Nasikitika kusema kwamba, Katiba Mpya tunayoitafuta kwa nguvu nyingi haiwezi kutusaidia

Nasikitika kusema kwamba, Katiba Mpya tunayoitafuta kwa nguvu nyingi haiwezi kutusaidia

Mnakuwa na viongozi na Rais ovyo kabisa hapa chini ya jua halafu mnakuwa na Katiba bora zaidi duniani. Tutatoboa?

Mnakuwa na Rais na wasaidizi wake bora zaidi lakini katiba ndo hii hii. Tutatoboa?

China tuijuayo haipigi kasi ya maendeleo sababu ya katiba bora zaidi duniani. Hapana. Ni timu tu ya watu wenye uwezo na nia ya kuipeleka China mbele ndio msingi wa kasi ya maendeleo ya China

Hata sisi tukipata vichwa vizuri vya viongozi vikakaa pamoja na kufanya kazi lazima tutoboe. Katiba ni miongozo Fulani ambayo inaweza isifuatwe au ikakanyagwa makusudi na mkanyagaji asifanywe chochote

MNA katiba Bomba lakini viongozi wenu kutwa kucha kuwapigia magoti wazungu, wachina, waarabu, wahindi na nk mtatoboa kweli?
Hiyo katiba ya china umeshaisoma?maana na yenyewe wamekua wakiifanyia maboresho kila baada ya miaka kadhaa.sasa jiulize kwanini wanafanya hivyo kama maendeleo yao hayachagizwi na uwepo wa katiba bora.
 
Nani kasema anataka katiba mpya ili kuondoa umasikini? Watu wengine mpaka kero, alafu unakuta jitu lenyewe ni jitu zima lakini la hovyo sana.
Kwako katiba mpya ina impact gani?
 
Akija jiwe mwingine hawa wote wanaobeza katiba mpya watalia na kusaga meno.
Ni kweli kwamba kwa katiba hii ya sasa tutakuja kupata rais wa hovyo ambaye Magufuli hataona ndani.

Eti katiba ya nchi inakuwa na ibara fulani fulani zinazosema "Kama ikimpendezea Mheshimiwa Rais". Hiyo sio katiba.. ni waraka fulani ya kihuni tu.
 
Hakuna kitu kinaogopwa na CCM hapa duniani kama katiba mpya ya Tanzania.
 
Hiyo amri iliwekwa na nani na inasimamiwa na nani?.Maana wewe umeuliza ni nani atakayeisimamia hiyo katiba na mimi nimekupa mfano rahisi sana kuuelewa.kwamba kama jeshini inawezekana kujiwekea utaratibu na wakazisimamia wenyewe ata sisi kama wananchi tunaweza kuweka utaratibu kupitia andiko linaloitwa katiba na tukaisimamia wenyewe.Ayo unayoyaona yamefanyika uko nyuma nikwasababu kama wananchi hatukuamua tuwe na kitu bora chakutusimamia ndo maana viongozi wachache wakaamua kuitumia hiyo nafasi kwa maslahi yao binafsi ila haimaanishi kwamba hatuwezi kua na katiba nzuri na ikajisimamia yenyewe.ata uko jeshini sheria zipo ni kazi ya askari kuifwata basi kinyume na hapo inakugharimu.
Mkuu, ili uwe mwanajeshi unahitaji upite wapi na wapi, au unahitaji upewe amri pekee??

Hao achana nao, kwani wao wanapitia mafunzo kwanza kabla ya kila kitu

Sasa wewe, unaenda kudai tu katiba bila ya kuwafundisha wananchi namna ya kuilinda hiyo katiba, na ndiyo maana hatutapata anayewajibika kuilinda kwa sababu kila mmoja anajua hiyo katiba ni ya watu fulani na fulani
 
Jamaa anakubaliana na wewe, ila anauliza, Mbona wanaoivunja katiba ni wengi tu na hata wale ambao katiba haiwalindi nao kwa nini hawadhughulikiwi?

Anasema, Je katiba mpya tunayoitaka, Itajipeleka mahakamani yenyewe kushitaki kwa nini inavunjwa?

Je, Itajiandamanisha kupinga kwa nini inavunjwa?

Au ni kwa namna gani hao wavunja katiba watashughurikiwa ikiwa Watanzania hawajui kudai haki zao na kama wakijua, sana sana wataandamana Mitandaoni na kudai haki hizo Mitandaoni?
Tatizo linaanzia ktk katiba yenyewe, maandamano na mahakama ndo kiboko ya kuwawajibisha wavunja katiba, haya tumeeandamana polisi hao wanatumwa na mamlaka ya juu kutawanya maandamano kwa silaha za moto, maaskari na mahakama hawawezi kukataa maagizo ya mamlaka toka juu make ndo inayomteua na kumfukuza, endapo katiba itamhakikishia security hawa maafisa pindi wakikataa maagizo batili toka juu, hakika wavunja katiba dawa yao ni maandamano yasiyo na kikomo mpaka waachie ngazi.
 
Tunawetaka katiba mpya lakini sio hiyo wanayoitaka wao ya kuwaingiza ikulu kufanya biashara
Huwa nahisi wewe ni ccm lakini hapa umeandika tofauti na ccm wenzako wanaodhani katiba ni kwaajili ya chadema.
Tudai katiba kwaajili ya nchi ,vyama vipambane vyenyewe kufuata matakwa ya wananchi.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo katiba ya china umeshaisoma?maana na yenyewe wamekua wakiifanyia maboresho kila baada ya miaka kadhaa.sasa jiulize kwanini wanafanya hivyo kama maendeleo yao hayachagizwi na uwepo wa katiba bora.
Hivi katiba itakataza viongozi wa nchi kuwapigia magoti wachina na wazungu?
 
Hii kwangu ndio hoja ya msingi! Unashabikia katiba ili Mbowe anufaike na kumuingiza Lissu madarakani 😂😂😂 ni akili au matope hayo!
Jamaa nakuonaga una akili kumbe na wewe ni pimbi tu, haya hata kama sio lissu au mbowe kwanini asishabikie katiba itakayotoa fursa kwa mtz yoyote kupata madaraka kwa njia halali na ya wazi hata kama atakuwa ni yeye mwenyewe au babu yake au Dada yako?
 
Mkuu, ili uwe mwanajeshi unahitaji upite wapi na wapi, au unahitaji upewe amri pekee??

Hao achana nao, kwani wao wanapitia mafunzo kwanza kabla ya kila kitu

Sasa wewe, unaenda kudai tu katiba bila ya kuwafundisha wananchi namna ya kuilinda hiyo katiba, na ndiyo maana hatutapata anayewajibika kuilinda kwa sababu kila mmoja anajua hiyo katiba ni ya watu fulani na fulani

..kuna nchi zimekuwa zikihubiri HAKI na wananchi wao wana mwamko wa kulinda katiba.

..hapa Tz tumekuwa tukihubiriwa kuhusu AMANI na wananchi wetu wamekuwa wapole wasioweza kuzi-challenge mamlaka.
 
Mkuu,Ujue sipika halindwi na katiba pindi anapovunja katiba

lakini kwa nini sasa hakuna anayemshughilikia?

Ni nani wa kumshughulikia
Ni kwasabb katiba yetu imemfanya rais kuwa juu ya katiba. Kwahiyo rais anamlinda spika. Hakuna wa kumgusa spika maana analindwa ña rais.
 
Wewe ndio hujui umuhimu wa katiba na jinsi inavyofanya kazi.jielimishe kwanza ndo urudi kwenye mjadala.

..labda ungeanza naye taratibu. Jamaa ni mgumu kuelewa, pia inawezekana ametumwa.

..swali la kwanza je tuwe na katiba, au tusiwe na katiba?

..kama anataka tuwe na katiba, je, iwe katiba mzuri inajali maslahi na haki za watu wote? Au iwe katiba mbaya inayojali na kuwalinda viongozi peke yao?
 
Kilichonishangaza kingine, ni kuona na kusikia MMK wa Chadema akisema, Katiba eti ni agenda ya nchi??

Alomdanganya hivyo ni nani Wakati wananchi wengi hawana habari na hicho kinachodaiwa ni agenda ya kiraifa, sisi tunaona ni kikundi kidogo tu tena ni chama kimoja pekee chadema ndio wanahangaika

Wameshindwa hata kuviunganisha na kuvishawishi vyama vingine pinzani ili angalau kuonekane hako kasura ka kitaifa ka uwongo na kweli
Hizi fikra ni duni kabisa, hakuna ubaya wowote hata kama anayelilia katiba mpya ni mmoja tu nchi nzima, cha msingi anayelilia hiyo katiba mpya kaanisha madhaifu ya zamani na kapendekeza mambo mapya bora kabisa, so cha muhimu hao wanaopinga waone umuhimu wa kumsapoti anayedai make wajue tz itaendelea kuwepo ila wao ni wapitaji.
 
Mimi pia huwa nashangaa jinsi watu wanavyoweka mkazo kwenye katiba mpya zaidi ya ubora wa elimu yetu.
Tungekuwa na elimu ya viwango stahili suala la katiba lingekuwa agenda ya wananchi karibia wote na sio sasa ambapo wenye shida nayo ni wanasiasa, wanaharakati na wasomi tu.
Tungekuwa na elimu bora watanzania wasingeruhusu kuvunjwa kwa katiba, kuchezewa uchaguzi na mihimili mingine ya serikali kama ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita.
Tunachohitaji haswa na elimu ya bora kwa ujumla na ya uraia ili tusije hata tukipata katiba mpya watu wakaendelea kuivunja maana watu ni walewale na uelewa ni ule ule na tabia zilizile.
Hizi ni fikra mfu na za kipumbavu, akina nyerere wkt wanapgania Uhuru haikuwa ajenda ya watz wote Bali ilikuwa ni kakundi kadogo tu, thanks God kwa ilikuwa ni kwa manufaa ya weusi wote bila kujali idadi ya waliokuwa mstari wa mbele kudai, pia ktk hili la katiba hakuna ubaya tukapata katiba bora hata kama alieishupalia ni lissu pekee, make itakuwa ni kwa faida ya watz wote bila kujali kakundi kadogo
 
Nikikuuliza wewe hio katiba iliyopo inakusaidia nini so far? Unaweza kunijibu kwa ufasaha labda! Inakunufaisha in what ways mpaka utake nyingine as if you have stakes on it!?
Katiba iliyopo ni mbovu inanufaisha waliopo madarakani ndo maana tunadai mpya itakayo nufaisha hata wasio na madaraka.
 
Ndiyo na ni ukweli kabisa, Katiba tunayojaribu kuitafuta kwa jasho jingi na Energy nyingi, nasikitika kusema, haitatusaidia popote kama nchi.

Kama kuna mtu anapingana na mimi, Embu atusaidie kujibu maswali haya

Ni kweli tumekuwa na katiba isiyokidhi matakwa yetu hususani katika midhania ya kisiasa, kwa maana, katiba iliyopo, ilitungwa chini ya Chama kimoja, hivyo kuvifanya vyama vingine kukosa uhalali wa kulindwa na katiba hii tuliyonayo

Kingine, Katiba hii iliyopo, inamfanya Rais wetu kuwa mfalme, ni kama yeye ni mtu wa kwanza na wa mwisho, kwa lugha ys kiyunani, ni Alfa na Omega, n.k

Sasa basi, Ukisikiliza kwa umakini, wengi wa wanaharakati wetu kwenye majukwaa ya kisiasa na majumkwaa mbalimbali mbali, Utasikia wakisema, Tunataka katiba itakayotuwezesha kuwaajibisha wote wanaovunja katiba

Ni jambo jema, maana mtu yeyote anayediriki kuvunja makubaliano yetu na katiba yetu , ni sawa na matusi kwa watu woote kama taifa

Tumeshuhudia katiba yetu ikivunjwa waziwazi na baadhi ya viongozi wetu,

Bahati mbaya ni kwamba, kuna waliovunja katiba hata kwa wale ambao, katiba hailindi ouvu wao kama ilivyo kwa Maraisi wa nchi, lakini wanapovunja, Hasira zetu tunazielekeza kwa kiongozi mkuu, tunamsagia meno, Wakati huohuo, Katiba yetu mbovu tuliyonayo, ni kumlinda Raisi wa nchi na maovu yote kipindi awapo madarakani, na kwamba Hawezi kushitakiwa kwa kosa lolote awapo madarakani

Na bila shaka, shida yetu inaanzia hapo


Okay, Achilia mbali makosa ya Rais kwa mjibu wa katiba mbovu tuliyonayo kwamba, hatoshitakiwa kwa makosa yoyote aliyotenda akiwa madarakani, Hili tunaweza kusema, lipo juu ya mamlaka ya kawaida ya mwananchi kumwajibisha Raisi wao kwa kuwa katiba inamlinda

Upande wa pili kwa kosa hilohilo la kikatiba, Tumeshuhudia Bunge lisilo halali, Ni bunge ambalo wabunge wenginewe waliomo humo bungeni si wabunge halali kwa mjibu wa katiba za vyama vyao pia kwa mjibu wa katiba ya nchi, kwamba hawana uhalali wa kuwa wabunge kwa kuwa, hawatambuliki na vyama vyao na katiba haitambui mtu wa aina hiyo kuwa sehemu ya bunge

Sasa basi

Nionyesheni ni wapi ambapo huyo mkuu wa mhimili huu wa Bunge alipohalalishiwa na katiba hii mbovu tuliyonayo kwamba naye hawezi kuwajibishwa,

Je sasa, ni nani wa kumwajibisha?
Ni kwa nini tunataka katiba mpya, Je, ni nani atakuwa mbadala wetu wa kusimama na kuwawawjibisha wote wavunja katiba?

Je, katiba hii mbovu ilipokuwa ikivunjwa, ni nani anafahamika ambaye yeye anapaswa kudili na wavunja katiba yetu? Je, alifanya kazi yake?


Na kama alishindwa kuwashughurikia hao waharifu wa kikatiba, Ni kwa vipi anadhani itakuwa rahisi kuwashughurikia kukiwepo katiba mpya?

Ni nani asiyejua kwamba, Watanzania, Watanzania kwao ni wazuri wa kuhamaki mitandaoni pekee ila nje ya hapo ni watu wanafiki na wapole kama maji ya mtungi? na ndiyo maana hata Asiyelindwa na katiba aweza kuvunja katiba na ikawa salama??

Mkinionyesha atakayekuwa zamu ya kuwashughurikia wahalifu wa kikatiba badala yetu, ndipo nitakubali kwamba, Tunataka kweli katiba na tumemaanisha

Katiba haijilimdi, haijipeleki mahakamani, haiandamani na wala haimtishi mvunja katiba, Nionyesheni mlinzi wa katiba

Tanzania hoye?

Hahaahaaa haa 😂😂😂😂.

"Nionyesheni ni wapi ambapo huyo mkuu wa mhimili huu wa Bunge alipohalalishiwa na katiba hii mbovu tuliyonayo kwamba naye hawezi kuwajibishwa,"

Kwamba hujui ilishapitishwa kuwa wakuu wa mihimili na manaibu wao hawawezi kushitakiwa kwa makosa yoyote yatokanayo na utekelezaji wa majukumu yao na hii sasa ni sehemu ya sheria kwa mujibu wa katiba?

Pia hutambui kuwa mapungufu ya katiba iliyopo ndiyo yanayoyaleta mikanganyiko unayoiongelea sasa?

Kimsingi kama hufahamu hali nzima ni kama hivi:

1. Katiba iliyopo haiwawajibishi baadhi ya watendaji wakuu kwa kuikiuka, na hii ni kwa mujibu wa katiba yenyewe.
2. kwa katiba iliyopo pana watu hata kama wakiiba, wakipora, wakiuwa, wakidhulumu nk hiyo ni halali kwa mujibu wa katiba yenyewe.
3. katiba iliyopo inawapa baadhi ya watu mamlaka ya kujifanyia lolote bila kuhojiwa au hata kuwajibishwa tu.
4. Katiba iliyopo haitoi haki sawa kwa watu wote ndani ya nchi.
5. Kuna mianya mingi katika katiba hii ambayo inaweza kuifanya mihimili mingine hata kupoteza uhuru wake wa kiutendaji kwa mujibu wa katiba yenyewe.
6. Kuna utitiri wa nafasi za uongozi wasio na tija wala ridhaa ya wananchi ambao pia ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi.
7. Kuna utitiri wa vigogo wenye mapato yasiyoakisi tija, wala kuwa na ridhaa ya wananchi na wasiolipa kodi (stahiki) wanaopata uhalali kwenye katiba hii.
8. Nk nk.

Kwenye mazingira haya asiyewajibishwa kwa mujibu wa katiba atawajibika vipi kwa katiba hiyo?

Hadi hapo bado huoni umuhimu wa katiba muafaka zaidi tena katika hali ya dharura inayowezekana?

Unadhani ni mazingira yapi yalitufikisha tulikofika na awamu ya ile?

Katiba mpya yenye kuyaangazia kikamilifu mapungufu yote yaliyomo ni suluhisho kwa haki, usawa, na uhuru wetu, watoto wetu na hata watoto wa watoto wetu.

Hili ni hitajio sahihi na la msingi ambalo si sawa kupuuzwa.
 
Back
Top Bottom