Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Mimi swali ninalojiuliza ni je, Nape ana uhakika Mungu ameshamaliza kuamua ugomvi? Ni muhimu kua na kiasi kwenye kunena.
 
Habarini JF GT!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani. Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Kifo cha Jiwe lazima kishangiliwe sababu Yuko peponi anawashughulikia MAITI HEWA,..
 
Jinsi ulivyoishi na binadamu wenzako ulipokuwa hai, ndivyo utakavyokumbukwa ukiwa mfu. Msilazimishe mazuri, kama yapo yatasemwa tu. Nimecheka hapo unaposema "mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi " 😀
Wacha na mimi nicheke😂😂😂
 
Acheni ujinga. Nyie mbona kila kukicha mnamsema vibaya Idd Amin au Hitler? Ukizuia watu wasikuseme ukiwa hai watakusema ukiwa mfu.

Kupanga ni kuchagua
Kabisa, ukiwa kiongozi na ukafanya UHUNI historia itakuhukumu tu. Ndio sababu Nduli Idd Amin Dadaa historia ya UHAYAWANI wake itaendelea kusomwa na kusimuliwa vizazi na vizazi, Magufuli ni nani yeye asisemwe?
 
Fikiria sasa hivi Ole Sabaya angekuwa RC wa Kilimanjaro na Muro wa Dar, Makonda waziri wa mambo ya ndani, Bashiru Katibu mkuu kiongozi, Polepole waziri wa Habari, Mnyeti waziri wa katiba na sheria, Mambosasa IGP, Musiba bado mwanaharakiti huru, Ndugai Spika.
Satan company....
 
It is total foolishness kucoment juu ya marehemu vibaya. Hata kama alikuwa mbaya. Kifukua makaburi unaweza ukafukua na hasira na chuki na vita. Magu alikuwa na wafuasi wengi innocent na chuki ikiibuka hakuna wa kupona. It is wiser kumzika marehemu na mambo yake yote. Nape is a fool na hana sifa ya kuwa kiongozi wa umma
Vipi Nape sio waziri mpaka leo?
Nyinyi ni watu wa ajabu. Mnamchukia Mtu anayemsema vibaya marehemu( maneno tu) ila mlikuwa mkimsifia mtu anayebambikiza nwenzake kesi ya ubakaji anaishia jela na kuacha familia yake kwa sababu tu za kutifautuana kisiasa?
 
Vipi Nape sio waziri mpaka leo?
Nyinyi ni watu wa ajabu. Mnamchukia Mtu anayemsema vibaya marehemu( maneno tu) ila mlikuwa mkimsifia mtu anayebambikiza nwenzake kesi ya ubakaji anaishia jela na kuacha familia yake kwa sababu tu za kutifautuana kisiasa?
Nape sijui yuko wapi na ile kauli yake ya Mungu kaamua ugomvi!
 
Mungu ameamua ugomvi kaka amerudi CCM tena, yalikuwa ni maneno ya mbunge wa Jimbo la Mtama Mh Nape Nauye wakati akimkaribisha aliyekuwa mgombea urais wa ACT Wazalendo marehemu Benard Membe.

Marehemu Benard Membe aliondoka CCM baada ya kutofautiana na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, lakini akatangaza kurejea CCM baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya 6 wa Tanzania.
 
Mungu ameamua ugomvi kaka amerudi CCM tena, yalikuwa ni maneno ya mbunge wa Jimbo la Mtama Mh Nape Nauye wakati akimkaribisha aliyekuwa mgombea urais wa ACT Wazalendo marehemu Benard Membe.

Marehemu Benard Membe aliondoka CCM baada ya kutofautiana na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, lakini akatangaza kurejea CCM baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya 6 wa Tanzania.
Mnalipwa sh ngapi kuandika haya?
 
Mungu ameamua ugomvi kaka amerudi CCM tena, yalikuwa ni maneno ya mbunge wa Jimbo la Mtama Mh Nape Nauye wakati akimkaribisha aliyekuwa mgombea urais wa ACT Wazalendo marehemu Benard Membe.

Marehemu Benard Membe aliondoka CCM baada ya kutofautiana na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, lakini akatangaza kurejea CCM baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya 6 wa Tanzania.
Uamuzi wa 17/03/2021 ndiyo ulikuwa wa maana
 
Mungu ameamua ugomvi kaka amerudi CCM tena, yalikuwa ni maneno ya mbunge wa Jimbo la Mtama Mh Nape Nauye wakati akimkaribisha aliyekuwa mgombea urais wa ACT Wazalendo marehemu Benard Membe.

Marehemu Benard Membe aliondoka CCM baada ya kutofautiana na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, lakini akatangaza kurejea CCM baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya 6 wa Tanzania.
Bado wengine!
 
Mungu ameamua ugomvi kaka amerudi CCM tena, yalikuwa ni maneno ya mbunge wa Jimbo la Mtama Mh Nape Nauye wakati akimkaribisha aliyekuwa mgombea urais wa ACT Wazalendo marehemu Benard Membe.

Marehemu Benard Membe aliondoka CCM baada ya kutofautiana na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, lakini akatangaza kurejea CCM baada ya Rais Samia kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya 6 wa Tanzania.
Membe hakutofautiana na Magufuli bali alishindwa azma yake ya kuwa mgombea urais 2020 badala ya Magufulu kupitia CCM. Hakuwa na jinsi kwani ilibidi atafute chama kingine ambacho kungemteua agombee urais 2020 na chama kilichokuwa tayari kilikuwa ACT
 
Back
Top Bottom