Nape: Sasa hivi vyuma vimelegea, Rais Samia kamwaga pesa mtaani tofauti na awamu iliyopita

Vitu ni bei juu ila hela ya kununua ipo.

Wakati wa jiwe vitu vilikuwa bei chee ila hela haikuwepo
Sidhani kama hili lina ukweli kiasi gani
But nachojua
Mwaka jana Petrol ~1923
Diesel ~1902
Nondo 12mm ~22,000
Cement ~14,500
Bei hizi ni kabla ya Uchaguzi

Mwaka huu petrol ~2365
Diesel ~2532
Nondo 12mm~26,000
Cement ~17,000

Bado hela hazijachanganya mtaani Ila dalili inaonesha hela zitaanza kuwa nyingi mwezi Novemba na kueleke Christmas huko
 
Hivyi hakuna njia nyingine ya kutafuta teuzi tofauti na kujipendekeza na kusema uongo?
 
Huyo kiazi hajui kwamba hizo pesa anazodai zipo kitaa zipo mikononi mwa mabwanyenye wachache walio kwenye mgao wa tozo na pesa ya mkopo wa IMF.......unawezaje kuingiza pesa kwenye mzunguko kwa kulipana watu wachache kiujanja ujanja badala ya kuweka ruzuku kwenye pembejeo za kilimo na kuwaongezea watumishi mishahara na kuwapa malimbikizo yao. Kwa sababu hii serikali ya maigizo haina control kwenye bei za bidhaa kwa sasa kutokana na kuvurugika kwa hali ya uchumi wa dunia tarajia hiyo nondo kufika elf 50 hadi mwishoni mwa mwaka huu..​
 
Hilo la kumuongeza mingine hata kumi ni lenu nyie CCM wenye nchi sisi ni wakuburuzwa tu halituhusu.
 
Mhe. NAPE anachanganya mambo mawili. Kuongeza muda wa Rais kuongoza ni kitu tofauti na vyuma kulegea. Atoe hoja zenye mashiko. Suala la vyuma kuanza kulegea atueleze ametumia vigezo vipi. Nakumbuka mjadala mkubwa kuhusu tozo na bei ya petrol hadi serikali kuchukua maamuzi ya kulegeza kamba. Yawezekana busara ya serikali ilitumika baada ya kutambua kuwa hali ya maisha ilikuwa haijatengemaa kwa mwananchi walio wengi. Yawezekana naishi nchi tofauti.
 
Kazimwaga mtaa gan, naomben jbu waungwana, nmekod🚕
 
Hizi hela zimemwagikia mtaa upi iliwanainchi tukaokote ilihali mfuko wa mbolea haukamatiki kwa mkulima mlala hoi??
 
Kujipendekeza kwake ndo kazi yake ,taaluma yake,fani yake,kibarua chake,yeye anaona ni sawa Ila kwako unaona Kama kulamba takoma
 
Kongole mkuu, walonga chindedi
 
Jamaa ana roho ngumu sana
 
Si pesa zimemwagwa nyingi unasema nondo chakula je?? Umeounguza unga na mchele vingine vimepanda ni mpishank tu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii kama kweli hivi, kuna mshikaji wetu hapa kitaa bodabod wiki iliyopita kanunua samsung galaxy S10+ kwa 600k, kutokana na kaz yake kavunja kioo, juzi kachukua macho matatu, kaz zinafanyika
 
Hao viongozi wapumbavu wanapo semaga tanzania umaanisha wao mafisadi maana kwa mafisadi ni kweli vyuma vimelegea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…