Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Nape Nnauye atishishiwa Bastola na kusukumizwa kwenye gari

Aidha tumeshasena na kunasihu mara nyingi kuwa hizi nyadhifa kubwa wagombea wapimwe afya ya akili
 
Hahahaha Nani kamuona Harmorapa alivyo kula kona baada ya jamaa kuonesha bastola
 
Nimeshtuka na kuhisi presha pale aliyekua Waziri wa Habari Ndg. Nape Nauye alipokoswakoswa kuuwawa kwa risasi na askari ambae hakujitambulisha

Je ilikua nisawa kwa askari kumkamata mwananchi bila ya kumtambulisha kua wewe ni askari?

Ingekuaje kama Ndg. Nape nae angetoa kipapatio chake ili kujihami?

Je, ilikua ni haki kwa askari kutaka kumpiga risasi Ndg. Nape mbele ya kadamnasi mpaka Ndg. Harmorapa akataharuki kwa kutimua mbio?

Wajuzi wa sheria tufafanulieni kuhusu hili:
 
"askari ni mbwa" ben mtobwa
kitabu _zawadi ya ushindi
 
Mara zote nimekuwa na mashaka sana na maaskari wetu hasa waliofuzu katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Sina hakika kama ni sababu ya nyadhifa na nafasi walizokuwa nazo wazazi wao au ni kiburi tu binafsi.

Miaka iliyopita mpaka ukamjue fulani ni askar wa Usalama wa Taifa ilikuwa ni shughuli pevu ila ikaja kuwa kinyume kwa kipindi cha miaka kumi na miwili, mtu alikuwa na uwezo wa kuanza kujigamba tu mkiwa bar au pahala popote penye mkusanyiko wa watu kuwa yeye ni usalama wa taifa au akaitoa kabisa silaha aliyonayo kwenye hadhar, binafsi simshangai huyu askari
 
Nafikiri umepata jibu la swali ulilouliza kutoka kwa wadau hapo juu.

Mie hoja yangu ni hii... Mbona leo umeweza kuhukumu kabla hata ujajua ni nini kilichopelekea yote haya? Ni ajabu sana leo eti hujapendezwa kuona hiyo bastola (tena kamoja tu) ikitolewa nje nje... wakati juzi hapa tuliona sote askari wa aina tofauti wasio na magwanda na wenye magwanda ya kijeshi wameshika silaa kubwa kubwa za kivita wakiongozwa na rc saa nne usiku wakiingia kwenye private premises, wewe mwenzetu ukatuambia kuwa huoni uvamizi wala shari yoyote ya lile tukio, kana kwamba kungeweza kukawa na explanation nyingine ya kawaida kabisa ya lile tukio...ambayo sijui ni ipi kwa mfano... Hueleweki ndugu.

Hivi kabisa hii ya leo Nape kunyooshewa bastola kwa namna ile unaweza kulinganisha na jinsi Makonda alivyoingia casually pale Clouds na wale askari?

Kabisa unaweza kulinganisha?

Nani pale Clouds alinyooshewa mtutu wa bunduki kama ilivyotokea kwa Nape?

Nani pale Clouds alikuwa roughed up kama ilivokuwa kwa Nape leo?

Nani?

Utakuwa zuzu kabisa wewe kama utayalinganisha haya matukio mawili.

Wengi wenu nyie mna akili duni sana aisee.

Dumb like a bucket of rocks.

Halafu wala sijahukumu na ndo maana nikauliza hayo maswali niliyouliza kama nilivyouliza kwenye ishu ya Clouds.

But again if you are dumb as a bucket of rocks you wouldn't see any difference.
 
hakika askari huyu atapandishwa cheo kidogo,angemtolea machine gun angepandishwa kumkaribia makondakta
 
Nape amevuna alichopanda tangu mwnzo Napenda alitetea uovu au dhuruma wakafunga gori la mkono sasa uovu umemrudia Pole Mr Nape siku zote smama ktk haki na kweli
 
Mara zote nimekuwa na mashaka sana na maaskari wetu hasa waliofuzu katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Sina hakika kama ni sababu ya nyadhifa na nafasi walizokuwa nazo wazazi wao au ni kiburi tu binafsi.

Miaka iliyopita mpaka ukamjue fulani ni askar wa Usalama wa Taifa ilikuwa ni shughuli pevu ila ikaja kuwa kinyume kwa kipindi cha miaka kumi na miwili, mtu alikuwa na uwezo wa kuanza kujigamba tu mkiwa bar au pahala popote penye mkusanyiko wa watu kuwa yeye ni usalama wa taifa au akaitoa kabisa silaha aliyonayo kwenye hadhar, binafsi simshangai huyu askari mpumbavu.
Hawa ni askari polisi upelelezi siyo wa TISS. Wale wa TISS wanafundishwa vyema na wana adabu na wala hawawezi kutumwa kwenye mission ya wazi namna hiyo.
 
Back
Top Bottom