Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Nape Nnauye: Mwenyezi Mungu ameamua ugomvi

Habarini JF GT!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani. Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Kwani ni uongo? Si ndio ukweli wenyewe huo au? 😆😆
 
Habarini JF GT…!!!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi…. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani… Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Kimaadili ya kiuongozi hili halipo sawa, inaonyesha Nape pia hakui pamoja na changamoto alizopitia, anasahau kwamba huyo Magu anayemtuhumu angeacha mpira udunde wenyewe kwenye uchaguzi uliopita hata yeye asingekuwa mbunge. kifupi hiyo mbegu wanayoipanda lazima wataivuna japo kwa sasa wanaona kama mzaha tu kukejeli wenzao.
 
Viongozi waandamizi wa chama kile kile hadharani wanamnanga Rais na mwenyekiti wao ambaye ni marehemu. Hawa ndio walikuwa wanalia baadhi ya wastaafu kusemwa lakini kumbe issue ilikuwa ma godfather wao kusemwa ila nao ni sehemu ya hako kaugonjwa.

Chama ni kama wamebariki haya matusi toka JPM afariki! Hii mbegu ilipandwa awamu ya 4 ikajikita awamu ya 5 na sasa imestawi na itawagharimu kuifuta maana kwa walivyo watu wa chama kile visasi havitakoma.
Acha upuuzi,kusemana alianzisha Mwendazake acha asiginwe hadi akili zikae sawa.
 
Heee... Kama upo nje ya nchi hongera...

Mimi ni shuhuda wa haya... Na sio kesi za kisiasa....
Unaambiwa futa hii kesi hata kama umeonewa.. Ukileta ujeuri usitulalamikie.. YAMENIKUTA HAYO
😅😅duuh
 
Viongozi waandamizi wa chama kile kile hadharani wanamnanga Rais na mwenyekiti wao ambaye ni marehemu. Hawa ndio walikuwa wanalia baadhi ya wastaafu kusemwa lakini kumbe issue ilikuwa ma godfather wao kusemwa ila nao ni sehemu ya hako kaugonjwa.

Chama ni kama wamebariki haya matusi toka JPM afariki! Hii mbegu ilipandwa awamu ya 4 ikajikita awamu ya 5 na sasa imestawi na itawagharimu kuifuta maana kwa walivyo watu wa chama kile visasi havitakoma.
Ni watu wa chama kile au watu wa Chama Chako?? Mbona unaongea kama vile ni chama cha ACT😅😅
 
Kimaadili ya kiuongozi hili halipo sawa, inaonyesha Nape pia hakui pamoja na changamoto alizopitia, anasahau kwamba huyo Magu anayemtuhumu angeacha mpira udunde wenyewe kwenye uchaguzi uliopita hata yeye asingekuwa mbunge. kifupi hiyo mbegu wanayoipanda lazima wataivuna japo kwa sasa wanaona kama mzaha tu kukejeli wenzao.
Mkuu kama angeacha mpira udunde wenyewe asingekuwa mbunge.. Ni kweli..
Na kama unakumbuka mpinzani wa Nape aliswekwa rumande wiki nzima ili asirudishe fomu...
Je, huoni ni lazima Magufuli asemwe ili liwekwe kwenye kumbukumbu... Na vizazi vijavyo vijue na lisijirudie tena?
 
Ni kweli alichosema Nape, Mungu amelata amani

Na kifo chake sio kimeleta amani kwa CCM tu, bali kwa vyama vingine na kwa nchi kiujumla, vyama vya upinzani walikuwa wakiwindwa kama swala,

hata ugomvi wetu na nchi jirani umeisha na sasa Tz inafanya biashara na majirani zetu vizuri

Na sio nchi jirani tu, hata jamii kubwa ya kimataifa ilikuwa na ugomvi na Tanzania ila baada ya Mungu kufanya yake, sasa hivi Tanzania ni rafiki wa kila nchi, za Mashariki na Magharibi

Ama kweli Mungu ameleta amani, MUNGU NI FUNDI
wabongo wengi waliotamani kuona Nyerere Dam na SGR vikiwa mzigoni bado hawaamini kama chuma Magufuli amekufa, bado hawaelewi Magu alikufa lini, bado hawaelewi kipi kilimuua? wanapenda kujua nani walikuwepo wakati Magu akifa? jitihada kiasi gani zilifanyika kuokoa uhai wake? haya maswali kuna siku moja hata ipite miaka mia majibu yatapatikana!!

Halafu ni ujinga kufurahi binadamu mwenzio kufa maana njia yetu ni moja tu!! hata kobe wanaotoboa miaka 200 nao one day wanadedi, hivi nani kati yetu anajua atakufaje? atafia wapi? je mnakumbuka wale wazungu ambao Islamic State kule Iraq walikuwa wakiwachinja hadharani kwa kurekodi video? je wale jamaa wakiwa huru walijua one day watachinjwa?

Unaposhiriki mazishi ya mtu ni muda wa kujiuliza nawe mazishi yako yatakuwaje!

Ni wakati sasa JPM aachwe apumzike
 

Nape Nnauye na Maza Lao ni moja kuhusu marehemu.​

Bora Nape ni mkweli Ana kibali kulisema la rohoni, Maza anapiga kimya.​

Kuna siku Dr Bashiru anasema ukweli kuhusu kifo cha JPM watanzania hawataamini.​

Hakuna mwenye akili timamu wa kumuamini Bashiru,ni mwizi tu yeye na polepole walipiga hela sana kwenye ile biashara haramu ya kununua wapinzani uchwara ni wahuni tu
 
tabu watanganyika tunawaza sana jana na jana ilishapita kibaya zaidi akili zao zinakumbatia mapungufu na maovu na sio mazuri yaliyofanywa. Idd Amini ndiye aliyewapa maisha waganda kwa kutaifisha biashara za wahindi na kini sisi tumekuwa chanzo cha ulalamika utafikiri alikuwa rais wetu na kiukweli hakutenda ubaya kwa kiasi hicho tuliingia kwenye vita kwa sababu ya urafiki wa Nyerere na Obote hata daraja la mto Kagera tulilivunja wenyewe.
Lazima tuwaze JANA ili kuifanya LEO na KESHO yetu kuwa BORA ZAIDI. Ikiwa hujui utokako (JANA) utafahamu vipi ulipo (LEO) na uendako (KESHO).Ikiwa hujui wapi tatizo lilipoanzia huwezi kupata utatuzi juu yake. Hatma bora huja kwa kurekebisha jana yetu.

Hivyo basi, mema husafiri POLEPOLE lakini hudumu vizazi, mabaya husafiri kwa KASI zaidi hufutika mapema moyoni.

Tujitathimi jinsi tunavyoishi na wengine,duniani sote tuko njiani.

MIAKA 80 IJAYO WATAKAOKUWA HAI HUMU JUKWAANI NI WACHACHE MNO,AU WASIWEPO KABISA.
 
Wakati magu anawashambulia kwa kejeli matusi na lugha za Kidhalilisha majukwaani watu, mlishangilia huku mkisema ni sawa tu...Leo watu wanatoa nyongo mnawaona wabaya tena. Wapuuzi.
 
Huu upuuzi si wa mbayuwayu Nape wa kulaumiwa ni viongozi wakuu wa nchi. Ndo wa kumwambia Nape afunge domo. Fitina zinawatafuna kiukweli ila zitawagharumu .system nzima iko against Magufuli its sickening wanavyopambana na marehemu kwa ajili tu ya vyeo .
 
Habarini JF GT!

Jana wakati Membe akirudishiwa kadi ya CCM, Mbunge wa Mtama na Wazari wa Habari nchini aliongea kauli mbaya Sana Na Yenye kufedhehesha kwa Marehemu.

Kwa tamaduni za kitanzia Sio sawa kumsema Marehemu, na hata Ukitaka kumsema Marehemu utamsema kwa Mazuri. Lakini hii imekuwa Tofauti kabisa kwa baadhi ya Wanachama wa CCM na Viongozi wa CCM, wamekuwa Wakimsema Hayati Magufuli Hadharani mbele ya wananchi waliomchagua kwa kura nyingi. Hakika CCM inajiua Yenyewe

Jana Ndugu Nape (Namuita Ndugu kwasababu kwangu mimi sioni kama Anafaa kupewa heshima ya Jina Mheshimiwa) wakati wa Sherehe zile alisimlia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na Yeye alivyo nusurika kufukuzwa CCM na Membe kumsadia, kipindi hicho naamini Magufuli hakuwa Kiongozi mkubwa wa CCM, Nape aliongea kumaanisha kuwa Magufuli alikuwa chanzo kikubwa cha Membe kuondoka CCM na Kutengeneza ugomvi mkubwa na Wana CCM wengine.

Nape akaenda mbali zaidi na Kusema Kuwa Ugomvi huo Mungu ndio ameamua na sasa bahari imetulia iko shwari, akimaanisha Kifo cha Magufuli ni Maamuzi ya Mungu katika Kutatua ugomvi wa Wana CCM na Membe… Akaendelea mbele na Kusema nani Kama Rais Samia Suluhu.

Ikumbukwe kuwa Huu utamaduni uliopo sasa kwa kumsifia rais hata pale anapo fanya Baya ulianza kipindi Cha Magufuli na Umeendelea hadi awamu hii kwa kusema Mama anaupiga mwingi. Nyakati za Kikwete, Mkapa hakukuwa na huu ujinga.

Turudi kwenye mada, Nape Nauye ni lini Ataacha kuwa na Kinyongo na Marehemu? Nilini ataacha Kumsema Marehemu? Huu umekuwa muendelezo wake toka Awe Waziri tena Wa Habari, Je aliteuliwa kuja Kumsema Marehemu?

Ni wakati sasa Wa Nape kumuacha Marehemu Apumzike Mahali pema na kwa amani. Asitafute chuki na watu zisizo za msingi
Alimtembeza kwa miguu Ikulu ya DSM
 
Sio kila kitu unakihusisha na chama kwani huyo ndugu yako Nape ni msemaji wa chama?. Acha dhana jumuishi ndugu yake Nape.
 
Hakuna mtu nimewahi kusoma sehemu yoyote akikejeri kifo Cha Hitler Wala Idd Amin, HAKUNA!

Kwanza Hitler aliamini hawezi kuuliwa na ni vigumu Sana yet kufa, aliwahi hata kutaja hadharani kwamba yeye hawezi kufa,
Kwahio kama wewe hujawahi kusoma hio kejeli ya Hitler then tukusaidiaje?
 
Viongozi waandamizi wa chama kile kile hadharani wanamnanga Rais na mwenyekiti wao ambaye ni marehemu. Hawa ndio walikuwa wanalia baadhi ya wastaafu kusemwa lakini kumbe issue ilikuwa ma godfather wao kusemwa ila nao ni sehemu ya hako kaugonjwa.

Chama ni kama wamebariki haya matusi toka JPM afariki! Hii mbegu ilipandwa awamu ya 4 ikajikita awamu ya 5 na sasa imestawi na itawagharimu kuifuta maana kwa walivyo watu wa chama kile visasi havitakoma.
Uzuri huyo marehemu yeye ndie alikua wa kwanza kuwananga wastaafu wenzake hadharani, kabla yake yeye wastaafu walikua hawasemi wenzao hadharani.Acha anyweshwe dawa aliyo itengeneza mwenyewe huko alipo.
 
Back
Top Bottom