Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Mkuu mimi sio mtaalamu wa magari wala sijawahi kufanya biashara ya magari lakini nimeukubali sana ushauri wako. Watu wanadanganyana sana mitaani kuhusu biashara za magari wakidhani ni rahisi kama wanavyofikiria.
Mimi nilianza biashara ya Usafirishaji miaka kama 10 iliyopita. Hata sasa hivi nafanya usafirishaji mizigo sana tu local ila kwakua imenibidi(Niko kwenye supply business) kwahiyo swala la kuwa na Gari linasaidia kupunguza gharama ya bidhaa nnazouza.

Ila kama ingekua ni uamuzi wangu nisingekuja kumiliki gari la mizigo tena KAMWE

Hio mil 100 tafuta biashara nyingine sio ya kuwa na gari moja.Ni Risk kubwa mno unajitafutia .Hakuna cha bima wala upuuzi wa bima .Utakufa siku sio zako

Ukiwa na magari mengi inasaidia kugawanyisha Risks. Madereva nao dahh kila siku ni kutishana na bastola mezani na kutiana lockup

Hakuna biashara pasua kichwa kama hii katika biashara zote nilizokwisha kufanya

Usione kina Usangu,Overland wanazungusha chuma tu kisauzi ila hii biashara sio mchezo.

Ungekua na mtaji wa Billion plus ningekushauri hata uanze kupambana na kina Sham Nunu na hao underdogs wengine na nisingekushauri huko kwenye Mascania. Howo anafanya vizuri sana saivi anaenda ligi za kina Daf/Volvo
 
Inategemea mkuu.
Usifanye kitu kwa kuwaiga wengine, fanya kitu pale inapobidi kufanya kutegemea na uwezo wako.
Biashara ya magari haina urafiki na mtu maskini, risks zake ni nyingi sana na zote zinahitaji pesa.
Matajiri wanaiwezea kwa sababu wanakuwa nazo nyingi so ikianguka moja wala hashtuki anajua atazitumia zingine na kupata pesa za kuiokoa iliyoanguka.
Tanzania yapo magari mangapi?? yote yametumbukia ? biashara zote zina risk mkuu, na zote zina risk za kuhatarisha na kuua mtaji wote , ndio maisha yalivyo, tuna options mbili tu either tufanye au tusifanye
 
Mkuu,

Nikupongeze sana kwa uthubutu huu.

Hii biashara ni nzuri ila ina changamoto zake za hapa na pale ila ina pesa.

Ili uweze kutoboa kwenye hii biashara jitahidi kumudu jazba zako kwa dereva wako tena hasa akiwa porini , Dereva ndiye mtu anayeweza kukufanya ufanikiwe na kukufanya ufeli mazima.

Trailer zipo za aina mbili,

Flatbed na Skelton

Kwa vile wewe ndiyo unaanza basi nakushauri uchukue flatbed kwa sababu kazi zote utabeba. Vilevile uchukue Trailer yenye (axles za BPW).

Kampuni zinazozalisha hizo trailer zipo nyingi hapo mjini, Superdoll, Simba na wengineo, Nashauri ununue trailer za mtumba.

Kikazi,
Kuna trip za local( za ndani)
Kuna trip za transit ( Nje ya nchi)

Trip za ndani sikushauri uzifanye kwasababu zinachosha gari na magurudumu. Ni bora ufanye hizo za Transit tu, tena za Dar - Lubumbashi tu.

Trip za Dar - Lubumbashi hazichoshi gari ingawa gari inachukua mwezi mzima au zaidi lakini pesa yake unaiona, Gari inaenda na mzigo na inarudi na mzigo (Copper)

Sasa ili uweze kufanya hizo trip za transit kwa mtu wa gari moja, nakushauri ufanye joint venture na mtu mwingine ambaye ana gari nyingi ili uweze kupata c28 ya TRA na hii itakusaidia kujikusanya na kujifunza mchezo.

Kwanini nasema hivyo, sijajua mfuko wako ukoje ila kuna mlolongo wa makadirio ya kodi, kukata vibali vya Zambia na mambo mengine, kwa gari moja ni story tu.

Mkuu, Magurudumu ya gari yako hakikisha umenote zile serial number na uwe mfwatiliaji wa kuyakagua kila baada ya trip.

Dereva mtaji wake ni Diseal na Magurudumu, akiishiwa huko njiani anayanywa fasta na yanauzika sana hapo Tunduma au huko Mpika.

Punguza wanawake (Mademu) magari ni kama Majini hayapendi uchafu wa mwili, na pia dereva asikuzooee sana maana wanakuwaga na vinasaba vya kiswahili unaweza kujikuta yeye ndiye kawa boss na wewe ukawa mfanyakazi wake. Zingatia Services ya gari, usifuge magonjwa kwenye gari!

Naomba niishie hapa,
Cheza na dola mkuu.

Shukrani
Hapa umeeleweka
 
Mkuu sorry, hiyo fuso tandem inapatikana kwa bei gani hapa Tanzania ikiwa used na haijachoka?
Mkuu mie nakushauri anza na Fuso Tandam ndio utapiga pesa zaid. Ninakushauri hvo kwa kuwa hapa home tuna Scania tatu na Fuso mbili ila Fuso ndio zinapiga kazi kuliko Scania.

Na pia km ni Scania kwa wewe unaeanza sikushauri kwa kuwa ni sumbufu sana hasa ikishaanza kuchoka. Scania za kukutoa umaskini ni zile model za kizaman.

Na pia wanaokushauri kuhusu magari ya abiria naomba usiwasikilize kabisaa, maana yana changamoto nyingi sana. Mie binafsi nina Nissan Caravan mbili ila ni kichefu chefu kitupu.

NB: nimekushauri kutokana na uzoefu wangu wa kuishi na hayo magari kwa muda mrefu.
 
Kama unavyojua kwny utumiaje wa mafuta Fuso inatumia kidogo zaid kulinganisha na kipisi, pia Fuso Tandam inapakia had tani 16 na ikipita mizan sio shida.

Ila kipisi ukipakia tani 16 lazima upigwe faini kwny mizani, kuna kitu wanaita GVT km sikosei yaan uzito wa gari ikiwa tupu kwa Kipisi inakuwa nzito zaid. Ndio maana kwny mizan inazid

Sie sana Tandam zinapga kazi kwenda kupeleka mahindi huko kwa Usukumani. Gari inakodishwa hadi 1.6 milion kwa trip na ukitoa gharama ya kila ktu had kulipa vijana inabaki hadi 1.1 milion.
Na gari ndani ya siku mbili tu inakuwa imeshaenda na kugeuza.

Mkuu mie ni mvivu sana ku-type text ndefu ila nadhan nmejitahid kadri ya uwezo wangu
Ina maana gharama ya mafuta haizidi laki tatu?
 
Inategemea mkuu.
Usifanye kitu kwa kuwaiga wengine,fanya kitu pale inapobidi kufanya kutegemea na uwezo wako.
Biashara ya magari haina urafiki na mtu maskini,risks zake ni nyingi sana na zote zinahitaji pesa.
Matajiri wanaiwezea kwa sababu wanakuwa nazo nyingi so ikianguka moja wala hashtuki anajua atazitumia zingine na kupata pesa za kuiokoa iliyoanguka.
Mkuu mambo yalivyo tofauti kabisa na wewe unavyofikiria, kila biashara inarisk zake.

Kuna mtu ana roli moja tu ama mawili na mambo yanaenda.

Eti kwa sababu kuna ndege imeanguka ikateketea basi mwenye wazo la kuanzisha biashara ya anga ahairishe!!?
Lori limetumbukia mtoni basi watu wasifanye biashara ya maroli kisa kuna lori liliingia mtoni!!?
 
Mtoa mada kama kweli kilimo cha vanilla kimeweza kukupatia mil 100 nakushauri endelea tu na kilimo.

Kuhamia kwenye biashara ambayo huijui tena ya magari hii inaweza kuwa ndo downfall yako na baadaye kwenda kwenye uzi uleeeee wa waliowahi kushika pesa ndefu halafu ghafla zikapotea.

Hili ni wazo tu lakini maana kuna wengine wameweza kubadili biashara pia wakafanikiwa.
 
mtoa mada kama kweli kilimo cha vanilla kimeweza kukupatia mil 100 nakushauri endelea tu na kilimo
kuhamia kwenye biashara ambayo huijui tena ya magari hii inaweza kuwa ndo downfall yako na baadaye kwenda kwenye uzi uleeeee wa waliowahi kushika pesa ndefu halafu gafla zikapotea
hili ni wazo tu lakini maana kuna wengine wameweza kubadili biashara pia wakafanikiwa
[emoji1][emoji1]
 
Tafuta Tandam kisha ingia kwenye biashara ya kupeleka mahindi/ng'ombe/mbuzi/mchele/nyanya/viazi/ndizi/maharage Dar.


Kwa heshima na taadhima nakuomba Tabutupu uje na uzi unao eleza kwa kina hiyo vanila iliyofanikisha kukupa 100m ili tujifunze na sisi.
Kweli ndugu Tabutupu tunaomba utupe muongozo umetoboa vipi kwenye vanilla
 
Nimepata kama mil 100 baada ya kuvuna vanila huko Bukoba. Sasa nahitaji nijiingize kwenye biashara ya usafirishaji na wazo langu ni kununua scania kama kwenye picha.

Nimepanga kuanza na moja kutokana na kiasi nilicho nacho.

Naomba wenye uzoefu, kama biashara ikienda vizuri, kwa mwezi naweza ingiza kiasi gani?View attachment 1484199

Nakushauri uendelee kulima vanila, uko unakotaka kwenda muda si mrefu utaingia kwenye imani za kishirikina, kwani yatakayokusibu kuhudumia hilo gari utasema umelogwa.
 
Scania ni Gari Nzuri sana
Tatizo kubwa kama ilivyo kwa biashara nyingi ni hulka ya Watanzania kutokupenda kazi na kuiheshimu. Hulka hiyo chafu iko kila sehemu.

Dereva wanaiba sana tairi na mafuta na kama huna Proper management atakumaliza.

Tatizo ninaloona kwako ni mtaji mdogo maana ukinunua hiyo R 440 kwa bei za Dar itasoma 80 Flatbed used nzuri ni 25 hapo unasoma 105.

Bado hujanunua Tairi say labda unaweka super single na zile zingine za deef ziko 4.

Baada ya muda utaona kabisa mtaji wako huo hautoshi nashauri uwe na 115. Ili ubadili tile zote za horse na pia ukate bima kubwa turubai na vitu vidogo kama jack na wheel spanner.

Jitahidi kuweka mpango mkali wa kuimanage hasa mafuta na tairi andika uwe na daftari unaandika. Kingine hakikisha unasaka maduka ya spea unaulizia spea.Kama hujui spea na zinapouzwa utaibiwa sana utafilisika.
 
Back
Top Bottom