Nape Nnauye: Rais Samia Suluhu aendelee mpaka 2030

Nape Nnauye: Rais Samia Suluhu aendelee mpaka 2030

Kwa Mujibu wa katiba iliyopo haiwezekani kwenda hadi 2030.

Awamu yake hii ya kwanza ,endapo chama kitampitisha 2025 basi ndio itakuwa term ya mwisho ya pili.
 
Ule msamaha alioenda kuomba akachukuliwa na makamera unafanya haya maoni ya Nape kukosa msingi,zaidi kujionyesha alivyo mnafiki. Alivyo tayari kwenda kinyume na nafsi yake Ili tu asipoteze nafasi za kisiasa hasa ubunge.

Kwakuwa aliyemuomba msamaha kwa kukosoa utawala wake hayupo tena basi anaanza tena kukosoa mambo yaleyale ambayo yalimfanya aombe msamaha!Nape ni miongoni mwa wanasiasa wachache wa CCM ya sasa ambaye anaweza kusema ukweli hata kama ni kinyume na wanachama walio wengi.Kinachomwaribia ni tabia yake ya uoga,kufikiria zaidi kesho yake kisiasa kuliko kusimamia anachokiamini.

Hii inafanya hata aseme nini,watu wenye upeo wasimtilie maanani.Kwakuwa hasemi hivyo kusaidia au kurekebisha.Bali kujaribu kuendana na maono ya serikali iliyopo Ili kukidhi haja zake za kisiasa na maisha yake binafsi kwa ujumla.Laiti kama angekubali kupigwa na utawala wa Magu na hata akakosa huo ubunge,lakini akaendelea kuwa critic wa serikali ya Magu bila kurudi nyuma wala sijui kuomba msamaha,angejenga bonge la legacy na hata mie ningekuwa shabiki wake kisiasa.Lakini hii kujaribu kuendana na upepo unavyovuma Ili kukidhi matarajio yake binafsi kisiasa kunamtoa katika kundi la wanasiasa muhimu wanaohitaji kufuatiliwa....
Legacy hailiwi. Unadhani familia yake itakula legacy. Kumbuka siasa ni ajira na huwezi kuchezea ajira. Hata upinzani hawatafuti legacy bali ajira, wanapoipata ajira kama ubunge wanatakiwa kuishikilia vizuri.
 
Chawa wanahangaika kweli
Screenshot_20210404-163141.png
Screenshot_20210329-172251.png
 
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Nape Moses Nnauye akihojiwa na Mwananchi amependekeza kwamba Rais Samia Suluhu Hassan aendelee kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka 2030.

-----
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri kwa kutoa maagizo yanayoliondoa Taifa kwenye kutumia mabavu na kujielekeza kwenye kutumia akili katika ukusanyaji kodi bila kuathiri walipakodi.

Mbali na hivyo, Nape alisema pia Rais Samia ameonyesha nia ya kuliongoza Taifa kwa kuwatendea haki Watanzania, hasa alipoitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuziangalia na ikiwezekana kuzifuta kesi zisizo na msingi wala uhalali ili kuleta haki.

Nape alisema hayo juzi kwenye mahojiano maalumu na Gazeti hili nyumbani kwake jijini Dodoma kuhusiana na Rais Samia alivyoanza kuliongoza Taifa.

Mbunge huyo wa Mtama na waziri wa zamani wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo alikuwa akizungumzia kauli ya Rais Samia ya kukataza matumizi ya kikosi kazi ‘task force’ katika kudai kodi na badala yake watumie akili na maarifa zaidi.

Sio mara ya kwanza kwa Samia kuonya matumizi ya ‘task force’ TRA, Februari 2018, wakati huo akiwa Makamu wa Rais aliwataka TRA kujenga uhusiano bora na wafanyabiashara ili walipe kodi kwa uhuru na uadilifu bila vitisho.

Pia, alionya tabia ya baadhi ya watumishi wa TRA ambao hujiunga vikundi na kuwatembelea wafanyabiashara wakijiita ‘special task force’ ambao kazi yake kubwa ni kuwatisha ili kulipa kodi.

Juzi, Rais Samia ambaye amechukua madaraka ya nchi baada ya kifo cha Rais Dk John Magufuli, alimuagiza Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba ambaye anasimamia pia TRA aache kutumia mabavu kudai kodi.

“Trend mnayokwenda nayo sasa hivi ni kuua walipa kodi. Mnatumia nguvu zaidi kuliko akili na maarifa, mnawakamua mnaenda mnachukua pesa kwa nguvu, mnazuia akaunti zao,” alisema Rais Samia.

Hata hivyo, Nape ambaye aliwahi kulalamikia matumizi ya ‘task force’ bungeni, jana akizungumza na gazeti hili alisema ukusanyaji kodi ni matokeo ya utendaji mzuri wa uchumi.

Alisema kama uchumi unafanya vizuri hata ulipaji kodi utakuwa mzuri.

“Watu watalipa kodi na mtakusanya sana. Lakini, kama uchumi unafanya vibaya mnaweza mkajikuta mnabinyana sana kwa sababu watu wanafunga biashara na wakiwa wanafunga biashara, makusanyo hamuwezi mkayapata.

“Kwa hiyo mama (Rais Samia) amelizungumza hili jambo kwa weledi mkubwa, hata ukisikiliza sauti yake alikuwa anamaanisha kwamba tutumie akili badala ya kutumia nguvu katika ukusanyaji wa kodi,” alisema Nape.

Alisema suala la ukusanyaji kodi ni nyeti na kuna vyuo nchini vinavyofundisha namna ya kukusanya kodi, hata hivyo alisema haoni sababu ya kutumia watu wa pembeni kufanya kazi hiyo.

“Ni vizuri tumsaidie huyu mlipa kodi, atulipe kodi lakini aendelee kuzalisha ili na kesho alipe kodi. Huu ndio msingi mkubwa. Mama (Rais Samia) amesema vizuri sana kwamba kuna wafanyabiashara wamefunga biashara (nadhani amepewa taarifa za kutosha) hapa nchini na wamekwenda kufanya biashara nchi nyingine na wanafanya vizuri huko waliko.

“Hapa tuliwaona ni wezi, wasio wazalendo lakini wako kule wanazalisha na kule wanakozalisha wanalipa kodi, maana yake wanalipa kodi kwenye nchi nyingine na hawalipi kwetu hapa,” alisema Nape.

Nape alisema kauli ya Rais Samia itafanya uchumi upumue na kuwafanya wafanyabiashara wajisikie fahari.

“Kulipa kodi lazima iwe ni fahari, usilipe kodi huku unalia,” alisema Nape.

Pia alizungumzia wigo wa kuongeza walipa kodi kwamba kwa takwimu alizonazo, watu wanaotakiwa kulipa kodi ni karibu milioni 14, lakini wanaolipa kodi kwa sasa ni kati ya milioni 2.5 hadi milioni tatu.

“Maana yake kodi ya watu milioni 14 inabebwa na watu milioni tatu. Utaona mzigo ulivyo mkubwa hapa,” alisema Nape.

Kesi zisizo na msingi

Nape alizungumzia kauli ya Rais Samia ya kuwataka Takukuru kuzifuta kesi ambazo hazina msingi wala uhalali kwamba, kumekuwa na tabia ya kukamatwa na kukaa muda mrefu jela, lakini baadaye wanakuja kuachiwa huru kuwa hawakuwa na makosa.

“Kulianza kujengekea ‘trend’ na hili limejitokeza muda mrefu kidogo la kudhani kuwa tukiwa na kesi nyingi ndio mafanikio, lakini mafanikio ya kuzuia uhalifu wowote ni elimu na ushawishi mnaoutoa kwa watu.

“Idadi ya adhabu mnazozitoa ‘actually’ (kwa kweli) zinaonyesha upungufu katika namna mnavyotekeleza shughuli zenu kwa sababu kama mnatoa adhabu kwa watu ili waache vitendo vya rushwa na bado vitendo vinaongezeka na ndio maana kesi zinaongezeka. Maana yake ni kwamba hili jambo lilikuwa halifanyiki vizuri sana.

“Mama (Rais Samia) amekwenda kurekebisha, kuboresha tu kuwa hebu tusijikite kwenye idadi ya kesi, hebu tujikite kwenye kesi ambazo ni za msingi ukienda nazo zinaenda kutupa matokeo.

“Lakini, jambo kubwa kumekuwa na malalamiko ya watu kupewa kesi nyingi, wakati mwingine hata ukizisikiliza unaona wanashinda. Yaani mtu anakamatwa, anawekwa ndani anakaa muda mrefu ndani, halafu mwisho wa siku anaachiwa kuwa ameshinda yaani hana hatia.

“Unajua hata haki zake mnakuwa mmezipoteza, maana iko haja ya kufikiria namna ya kubadilisha baadhi ya sheria tuongeze wigo wa dhamana. Mtu aadhibiwe baada ya kuwa ameshapitia kwenye mchakato wa kimahakama na amekutwa na makosa,” alisema Nape.

Alisema kwa mfumo wa sasa ulivyo kuna watu wanaadhibiwa hata kabla ya mahakama haijawahukumu, kwa kesi pengine kuhisiwa.

“Unaambiwa huna kesi, lakini umeshakaa miaka, umeshasota, umeshaumia kwa hivyo nadhani wito wa mama (Rais Samia) katika masuala ya kesi ni kuzingatia haki,” alisema Nape.

Credit: Mwananchi
Jamani Nchi yetu ina matatizo sana ina Viongozi ambao hawatumii akili zao kupata wanachotaka badala yake wanatumia tabia iliyojengeka Awamu hii ya sifu unufaike au pinga upotee. Huyu ni Mbunge na aliwahi kuwa Waziri anamsifu na kushauri, kwa maneno tu ya Rais, aongezewe Kipindi kingine Kiongozi ambaye hata mwezi mmoja wa Kipindi hiki alichopo madarakani hajamaliza. Mtu hatathiminiwi kwa maneno anayotamka bali kwa matokeo ya mchango wa maneno yaliyotamkwa, lazima kuwe na muda wa kutosha kufuatilia utekelezaji wa yaliyosemwa. Mnauye angeeleweka kama angependekeza mwezi mmoja kabla ya Mheshimiwa Rais kumaliza Kipindi hiki cha uongozi wake maana sote tungekuwa tumeona matokeo ya maneno ya Rais. Kipindi cha Kwanza cha Awamu ya Tano, Mwendazake na mrithi wake walitamka na kuagiza mengi sana ya kuleta Tanzania Mpya itakayokuwa kama Ulaya na MaCCM yakaimba sana "mi5 tena" na mbinu mbalimbali zikatumika kuhakikisha hilo linatokea na matokeo yake tumeona Mwendazake anaenda zake akituacha na Tanzania yetu ileile na watu wake hali mbaya zaidi.
 
Mbunge wa Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Nape Moses Nnauye akihojiwa na Mwananchi amependekeza kwamba Rais Samia Suluhu Hassan aendelee kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mpaka 2030.

-----
Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameanza vizuri kwa kutoa maagizo yanayoliondoa Taifa kwenye kutumia mabavu na kujielekeza kwenye kutumia akili katika ukusanyaji kodi bila kuathiri walipakodi.

Mbali na hivyo, Nape alisema pia Rais Samia ameonyesha nia ya kuliongoza Taifa kwa kuwatendea haki Watanzania, hasa alipoitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuziangalia na ikiwezekana kuzifuta kesi zisizo na msingi wala uhalali ili kuleta haki.

Nape alisema hayo juzi kwenye mahojiano maalumu na Gazeti hili nyumbani kwake jijini Dodoma kuhusiana na Rais Samia alivyoanza kuliongoza Taifa.

Mbunge huyo wa Mtama na waziri wa zamani wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo alikuwa akizungumzia kauli ya Rais Samia ya kukataza matumizi ya kikosi kazi ‘task force’ katika kudai kodi na badala yake watumie akili na maarifa zaidi.

Sio mara ya kwanza kwa Samia kuonya matumizi ya ‘task force’ TRA, Februari 2018, wakati huo akiwa Makamu wa Rais aliwataka TRA kujenga uhusiano bora na wafanyabiashara ili walipe kodi kwa uhuru na uadilifu bila vitisho.

Pia, alionya tabia ya baadhi ya watumishi wa TRA ambao hujiunga vikundi na kuwatembelea wafanyabiashara wakijiita ‘special task force’ ambao kazi yake kubwa ni kuwatisha ili kulipa kodi.

Juzi, Rais Samia ambaye amechukua madaraka ya nchi baada ya kifo cha Rais Dk John Magufuli, alimuagiza Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba ambaye anasimamia pia TRA aache kutumia mabavu kudai kodi.

“Trend mnayokwenda nayo sasa hivi ni kuua walipa kodi. Mnatumia nguvu zaidi kuliko akili na maarifa, mnawakamua mnaenda mnachukua pesa kwa nguvu, mnazuia akaunti zao,” alisema Rais Samia.

Hata hivyo, Nape ambaye aliwahi kulalamikia matumizi ya ‘task force’ bungeni, jana akizungumza na gazeti hili alisema ukusanyaji kodi ni matokeo ya utendaji mzuri wa uchumi.

Alisema kama uchumi unafanya vizuri hata ulipaji kodi utakuwa mzuri.

“Watu watalipa kodi na mtakusanya sana. Lakini, kama uchumi unafanya vibaya mnaweza mkajikuta mnabinyana sana kwa sababu watu wanafunga biashara na wakiwa wanafunga biashara, makusanyo hamuwezi mkayapata.

“Kwa hiyo mama (Rais Samia) amelizungumza hili jambo kwa weledi mkubwa, hata ukisikiliza sauti yake alikuwa anamaanisha kwamba tutumie akili badala ya kutumia nguvu katika ukusanyaji wa kodi,” alisema Nape.

Alisema suala la ukusanyaji kodi ni nyeti na kuna vyuo nchini vinavyofundisha namna ya kukusanya kodi, hata hivyo alisema haoni sababu ya kutumia watu wa pembeni kufanya kazi hiyo.

“Ni vizuri tumsaidie huyu mlipa kodi, atulipe kodi lakini aendelee kuzalisha ili na kesho alipe kodi. Huu ndio msingi mkubwa. Mama (Rais Samia) amesema vizuri sana kwamba kuna wafanyabiashara wamefunga biashara (nadhani amepewa taarifa za kutosha) hapa nchini na wamekwenda kufanya biashara nchi nyingine na wanafanya vizuri huko waliko.

“Hapa tuliwaona ni wezi, wasio wazalendo lakini wako kule wanazalisha na kule wanakozalisha wanalipa kodi, maana yake wanalipa kodi kwenye nchi nyingine na hawalipi kwetu hapa,” alisema Nape.

Nape alisema kauli ya Rais Samia itafanya uchumi upumue na kuwafanya wafanyabiashara wajisikie fahari.

“Kulipa kodi lazima iwe ni fahari, usilipe kodi huku unalia,” alisema Nape.

Pia alizungumzia wigo wa kuongeza walipa kodi kwamba kwa takwimu alizonazo, watu wanaotakiwa kulipa kodi ni karibu milioni 14, lakini wanaolipa kodi kwa sasa ni kati ya milioni 2.5 hadi milioni tatu.

“Maana yake kodi ya watu milioni 14 inabebwa na watu milioni tatu. Utaona mzigo ulivyo mkubwa hapa,” alisema Nape.

Kesi zisizo na msingi

Nape alizungumzia kauli ya Rais Samia ya kuwataka Takukuru kuzifuta kesi ambazo hazina msingi wala uhalali kwamba, kumekuwa na tabia ya kukamatwa na kukaa muda mrefu jela, lakini baadaye wanakuja kuachiwa huru kuwa hawakuwa na makosa.

“Kulianza kujengekea ‘trend’ na hili limejitokeza muda mrefu kidogo la kudhani kuwa tukiwa na kesi nyingi ndio mafanikio, lakini mafanikio ya kuzuia uhalifu wowote ni elimu na ushawishi mnaoutoa kwa watu.

“Idadi ya adhabu mnazozitoa ‘actually’ (kwa kweli) zinaonyesha upungufu katika namna mnavyotekeleza shughuli zenu kwa sababu kama mnatoa adhabu kwa watu ili waache vitendo vya rushwa na bado vitendo vinaongezeka na ndio maana kesi zinaongezeka. Maana yake ni kwamba hili jambo lilikuwa halifanyiki vizuri sana.

“Mama (Rais Samia) amekwenda kurekebisha, kuboresha tu kuwa hebu tusijikite kwenye idadi ya kesi, hebu tujikite kwenye kesi ambazo ni za msingi ukienda nazo zinaenda kutupa matokeo.

“Lakini, jambo kubwa kumekuwa na malalamiko ya watu kupewa kesi nyingi, wakati mwingine hata ukizisikiliza unaona wanashinda. Yaani mtu anakamatwa, anawekwa ndani anakaa muda mrefu ndani, halafu mwisho wa siku anaachiwa kuwa ameshinda yaani hana hatia.

“Unajua hata haki zake mnakuwa mmezipoteza, maana iko haja ya kufikiria namna ya kubadilisha baadhi ya sheria tuongeze wigo wa dhamana. Mtu aadhibiwe baada ya kuwa ameshapitia kwenye mchakato wa kimahakama na amekutwa na makosa,” alisema Nape.

Alisema kwa mfumo wa sasa ulivyo kuna watu wanaadhibiwa hata kabla ya mahakama haijawahukumu, kwa kesi pengine kuhisiwa.

“Unaambiwa huna kesi, lakini umeshakaa miaka, umeshasota, umeshaumia kwa hivyo nadhani wito wa mama (Rais Samia) katika masuala ya kesi ni kuzingatia haki,” alisema Nape.

Credit: Mwananchi
Sifia sana lakini cheo hupati,ulishaharibu kabla.Rekodi zipo.
 
[emoji3516] Hii ni dalili wazi kwamba wote walikuwa wanaimba pambio wakijua wazi.kabisa yanayofanywa na Mungu mtu sio halali! Lakini hapkuwa na wakusemea lolote.
Nadhani huko.aliko Huyo Mungu anayasikia !!
 
Samia asipokuwa makini na Wana siasa wa nchi hii atapoteana mapema Sana.

Kuwa Rais sio kitu Cha kitoto.


Aamini tu kwamba hadi Sasa Kuna watu hawaamini kama yeye Ndio Rais ama wao wataweza kuongoza nchi wakiwa nje ya mfumo.

Unataka Rais aongoze hadi 2030 kwani Katiba hajaisoma huyu Nape?

Viongozi wetu wengi wanajipendekeza Sana hadi Aibu.
 
Mbona wanamnanga marehemu hata kabla hajaoza huko aliko? Si wangesubiri hata tumalize maombolezo?
 
Nape amesahau hana tena Godfather.

Sidhani atamrubuni SSH,Lakini ajikite kwenye Chama,yawezekana akasikika na kulamba nyadhifa za serikali.
 
Goli la mkono linamtesa huyu ndugu wa kijani

Unafiki unamtesa huyu mganga njaa. Huyu akiwa Waziri ndio alifungia television zisioneshe shuhuri za Bunge!! Leo hii ukimuuliza sababu ya sera ile na faida yake kwa wananchi hawezi kujibu kwasababu alifanya kwa kujipendekeza kwa mwendazake!!
 
Unafiki unamtesa huyu mganga njaa. Huyu akiwa Waziri ndio alifungia television zisioneshe shuhuri za Bunge!! Leo hii ukimuuliza sababu ya sera ile na faida yake kwa wananchi hawezi kujibu kwasababu alifanya kwa kujipendekeza kwa mwendazake!!
Malipo hapa hapa duniani
 
Nape nnauye unaharibu
Unaanza kutanish imge yako
Ilishaanza kuimarika ila unaanza ujinga
Unarudia kosa lilelile la wapambe wa jiwe.
Hiyo haitakujenga
Itakubomoa.
Unataka kutuambia waliosemajiwe aongezewe muda walikuwa sahihi?
Unarudia makosa nape anyway utafunzwa na wakati.
Tunapoelekea Tanzania tutakua na chawa wengisana kwasababu kila siku wanaongezeka
 
Back
Top Bottom