kumrudisha garini, Pole sana Mp Nape Nauye
 
Hivi hawezi kushitakiwa kwa kutishia uhai wa mtu?
 
Mleta uzi kipi cha kushangaza huyo jamaa kutoa bastola? Kumbuka Bashite alienda Clouds TV akiwa na askari wanne wote wakiwa na bundiki nzito kuliko hizo bastola. Hapo inaonyesha hayo ndio maagizo aliyopewa na aliyemtuma na usishangae akipandishwa cheo. Hizo amri za kutaka polisi watumie nguvu zinatoka kwa mkuu, mmesahau amri zake kwa askari dhidi ya raia?
 
Back
Top Bottom