Huwezi pakia mzigo njian , viaz ni vizito balaa.. unapakia kati ya gunia 100 au 110, gunia unakuta lina kilo 130 hadi 150 , so hapo tayari una tani zako 15 au 16 zinazotakiwa kwenye mizani (wengine wanajua chekecha zinapakia hadi 18) ila ni risk sana, miaka miwili nyuma ninasafirisha fain ilikua dolla 200, saiv sijui n bei gani karibu lak 5 hiyo , njian ni mizigo midogo midogo tu ambayo unaweza mwachia dereva apate pesa ya kuhonga michepuko yake
Sio sahihi, alichosema offshore ndio usahihiKwa hiyo maelezo ya engineer wa jeshi sio sahihi?
Ila wabongo kwa kurekebisha vitu tumeshindikana tani 5 mpaka tani 18 sio poa kabisaJapo sipo kwenye mood ya kuandika, lakini nikipita kimya nitakua sijakutendea vema wala kuitendea vyema nafsi yangu.
Nina uzoefu niseme wa kutosha kuweza kutoa 'expart opinions' kwa mtu anyetaka kuanza biashara ya usafirishaji kwa kumiliki malori.
Nawapongeza wachangiaji wenzangu kwenye uzi huu, ila kuna mawili matatu nimegundua toka kwa hao wenzangu japo kuu hasa ni hili.
-Wengi hawana taarifa kamili na sahihi juu ya bei na uhalisia wa aina anuai za magari pia uhalisia katika sekta nzima ya usafirishaji hapa nchini.
Wengi wameshauri na umeonesha kuridhika na ushauri juu ya kuanza na Fusi-tandam. Mimi kwa uzoefu wangu sikushauri kuanza na tandam kwa sababu zifuatazo;
+ Gharama. Ununuaji na ubireshaji wa tandam huweza kufika 80-100mil hii ni gharama kubwa sana kwa gari ya tandam ukilinganisha na performance yake barabarani.
+Matunzo. Tandam ina gharama kubwa sana katika matunzo hasa hasa engine. Ukumbuke ile ni engine yenye HP kama 200 hivi lakini inabebeshwa tani 18 hivyo injini huchoka haraka na kuhitaji kubadilishwa. Ni kawaida kwa life span ya injini kwenye tandam kuwa miaka minne japo mara nyingine huweza kujikongoja hadi 8 kutokana na nidhamu yako ya kuibebesha mzigo
+Mifumo ya uendeshaji. Tandam nyingi hasa hasa nikiwa ni mzigo hata tani 12 tu ujue haina uwezo wa breaking za ghafla so katika kipengere hiki tegemea neema ya Mungu na kuthibitisha hili fuatilia ajali za tandam kugonga gari nyingine kwa nyuma utaambiwa sababu.
Kama utaamua kuanza na gari toka ukoo wa mzee Mitsubishi basi achana na tandam ila chukua fuso kipisi beba tani zako 7au 8 baas. We mwenyewe jiulize tu gari ulikua designed kubeba tani 5 ila Bongo Pasua Kichwa Engineering wanaifanya ibebe tani 18.
USHAURI WANGU SASA.
Kwa mtaji wa milion 100, anza na gari ambayo gharama ya manunuzi yake hadi kuingia road yaani horse na trailer yake isizidi 80ml.
Hapa utaona kipi rahisi kwako either kuagiza used ulaya au used ya kibongo bongo, ambapo kwangu naona ni sawa tu japo hakikisha kama ni used ya kibongo bongo usichukue iliyoingia nchini zaidi ya miaka miwili nyuma.
Hapo ukitaka kuagiza ni vema ukaanza na gari ambazo ni rafiki kwa mafundi na vipuri vyake mara ipatapo faida. Nashauri Scania series 4 yoyote kati ya 114 au 124 horsepower yoyote hamna shida najua hiyo hadi inakaa road itakugharimu kwenye 60ml hivi na trela lake ni 20ml tu.
Anza na safari za local na kwa kuwa wewe ni mgeni basi kichwa chako ni halali ya Dalali na atakupiga sana katika miezi mitatu ya kwanza hadi kichwa kikukae sawa utengeneze wateja wako. Route zinatofautiana na msimu kwani kuna wakati nyanda za juu kubalipa na kuna wakati kanda ya ziwa kunalipa.
Oya nimechoka kutype, ntaendelea kesho
Ila shida inakuja kwenye matairi, yan Fuso zinaongoza kwa kupasua matairi.Ila wabongo kwa kurekebisha vitu tumeshindikana tani 5 mpaka tani 18 sio poa kabisa
Gharama za kazi hii hutofautiana kulingana na kazi itakayofanywa kwa gari hisika. Fuso zote za tani 3 huitajiwa kuwekewa double chasis ili ziweze kubeba tani 10 kwa single au 16 kwa tandam
Kwa nini mkuu magari haya hayatakiwi kubeba mkaa? Kuna siri gani?Chonde chonde usiruhusu lori lako kubeba mkaa, (kama ni kagunia kamoja basi akamwagie maji ndiyo akabebe)
Kuna kitu inaitwa axle configuration kwa magari yenye GVM zaidi ya 3500, hii ndio huamua gari ibebe mzigo kiasi gani regardless ya engine na uwezo wa gari husika. Mfano gari yenye axle mbili yenye tairi moja moja kwenye axle ya mbele na mbili mbili kwenye axle ya nyuma itakuwa configured as 1:2 na GVM yake utakuwa 18000kg.Kwahiyo tani 10 ndiyo mwisho mwa single diff?
Jee kama una DAF LF truck yenye GVW 12 tonnes, nayo pia huruhusiwi kuzidisha tani 10?
naombeni elimu hapo, wanaojua mambo ya mizani
Uzi unamadini huu.basi tu lakini nyuzi kama hizi ni za kuzitunza hazina kabisa.
Ila kuna bingwa mtaalam wa haya mambo hajaja hapa sijamuona.
Je nikiwa na gari yenye configuration hiyo ya 1:2, lakini GVW ya gari ni tani 7.5, Jee gari hiyo pia mwisho wake kubeba ni tani 18?Kuna kitu inaitwa axle configuration kwa magari yenye GVM zaidi ya 3500, hii ndio huamua gari ibebe mzigo kiasi gani regardless ya engine na uwezo wa gari husika. Mfano gari yenye axle mbili yenye tairi moja moja kwenye axle ya mbele na mbili mbili kwenye axle ya nyuma itakuwa configured as 1:2 na GVM yake utakuwa 18000kg.
GVM ni uzito wa gari pamoja na mzigo uliobebwa kwa hiyo kama gari likiwa tupu uzito wake ni 8000kg (tani 8) basi gari hili litabeba kilo 10,000 (tani 10) na iwapo gari hilo likiwa tupu uzito wake ni tani 10, basi mzigo itakaoruhusiwa utakuwa tani 8.
Kwa axle configuration ya 1:2 GVM yake ni 18000kg (tani 18) na GVM ni uzito wa gari pamoja na mzigo uliobebwa. Ili kujua mzigo unaoweza kubebwa chukua GVM (kwa kuangalia axle configuration husika) toa uzito wa gari likiwa tupu.Je nikiwa na gari yenye configuration hiyo ya 1:2, lakini GVW ya gari ni tani 7.5, Jee gari hiyo pia mwisho wake kubeba ni tani 18?
Asante kwa maelezo yako. Ni kweli biashara yoyote ni kujitolea muda wako kwa asilimia zote, hasa nchi kama yetu yenye culture ya watu kupenda kusukumwa kama ng'ombe. Kwa upande wa gari ndiyo zaidi kabisa. Bila wewe kuwepo mwenyewe kuwepo lazima utaumizwa.Sio muandishi mzuri bali naomba nichangie kidogo kwa uzoefu niliopata baada ya kuamua kuingia kwenye hiyo biashara 2011 to 2015.
1. Nilisajili kampuni na kupata investor Exemption TIC, unapata break kubwa ya kodi na zoezi likaanza.
2. Tuliagiza gari 4 na tela 4 Daf XF 3 flatbed trailer na 124 moja yenye tela ya tiper. 124 ilikuja single excel ikaongezwa hapa bongo kwa gharama ya 5M kila kitu.
3. Kazi ikaanza mwaka wa kwanza ulikuwa sio mbaya kazi zilikuwepo na madereva wa mwanzo walikuwa wanajielewa ikawa angalau si haba dola zilikaa mkononi. Shida ikaanza baada ya kuondoka kurudi ninapoishi nje ya Tanzania hapo madereva na wasimamizi ikaanza shughuli nzito madereva wakaondoka na kuanza na madereva vishoka hali ikawa tete nikaamua kuuza Daf zote nikabaki na 124 tipper nikatafuta kampuni ya ujenzi nikaingia now mkataba wa kazi na kuacha majukumu kwa mtu wa kusimamia hiyo tu.
My point.
Gari ya kuanza nayo kama unataka kusogea tafuta 124L haitakuangusha kama utaihudumia vizuri, unawezanunua single excel ukaongeza excel bongo maana kununua single ni bei chini na zipo nyingi europe.
Pia kama unataka kuingia kwenye hii biashara ni kweli pesa ipo sana ila unahitajika kujitoa kwenye hiyo biashara 120% hakikisha gari imepakia mzigo bandarini usimuamini agent, Ukiweza safiri mpaka nchi za jirani kutana na ma agent na jenga nao ukaribu na muaminiane sana.
Dereva makini ndio mtaji na mafanikio yako ,kama ukipata dereva mzuri basi mtunze na muhudumie kama nyumba ndogo yako sababu utapata return kwake ya kuhudumia chombo kinachompa mazuri yote unayompa.
Mwisho Nasisitiza hili. Muda wako wote ujitoe kwenye hiyo kazi na uwepo wako ndio mafanikio yako.
Mimi ilinishinda kutokuwepo sehemu ya tukio ila kwa biashara ni nzuri sana ,ingawa sasa hivi kidogo ina misukosuko ya hapa na pale lakini muda utapita itarudi kama zamani.
Nipo njia kuirudia 2026 kunapo uhai.
Asanteni.
Scania? Moshi naona wako njema .. HP ngap mkuuKuna siku niliongelea kuhusu bei za Scania 93 na model za aina hyo kuwa unaweza kuchukua kwa bei ndogo na ukaifanyia service ila baadhi ya wanajamvi waligoma kuwa sikuwa sahih kwenye bei.
Sasa chuma hiyo hapo kesho mungu akipenda tunaenda kuilipia kwa milion 17 tu, baada ya hapo inaingia garage moshi ikitoka huwez kuifaham.
NB: kama ni mgeni na chuma usijaribu kununua kwa mfumo huu.View attachment 1502384View attachment 1502380View attachment 1502382View attachment 1502383View attachment 1502381View attachment 1502385
Hiyo ni HP 280 mkuu.Scania? Moshi naona wako njema .. HP ngap mkuu