Nape Nnauye: Tuhangaike kujenga mifumo imara na siyo kutumainia mtu mmoja

Nape Nnauye: Tuhangaike kujenga mifumo imara na siyo kutumainia mtu mmoja

sio kweli sasa hivi utendaji serikalini uko juu mno vyombo vya habari havina cha kuandika sasa hivi kuhusu utendaji wa kizembe serikalini ni almost haupo

taja eneo walau moja lenye uzembe humu

Nenda polisi uone kama kuna tatizo lako litatuliwa bila kutoa rushwa na huna pa kushtaki. Nenda hospitalini kama rushwa zimeisha. Nenda mahakamani kama hakuna mlundikano wa kesi. Juzi hapa tume ya uchaguzi imeshiriki kimachomacho kuhujumu wagombea wa upinzani. Na ole wako ukathubu kusema hayo hadharani uone utakachofanyiwa ikiwemo kuhujumiwa shughuli zako za kujiingizia kipato.

Siku moja rais alifanya mkutano na wafanyabishara kusikiliza kero zao, kuna mzee mmoja wa Mbeya akafunguka kuhusu rushwa za TRA, nenda kamuulize leo hii ana hali gani baada ya kuweka ukweli ule hadharani. Nenda leo TRA ukaone barua za kufunga biashara kisha usikilize matatizo ya hao wafanya biashara kuhusu kubambikiziwa kodi. Funga kazi, unaweza kusema zile pesa zilizochukuliwa kwenye Bureau de change zikipelekwa wapi kama sasa hivi kuna utendaji wa weledi huko serikalini?
 
Shida ya sasa watanzania wanageuka kuwa mambumbumbu kisa hawapati taarifa sahihi ,zinazowafikia ni pambio kupitia redio,tv,magazeti na social media za utambulishi usio na kificho.

Exactly.
 
Wabunge wengi wa CCM wakisikia hoja ya kumuongezea mtu miaka wanasonya.
2025 ni muda wa akili mpya, haya ya flani aendelee ni maneno ya wajumbe tuu wanaolinda ugali wao.
 
JF bana, leo nape amekua mtuu wa maaana na kupongezwa na kila mtu,
 
Umemjibu vizuri sana. Bunge hili hili letu? Haya mambo yalishapangwa na ndiyo maana safari hii wamepitishwa wabunge wa hovyo hovyo. Nasema kupitishwa kwa sababu hakukuwa na uchaguzi. Atakachokifanya Magufuli ni kuwaambia (kwa njia kutumia wapiga debe) kubalini hoja ipite na nitahakikisha mnakuwa wabunge wangu muda wote nitakaokuwa madarakani ili tusaidia kupiga kazi.
Eti hapana watatoa wale 19 na 300 watasema ndiyo
 
Ameongea ukweli sio sahihi kumtegemea mtu mmoja, tatizo lenyewe tunaenda mwaka wa sita culture ya ufanyaji kazi serikalini aijabadilika pamoja na kwamba amejaribu kuwaacha wakurugenzi na wakuu wa wilaya/mikoa wale wale ulitegemea by now wawe na experience ndio kwanza ata kusimamia miradi yao shida.

Wizarani wataalamu pia awajabadilishwa ovyo lakini bado hakuna consitent serikalini matatizo aliyoyakuta mpaka leo yapo kwa percent kubwa inabidi aanze trouble shooting kila mara anaposimama kukutana na wananchi mpaka yeye mwenyewe anajiuliza kazi za watu wengine serikalini ni nini kama kila anapofika ni yeye ndio atupiwe shida.

Mtu pekee anaelekea kuweza kuendesha wizara aliyokabidhiwa ni Dr Gwajima ila apunguze mapepe. Huyo mrithi wa Magufuli given the social contexts za jamii yetu aonekani.

Hao mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya; raisi akinyuti na wao uwaoni tena kwenye camera mpaka aibuke.

Let’s face it ignorance is another major issue watanzania bado awajajua ku deal na consequences of their action ppl take life so easy in Tanzania; ningekuwa naishi mjini nikapata ata wenyekiti wa mtaa watu ndio wangeelewa I do not tolerate stupidity ukitupa taka mtaani unakula fine hapo hapo au nakupa fagio ufagie mtaa mzima.

In short serikali imejaza mapambo kwa majina ya wasimamizi wasio na managerial skills husika za kuendesha wizara yaani wewe waziri mpaka ufike site ndio ujue mradi upo 40% badala ya 90% kama ulivyoambiwa huna supervision matrix ya kila mradi na communication zako za watu chini je.

Akiondoka Magufuli tunarudi square 1 jumlisha na hizi pressure za wafanyakazi wa serikali atakaefuata akiendekeza kelele za hawa watu atakuta mapato yote anawapa wao kama mishahara na marupurupu; hana kinachobaki kwa ajili ya miradi ya kimkakati ya maendeleo.
Mchanganyiko wa pumba na mchele kwenye andiko. Ujumbe ni kwamba tujenge mifumo bora na sio kumtegemea mtu mmoja ambaye ukiangalia style yake ya uongozi pia ina mapungufu mengi
 
Naongelea kwenye kero za watu wengi sio wagombea ubunge wachache wa CHADEMA waliopigwa chini au wahalifu wachache wenye mikesi Polisi au Mahakamani au TRA naongelea utendaji wa serikali kuwa ni mzuri kwa majority ya wa Tanzania siongelei minority unaoongelea wewe
 
Nape CCM yenu ishawatema hamna chenu... yaani wewe na wenzako ni kama sisi tu...uliopokonywa form za uteuzi njiani.

tena shukuru mno bila kupiga magoti hata hako ka ubunge ungekasikia kwa radio.
 
naongelea kwenye kero za watu wengi sio wagombea ubunge wachache wa chadema waliopigwa chini au wahalifu wachache wenye mikesi polisi au mahakamani au TRA naongelea utendaji wa serikali kuwa ni mzuri kwa majority ya wa Tanzania siongelei minority unaoongelea wewe

Hiyo serikali inachagua maeneo ya kuhudumia? Polisi, hospitali, Tra nk zinahudumia minority? Nasema hivi, serikali kudhibiti vyombo vya habari na kuvifungia vinapotangaza ukweli isioupenda, hiyo haiondoi ukweli wa matatizo ya watu au utendaji duni wa serikali fullstop.
 
mifumo tayari imewekwa culture ya utendaji kazi imebadilika serikalini sasa hivi mteja mfalme ile cukture ya mfumo zembe ya mtu kujiona Mungu mtu kwa wananchi imekufa sasa hivi ni mtu kutumikia wananchi

mfumo bila kujenga cukture ni hopeless .Magufuli kahakikisha culture ya utendaji kazi inabadilika.Mfano sasa hivi mtendaji kijiji au kata ana nguvu ya kusimamia miradi eneo lake kuhakikisha iko kwenye kiwango vinginevyo anakuripoto ngazi ya juu kwa ubabaishaji

huko nyuma tulikuwa na mifumo ndani ya chama na serikali lakini ilikuwa hopeless inafuga wazembe na matapeli na vibaka na mafisadi ndani ya chama na serikali.Magufuli kafanya mapunduzi makubwa kiasi kuwa atakayekuja kumpokea hatapata shida kuongoza
Sasa kama mifumo ipo kwanini mnataka Magufuli aongezewe muda?
 
Kumbe bila hata mguu wa mtoto anaongea points
 
sio kweli sasa hivi utendaji serikalini uko juu mno vyombo vya habari havina cha kuandika sasa hivi kuhusu utendaji wa kizembe serikalini ni almost haupo

taja eneo walau moja lenye uzembe humu
Hakuna tofauti kubwa ya ufanisi kati ya huyu na watangulizi wake. Ubunifu pekee alionao ni vitisho na kupambana na watoa habari. Rais ajaye akitokea kambi tofauti, itabidi kupanua magereza zetu kukabiliana na waliotenda makosa chini ya utawala huu.
 
Back
Top Bottom